Rais wa Tanzania

  • #ZiaraYaMamaUturuki ni heshima na fursa kwa Tanzania kidiplomasia, kiuchumi na kijamii

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameanza ziara yake rasmi nchini Uturuki kwa mwaliko wa Rais wa nchi hiyo, Mheshimiwa Recep Erdoğan. Ziara hiyo ya kimkakati inatarajiwa kuwa na matokeo chanya kidiplomasia, kiuchumi na kimaendeleo ambapo inafanyika kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 14 (tangu mwaka 2010), na miaka saba tangu ziara ya Rais Erdoğan nchini. Tanzania na Uturuki zina uhusiano wa miaka 61 (tangu mwaka 1963), ambapo Uturuki ilifungua ubalozi wake nchini mwaka 1969, ikaufunga mwaka 1984 na kuufungua tena mwaka 2009, na hivyo kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano na uhusiano baina ya mataifa haya. Malengo makuu matatu ya ziara hiyo ya kimkakati ni kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia uliopo, kufungua fursa mpya za ushirikiano wa kiuchumi, na kuendeleza ushirikiano wa kimaendeleo. Maeneo hayo yanatarajia yatapewa uzito katika mazungumzo atakayofanya na mwenyeji wake, Mheshimiwa Rais Erdoğan. Nchi hizi zina ushirikiano mkubwa kwenye biashara na uwekezaji ambapo Uturuki ni miongoni mwa nchi 20 zenye uchumi mkubwa zaidi duniani imewekeza nchini zaidi ya TZS trilioni 1.3 na kuzalisha ajira zaidi ya 6,700. Kwa upande wa Tanzania, huuza wastani wa bidhaa zenye thamani ya TZS bilioni 41 kila mwaka nchini Uturuki. Mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) unaotekelezwa na kampuni ya Uturuki, Yapi Merkez ni kielelezo kikubwa cha ushirikiano baina ya nchi, na ziara hii inatarajiwa kuwa chachu ya kuongeza kasi ya kutekeleza mradi huo utakaobadili maisha na uchumi wa Tanzania. Aidha, Uturuki ni mshirika mkubwa katika kukuza utalii nchini ambapo safari za ndege za moja kwa moja kwenda Dar es Salaam na Kilimanjaro zimerahisisha usafiri wa watalii, sekta ambayo ina mchango mkubwa katika uchumi wetu. Katika kufanikisha lengo la kufungua fursa mpya za ushirikiano, akiwa nchini Uturuki, Mheshimiwa Rais Samia atashiriki jukwaa la uwekezaji pamoja na kuzungumza na kampuni 15 kubwa zaidi nchini humo na kuwashawishi kuja kuwekeza nchini. Mheshimiwa Rais… Read More

  • Tanzania yaweka historia kununua hisa za kitalu gesi cha Mnazi Bay

    Katika kitabu cha historia na rekodi za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa taifa letu, leo amefungua sura mpya ambapo Tanzania kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa mara ya kwanza limeongeza hisa za umiliki na ushiriki kwenye kitalu cha gesi kwa kununua hisa asilimia 20 kati ya hisa asilimia 31.94 za kampuni ya WentWorth Resources katika kitalu cha gesi asilia cha Mnazi Bay mkoani Mtwara. Kufuatia hatua hiyo, umiliki wa Tanzania kwenye kitalu hicho umefikia asilimia 40, huku kampuni ya Maurel & Prom Tanzania ikinunua hisa asilimia 11.94, na hivyo kufikisha umiliki wa asilimia 60 wa kitalu hicho, na leo kampuni hizo mbili zimesaini mikataba miwili; wa kwanza wa mauziano ya hisa na wa pili wa uendeshaji wa kitalu cha gesi asilia cha Mnazi Bay Hatua ya Tanzania kuongeza umiliki kwenye kitalu hicho ina manufaa mengi ikiwa ni pamona na kuongeza mapato ya Serikali, kuimarisha usalama wa upatikanaji wa nishati nchini, ikiwafahamika kuwa asilimia 65 ya umeme unaotumika nchini ni wa gesi asilia. Manufaa mengine ni kuepusha kitalu kumilikiwa na kuendeshwa na kampuni moja, pamoja na TPDC kuwa na nguvu katika uendeshaji na uendelezaji za kitalu hicho hatua itakayowajengea uwezo zaidi. Kupitia mkataba mpya, sasa uamuzi wa uendeshaji na uendelezaji wa kitalu utafanywa na wanahisa wote, tofauti na awali ambapo Maurel & Prom ambayo ilikuwa inamiliki asilimia 48.05 ilikuwa ifanya shughuli hizo kwa niaba ya wanahisa wengine. Aidha, TPDC imepata haki ya kupeleka wafanyakazi katika shughuli za uendeshaji na uendelezaji kitalu kwa muda mrefu tofauti na awali ambapo walikuwa wanakwenda kwa muda mfupi tu, hivyo kutawajengea uwezo wataalamu wa ndani. Mageuzi haya ya kihistoria yanayofanyika chini ya Mheshimiwa Rais Samia ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (2020-2025) ambayo imeelekeza Serikali kutekeleza mapinduzi ya kiuchumi kwa maendeleo ya watu ambao ndio wanapaswa kuwa wanufaika wakuu wa… Read More

  • Sera nzuri za uchumi za Rais Samia zaleta neema kwa mabenki

    Sera nzuri za uchumi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimi wa Rais Samia Suluhu Hassan zimeendelea kuleta neema kubwa kwenye sekta ya benki nchini, moja ya uthibitisho huo ukiwa ni namna benki za kibiashara zinavyovunja rekodi ya mapato na faida mwaka. Faida ya benki hizo ni ishara ya usimamizi imara wa sera ya fedha inayopelekea uchumi kuwa tulivu na kuwa moja ya uchumi unaokua kwa kasi zaidi duniani pamoja na kutanuka kwa huduma za kifedha zinazoendelea kuifnya Tanzania kusogea karibu zaidi na lengo la kuwa na huduma za kifedha jumuishi. Taarifa za robo ya nne ya mwaka (Oktoba-Desemba 2023) za mabenki ambazo zimechapishwa Januari 2024 zinaonesha kuwa benki mbili kubwa nchini, CRDB na NMB, zinaendelea kuwa vinara wa sekta ya fedha nchini ambapo NMB imevunja rekodi kwa kupata faida ghafi shilingi bilioni 775. Kutokana na mazingira mazuri ya uchumi nchini tangu Rais Samia aingie madarakani NMB imeongeza kiasi cha mikopo inayotoa kwa asilimia 28, hadi kufikia Shilingi trilioni 7.7 mwaka jana, hatua ambayo imewanufaisha maelfu ya wananchi, huku wengine wakinufaika kwa kuwa mawakala na kupata ajira kutokana na kupanuka kwa shughuli za benki hiyo. Kwa upande wa CRDB imeongeza jumla ya mali (total assets) kufikia shilingi trilioni 13.2, amana za wateja (customer deposits) ziliongezeka hadi kufikia shilingi trilioni 8.8 na mikopo inayotoa imeongezeka hadi kufikia shilingi trilioni 8.8. Benki za biashara zinatarajiwa kuweka rekodi mpya ya faida mwaka huu mpya wa 2024 na kutoa ajira kwa Watanzania wengi zaidi kutokana na mazingira mazuri ya uchumi na uwekezaji chini ya serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Samia. Uamuzi wa Benki Kuu ya Tanzania kuanza kutekeleza Sera ya Fedha kwa kigezo cha riba ya mikopo kwenda benki za kibiashara kunatarajiwa kuinufaisha maradufu Tanzania kwa kuhakikisha ukwasi wa kutosha kwenye shughuli za kiuchumi na kupunguza mfumuko wa bei nchini.… Read More

  • Tanzania kuvutia uwekezaji wa trilioni 2.5 toka Indonesia

    Mwanadiplomasia namba moja wa Tanzania, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu anaendelea kutekeleza kwa vitendo Diplomasia ya Uchumi ambapo sasa Tanzania inakusudia kuvutia uwekezaji wa dola za Kimarekani bilioni 1 (zaidi ya TZS trilioni 2.5) ndani ya miaka michache ijayo, kutoka uwekezaji wa sasa wenye thamani ya TZS bilioni 6.5 ambao umefanyika katika sekta za kilimo, uzalishaji wa viwandani na ujenzi. Ameeleza hayo akifungua Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Indonesia na ambapo ametumia nafasi hiyo kuwaeleza wafanyabiashara na wawekezaji wa Indonesia sababu zinazowafanya kwanini Tanzania ni sehemu nzuri zaidi kuwekeza. Kwanza amesema ni amani na utulivu uliyopo nchini na Serikali inayofuata misingi ya demokrasia na utawala bora, pili ni eneo la kimkakati la Tanzania ambayo imepaka na nchi nane na ni lango kwa nchi sita kupitia anga, barabara, reli na maji. Aidha, amesema Tanzania inatoa uhakika wa soko la bidhaa zao kwa kuwa na idadi ya watu zaidi ya milioni 61, huku pia ikiwa mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) yenye watu milioni 281.5, Jumuiya ya Mendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) yenye watu milioni 390 na Eneo Huru la Biashara Afrika (AfFTA) lenye watu bilioni 1.2. Tatu ni Tanzania kuwa na mazingira mazuri ya biashara na uwekezaji ikiwa ni pamoja na kuridhia sheria na mikataba ya kimataifa inayolinda mitaji na uwekezaji wa kigeni. Nne ni utashi wa kisiasa na nafasi ya Serikali kutambua umuhimu wa sekta binafsi kama injini ya maendeleo ya kiuchumi na kuweka msimamo wa kusaidia biashara na wafanyabiashara kukua. Sababu ya tani ni usimamizi imara wa sera ya fedha na uchumi unaowezesha uchumi kuzidi kukua na kufikia viwango vya kabla ya janga la UVIKO19. Kuthibitisha hilo, ripoti ya Shirika la Kimataifa la Fedha (IMF) imeitaja Tanzania kama moja ya nchi 20 duniani ambazo uchumi wake utakua kwa kasi zaidi mwaka 2024. Katika ziara yake… Read More

  • Mheshimiwa Rais aanzisha mageuzi yatakayoleta ufanisi kwenye mashirika ya umma

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameianzisha safari itakayoshuhudia mageuzi makubwa ya mashirika ya umma, taasisi na wakala za Serikali ikiwa ni utekelezaji wa maono ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere pamoja na kuziwezesha taasisi hizo kujiendesha kwa tija na ufanisi ili kupunguza utegemezo kutoka Serikalini. Mageuzi hayo yametokana na uhalisia kuwa licha ya wingi wa mashirika na wakala hizo (248) ambazo Serikali imewekeza mtaji wa TZS trilioni 73, bado mchango wake kwenye uchumi ni mdogo sana, kwani kwa sasa taasisi hizo zinachangia asilimia 3 tu kwenye bajeti ya Serikali, huku nyingi zikitegemea ruzuku ili kujiendesha. Mheshimiwa Rais ameeleza kuwa maono ya Mwalimu Nyerere kuanzisha mashirika ya umma alitaka yamilikiwe na wananchi wenyewe kupitia hisa na kwamba wananchi washirikishwe kwenye masuala ya mashirika hayo, na hivyo ameagiza hatua zichukuliwe ili kurudi kwenye msingi huo. “Kwa kuwa kwa sasa wapo wananchi wenye uwezo wa kununua hisa, hata kama ni kidogo kidogo, nadhani turejee kwenye mwelekeo huo,” ameagiza. Ili kufikia malengo hayo, Mheshimiwa Rais ameridhia mabadiliko mbalimbali ambayo ni pamoja na kutoa uhuru kwa taasisi kujiendesha katika mambo ya msingi, kufanya maboresho katika taratibu za ajira kwa watumishi wao na katika sheria ya ununuzi wa umma, na kuongeza kusiwepo kwa kuingiliwa kisiasa kwenye utendaji wa taasisi hizi. Pia, Serikali ipo kwenye mchakato wa kutunga sheria itakayobadili hadhi ya Ofisi ya Msajili wa Hazina kuwa Mamlaka ya Uwekezaji wa Umma, na kuangalia uwezekano wa kuanzishwa kwa Mfuko wa Uwekezaji wa Umma ili kuondoa utegemezi kutoka mfuko mkuu wa Serikali. Kutokana na uchunguzi uliobaini uwepo wa taasisi ambazo majukumu yake yanashabihiana au hayana umuhimu kwa sasa na zile ambazo zinalega lega Serikali itaziunganisha au kutatua changamoto zao ziwezeshe kujiendesha kwani mashirika hayo ni muhimu kwa uchumi zikiwa zinatoa asilimia 17 ya ajira zote nchini. Amewatoa hofu watumishi kuwa mabadiliko yatakayofanyika hayataathiri ajira zao… Read More

  • Mageuzi ya Mheshimiwa Rais yanayoongeza ufanisi wa mashirika ya umma

    Katika kutelekeza maelekezo ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha kuwa mashirika na taasisi nyingine za Serikali au zile ambazo Serikali ina hisa nyingi zinajiendesha kwa faida, Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechua ameainisha hatua tano za kimkakati ambazo zitachochea mabadiliko katika ufanisi wa taasisi hizo. Kwanza amesema ni kujenga utamaduni wa kukutana katika kikao kazi kila mwaka na watendaji na wenyeviti wa taasisi hizo. Pili, ni mabadiliko ya sheria ambayo yatahusisha kuondoa sheria zilizopitwa na wakati au zinazokwamisha mashirika kujiendesha kwa ufanisi. Hatua ya tatu ni kuangalia namna ya kuwapata viongozi wa kuendesha taasisi hizo ili kuhakikisha kuwa wanaopewa dhamana ni wenye ujuzi stahiki ambapo Mheshimiwa Rais amewahi kupendekeza kuwa nafasi hizo ziwe zinatangazwa, ili watu wenye sifa watume maombi. Nne ni uboresha wa bodi za taasisi hizo kwa kuangalia namna zinavyoteuliwa ambapo amesema lengo ni kuchagua watu wenye uwezo wa kiutendaji na kukabiliana na changamoto zinazojitokeza. Hatua ya tano ni kutoa uhuru kwa taasisi hizo kuajiri ambapo mchakato huo tayari umeanza na kwa hatua ya kwanza wanaanza na taasisi za kibiashara na vyuo vikuu. Mchechu amesema baada ya hatua hizi, hatua zaidi za kimabadiliko zitachukuliwa ndani ya taasisi moja moja na viongozi husika na kuwa lengo ni kuziwezesha kuwa na ufanisi, kuongeza faida na kutoa gawio serikalini ili kupunguza utegemezi wa ruzuku. Read More

  • Tanzania ni ya mfano Afrika kwa uwekezaji katika rasilimali watu

    Wakuu wa nchi za Afrika, viongozi wa ngazi mbalimbali na wadau wengine wamekusanyika Tanzania kujadili mustakabali wa rasilimali watu barani Afrika ambapo Rais wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu ametumia jukwaa hilo kueleza hatua mbalimbali ambazo Tanzania imezichukua kuimarisha sekta hiyo ambayo ni pamoja na kutenga fedha kwa ajili ya afua mbalimbali za lishe na huduma za afya ya uzazi wa mama na mtoto. Hatua nyingine ni kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya na elimu ili kuondoa udumavu ambao, mara nyingi, hupunguza kiwango cha uelewa na uwezo wa kusoma kwa waoto na kuhakikisha watoto wanaandaliwa kimwili, kiakili, kiisimu/kijinsia kiubunifu na kiakili-hisia. Aidha, Serikali imetoa afua kwa kaya masikini, inatoa elimu bila malipo kuanzia ngazi ya awali hadi kidato cha sita, inapanua elimu ya ufundi na mafunzo ya amali, imefuta ada kwa baadhi ya vyuo vya ufundi, imeanza kutoa mikopo kwa vyuo vya kati, inatoa mikopo kwa vijana, inaruhusu waliokatisha masomo kurejea shule pamoja na kuweka mkakati wa kuvutia vijana kwenye kilimo, yote haya yakilenga kuongeza mchango wao kwenye uchumi. Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022, vijana ndio kundi lenye watu wengi zaidi nchini Tanzania, hivyo hatua ambazo Rais ameeleza kuwa Tanzania imezichukua kwa asilimia kubwa zimewalenga vijana kwani anaamini kwamba maisha bora ambayo vijana wengi hukimbilia Ulaya kuyafuata yanaweza kupatikana barani Afrika endapo Serikali zao zitawawezesha. “Viongozi wenye maono hujenga sera zao kwenye maendeleo ya watu na kufuatiwa na maendeleo ya vitu,” amesema Rais Samia akitoa wito kwa viongozi wenzake wa Afrika na kusisitiza kwamba Afrika haitoweza kuendelea endapo rasilimali watu isipoendelezwa. Read More

  • Rais Samia aimarisha ushiriki wa sekta binafsi kwenye miradi ya maendeleo

    Dhamira za dhati ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ya kukuza sekta binafsi na kuhakikisha inashiriki katika kuchochea maendeleo ya wananchi inazidi kudhihirika kufuatia marekebisho yaliyofanyika kwenye Sheria ya Ubia Baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi wa Mwaka 2023 ili kuondoa changamoto zilizosababisha ushiriki hafifu wa sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa utaratibu wa ubia. Maboresho yaliyofanyika yataongeza kasi ya ushiriki wa sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kupunguza muda wa maandalizi ya miradi na hivyo kuharakisha utekelezaji wa miradi ya PPP, hatua ambazo zitaipunguzia Serikali mzigo wa kibajeti sambamba na kukuza sekta binafsi. Changamoto zilizotatuliwa ni pamoja na sheria kutotoa haki kwa wabia kutoka sekta binafsi kuwasilisha migogoro kwenye mahakama za kimataifa kwa utatuzi, kutoainisha aina ya misaada ya kifedha (public funding) itakayoidhinishwa kupitia Sheria ya Mikopo, Dhamana na Misaada. Nyingine ni sheria kutoruhusu mamlaka za Serikali kufanya ununuzi wa moja kwa moja wa mbia kutoka sekta binafsi kwa ajili ya kutekeleza miradi inayoibuliwa na mamlaka hizo na kutoweka masharti kwa mwekezaji kutoka sekta binafsi aliyeshinda zabuni ya kutekeleza mradi wa PPP kuunda Kampuni. Tayari Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali kwa kushirikiana na sekta binafsi ikiwemo barabara (Expressway) kutoka Kibaha – Chalinze – Morogoro, mradi ambao utaweka historia ya kuwa mradi mkubwa zaidi wa barabara kujengwa kwa kushirikiana na sekta binafsi. Read More

  • Rais Samia anatimiza ndoto ya Tanzania kuwa kitovu cha uwekezaji Afrika Mashariki na Kati

    Hatua ya Bunge la Tanzania kupitisha azimio la kuridhia ushirikiano kati ya Tanzania na Dubai kuhusu ushirikiano wa kiuchumi na kijamii katika uendelezaji na uboreshaji utendaji kazi wa bandari Tanzania ni hatua nyingine kubwa katika mkakati wa Tanzania kuelekea kuwa kitovu cha biashara na uwekezaji Afrika Mashariki na Kati ndani ya muongo mmoja ujao. Kupitishwa kwa azimio hilo kunaipa nafasi Tanzania kupitia Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Dubai kupitia Kampuni ya DP World kuanza majadiliano yanayolenga kuangazia namna ya kushirikiana ili kuongeza ufanisi wa bandari nchini, hasa Bandari ya Dar es Salaam ambayo imekuwa lango la kibiashara kwa nchi za Afrika ya Mashariki, Kati na Kusini wa Afrika. Kufanikiwa kwa ushirikiano baina ya Serikali hizi mbili kutatimiza ndoto ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ya kuongeza mapato ya bandari kutoka TZS trilioni 7.7 za sasa hadi TZS trilioni 26 ndani ya muongo mmoja, ambayo yataweza kufadhili shughuli za kijamii na kimaendeleo nchini, hivyo kupunguza utegemezi kwa washirika wa maendeleo, jambo ambalo ni msingi katika kudhihirisha Uhuru wa nchi kwenye kupanga na kuamua mambo yake. Mafanikio mengine ambayo Tanzania itayapata ni kuongezeka kwa ajira kutoka nafasi 28,990 za sasa hadi ajira 71,907, kupunguza muda wa meli kukaa nangani kutoka siku 5 hadi saa 24, kupunguza muda wa ushushaji makontena kutoka siku 4.5 hadi siku 2, kupunguza muda wa uondoshaji mizigo kutoka saa 12 hadi saa 1, kupunguza gharama ya usafirishaji mizigo kutoka nje ya nchi kwenda nchi jirani kwa asilimia 50, pamoja na kuongeza shehena ya mizigo kutoka tani milioni 18 hadi tani milioni 47. Mbali na manufaa hayo, uendelezaji wa bandari pia utachochea ukuaji wa sekta nyingine kama uvuvi, kilimo, ufugaji, viwanda na biashara, usafirishaji (anga, reli, barabara), kiimarisha diplomasia pamoja na Watanzania kunufaika na teknolojia na ujuzi wa uendeshaji wa bandari kisasa. Ili kuendeleza uwazi na uwajibika, Serikali chini… Read More

  • Mradi wa gesi asilia Lindi kutoa ajira za moja kwa moja 8,000

    Fursa za Watanzania kuendelea kunufaika na rasilimali zao zinaendelea kuongezeka ambapo awamu hii ni mradi kusindika gesi asilimia mkoani Lindi ambao unatajiwa kutoa ajira zaidi ya 8,000 kwa Watanzania pamoja na kuongeza matumizi ya nishati salama majumbani na maeneo mengine, kukuza uchumi na kuchochea ukuaji wa sekta nyingine. Baada ya majadiliano yaliyodumu kwa takribani miaka miwili Tanzania na kampuni za uchimbaji wa mafuta na gesi za Equinor, Shell pamoja na Exxon Mobil zimefikia makubaliano kwa ajili ya uchimbaji wa gesi asilia, mradi ambao utagharimu zaidi ya TZS trilioni 70. Kupitia mradi huo ambao ujenzi wake unatarajiwa kuanza Juni 2025 mbali na ajira hizo za moja kwa moja, Watanzania zaidi watanufaika kwa ajira zisizo za moja kwa moja kwa kutoa huduma za kifedha, chakula na malazi, usafiri na usafirishaji, ulinzi, afya na mawasiliano. Aidha, kuhakikisha Watanzania wananufaika na uwekezaji huo mikataba yote inayoingiwa itapitiwa na kuidhinishwa na Baraza la Mawaziri kama ambavyo Sheria ya Petroli ya mwaka 2015 ambapo mikataba mitano iliyoingiwa ikipitishwa na baraza itasainiwa Juni 2023. Mradi huo utaongeza mapato ya Serikali, Shirika la Maendeleo Tanzania (TPDC) litapata gawio kubwa, pia Watanzania watajengewa uwezo katika sekta ya gesi ikihusisha pia uhamilishaji teknolojia. Read More