April 2023

  • Umoja wa Mataifa: Tanzania ya tatu kwa kasi kubwa ya ukuaji wa uchumi Afrika

    Licha ya kuwa ukuaji wa bara la Afrika unatarajiwa kushuka kutoka asilimia 4.1 mwaka 2022 hadi asilimia 3.8 mwaka 2023, uchumi wa Tanzania unatarajiwa kukua zaidi huku Umoja wa Mataifa (UN) ukiitaja kuwa ni nchi ya tatu barani Afrika kwa kuwa na kasi kubwa ya ukuaji wa uchumi mwaka 2023. Tanzania ambayo inaendelea kuwa mfano Afrika kwa mageuzi makubwa ya kiuchumi chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, inatarajiwa kushuhudia ukuaji wa uchumi wa asilimia 5.6, ikitanguliwa na Ivory Coast ambayo uchumi wake utakua kwa asilimia 6.5 pamoja na Rwanda itakayoshuhudia ukuaji wa asilimia 7.8. Mafanikio hayo ni matokeo ya mikakati ya Rais Samia ambapo katika miaka miwili ya uongozi wake amesajili miradi ya uwekezaji ya TZS trilioni 17, ambayo imechochea ukuaji wa sekta nyingine pamoja na kutoa fursa za ajira kwa maelfu ya Watanzania. Mikakati hiyo pia imewezesha uchumi kukabiliana na changamoto za dunia kama mfumuko wa bei, gharama kubwa za ukopaji na mabadiliko ya tabianchi. Wakati ripoti ya UN ikionesha hivyo, Benki ya Dunia (WB) imeitaja Tanzania kuwa nchi ya 10 kwa utajiri barani Afrika kwa kwa kuzingatia Pato Ghafi la Taifa (FDP) kwa kuangalia viwango vya sasa vya kubadili fedha. Ukuaji huo mbali na kuendelea kuboresha maisha ya Watanzania lakini pia unawapa imani wawekezaji waliopo na wanaokusudia kuwekeza nchini, kwa kuwafanya waamini Tanzania ni sehemu salama kuwekeza mitaji yao ya mabilioni, hivyo kufanya uchumi kukua zaidi na zaidi. Read More

  • Matunda ya mikakati ya kiuchumi ya Rais Samia yanavyozidi kuonekana

    Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) limetoa takwimu zinazoonesha kuongezeka kwa pato la Taifa la Tanzania kutoka Dola za Marekani Bilioni 69.9 (TZS trilioni 163.5 trilioni) kwa mwaka 2021, wakati ambapo Rais Samia alipoingia madarakani hadi kufikia Dola za Marekani Bilioni 85.42 (TZS trilioni 200) kwa mwaka huu wa 2023, Huu ni ukuaji mkubwa zaidi katika kipindi cha muda mfupi cha uongozi wa awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ambapo ndani ya miaka miwili pato hilo limeongezeka kwa Dola za Marekani Bilioni 16 (TZS trilioni 37.616) ikilinganishwa na ukuaji wa miaka sita ya awamu ya tano ambapo pato hilo lilikua kwa Dola za Marekani Bilioni 12 pekee (TZS trilioni 28.212). Vilevile IMF imeonesha kuwa kwa mwenendo uliopo hadi mwaka 2028 Tanzania kutakuwa na watu milioni 73.36 huku pato la Taifa likitarajiwa kukua hadi dola bilioni 136.09 (TZS trilioni 318.8) na pato la mtu mmoja mmoja likitarajiwa kukua hadi dola 1,860 (TZS milioni 4.3), huku kasi ya ukuaji wa uchumi ikitarajiwa kuwa asilimia 7. Ukuaji huu wa uchumi ni matokeo ya jitihada za makusudi za Mheshimiwa Rais ambapo tangu alipoingia madarakani Machi mwaka 2021, ametekeleza sera rafiki kwa sekta binafsi, ambayo imeongeza kasi ya uwekezaji, biashara na ukuaji wa uchumi nchini huku akifungua fursa za ajira kwa wananchi kote nchini. Kazi hii kubwa ya ukuaji wa uchumi ni utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambayo inaeleza lengo la kukuza kwa Pato la Taifa pamoja na kujenga uchumi wa kisasa, shirikishi na shindani, utakaowezesha ustawi wa wananchi. Read More

  • Miaka miwili ya Mama: Uwekezaji wa trilioni 17 wazalisha maelfu ya ajira

    Katika kipindi cha mwaka 2021 hadi Januari 2023 Serikali imesajili miradi ya uwekezaji 537 yenye thamani ya TZS trilioni 17, ikiwa ni matokeo mazuri katika mkakati wa Mheshimiwa Rais wa kukuza biashara na uwekezaji nchini. Ongezeko la usajili wa miradi hiyo linatarajiwa kutoa ajira takribani 92,770 ikiwa ni kiwango kikubwa zaidi kuwahi kuandikishwa katika kipindi chochote tangu Tanzania ipate uhuru mwaka 1961. Hatua alizochukua Rais Samia kuboresha Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), kuimarisha Kituo cha Huduma za Mahala Pamoja na maboresho ya Sheria ya Uwekezaji Tanzania zimevutia wawekezaji wapya, zimetatua changamoto zilizokuwa zikiwakabilia wafanyabiashara na kuvutia wawekezaji na kurahisisha utoaji huduma. Aidha, Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Mauzo ya Nje (EPZA) imesajili miradi 38 yenye thamani ya TZS bilioni 327.7 na mauzo nje yenye thamani ya TZS bilioni 448.2. Miradi hiyo ni mahsusi katika sekta zinazozalisha bidhaa zitokanazo na kilimo, bidhaa za viwandani, bidhaa za mifugo, bidhaa za kemikali, bidhaa za madini na bidhaa za misitu. Kuendelea kuongezeka kwa uwekezaji nchini kunakuza mzunguko wa fedha nchini, kunajenga imani ya wawekezaji waliopo pamoja na kuvutia uwekezaji zaidi. Read More

  • Mheshimiwa Rais awezesha vijana wajasiriamali kupata mkopo wa bilioni 1.9

    Moja ya ahadi za Chama cha Mapinduzi (CCM) katika ilani ya mwaka 2020-2025 ni kutengeneza ajira zisizopungua milioni 8 katika sekta rasmi na isiyo rasmi kwa ajili ya vijana nchini. Ndani ya muda mfupi Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameendelea kuweka mikakati ya kufikia lengo hilo ambapo anaendelea kutoa ajira rasmi kwenye kada mbalimbali, ameboresha mazingira ya biashara yanayowezesha vijana kujiajiri na kupata ajira kupitia uwekezaji unaosajiliwa nchini pamoja na kuwezesha upatikanaji wa mitaji na mafunzo ya ujasirimali kwa vijana nchini. Kwa kutambua umuhimu mkubwa wa vijana katika maendeleo ikiwa ndio nguvu kazi kubwa, Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana imetoa mikopo ya TZS bilioni 1.88 kwa ajili ya kuwezesha miradi 85 ya vijana katika sekta za kilimo, viwanda na biashara kwenye halmashauri 28. Aidha, Serikali imetoa fursa za mafunzo ya ujuzi wa kujiajiri au kuajiriwa kwa vijana 118,415 katika fani za uanagenzi, uzoefu wa kazi, ufugaji wa samaki na viumbe maji na kilimo cha kisasa kwa njia ya vizimba. Pamoja na hayo, Serikali imefungua fursa zaidi kupitia kilimo, TEHAMA na pia vijana na wajasiriamali wengine wanaofungua biashara mpya wamepewa neema ya miezi sita hadi mwaka mmoja kutokulipa kodi tangu kuanza kwa biashara zao, mpango unaolenga kulea biashara ndogo ili ziweze kukua zaidi. Read More

  • Rais Samia afungua fursa: Mchango wa Diaspora wavuka trilioni 2

    Moja ya mikakati ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan aliyoiweka wazi baada ya kuingia madarakani ni kutoa fursa zaidi kwa Watanzania waishio nje kushiriki katika shughuli za maendeo na kijamii nchini kwa kuweka mazingira yatakayowawezesha kufanya shughuli zao nchini. Mafanikio yameendelea kuonekana ambapo kwa mwaka 2022 pekee diaspora walituma nchini TZS trilioni 2.6, na pia wamewekeza kupitia ununuzi wa nyumba na viwanja wenye thamani ya TZS bilioni 4.4 na ununuzi wa hisa za TZS bilioni 2.5. Ili kupanua ushiriki wa diaspora katika maendeo ya Tanzania Serikali inatarajia kuwa imekamilisha mfumo wa kidigitali wa uandikishaji wa diaspora Juni mwaka huu ili kuwezesha ukusanyaji endelevu wa takwimu zao. Mbali na kutuma fedha na kuwekeza nchini, diaspora pia huchangia ukuaji wa uchumi kwa kutangaza fursa za kiuchumi, biashara, utalii na uwekezaji zinazopatikana nchini. Mchango mwingine ni kuleta mitaji, utaalam na teknolojia ambavyo huchangia katika kukuza uzalishaji wa mazao, bidhaa na huduma mbalimbali zenye tija kiuchumi. Hadi sasa idadi ya diaspora wa Tanzania ni milioni 1.5, idadi ambayo Rais anaamini itakuwa na mchango mkubwa kwenye uchumi ikiwekewa mazingira rafiki. Read More

  • Uchumi wa Tanzania wakua kwa 23% miaka miwili ya Rais Samia

    Ndani ya miaka miwili ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan Pato la Ghafi la Taifa (GDP) limekua kutoka TZS trilioni 163.3 mwaka 2021 hadi TZS trilioni 200, sawa na ukuaji wa asilimia 23. Takwimu hizo za Shirika la Fedha Duniani (IMF) zinadhihirisha matokeo chanya ya mkakati wa Rais wa kuifungua nchi na kukaribisha wafanyabiashara na wawekezaji pamoja na kufufua biashara za ndani ambazo zilikuwa zimefungwa. Kwa ukuaji huo, ni dhahiri kuwa uchumi wa Tanzania sasa ni mkubwa kuliko baadhi ya nchi za Ulaya kama Croatia, Lithunia, Serbia na Slovenia, hatua ambayo imerejesha imani ya wawekezaji kuendelea kuwekeza nchini. Tanzania sasa inashika nafasi ya 6 kati ya nchi 10 za Kusini mwa Jangwa la Sahara zenye uchumi mkubwa zaidi, ikitanguliwa na Nigeria, Afrika Kusini, Ethiopia, Kenya na Angola. Aidha, kwa mujibu wa IMF, uchumi wa Tanzania unatarajiwa kukua kufikia TZS trilioni 318 ifikapo mwaka 2028, ukuaji ambapo utaakisi uwezo wa Serikali kutekeleza miradi ya maendeleo pamoja na huduma za kijamii. Read More

  • Taarifa ya nafasi zaidi za ajira Januari – Machi 2023

    Tanzania imevutia uwekezaji wa TZS trilioni 2.8 katika kipindi cha miezi mitatu (Januari – Machi 2023) kutokana na mikakati ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ya kuifanya Tanzania kuwa eneo bora la biashara na uwekezaji. Takwimu za Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) za Machi 2023 zinaonesha kuwa kutokana na miradi 93 iliyosajiliwa katika robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2022/23, Watanzania watanufaika na fursa za ajira zaidi ya 16,400. Idadi hiyo ya uwekezaji ni ukuaji wa asilimia 48.9 ikilinganishwa na miradi ya uwekezaji wa TZS trilioni 1.8 iliyosajiliwa kipindi kama hicho mwaka 2022. Aidha, ni ongezeko la asilimia 160 ikilinganishwa na uwekezaji wa TZS trilioni 1.1 uliosajiliwa kipindi kama hicho mwaka 2021. Kwa miradi 37 iliyosajiliwa Machi 2023 pekee, nusu inamilikiwa na wazawa, huku wageni na ubia ikiwa ni asilimia 31 na asilimia 19 mtawala, hali inayoashiria kukua kwa uchumi na mazingira bora ya uwekezaji. Ziara ya Rais Samia nchini Afrika Kusini na ziara ya Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Harris nchini Tanzania imetoa fursa ya kutangaza fursa za uwekezaji, ambapo kati ya kampuni 12 za Afrika Kusini zilizoonesha utayari wa kuwekezaji nchini, tayari moja imekuja kuangalia fursa za uwekezaji. Uamuzi wa Tanzania kurejea kwenye taasisi za kimataifa za usuluhishi pia umechangia kuongeza wawekezaji, ikiwa ni pamoja na kuimarika kwa huduma za usafirishaji, pamoja na ufanisi wa bandari. Read More

  • Benki ya Dunia: Tanzania ni nchi ya mfano katika usimamizi wa uchumi

    Benki ya Dunia imeimwagia sifa Tanzania chini Rais Rais Samia Suluhu Hassan kwa usimamizi mzuri wa uchumi na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayopata fedha kutoka kwenye taasisi hiyo ikilinganishwa na nchi nyingine nyingi za Afrika. Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayesimamia Kundi la Kwanza la nchi za Kanda ya Afrika (Africa Group 1 Constituency), Dkt. Floribert Ngaruk amesema Tanzania ni nchi ya mfano katika usimamizi wa sera za uchumi na fedha ambapo licha ya changamoto za UVIKO-19 na vita inayoendelea baina ya Urusi na Ukraine, tathimini ya benki hiyo inaonesha kuwa uchumi wa Tanzania uko imara ikilinganishwa na nchi nyingine za Afrika. “Tanzania ni nchi ya kupigiwa mfano kwa usimamizi mahiri wa masuala ya uchumi mpana, si tu kwa nchi za Afrika Mashariki, bali kwa nchi za Afrika, ambapo kiwango cha ukuaji uchumi cha wastani wa asilimia 5.4 ni cha juu, na ninawapongeza sana” amesema Dkt. Ngaruko Aidha, amepongeza uhusiano imara uliopo kati ya Tanzania na Benki ya Dunia na kuahidi kuwa benki yake itaendelea kuisaidia Tanzania katika jitihada zake za kukuza uchumi na kuwaondolea umasikini wananchi wake kwa kusaidia fedha zitakazotumika kutekeleza miradi mbalimbali ya kiuchumi na kijamii pamoja na kutoa misaada ya kiufundi. Mpaka sasa Benki ya Dunia imewekeza zaidi ya TZS trilioni 16.7 kwa ajili ya kutekeleza miradi zaidi ya 29 nchini ambapo kati ya miradi hiyo, 24 yenye thamani ya TZS trilioni 15 ni ya kitaifa, na mingine 5 yenye thamani ya TZS trilioni 1.7 ni ya kikanda. Read More

  • Taratibu za kuomba ajira zaidi ya 21,000 zilizotangazwa na Serikali

    Read More

  • Ziara ya Kamala Harris yaleta TZS Trilioni 3.5 za maendeleo Tanzania

    Ziara ya Makamu wa Rais wa Marekani nchini Tanzania, Kamala Harris si tu imekuwa na matokeo chanya kwenye kuendeleza ushirikiano wa kisiasa, bali pia ina mafanikio kiuchumi ambapo Tanzania imepata TZS trilioni 3.5 zitakazotumika kuiwezesha Tanzania kufikia malengo yake. Fedha hizo zitagusa maisha ya Watanzania kupitia sekta mbalimbali ikiwemo biashara, kuunganishwa na huduma za kidijitali, kuinua ustawi wa wanawake na vijana, kuimarisha usalama wa chakula, uhifadhi wa rasilimali za baharini na maziwa pamoja na afya. Aidha, taarifa kutoka Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania imeeleza baadhi ya maeneo ambayo wafanyabiashara wa Marekani wamevutiwa nayo ni biashara na uwekezaji hasa katika kilimo, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, huduma za afya na madini. Wakati Serikali ya Rais Samia Suluhu ikiweka mkazo kwenye kilimo ambacho kimetoa ajira kwa mamilioni ya Watanzania, TZS bilioni 89 zitatumika kuongeza tija kwenye kilimo hasa cha mbogamboga na matunda, mkazo zaidi ukiwa kwa wanawake na vijana ambao pia ndio wanufaika wa mradi wa Building A Better Tommorow. Read More