Rais Samia Suluhu

  • Mheshimiwa Rais awezesha vijana wajasiriamali kupata mkopo wa bilioni 1.9

    Moja ya ahadi za Chama cha Mapinduzi (CCM) katika ilani ya mwaka 2020-2025 ni kutengeneza ajira zisizopungua milioni 8 katika sekta rasmi na isiyo rasmi kwa ajili ya vijana nchini. Ndani ya muda mfupi Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameendelea kuweka mikakati ya kufikia lengo hilo ambapo anaendelea kutoa ajira rasmi kwenye kada mbalimbali, ameboresha mazingira ya biashara yanayowezesha vijana kujiajiri na kupata ajira kupitia uwekezaji unaosajiliwa nchini pamoja na kuwezesha upatikanaji wa mitaji na mafunzo ya ujasirimali kwa vijana nchini. Kwa kutambua umuhimu mkubwa wa vijana katika maendeleo ikiwa ndio nguvu kazi kubwa, Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana imetoa mikopo ya TZS bilioni 1.88 kwa ajili ya kuwezesha miradi 85 ya vijana katika sekta za kilimo, viwanda na biashara kwenye halmashauri 28. Aidha, Serikali imetoa fursa za mafunzo ya ujuzi wa kujiajiri au kuajiriwa kwa vijana 118,415 katika fani za uanagenzi, uzoefu wa kazi, ufugaji wa samaki na viumbe maji na kilimo cha kisasa kwa njia ya vizimba. Pamoja na hayo, Serikali imefungua fursa zaidi kupitia kilimo, TEHAMA na pia vijana na wajasiriamali wengine wanaofungua biashara mpya wamepewa neema ya miezi sita hadi mwaka mmoja kutokulipa kodi tangu kuanza kwa biashara zao, mpango unaolenga kulea biashara ndogo ili ziweze kukua zaidi. Read More

  • Benki ya Dunia: Tanzania ni nchi ya mfano katika usimamizi wa uchumi

    Benki ya Dunia imeimwagia sifa Tanzania chini Rais Rais Samia Suluhu Hassan kwa usimamizi mzuri wa uchumi na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayopata fedha kutoka kwenye taasisi hiyo ikilinganishwa na nchi nyingine nyingi za Afrika. Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayesimamia Kundi la Kwanza la nchi za Kanda ya Afrika (Africa Group 1 Constituency), Dkt. Floribert Ngaruk amesema Tanzania ni nchi ya mfano katika usimamizi wa sera za uchumi na fedha ambapo licha ya changamoto za UVIKO-19 na vita inayoendelea baina ya Urusi na Ukraine, tathimini ya benki hiyo inaonesha kuwa uchumi wa Tanzania uko imara ikilinganishwa na nchi nyingine za Afrika. “Tanzania ni nchi ya kupigiwa mfano kwa usimamizi mahiri wa masuala ya uchumi mpana, si tu kwa nchi za Afrika Mashariki, bali kwa nchi za Afrika, ambapo kiwango cha ukuaji uchumi cha wastani wa asilimia 5.4 ni cha juu, na ninawapongeza sana” amesema Dkt. Ngaruko Aidha, amepongeza uhusiano imara uliopo kati ya Tanzania na Benki ya Dunia na kuahidi kuwa benki yake itaendelea kuisaidia Tanzania katika jitihada zake za kukuza uchumi na kuwaondolea umasikini wananchi wake kwa kusaidia fedha zitakazotumika kutekeleza miradi mbalimbali ya kiuchumi na kijamii pamoja na kutoa misaada ya kiufundi. Mpaka sasa Benki ya Dunia imewekeza zaidi ya TZS trilioni 16.7 kwa ajili ya kutekeleza miradi zaidi ya 29 nchini ambapo kati ya miradi hiyo, 24 yenye thamani ya TZS trilioni 15 ni ya kitaifa, na mingine 5 yenye thamani ya TZS trilioni 1.7 ni ya kikanda. Read More

  • Miaka miwili ya Mheshimiwa Rais inavyonufaisha vijana na wanawake kwa mitaji

    Msemo wa Wahenga kuwa Mgaagaa na upwa hali wali mkavu umejirihirisha kwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na manufaa lukuki yanayowafaidisha Watanzania kutokana na safari za nje ya nchi ambapo manufaa hayo awamu hii yanagusa zaidi wanawake na vijana. Ziara zake zimewezesha wafanyabiashara kutoka Ulaya kuja nchini wiki iliyopita ambapo kupitia Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (EIB) walitoa mikopo yenye masharti nafuu ya TZS trilioni 1.4 kwenye benki za CRDB, NBC na KCB ambayo itawanufaisha wajasiriamali, pamoja na TZS bilioni 318 kutoka Benki ya Maendeleo ya Ujasiriamali ya Uholanzi (FMO) na Taasisi ya Ufaransa ya Kufadhili Maendeleo (PROPARCO). Nusu ya fedha za EIB, TZS bilioni 700 zitatumika kukuza biashara za wajasiriamali ambapo TZS bilioni 421 zitaelekezwa kufanikisha miradi na biashara zinazoendeshwa na kusimamiwa na wanawake na TZS bilioni 248 zitatumika kwenye miradi iliyopo kwenye uchumi wa bahari. Kupitia mikopo hiyo, benki za ndani zitakuwa na uwezo wa kutoa mikopo kwa wanawake na wajasiriamali wengi zaidi ambao changamoto ya mitaji imekuwa kubwa kwao. Tukio hili moja ni ushuhuda namna kila safari ambayo Mheshimiwa Rais anafanya nje ya nchi imeleta fursa zaidi za kibiashara na kuvutia wawekezaji nchini. Read More

  • Miaka Miwili: Mageuzi (Reforms) ya Mheshimiwa Rais Samia yanavyoimarisha biashara nchini

    Ikiwa mageuzi (reforms) ni moja ya nguzo nne (4Rs) za uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, ndani ya kipindi kifupi amefanya mageuzi makubwa kwa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji, hatua ambayo imefufua biashara na kuvutia uwekezaji ndani na nje ya nchi. Mageuzi hayo yaliyofanyika, Rais amelenga kuimarisha taasisi na kuhakikisha sera, sheria, na kanuni zinazosimamia biashara na uwekezaji zinatabirika, lakini pia zinachochea uwazi, zinaondoa ukiritimba na changamoto nyingine ambazo zimekuwa zikikwamisha ustawi wa biashara nchini. Mafanikio makubwa yamepatikana katika mageuzi hayo ambayo ni pamoja na kufuta kodi na tozo zaidi ya 230 ambazo ziliathiri ukuaji wa biashara. Aidha, Tanzania imeimarisha ushirikiano na mataifa mengine katika masuala ya kikodi ambapo tayari imetia saini makubaliano na nchi 10 kuondoa utoaji kodi mara mbili na kuzuia ukwepaji kodi, moja ya nchi hizo ni Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE). Zaidi ya hapo mageuzi yamefanyika katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji na usimamizi wa mapato ikiwa ni pamoja na kuhakikisha shughuli za ukadiriaji kodi zinafanyika kwa haki, kuhakiksha ritani za kodi zinafanyika kwa wakati, kutumia mifumo ya kodi ya kidijitali ikiwa ni pamoja na dirisha la mtandaoni linalowawezesha wateja kujihudumia na dirisha la pamoja la kielektroniki linalorahisisha ufanyaji wa miamala. Pia, Serikali imefanya mabadiliko Sheria ya Rufaa za Kodi, Sura ya 408 na kujumuisha njia mbadala ya usuluhishi wa migogoro na hivyo kupunguza mlolongo mrefu katika kushughulikia rufaa za kikodi. Katika muktadha huo huo, Rais Samia amefanikisha upatikanaji wa sheria mpya ya uwekezaji (Sheria ya Uwekezaji Tanzania ya Mwaka 2022) ambayo imeiondoa Sheria ya Uwekezaji Tanzania ya Mwaka 1997. Sheria mpya imeweka mazingira bora zaidi ya biashara ikipunguza muda wa kupata leseni kutoka siku 14 za kazi hadi siku 7 za kazi na pia kutoa nafasi usuluhishi wa migogoro kwenye taasisi za kimataifa. Kutokana na ukweli kuwa mazingira ya biashara yatafanikiwa kukiwa na… Read More

  • Historia nyingine chini ya Mheshimiwa Rais Samia, faida ya benki yavunja rekodi ikivuka trilioni 1

    Faida ya benki za kibiashara nchini imeongezeka kwa TZS bilioni 400 mwaka 2022 na kuvuka ukomo wa shilingi trilioni moja kwa mara ya kwanza katika historia ya sekta ya fedha nchini Tanzania. Kwa mujibu wa taarifa za benki ambazo zimetoa taarifa zao za fedha hadi Januari 30 mwaka huu, zinaonesha kuwa zaidi ta TZS trilioni 1.164 zilikusanywa kama faida (net profit) ikiwa ni ongezeko kutoka TZS bilioni 740 zilizokusanywa mwaka 2021. Ongezeko hilo la faida ambalo limeambatana na kupungua kwa mikopo chechefu, kuongezeka kwa kiwango cha fedha kinachowekwa na wateja wa benki pamoja na mikopo kwa wateja kumetokana kuimarika kwa mazingira mazuri ya biashara nchini chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan. Benki hizo zimesema kuwa ongezeko hilo la faida ni ishara kuwa ajenda ya Serikali ya kukuza biashara inafanya vizuri ambayo inatokana na usimamizi mzuri ikiwemo wa kisera ambazo zinatoa nafasi kwa sekta binafsi kukua. Ukuaji huo unatarajiwa kuwa na matokeo chanya kwa wananchi kwani unaongeza uwezo wa benki kupanua huduma za kifedha kuwafikia wananchi wengi zaidi lakini pia kuongeza kiwango cha mikopo kwenda sekta binafsi ambayo ina mchango mkubwa kwa maendeleo na kuzalisha ajira. Read More

  • Mheshimiwa Rais Samia alivyotoa ahueni kwa wananchi kupitia ruzuku ya mafuta

    Ruzuku ya Serikali kwenye mafuta iliyoanza kutolewa na Rais Samia Suluhu Hassan imetoa ahueni kubwa kwa wananchi kutokana na bei ya mafuta kuendelea kupungua katika soko la ndani. Takwimu zinaonesha kuwa bei ya petroli kwa kipindi hicho imepungua kwa wastani wa asilimia 14 kwa petroli iliyoingizwa nchini kupitia bandari za Dar es Salaam, Tanga na Mtwara. Kuanzia Agosti hadi Januari 2023 bei ya petroli iliyopokelewa Bandari ya Dar es Salaam baada ya ruzuku imepungua kutoka TZS 3,410 hadi TZS 2,819. Wakati huo huo, bei ya petroli kupitia bandari ya Tanga imeshuka kutoka TZS 3,435 hadi TZS 2,989, huku petroli iliyopita Bandari ya Mtwara ikishuka kutoka TZS 3,393 hadi TZS 2,993. Kuendelea kushuka kwa bei ya mafuta nchini ni matokeo ya hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ili kumpa kila mwananchi nafuu ya maisha. Ruzuku ya TZS 100 bilioni ilianza kutumika kuanzia Juni 1, 2022 ambapo wadau na wananchi wamekiri kwamba imekuwa ahueni kubwa kwao, hasa ikilinganishwa na nchi nyingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo Tanzania ndio ina bei ndogo zaidi ya petroli. Read More

  • BWAWA LA KIDUNDA: RAIS SAMIA ATEGUA KITENDAWILI KILICHOSHINDIKANA TANGIA UHURU

    Waswahili wana msemo wao usemao “Lisilo budi hutendwa”, kwa kadhia ya upatikanaji wa maji waliyoipata wakaazi wa mkoa wa Dar es Salaam na mkoa wa Pwani mtawalia ndani wiki kadhaa nyuma, serikali ya Rais Samia Suluhu haikuwa na budi kuidhinisha utekelezaji wa ujenzi wa bwawa la Kidunda. Leo tarehe 11.11.2022 Rais Samia Suluhu ameshuhudia utiaji wa saini wa ujenzi wa mradi wa bwawa kubwa la Kidunda, ambapo saini hiyo ilifuatia na kumkabidhi mkandarasi eneo la mradi tayari kwa kuanza utekelezaji. Wazo la kujenga bwana la Kidunda lilikuwepo tangu baada ya nchi yetu kupata Uhuru mwaka 1961. 1961 chini ya Shirika la Chakula Duniani (FAO) Tanzania ilifanya upembuzi yakinifu ya ujenzi wa bwawa hilo, 1992 ukafanyika utafiti kwa mara ya pili, utafiti wa tatu ukafanywa Shirika la Maendeleo ya Japan (JICA) mwaka 1994 na 2008 Wizara ya Maji na Umwagiliaji ikafanya nayo upembuzi yakinifu ya ujenzi wa mradi huo mkubwa. Katika nyakati zote hizo, licha ya maazimio mengi kuwekwa bungeni, mradi huo ulikuwa ni kitendawili kigumu kwenye utekelezaji kutokana na ufinyu wa bajeti. Baada ya miaka zaidi ya sitini leo tarehe 11.11.2022 Rais Samia Suluhu anashuhudia utiaji wa saini wa mradi mkubwa wa ujenzi wa bwana la Kidunda. Mradi huu unakwenda kuwa suluhu ya kudumu ya upungufu wa maji katika jiji la Dar es Salaam na mkoa wa Pwani na habari njema zaidi utatekelezwa kwa fedha za ndani. Bwawa la Kidunda litakuwa na uwezo wa kukusanya na kuhifadhi maji mita za ujazo milioni 150, na kisha kutiririsha maji hayo kwenye Mto Ruvu nyakati za uhaba na kupelekea uhakika wa kupatikana maji katika jiji la Dar es Salaam na Pwani ambao hutegemea maji katika Mto Ruvu kwa zaidi ya asilimia 90. Mradi huu utatumia gharama ya shilingi bilioni 329 na utatumia muda wa miaka miwili na miezi sita kukamilika. Mradi huu wa… Read More

  • Rais Samia aja na suluhu kukamilisha mradi wa maji Same – Mwanga – Korogwe baada ya kukwama kwa zaidi ya miaka 10

    “Katika miradi mirefu, ya siku nyingi, inatengenezwa na kusita, na kusimama, ni Same – Mwanga. Tutakwenda kutafuta fedha tuhakikishe unatekelezwa na mwakani […] wapate maji.” Ni maneno ya matumani aliyoyatoa Rais Samia Suluhu Hassan Juni 2022 akiuelezea mradi wa maji wa Same – Mwanga – Korogwe ambao ulikwama kwa zaidi ya miaka 10, na kuyeyusha matumaini ya wananchi zaidi ya nusu milioni kupata maji safi, salama na ya uhakika. Alipoingia madarakani Machi 2021, Rais alikuta mradi huo wa bilioni 262 wenye uwezo wa kuzalisha maji lita milioni 65 kutoka katika Bwawa la Nyumba ya Mungu ukikabiliwa na changamoto za kisheria na kifedha, akafanikisha kutatuliwa kwa changamoto za kisheria na kuingiza TZS bilioni 36 ili mradi ukamilike wananchi wapate maji safi na salama. Kwa sasa, wakazi wa maeneno hayo wana matumaini ya kupata maji mapema mwaka 2023 ambapo hadi Aprili 2022 utekelezaji ulikuwa umefikia asilimia 70.4. Kutokana na changamoto za kisheria, Serikali ilivunja mkataba na wakandarasi M.A Kharafi & Sons na kampuni ya Badr East Africa Enterprises kwa makosa ya kugushi nyaraka muhimu za kimkataba pamoja na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, kisha mradi huo ukakabidhiwa kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA). Read More

  • Rais amesikia, ametekeleza: Watumishi 14,500 walioondolewa kwa vyeti feki kurejeshewa mafao yao

    Rais Samia Suluhu Hassan ameutafsiri kwa vitendo msemo ‘Haki haipaswi tu kutendeka, ni lazima ionekane inatendeka,’ baada ya kuridhia kurejeshwa michango ya watumishi 14,516 waliobainika kuwa na vyeti vya kughushi na waliondolewa kwenye utumishi wa umma. Ridhaa hiyo ya Rais inamaanisha kuwa Serikali itatoa TZS bilioni 46.8 ambazo zitarejeshwa kwa watumishi hao walioondolewa kazini kati ya mwaka 2016 na 2017 katika zoezi la uhakiki wa watumishi wa umma. Fedha hizo ni makato ya asilimia 5 ambayo watumishi hao walikatwa kwa muda waliofanya kazi. Kurejeshwa kwa fedha hizo kunadhihirisha azma ya Rais Samia kuona haki ikitendeka kwa Watanzania wote na kwa wakati wote. Ikiwa ni miaka 5 imepita tangu watumishi hao walipoondolewa kwenye utumishi wa umma, kwa muda wote wamekuwa wakiiomba Serikali kufanya hivyo, huku wabunge na vyama vya wafanyakazi pia vikishinikiza hilo, hivyo uamuzi wa kutekeleza ombi hilo kunaonesha namna Rais alivyomsikivu na anayafanyia kazi maoni na mapendekezo ya Watanzania. Wanufaika wote hao ambao waliondolewa kazini bila kujiandaa hivyo kukumbana na changamoto mbalimbali za kimaisha, sasa wataweza kutumia fedha hizo kuboresha maisha yaona kujiendeleza kiuchumi. Baadhi ya waliohojiwa na vyombo vya habari wamesema kwamba hawaamini hilo limefanyika huku wakielekeza shukrani zao kwa Rais Samia kwa kuwezesha jambo hilo ambalo lilikwama kwa muda mrefu, na kwamba tayari walikuwa wamekata tamaa kuwa hatitofanyika tena. Read More

  • Namna 5 ambazo umeme wa gridi ya Taifa unaubadili mkoa wa Kigoma

    Oktoba 17 mwaka huu ilikuwa siku ya historia kwa Tanzania, hasa mkoa wa Kigoma baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzima jenereta la kuzalisha umeme la Kasulu na kuwasha umeme wa gridi ya Taifa uliofika mkoani humo kwa mara ya kwanza. Jenereta la Kasulu ambalo lilikuwa likizalisha umeme megawati 3.75 zilizotumika wilayani Kasulu na Buhigwe lakini hazikutosheleza ni moja ya majenereta matano yaliyozimwa mengine yakiwa ni Loliondo, Biharamulo, Kibondo na Ngara. Kuzimwa kwa mtambo wa Kasulu na kuwashwa umeme wa gridi ya Taifa kutabadilisha kabisa hadithi ya mkoa wa Kigoma pamoja na maisha ya wakazi wa mkoa huo kwa namna tofauti pamoja na uendeshaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). 1. Kutaipunguzia TANESCO mzigo wa kuendesha mitambo hiyo ambapo kwa mwaka kwa mkoa wa Kigoma ilikuwa ikizalisha umeme kwa gharama ya TZS bilioni 52 huku ikikusanya TZS bilioni 14 tu, hivyo kupelekea kutenga zaidi ya TZS bilioni 38 kila mwaka ili kuhakikisha wananchi wa Kigoma wanapata nishati hiyo muhimu. Uwepo wa umeme wa gridi utaiwezesha Serikali kuelekeza fedha hizo kwenye shughuli nyingine za kimaendeleo na kijamii kama vile shule, afya, maji na miundombinu. 2. Uhitaji wa umeme kwa sasa katika mkoa wa ni megawati 14, lakini umeme uliopelekwa ni megawati 20, hivyo kuufanya kuwa na ziada, huku miradi mingine ya kuongeza umeme ikiendelea. Umeme wa uhakika utavutia wawekezaji hasa wa viwanda vikubwa kuwekeza mkoani humo katika viwanda vya kuchakata mawese na samaki, ambapo awali ingekuwa vigumu kutokana na kutokuwepo umeme wa kutosheleza. 3. Viwanda vikubwa na vidogo vitakavyoanzishwa kwa uwepo wa umeme vitawezesha wakazi wa mkoa huo, hasa vijana na wanawake kupata ajira za moja kwa moja au zisizo za moja kwa moja zitalazobadili maisha yao, na kuchangia ukuaji wa mkoa na Taifa. 4. Kukosekana kwa umeme wa uhakika kuliathiri hali ya maisha ya wakazi wa mkoa huo kutokana na… Read More