• BWAWA LA KIDUNDA: RAIS SAMIA ATEGUA KITENDAWILI KILICHOSHINDIKANA TANGIA UHURU

    Waswahili wana msemo wao usemao “Lisilo budi hutendwa”, kwa kadhia ya upatikanaji wa maji waliyoipata wakaazi wa mkoa wa Dar es Salaam na mkoa wa Pwani mtawalia ndani wiki kadhaa nyuma, serikali ya Rais Samia Suluhu haikuwa na budi kuidhinisha utekelezaji wa ujenzi wa bwawa la Kidunda. Leo tarehe 11.11.2022 Rais Samia Suluhu ameshuhudia utiaji wa saini wa ujenzi wa mradi wa bwawa kubwa la Kidunda, ambapo saini hiyo ilifuatia na kumkabidhi mkandarasi eneo la mradi tayari kwa kuanza utekelezaji. Wazo la kujenga bwana la Kidunda lilikuwepo tangu baada ya nchi yetu kupata Uhuru mwaka 1961. 1961 chini ya Shirika la Chakula Duniani (FAO) Tanzania ilifanya upembuzi yakinifu ya ujenzi wa bwawa hilo, 1992 ukafanyika utafiti kwa mara ya pili, utafiti wa tatu ukafanywa Shirika la Maendeleo ya Japan (JICA) mwaka 1994 na 2008 Wizara ya Maji na Umwagiliaji ikafanya nayo upembuzi yakinifu ya ujenzi wa mradi huo mkubwa. Katika nyakati zote hizo, licha ya maazimio mengi kuwekwa bungeni, mradi huo ulikuwa ni kitendawili kigumu kwenye utekelezaji kutokana na ufinyu wa bajeti. Baada ya miaka zaidi ya sitini leo tarehe 11.11.2022 Rais Samia Suluhu anashuhudia utiaji wa saini wa mradi mkubwa wa ujenzi wa bwana la Kidunda. Mradi huu unakwenda kuwa suluhu ya kudumu ya upungufu wa maji katika jiji la Dar es Salaam na mkoa wa Pwani na habari njema zaidi utatekelezwa kwa fedha za ndani. Bwawa la Kidunda litakuwa na uwezo wa kukusanya na kuhifadhi maji mita za ujazo milioni 150, na kisha kutiririsha maji hayo kwenye Mto Ruvu nyakati za uhaba na kupelekea uhakika wa kupatikana maji katika jiji la Dar es Salaam na Pwani ambao hutegemea maji katika Mto Ruvu kwa zaidi ya asilimia 90. Mradi huu utatumia gharama ya shilingi bilioni 329 na utatumia muda wa miaka miwili na miezi sita kukamilika. Mradi huu wa… Read More

  • Wanayoyatamani Watanzania kwenye ziara ya Mheshimiwa Rais Samia nchini China

    Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi ya siku tatu nchini China kuanzia Novemba 2 hadi 4 mwaka huu kufuatia mwaliko wa Rais Xi Jinping suala la uendelezaji wa eneo maalum la kiuchumila Bagamoyo (BSEZ) ni moja ya ajenda atakazozibeba. Mwaliko huo uliokuja siku chache baada ya Rais huyo wa Taifa kubwa la Asia kuchaguliwa kwa muhula wa tatu kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Kikomunisti cha Watu wa China (CCP) unamfanya Rais Samia kuwa mkuu wa nchi wa kwanza kutoka Afrika kuzuru nchi hiyo. Kufuatia mwaliko huo unaolenga kukuza ushirikiano baina ya mataifa haya mawili, baadhi ya Watanzania wameeleza matamanio yao ikiwa ni pamoja na China iombwe kukarabati reli ya TAZARA na kujenga daraja juu ya bahari kutoka Dar es Salaam hadi Zanzibar. “Ni faraja kusikia Rais Samia amepata mwaliko wa Rais Jinping, ningetamani sana pamoja na mambo mengine hili la kuboresha TAZARA na kujenga daraja yame miongoni mwa vitu ambavyo ataviomba,” amesema Profesa Humphrey Moshi. Kwa upande wake Msemaji Mkuu Serikali, Gerson Msigwa amesema miradi inayofanyika na nchi hizi mbili ni mingi na mingine inakuja na kwamba na kwamba itakapokamilika Watanzania watajulishwa. Kwa mujibu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) hadi January 2021 kwa upande wa Tanzania Bara China ilikuwa ina jumla ya miradi 940 iliyozalisha ajira takribani 120,000. Read More

  • Rais Samia aja na suluhu kukamilisha mradi wa maji Same – Mwanga – Korogwe baada ya kukwama kwa zaidi ya miaka 10

    “Katika miradi mirefu, ya siku nyingi, inatengenezwa na kusita, na kusimama, ni Same – Mwanga. Tutakwenda kutafuta fedha tuhakikishe unatekelezwa na mwakani […] wapate maji.” Ni maneno ya matumani aliyoyatoa Rais Samia Suluhu Hassan Juni 2022 akiuelezea mradi wa maji wa Same – Mwanga – Korogwe ambao ulikwama kwa zaidi ya miaka 10, na kuyeyusha matumaini ya wananchi zaidi ya nusu milioni kupata maji safi, salama na ya uhakika. Alipoingia madarakani Machi 2021, Rais alikuta mradi huo wa bilioni 262 wenye uwezo wa kuzalisha maji lita milioni 65 kutoka katika Bwawa la Nyumba ya Mungu ukikabiliwa na changamoto za kisheria na kifedha, akafanikisha kutatuliwa kwa changamoto za kisheria na kuingiza TZS bilioni 36 ili mradi ukamilike wananchi wapate maji safi na salama. Kwa sasa, wakazi wa maeneno hayo wana matumaini ya kupata maji mapema mwaka 2023 ambapo hadi Aprili 2022 utekelezaji ulikuwa umefikia asilimia 70.4. Kutokana na changamoto za kisheria, Serikali ilivunja mkataba na wakandarasi M.A Kharafi & Sons na kampuni ya Badr East Africa Enterprises kwa makosa ya kugushi nyaraka muhimu za kimkataba pamoja na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, kisha mradi huo ukakabidhiwa kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA). Read More

  • Rais amesikia, ametekeleza: Watumishi 14,500 walioondolewa kwa vyeti feki kurejeshewa mafao yao

    Rais Samia Suluhu Hassan ameutafsiri kwa vitendo msemo ‘Haki haipaswi tu kutendeka, ni lazima ionekane inatendeka,’ baada ya kuridhia kurejeshwa michango ya watumishi 14,516 waliobainika kuwa na vyeti vya kughushi na waliondolewa kwenye utumishi wa umma. Ridhaa hiyo ya Rais inamaanisha kuwa Serikali itatoa TZS bilioni 46.8 ambazo zitarejeshwa kwa watumishi hao walioondolewa kazini kati ya mwaka 2016 na 2017 katika zoezi la uhakiki wa watumishi wa umma. Fedha hizo ni makato ya asilimia 5 ambayo watumishi hao walikatwa kwa muda waliofanya kazi. Kurejeshwa kwa fedha hizo kunadhihirisha azma ya Rais Samia kuona haki ikitendeka kwa Watanzania wote na kwa wakati wote. Ikiwa ni miaka 5 imepita tangu watumishi hao walipoondolewa kwenye utumishi wa umma, kwa muda wote wamekuwa wakiiomba Serikali kufanya hivyo, huku wabunge na vyama vya wafanyakazi pia vikishinikiza hilo, hivyo uamuzi wa kutekeleza ombi hilo kunaonesha namna Rais alivyomsikivu na anayafanyia kazi maoni na mapendekezo ya Watanzania. Wanufaika wote hao ambao waliondolewa kazini bila kujiandaa hivyo kukumbana na changamoto mbalimbali za kimaisha, sasa wataweza kutumia fedha hizo kuboresha maisha yaona kujiendeleza kiuchumi. Baadhi ya waliohojiwa na vyombo vya habari wamesema kwamba hawaamini hilo limefanyika huku wakielekeza shukrani zao kwa Rais Samia kwa kuwezesha jambo hilo ambalo lilikwama kwa muda mrefu, na kwamba tayari walikuwa wamekata tamaa kuwa hatitofanyika tena. Read More

  • Namna 5 ambazo umeme wa gridi ya Taifa unaubadili mkoa wa Kigoma

    Oktoba 17 mwaka huu ilikuwa siku ya historia kwa Tanzania, hasa mkoa wa Kigoma baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzima jenereta la kuzalisha umeme la Kasulu na kuwasha umeme wa gridi ya Taifa uliofika mkoani humo kwa mara ya kwanza. Jenereta la Kasulu ambalo lilikuwa likizalisha umeme megawati 3.75 zilizotumika wilayani Kasulu na Buhigwe lakini hazikutosheleza ni moja ya majenereta matano yaliyozimwa mengine yakiwa ni Loliondo, Biharamulo, Kibondo na Ngara. Kuzimwa kwa mtambo wa Kasulu na kuwashwa umeme wa gridi ya Taifa kutabadilisha kabisa hadithi ya mkoa wa Kigoma pamoja na maisha ya wakazi wa mkoa huo kwa namna tofauti pamoja na uendeshaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). 1. Kutaipunguzia TANESCO mzigo wa kuendesha mitambo hiyo ambapo kwa mwaka kwa mkoa wa Kigoma ilikuwa ikizalisha umeme kwa gharama ya TZS bilioni 52 huku ikikusanya TZS bilioni 14 tu, hivyo kupelekea kutenga zaidi ya TZS bilioni 38 kila mwaka ili kuhakikisha wananchi wa Kigoma wanapata nishati hiyo muhimu. Uwepo wa umeme wa gridi utaiwezesha Serikali kuelekeza fedha hizo kwenye shughuli nyingine za kimaendeleo na kijamii kama vile shule, afya, maji na miundombinu. 2. Uhitaji wa umeme kwa sasa katika mkoa wa ni megawati 14, lakini umeme uliopelekwa ni megawati 20, hivyo kuufanya kuwa na ziada, huku miradi mingine ya kuongeza umeme ikiendelea. Umeme wa uhakika utavutia wawekezaji hasa wa viwanda vikubwa kuwekeza mkoani humo katika viwanda vya kuchakata mawese na samaki, ambapo awali ingekuwa vigumu kutokana na kutokuwepo umeme wa kutosheleza. 3. Viwanda vikubwa na vidogo vitakavyoanzishwa kwa uwepo wa umeme vitawezesha wakazi wa mkoa huo, hasa vijana na wanawake kupata ajira za moja kwa moja au zisizo za moja kwa moja zitalazobadili maisha yao, na kuchangia ukuaji wa mkoa na Taifa. 4. Kukosekana kwa umeme wa uhakika kuliathiri hali ya maisha ya wakazi wa mkoa huo kutokana na… Read More

  • Benki ya Dunia yataja miujiza mitano uchumi wa Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu

    Benki ya Dunia (WB) imeipongeza Tanzania kwa usimamizi mzuri wa uchumi hali inayoonekana kama miujiza wakati huu ambapo chumi za nchi mbalimbali duniani zinadorora kutokana na athari za janga la UVIKO19, vita ya Urusi na Ukraine, kupanda kwa bei ya mafuta na mabadiliko ya tabianchi. Akitoa pongezi hizo, Makamu Rais wa Benki ya Dunia wa Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Victoria Kwaka amesema kuwa wakati nchi mbalimbali zikihangaika na janga la mfumuko wa bei wa tarakimu mbili, huku akiitaja Ghana kuwa na mfumuko wa bei wa 30%, Tanzania imeweza kuwa na mfumuko wa bei wa tarakimu moja tu, ambapo kwa Septemba ulikuwa 4.8%. Athari za kuwa na mfumuko mkubwa wa bei ni kuwa kunapandisha bei za bidhaa, kunapunguza uwezo wa kufanya manunuzi, hivyo kuathiri hali ya maisha ya wananchi. “Tumeona karibu nchi nyingi duniani zikiwa na akiba ndogo ya fedha za kigeni, lakini Tanzania imeweza kuwa na akiba ya fedha za kigeni inayotosha kuagiza bidhaa na huduma kutoka nje kwa miezi mitano,” amesema Kwaka. Fedha za kigeni zinaiwezesha serikali kutimiza mahitaji yake ya fedha za kigeni na mahitaji ya kuagiza bidhaa kutoka nje, kutoa imani kwamba serikali inaweza ikatimiza majukumu yake ya muda mfupi kulipa madeni ya nje na kusaidia utekelezaji wa sera za fedha na kubadilisha fedha za kigeni, pamoja na uwezo wa kuingilia kuhakikisha fedha ya taifa ni imara. Kuhusu nakisi ya bajeti amesema mataifa mataifa mengi yakihangaika kwa kuwa na nakisi kubwa ya bajeti, Tanzania ina nakisi ndogo ya 3.5% ya Pato la Taifa. Nakisi ndogo ya bajeti kwanza ni ishara nzuri kuwa uchumi wa Taifa unaimarika na ina maana kuwa nchi itahitaji kukopa kiasi kidogo cha fedha au kutokuweka kodi kubwa ili kupata fedha za kufadhili bajeti yake. Kwaka pia ameipongeza Tanzania kwa kuwa na sera nzuri za fedha na uchumi zinazoleta utulivu kwenye… Read More

  • Historia, Rais Samia akizima majenereta na kuwasha umeme wa gridi ya Taifa Kigoma

    Rais Samia Suluhu Hassan leo Oktoba 17, 2022 kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi amewasha umeme wa Gridi ya Taifa katika Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma na kuzima mitambo mitatu ya mafuta yenye iliyokuwa ikizalisha umeme megawati 3.75 zilizotumika Wilaya ya Kasulu na Buhigwe. Uzimaji wa majenereta wilayani Kasulu ni mwendelezo wa uzimaji majenerata katika maeneo mbalimbali baada ya umeme wa gridi ya Taifa, ambapo maeneo mengine ni Kibondo, Loliondo, Ngara na Biharamulo. Kwa kuendesha majenereta kwa mkoa wa Kigoma pekee, Serikali ilikuwa ikipata hasara ya TZS bilioni 36 kila mwaka, kwani gharama za uendeshaji majenereta ilikuwa TZS bilioni 52 huku mapato yakiwa TZS bilioni 14. Mbali na kuondoa hasara hiyo umeme wa gridi ya Taifa utawezesha wakazi wa Kigoma kupata umeme wa kutosha ambapo uhitaji ni megawati 14, na Serikali imepeka megawati 20. Aidha, umeme utachochea shughuli za kiuchumi na uwekezaji katika sekta za biashara, viwanda, madini na kilimo, hivyo kuongeza mapato ya wananchi na Taifa. Pia, umeme utaimarisha shughuli za ulinzi na usalama na utoaji huduma zakijamii kwa wananchi na kuchochea ukuaji wa sekta nyingine. Read More

  • #MamaYukoKazini: Asilimia 79 ya vikwanzo vya biashara kati ya Kenya Tanzania vyatatuliwa

    Mauzo ya Tanzania nchini Kenya mwaka 2021 yalikua kwa asilimia 42 kutoka TZS bilioni 537 mwaka 2020 hadi TZS bilioni 929 mwaka 2021, mchango mkubwa ukitokana na kutatuliwa kwa vikwazo vya kibiashara. Kwa mujibu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) katika kipindi tajwa, Tanzania ilishuhudia ongezeko la usafirishaji wa chai, mahindi, ngano, alizeti, mchele, maharagwe, mbogamboga, karatasi, bidhaa za chuma, marumaru, saruji, vioo na bidhaa za vioo, sabuni na vipodozi kwenda Kenya. Akizungumza leo wakati wa ziara ya Rais wa Kenya, Dkt. William Ruto nchini Tanzania, Rais Samia Suluhu amesema kwamba wataalamu wa pande zote walibaini uwepo wa vikwazo 68 visivyo vya kikodi, ambapo vikwazo 54 vimetatuliwa na 14 bado havijatatuliwa ambapo wametumia jukwaa kueleza kuwa wamedhamiria kutatua vikwazo vilivyobaki, ili wananchi wa pande zote ambao wana uhusiano wa kindugu, kihistoria na kijiografia wanafanya biashara kwa uhuru kwani kukua kwa biashara kunanufaisha pande zote. “Tumekubaliana ya kwamba mawaziri wakutane, maafisa wengine wakutane, tuyakamilishe, tuyaondoe ili biashara iweze kukua zaidi kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania na Kenya tukiwa sote ni watu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,” amesema Rais Ruto. Aidha, amesema “wakati wewe [Rais Samia] na Rais Uhuru Kenyatta mlipokuwa mnafanyia kazi vikwazo hivi, watu walidhani Kenya itanufaika zaidi kuliko Tanzania, lakini Tanzania imenufaika zaidi Kenya. Kwa kuangazia takwimu za biashara, Kenya ni mshirika mkubwa wa kibiashara na utalii kwa Tanzania, na hiyo huenda imechangia Tanzania kuwa nchi ya kwanza Afrika Mashariki ambayo Rais Ruto amefanya ziara ya kikazi tangu alipoapishwa Septemba 13 mwaka huu. Read More

  • Rais Samia aidhinisha bilioni 160 kujenga madarasa 8,000

    Jumla ya wanafunzi 1,384,340 wamefanya mtihani wa kuhitimu darasa la saba mwaka huu ikiwa ni ongezeko la asilimia 22 ikilinganishwa na mwaka 2021. Wanafunzi wao ni zao la kwanza mpango wa elimu bila ada ulioanza mwaka 2016, ulioshuhudia idadi kubwa ya watoto wakiandikishwa darasa la kwanza. Rais Samia Suluhu Hassan ameidhinisha TZS bilioni 160 ambazo zitatumika kujenga madarasa 8,000 kwenye shule za sekondari 2,439 zilizoainishwa kuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa nchini. Madarasa hayo yatakuwa na uwezo wa kupokea wanafunzi 400,000 ambao ni sehemu ya wanafunzi 1,148,512 wanaotarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2023. Idadi ya wanafunzi wanaobaki watatumia vyumba vya madarasa vilivyoachwa na wanafunzi 422,403 waliohitimu kidato cha nne mwaka huu, pamoja na madarasa katika shule mpya za kata 231 zilizojengwa. Katika salamu za heri kwa watahiniwa hao Rais amewaahidi kuwa “Serikali itahakikisha maandalizi ya miundombinu ya kuwapokea wote watakaoendelea na kidato cha kwanza mwakani 2023 inakamilika.” Mwaka 2021 aliweka historia kwa kuwezesha wanafunzi wote waliofaulu kidato cha kwanza kuanza masomo kwa wakati mmoja baada ya kufanikisha ujenzi wa vyumba vya madarasa 15,000, hivyo kuweka mazingira rafiki ya ufundishaji na watoto wote kupata muda sawa masomo. Kwa hatua hii, Rais Samia anatekeleza matakwa ya ibara ya 11(3) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoitaka Serikali kufanya jitihada kuhakikisha kwamba watu wote wanapata fursa sawa na za kutosha kuwawezesha kupata elimu na mafunzo ya ufundi katika ngazi zote za shule na vyuo vinginevyo vya mafunzo. Read More

  • Orodha ya vigezo vya udahili kwa wanufaika wa Samia Scholarship

    Wanafunzi 640 wanatarajiwa kunufaika na mpango wa ufadhili wa masomo ya chuo kikuu, Samia Scholarship, utakaoanza mwaka wa masomo 2022/23 kwa kutoa ufadhili wa asilimia 100 kwa wanafunzi wenye ufaulu wa juu katika masomo ya sayansi na hisabati kwenye mtihani wa kidato cha sita. Licha ya kuwa wanafunzi 640 (wavulana 396 na wasichana 244) wamekidhi kigezo cha ufaulu cha kupata ufadhili, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeainisha vigezo vingine vitakavyozingatiwa ambavyo ni; 1. Lazima awe Mtanzania 2. Awe amefaulu ufaulu wa juu katika mtihani wa kidato cha sita kwa mwaka 2022 iliyoendeshwa na NECTA katika tahasusi za sayansi (PCB, PCM, PGM, CBG, CBA, PMC na CBN). 3. Mwombaji awe amepata udahili kusoma fani ya teknolojia, hisabati, uhandisi na elimutiba katika chuo kikuu kinachotambuliwa na Serikali hapa nchini. 4. Aombe ufadhili kwa usahihi kwa njia iliyoelekezwa. Mpango huu utakuwa na manufaa mbalimbali ambayo ni; 1. Kuchochea ari ya wanafunzi kupenda na kusoma masomo ya sayansi 2. Kutoa ahueni kubwa wazazi ambao pengine wangelazimika kuuza mali zao ili kumudu gharama za kusomesha watoto fani za sayansi. 3. Kukuza sekta ya sayansi na teknolojia nchini ili kunufaika zaidi na mapinduzi ya nne ya viwanda. 4. Kuongeza idadi ya wasichana/wanawake kwenye fani za sayansi ambao wamebaki nyuma kutokana na mifumo na imani potofu za jamii. Ufadhili huo ambao utazingatia vigezo vya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) utagharamia maeneo yafuatayo; Ada ya mafunzo, posho ya chakula na malazi, posho ya vitabu na viandikwa, mahitaji maalum ya vitivo, mafunzo kwa vitendo, tafiti, vifaa saidizi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum na bima ya afya. Wanafunzi watakaofadhiliwa watagharamiwa kwa miaka mitatu hadi mitano kulingana kila mmoja programu aliyodahiliwa, na atatakiwa kuwa na ufaulu usiopungua GPA ya 3.8 katika mwaka wa masomo ili kukidhi kigezo cha kuendelea na ufadhili. Read More