• Benki ya Dunia yataja miujiza mitano uchumi wa Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu

    Benki ya Dunia (WB) imeipongeza Tanzania kwa usimamizi mzuri wa uchumi hali inayoonekana kama miujiza wakati huu ambapo chumi za nchi mbalimbali duniani zinadorora kutokana na athari za janga la UVIKO19, vita ya Urusi na Ukraine, kupanda kwa bei ya mafuta na mabadiliko ya tabianchi. Akitoa pongezi hizo, Makamu Rais wa Benki ya Dunia wa Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Victoria Kwaka amesema kuwa wakati nchi mbalimbali zikihangaika na janga la mfumuko wa bei wa tarakimu mbili, huku akiitaja Ghana kuwa na mfumuko wa bei wa 30%, Tanzania imeweza kuwa na mfumuko wa bei wa tarakimu moja tu, ambapo kwa Septemba ulikuwa 4.8%. Athari za kuwa na mfumuko mkubwa wa bei ni kuwa kunapandisha bei za bidhaa, kunapunguza uwezo wa kufanya manunuzi, hivyo kuathiri hali ya maisha ya wananchi. “Tumeona karibu nchi nyingi duniani zikiwa na akiba ndogo ya fedha za kigeni, lakini Tanzania imeweza kuwa na akiba ya fedha za kigeni inayotosha kuagiza bidhaa na huduma kutoka nje kwa miezi mitano,” amesema Kwaka. Fedha za kigeni zinaiwezesha serikali kutimiza mahitaji yake ya fedha za kigeni na mahitaji ya kuagiza bidhaa kutoka nje, kutoa imani kwamba serikali inaweza ikatimiza majukumu yake ya muda mfupi kulipa madeni ya nje na kusaidia utekelezaji wa sera za fedha na kubadilisha fedha za kigeni, pamoja na uwezo wa kuingilia kuhakikisha fedha ya taifa ni imara. Kuhusu nakisi ya bajeti amesema mataifa mataifa mengi yakihangaika kwa kuwa na nakisi kubwa ya bajeti, Tanzania ina nakisi ndogo ya 3.5% ya Pato la Taifa. Nakisi ndogo ya bajeti kwanza ni ishara nzuri kuwa uchumi wa Taifa unaimarika na ina maana kuwa nchi itahitaji kukopa kiasi kidogo cha fedha au kutokuweka kodi kubwa ili kupata fedha za kufadhili bajeti yake. Kwaka pia ameipongeza Tanzania kwa kuwa na sera nzuri za fedha na uchumi zinazoleta utulivu kwenye… Read More

  • Historia, Rais Samia akizima majenereta na kuwasha umeme wa gridi ya Taifa Kigoma

    Rais Samia Suluhu Hassan leo Oktoba 17, 2022 kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi amewasha umeme wa Gridi ya Taifa katika Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma na kuzima mitambo mitatu ya mafuta yenye iliyokuwa ikizalisha umeme megawati 3.75 zilizotumika Wilaya ya Kasulu na Buhigwe. Uzimaji wa majenereta wilayani Kasulu ni mwendelezo wa uzimaji majenerata katika maeneo mbalimbali baada ya umeme wa gridi ya Taifa, ambapo maeneo mengine ni Kibondo, Loliondo, Ngara na Biharamulo. Kwa kuendesha majenereta kwa mkoa wa Kigoma pekee, Serikali ilikuwa ikipata hasara ya TZS bilioni 36 kila mwaka, kwani gharama za uendeshaji majenereta ilikuwa TZS bilioni 52 huku mapato yakiwa TZS bilioni 14. Mbali na kuondoa hasara hiyo umeme wa gridi ya Taifa utawezesha wakazi wa Kigoma kupata umeme wa kutosha ambapo uhitaji ni megawati 14, na Serikali imepeka megawati 20. Aidha, umeme utachochea shughuli za kiuchumi na uwekezaji katika sekta za biashara, viwanda, madini na kilimo, hivyo kuongeza mapato ya wananchi na Taifa. Pia, umeme utaimarisha shughuli za ulinzi na usalama na utoaji huduma zakijamii kwa wananchi na kuchochea ukuaji wa sekta nyingine. Read More

  • #MamaYukoKazini: Asilimia 79 ya vikwanzo vya biashara kati ya Kenya Tanzania vyatatuliwa

    Mauzo ya Tanzania nchini Kenya mwaka 2021 yalikua kwa asilimia 42 kutoka TZS bilioni 537 mwaka 2020 hadi TZS bilioni 929 mwaka 2021, mchango mkubwa ukitokana na kutatuliwa kwa vikwazo vya kibiashara. Kwa mujibu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) katika kipindi tajwa, Tanzania ilishuhudia ongezeko la usafirishaji wa chai, mahindi, ngano, alizeti, mchele, maharagwe, mbogamboga, karatasi, bidhaa za chuma, marumaru, saruji, vioo na bidhaa za vioo, sabuni na vipodozi kwenda Kenya. Akizungumza leo wakati wa ziara ya Rais wa Kenya, Dkt. William Ruto nchini Tanzania, Rais Samia Suluhu amesema kwamba wataalamu wa pande zote walibaini uwepo wa vikwazo 68 visivyo vya kikodi, ambapo vikwazo 54 vimetatuliwa na 14 bado havijatatuliwa ambapo wametumia jukwaa kueleza kuwa wamedhamiria kutatua vikwazo vilivyobaki, ili wananchi wa pande zote ambao wana uhusiano wa kindugu, kihistoria na kijiografia wanafanya biashara kwa uhuru kwani kukua kwa biashara kunanufaisha pande zote. “Tumekubaliana ya kwamba mawaziri wakutane, maafisa wengine wakutane, tuyakamilishe, tuyaondoe ili biashara iweze kukua zaidi kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania na Kenya tukiwa sote ni watu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,” amesema Rais Ruto. Aidha, amesema “wakati wewe [Rais Samia] na Rais Uhuru Kenyatta mlipokuwa mnafanyia kazi vikwazo hivi, watu walidhani Kenya itanufaika zaidi kuliko Tanzania, lakini Tanzania imenufaika zaidi Kenya. Kwa kuangazia takwimu za biashara, Kenya ni mshirika mkubwa wa kibiashara na utalii kwa Tanzania, na hiyo huenda imechangia Tanzania kuwa nchi ya kwanza Afrika Mashariki ambayo Rais Ruto amefanya ziara ya kikazi tangu alipoapishwa Septemba 13 mwaka huu. Read More

  • Rais Samia aidhinisha bilioni 160 kujenga madarasa 8,000

    Jumla ya wanafunzi 1,384,340 wamefanya mtihani wa kuhitimu darasa la saba mwaka huu ikiwa ni ongezeko la asilimia 22 ikilinganishwa na mwaka 2021. Wanafunzi wao ni zao la kwanza mpango wa elimu bila ada ulioanza mwaka 2016, ulioshuhudia idadi kubwa ya watoto wakiandikishwa darasa la kwanza. Rais Samia Suluhu Hassan ameidhinisha TZS bilioni 160 ambazo zitatumika kujenga madarasa 8,000 kwenye shule za sekondari 2,439 zilizoainishwa kuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa nchini. Madarasa hayo yatakuwa na uwezo wa kupokea wanafunzi 400,000 ambao ni sehemu ya wanafunzi 1,148,512 wanaotarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2023. Idadi ya wanafunzi wanaobaki watatumia vyumba vya madarasa vilivyoachwa na wanafunzi 422,403 waliohitimu kidato cha nne mwaka huu, pamoja na madarasa katika shule mpya za kata 231 zilizojengwa. Katika salamu za heri kwa watahiniwa hao Rais amewaahidi kuwa “Serikali itahakikisha maandalizi ya miundombinu ya kuwapokea wote watakaoendelea na kidato cha kwanza mwakani 2023 inakamilika.” Mwaka 2021 aliweka historia kwa kuwezesha wanafunzi wote waliofaulu kidato cha kwanza kuanza masomo kwa wakati mmoja baada ya kufanikisha ujenzi wa vyumba vya madarasa 15,000, hivyo kuweka mazingira rafiki ya ufundishaji na watoto wote kupata muda sawa masomo. Kwa hatua hii, Rais Samia anatekeleza matakwa ya ibara ya 11(3) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoitaka Serikali kufanya jitihada kuhakikisha kwamba watu wote wanapata fursa sawa na za kutosha kuwawezesha kupata elimu na mafunzo ya ufundi katika ngazi zote za shule na vyuo vinginevyo vya mafunzo. Read More

  • Orodha ya vigezo vya udahili kwa wanufaika wa Samia Scholarship

    Wanafunzi 640 wanatarajiwa kunufaika na mpango wa ufadhili wa masomo ya chuo kikuu, Samia Scholarship, utakaoanza mwaka wa masomo 2022/23 kwa kutoa ufadhili wa asilimia 100 kwa wanafunzi wenye ufaulu wa juu katika masomo ya sayansi na hisabati kwenye mtihani wa kidato cha sita. Licha ya kuwa wanafunzi 640 (wavulana 396 na wasichana 244) wamekidhi kigezo cha ufaulu cha kupata ufadhili, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeainisha vigezo vingine vitakavyozingatiwa ambavyo ni; 1. Lazima awe Mtanzania 2. Awe amefaulu ufaulu wa juu katika mtihani wa kidato cha sita kwa mwaka 2022 iliyoendeshwa na NECTA katika tahasusi za sayansi (PCB, PCM, PGM, CBG, CBA, PMC na CBN). 3. Mwombaji awe amepata udahili kusoma fani ya teknolojia, hisabati, uhandisi na elimutiba katika chuo kikuu kinachotambuliwa na Serikali hapa nchini. 4. Aombe ufadhili kwa usahihi kwa njia iliyoelekezwa. Mpango huu utakuwa na manufaa mbalimbali ambayo ni; 1. Kuchochea ari ya wanafunzi kupenda na kusoma masomo ya sayansi 2. Kutoa ahueni kubwa wazazi ambao pengine wangelazimika kuuza mali zao ili kumudu gharama za kusomesha watoto fani za sayansi. 3. Kukuza sekta ya sayansi na teknolojia nchini ili kunufaika zaidi na mapinduzi ya nne ya viwanda. 4. Kuongeza idadi ya wasichana/wanawake kwenye fani za sayansi ambao wamebaki nyuma kutokana na mifumo na imani potofu za jamii. Ufadhili huo ambao utazingatia vigezo vya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) utagharamia maeneo yafuatayo; Ada ya mafunzo, posho ya chakula na malazi, posho ya vitabu na viandikwa, mahitaji maalum ya vitivo, mafunzo kwa vitendo, tafiti, vifaa saidizi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum na bima ya afya. Wanafunzi watakaofadhiliwa watagharamiwa kwa miaka mitatu hadi mitano kulingana kila mmoja programu aliyodahiliwa, na atatakiwa kuwa na ufaulu usiopungua GPA ya 3.8 katika mwaka wa masomo ili kukidhi kigezo cha kuendelea na ufadhili. Read More

  • Mheshimiwa Rais Samia Suluhu aidhinisha shilingi bilioni 150 kutumika kwa ajili ya ruzuku ya mbolea

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameidhinisha Shilingi za Kitanzania bilioni 150 kwa ajili ya ruzuku ya mbolea. Kufuatia hatua hii, wakulima 956,920 katika maeneo mbalimbali nchini wameanza kunufaika na mbolea ya gharama nafuu.   Hatua hii ni sehemu ya malengo ya kisera ya serikali katika kumpunguzia mkulima gharama na kuongeza uzalishaji.   Kilimo kinachangia takribani asilimia 30 ya pato ghafi la Taifa ikiwa na maana kwamba katika kila shilingi mia moja ya pato ghafi la Taifa walau shilingi 30 inachangiwa na kilimo.   Mbali na hatua hii ya kupunguza bei ya mbolea, Mheshimiwa Rais ameendelea kuwa muumini mkubwa wa mageuzi katika kilimo akiongoza serikali katika kasi ya kuhakikisha pembejeo zinapatikana, ardhi inarasimishwa na uhuru wa mkulima kuuza mazao yake kwa bei ifaanyo. Uamuzi mkubwa pia wa kisera na kibajeti kuleta mapinduzi ya kilimo umefanyika katika Bajeti ya Mwaka huu 2022/23 ambapo Mhe. Rais Samia ongeza bajeti ya kilimo kutoka shilingi bilioni 250 hadi shilingi bilioni 990.   Wanufaika wakubwa katika ruzuku hii ya kwanza ya mbolea ni mikoa ya Mbeya, Iringa, Ruvuma, Rukwa, Arusha na Songwe.   #MamaYukoKazini #KaziInaendelea Read More

  • Dodoma, London, Maputo: Septemba ya Rais Samia na Diplomasia ya Uchumi

    Septemba 17 mwaka huu Rais Samia aliondoka nchini kuelekea Uingereza kuhudhuria mazishi wa Malkia Elizabeth II baada ya kualikwa kama mmoja wa viongozi wa nchi wananchama wa Jumuiya ya Madola. Watu mashuhuri dunianiani takribani 500 walipewa mualiko huo ambao ulizingatia si tu uanachama wa Jumuiya ya Madola lakini pia rekodi ya haki za binadamu kwa kiongozi mwalikwa na nchi anayotoka. Pamoja na mambo na kupata nafasi ya kukutana na viongozi wa mataifa mengine, kuhudhuria mazishi hayo kitendo hicho ni ishara ya uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Uingereza pamoja na jumuiya hiyo ambayo imekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya Tanzania kwa kwa zaidi ya miaka 50 hivi sasa. Kwa mujibu wa takwimu za kituo cha uwekezaji Tanzania, Uingereza ni moja ya wawekezaji wakubwa zaidi Tanzania ikiwa na zaidi ya 30% ya uwekezaji wa Tanzania unaotoka nje (FDI). Mfano kati ya mwaka 1990 hadi 2013 Uingereza iliwekeza Tanzania zaidi ya shilingi Trilioni 8.5 ikizalisha ajira 271,000 kwa Watanzania. Baada ya shughuli hiyo, Rais Samia alielekea nchini Msumbiji kwa  ziara ya kiserikali ya siku tatu ambayo imekuwa na manufaa makubwa kati ya mataifa haya jirani katika kuimarisha ushirikiano wake. Tanzania na Msumbiji zina uhusiano mkubwa wa kihistoria. Nchi hizi zinashea mpaka wa pamoja wa zaidi ya kilometa 800, eneo muhimu katika usalama na uchumi hasa nyakati hizi za ugunduzi wa gesi kwenye mikoa ya kusini mwa nchi yetu.  Mwenendo huu unafanya Msumbiji kuwa mbia muhimu wa Tanzania katika uchumi, ulinzi na usalama. Ili kuimarisha ulinzi na usalama ambao ni muhimu katika maendeleo ya kiuchumi, Tanzania na Msumbiji zilitia saini hati mbili za makubaliano, moja ikiwa ni ushirikiano katika masuala ya ulinzi na ya pili ikiwa Uratibu wa Huduma za Utafutaji na Uokoaji ikikumbukwa kuwa Taifa hilo limekuwa likipambana na magaidi katika jimbo la Cabo Delgado ambalo kwa Tanzania limepakana na… Read More

  • Barua ya wazi ya Rais Samia Suluhu

    Tanzania inatimiza miaka 30 tangu turejee rasmi katika siasa za mfumo wa vyama vingi katika kipindi hicho, Taifa letu limepitia kipindi cha furaha, majonzi, misukusuko na changamoto zote wakati Taifa linapoanza njia mpya. Jambo hili si jepesi, kwa sababu nyakati hizo hazikuwa rahisi duniani kote. Miaka ambayo Tanzania ilirejea katika mfumo huo ilikuwa migumu. Miaka ya mwanzoni ya 1990, ndiyo ilishuhudia changamoto kama vile kuanguka kwa iliyokuwa Urusi, vita vya wenyewe kwa wenyewe Afrika, mauaji ya Kimbari na migogoro mingi ya kisiasa na kiuchumi katika nchi zinazoendelea kama yetu Lakini Watanzania walipita wakati wote huo, wakiwa wamoja na tumeendeleza utamaduni huo miaka 30 baadaye. Napenda kutumia nafasi hii kuwapongeza wote, na ni matumaini yangu makubwa, kwamba viongozi watakaokuja miaka 50 hadi 100 baadaye wataendelea kuongoza nchi iliyo moja na wananchi wasiobaguana na kupigana, hata kama wanapingana kuhusu namna ya kuendesha nchi yao. Ni vizuri kuzungumza kuhusu nana tulivyoingia katika mfumo huu. Rais Ali Hassan Mwinyi aliunde Tume ya Jaji Francis Nyalali iliykuja na majibu kwamba ni azilimia 20 tu ya Watanzania ndio walitaka mfumo wa vyama vingi. Ni busara ya Mzee Mwinyi na viongozi wenzake wa wakati huo walioamua kusikiliza wachache. Kama wazee wetu wangesubiri mpaka asilimia 80 itake vyama vingi ndiyo tukubali pengine leo tusingekuwa tulipo. Hili ni miongoni mwa mafunzo makubwa kwa wanasiasa wa kizazi changu na watakaokuja baadaye. Kwenye jambo la maslahi ya nchi, maarifa na busara ndiyo muhimu kuliko namba. Kutoka kuwa na chama kimoja cha siasa – Chama Cha Mapinduzi (CCM), sasa tuna vyama vilivyosajiliwa 20. Badala ya kusikia sauti moja. Badala ya kusikia sauti moja na wakati mwingine tukisema “Zidumu Fikra za Mwenyekiti”. Sasa Watanzania wanasikia kuhusu fikra za sauti tofauti. Kwa bahati nzuri, hata Mwenyekiti Mao alipata kusema “acha maua 100 yamee kwa pamoja”. Kipekee kabisa, nitumie nafasi hi kuwapongeza wote waliofanikisha safari… Read More

1 12 13 14