Rais Samia Suluhu

  • 4R Zinajibu: Tanzania namba moja Uhuru wa Vyombo vya Habari Afrika Mashariki

    Matokeo ya mageuzi ambayo Mheshimiwa Rais Samia Suluhu anayasimamia kupitia falsafa yake ya 4R yanazidi kuonekana kupitia sekta mbalimbali ambapo utashi wake wa kisiasa umeendelea kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari. Mei 3 ya kila mwaka dunia huadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari ambavyo huchukuliwa kuwa ni mhimili wa nne wa dola, vikiwa na kazi ya kuwa daraja kati ya Serikali na wananchi, kulinda maslahi ya wananchi, kuunganisha wananchi na kuchochea maendeleo. Mwaka 2024 yamefanyika maadhimisho ya 31 tangu azimio la Windhoek, na maadhimisho ya nne tangu Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan aingie madarakani ambapo uongozi wake umekuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha uhuru na hali ya kiuchumi wa vyombo vya habari. Uthibitisho huo unaonekana kwenye ripoti ya Reporters Without Boarders (RWB) ambayo imeitaja Tanzania kuwa namba moja Afrika Mashariki kwa kulinda uhuru wa vyombo vya habari. Aidha, utafiti huo umeonesha Tanzania imepiga hatua kubwa duniani ikipanda toka nafasi ya 143 mwaka 2023 hadi nafasi ya 97 mwaka huu. Utafiti huo umeangazia mambo mbalimbali yakiwemo misingi ya kisheria, hali ya kiuchumi, hali ya kisiasa, usalama wa wanahabari na dhana ya kijamii na kitamaduni. Haya ni matokeo ya dhamira ya Mheshimiwa Rais Samia ya kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari ambapo alipoingia madarakani alifungulia magazeti na televisheni za mitandaoni zilizokuwa zimefungiwa, ameunda kamati ambayo imekamilisha kazi ya kuangalia hali ya kiuchumi ya vyombo vya habari pamoja na kuruhusu taasisi za Serikali kupeleka matangazo kwenye vyombo binafsi. Mafanikio haya pia yamechangiwa na mabadiliko ya Sheria ya Huduma ya Vyombo vya Habari 2016 na baadhi ya Kanuni za Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (EPOCA) 2010, na mikakati ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kutoa elimu sheria za utangazaji na kimtandao hivyo kuviwezesha vyombo vya habari kuzingatia sheria. Mwaka 2022 Mheshimiwa Rais aliweka rekodi ya kuwa Rais wa kwanza wa… Read More

  • #ZiaraYaMamaUturuki ni heshima na fursa kwa Tanzania kidiplomasia, kiuchumi na kijamii

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameanza ziara yake rasmi nchini Uturuki kwa mwaliko wa Rais wa nchi hiyo, Mheshimiwa Recep Erdoğan. Ziara hiyo ya kimkakati inatarajiwa kuwa na matokeo chanya kidiplomasia, kiuchumi na kimaendeleo ambapo inafanyika kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 14 (tangu mwaka 2010), na miaka saba tangu ziara ya Rais Erdoğan nchini. Tanzania na Uturuki zina uhusiano wa miaka 61 (tangu mwaka 1963), ambapo Uturuki ilifungua ubalozi wake nchini mwaka 1969, ikaufunga mwaka 1984 na kuufungua tena mwaka 2009, na hivyo kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano na uhusiano baina ya mataifa haya. Malengo makuu matatu ya ziara hiyo ya kimkakati ni kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia uliopo, kufungua fursa mpya za ushirikiano wa kiuchumi, na kuendeleza ushirikiano wa kimaendeleo. Maeneo hayo yanatarajia yatapewa uzito katika mazungumzo atakayofanya na mwenyeji wake, Mheshimiwa Rais Erdoğan. Nchi hizi zina ushirikiano mkubwa kwenye biashara na uwekezaji ambapo Uturuki ni miongoni mwa nchi 20 zenye uchumi mkubwa zaidi duniani imewekeza nchini zaidi ya TZS trilioni 1.3 na kuzalisha ajira zaidi ya 6,700. Kwa upande wa Tanzania, huuza wastani wa bidhaa zenye thamani ya TZS bilioni 41 kila mwaka nchini Uturuki. Mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) unaotekelezwa na kampuni ya Uturuki, Yapi Merkez ni kielelezo kikubwa cha ushirikiano baina ya nchi, na ziara hii inatarajiwa kuwa chachu ya kuongeza kasi ya kutekeleza mradi huo utakaobadili maisha na uchumi wa Tanzania. Aidha, Uturuki ni mshirika mkubwa katika kukuza utalii nchini ambapo safari za ndege za moja kwa moja kwenda Dar es Salaam na Kilimanjaro zimerahisisha usafiri wa watalii, sekta ambayo ina mchango mkubwa katika uchumi wetu. Katika kufanikisha lengo la kufungua fursa mpya za ushirikiano, akiwa nchini Uturuki, Mheshimiwa Rais Samia atashiriki jukwaa la uwekezaji pamoja na kuzungumza na kampuni 15 kubwa zaidi nchini humo na kuwashawishi kuja kuwekeza nchini. Mheshimiwa Rais… Read More

  • #MiakaMitatuYaMama: Wananchi waanza kunufaika na mageuzi ya sekta ya kilimo

    Kujua unakokwenda ni muhimu ili kuweza kufika, lakini njia ipi uitumie si tu ili ufike, bali ufike kwa wakati, ni muhimu zaidi. Tanzania inalenga kujenga uchumi ambao pamoja na mambo mengine utapunguza kiwango cha umasikini kwa mamilioni ya wananchi, ili kufanikisha hilo Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameamua kuitumia sekta ya kilimo ambayo inagusa maisha ya Watanzania saba katika kila Watanzania 10. Takwimu zinaunga mkono uamuzi wake kuwa kilimo kinachangia asilimia 26 ya Pato la Taifa, kinatoa ajira kwa zaidi ya asilimia 62 ya wananchi, kinachangia dola bilioni 2.3 kwa mwaka, hutoa malighafi za kiwandani kwa asilimia 65 na kinahakikisha usalama wa chakula nchini kwa asilimia 100. Hili ni wazi kuwa mageuzi ya kweli katika maisha ya wananchi ni lazima yahusishe kilimo, siri ambayo MAMA anaijua. Ni vigumu kueleza yote yaliyofanyika katika miaka mitatu ya MAMA madarakani kwani ni mengi mno. Baadhi ya mambo hayo ni bajeti ya kilimo imeongezwa zaidi ya mara tatu kutoka TZS bilioni 294 mwaka 2021/22 hadi TZS bilioni 970 mwaka 2023/24, ongezeko ambalo ni msingi wa mageuzi yote kwenye sekta hiyo. Ongezeko hilo limepelekea mafanikio makubwa katika uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia ambapo matumizi ya mbolea yameongezeka kutoka tani 363,599 hadi tani 580,628 kutokana na mpango wa mbolea ya ruzuku. Matumizi ya mbolea yameongeza uzalishaji wa mazao ulioiwezesha nchi kuongeza mauzo ya nje takribani mara mbili kutoka TZS trilioni 3 hadi TZS trilioni 5.7. Mageuzi yaliyofanyika yamemfikia mkulima katika ngazi ya kijiji kupitia vifaa vilivyotolewa kwa maafisa ugani wa halmashauri 166 zikiwemo pikipiki 5,889, vishkwambi 805, seti za vifaa vya kupimia udogo 143 ambavyo vimemwezesha mkulima kulima kisasa akijua atumie mbegu gani na mbolea gani kwenye aina fulani ya udongo. Kama hayo hayatoshi kuondoa kilimo cha mazoea tena cha msimu, MAMA amewekeza katika kilimo umwagiliaji kwa kuongeza bajeti ya umwagiliaji kwa takribani mara nane kutoka TZS… Read More

  • Mheshimiwa Rais Samia: Chaguzi zitakuwa huru na haki

    Watanzania mwaka huu na mwaka 2025 watatimiza haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi ambao watawaongoza kwa miaka mitano ijayo, ambapo katika mchakato wote huo, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameahidi kuwa misingi ya demokrasia, utawala wa sheria, haki vitadumishwa ili wananchi wapate viongozi wanaostahili. Ili kutimiza azma hiyo, ameeleza kuwa mabadiliko ya sheria zinazosimamia vyama vya siasa na uchaguzi yamefanyika kwa kuzingatia maoni yaliyotolewa na wananchi na wadau mbalimbali baada ya kuunda kikosi kazi huru kupitia mazingira ya kisiasa nchini, ambapo kwa kiasi kikubwa maoni yaliyotolewa yamehimiza kuongeza uwazi katika michakato ya uchaguzi ikiwa ni pamoja na uteuzi wa mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi. Maoni mengine ambayo tayari yamefanyiwa kazi ni kubadili jina la Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ili kuakisi uhuru wake. Aidha, amesema baadhi ya maoni yaliyotolewa yalikinzana na Katiba ya nchi, na kuahidi kuwa yatafanyiwa kazi wakati wa maboresho ya kati. “Maboresho haya yatawezesha uchaguzi kufanyika katika mazingira huru na ya haki. Muwe na uhakika kuwa amani na utulivu vitatawala wakati wote kwa gharama yoyote, amesema Rais Samia Suluhu. Akizungumza katika sherehe za mwaka mpya 2024 kwa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, amewahakikishia kuwa Tanzania itaendeleza ushirikiano ulipo kwa kuzingatia Katiba, tunu za taifa, usawa na umoja wetu wa kitaifa na kwamba watafuta sheria, na uingiliaji wa uchaguzi kutoka nje hautakuwepo.   Read More

  • Sera nzuri za uchumi za Rais Samia zaleta neema kwa mabenki

    Sera nzuri za uchumi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimi wa Rais Samia Suluhu Hassan zimeendelea kuleta neema kubwa kwenye sekta ya benki nchini, moja ya uthibitisho huo ukiwa ni namna benki za kibiashara zinavyovunja rekodi ya mapato na faida mwaka. Faida ya benki hizo ni ishara ya usimamizi imara wa sera ya fedha inayopelekea uchumi kuwa tulivu na kuwa moja ya uchumi unaokua kwa kasi zaidi duniani pamoja na kutanuka kwa huduma za kifedha zinazoendelea kuifnya Tanzania kusogea karibu zaidi na lengo la kuwa na huduma za kifedha jumuishi. Taarifa za robo ya nne ya mwaka (Oktoba-Desemba 2023) za mabenki ambazo zimechapishwa Januari 2024 zinaonesha kuwa benki mbili kubwa nchini, CRDB na NMB, zinaendelea kuwa vinara wa sekta ya fedha nchini ambapo NMB imevunja rekodi kwa kupata faida ghafi shilingi bilioni 775. Kutokana na mazingira mazuri ya uchumi nchini tangu Rais Samia aingie madarakani NMB imeongeza kiasi cha mikopo inayotoa kwa asilimia 28, hadi kufikia Shilingi trilioni 7.7 mwaka jana, hatua ambayo imewanufaisha maelfu ya wananchi, huku wengine wakinufaika kwa kuwa mawakala na kupata ajira kutokana na kupanuka kwa shughuli za benki hiyo. Kwa upande wa CRDB imeongeza jumla ya mali (total assets) kufikia shilingi trilioni 13.2, amana za wateja (customer deposits) ziliongezeka hadi kufikia shilingi trilioni 8.8 na mikopo inayotoa imeongezeka hadi kufikia shilingi trilioni 8.8. Benki za biashara zinatarajiwa kuweka rekodi mpya ya faida mwaka huu mpya wa 2024 na kutoa ajira kwa Watanzania wengi zaidi kutokana na mazingira mazuri ya uchumi na uwekezaji chini ya serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Samia. Uamuzi wa Benki Kuu ya Tanzania kuanza kutekeleza Sera ya Fedha kwa kigezo cha riba ya mikopo kwenda benki za kibiashara kunatarajiwa kuinufaisha maradufu Tanzania kwa kuhakikisha ukwasi wa kutosha kwenye shughuli za kiuchumi na kupunguza mfumuko wa bei nchini.… Read More

  • Tanzania yatenga hekta 63,000 za uwekezaji mkubwa wa kilimo na ufugaji

    Serikali kupitia Kituo cha Uwekezaji Tanzania imetenga eneo lenye rutuba la ukubwa wa hekta 60,103 kwaajili ya mji wa kilimo (kilimo kikubwa cha kibiashara pamoja na ufugaji wa kisasa) litakalotolewa kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi. Eneo hilo lipo Mkulazi mkoani Morogoro, pembezoni mwa reli ya TAZARA na linafaa kwaajili ya kilimo cha miwa, mpunga, mahindi, mtama na mengineyo. Kupitia uwekezaji huo, Tanzania inakusudia kupunguza uagizaji wa mazao kutoka nje, pamoja na kuwa kapu la chakula la kulisha nchi nyingine. Kilimo cha miwa kitaongeza malighafi kwenye viwanda vya uzalishaji wa sukari na hivyo kuiwezesha nchi kuachana na uagizaji wa bidhaa hiyo kutoka nje. Katika kipindi cha mwaka 2021/22 Tanzania iliagiza tani 30,000 za sukari ili kufidia nakisi ya uzalishaji wa ndani. Mashamba manne (kila moja likiwa na ukubwa wa hekta 10,000) zitatumiwa kwa ajili kilimo cha mazao mbalimbali kulingana na aina ya udongo, shamba jingine lenye ukubwa wa hekta 10,000 litatengwa kwa ajili ya ufugaji wa kisasa na usindikaji wa mazao ya mifugo, huku hekta 10,103 zilizobaki zikihifadhiwa kwa matumizi ya baadaye kwa ajili ya kuanzisha maeneo ya usindikaji wa bidhaa za kilimo na viwanda vya kuongezea thamani bidhaa za kilimo. Katika hatua nyingine ya kuvutia uwekezaji, TIC imetenga eneo lenye ukubwa wa hekta 3,200 mkoani Kigoma kwa ajili kilimo cha michikichi, usindikaji wa mawese na kilimo cha mazao mengine. Hatua hii pia itaiwezesha nchi kupunguza uagizaji wa mafuta ya kula ambapo kwa takwimu za sasa 60% ya bidhaa hiyo muhimu inatoka nje ya nchi ikiigharimu nchi zaidi ya TZS bilioni 627 kwa mwaka. Ripoti ya Benki ya Dunia (WB) inaonesha kuwa Tanzania imetumia 33% tu ya ardhi yote inayofaa kwa kilimo, hivyo kuwa na fursa kubwa ya kujikuza kupitia kilimo cha kibiashara, ambapo sasa serikali imeweka mkakati wa kuifungua. Read More

  • Mheshimiwa Rais Samia alivyoipa kipaumbele sekta binafsi kwenye mageuzi ya kilimo nchini

    Tanzania imeweka mkakati wa kutumia mageuzi ya kilimo kupunguza umaskini wa wananchi ikizingatiwa kuwa takribani asilimia 70 ya Watanzania wanategemea sekta hiyo. Akizungumza katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi na Usalama wa Chakula, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu amesema Tanzania imekuja na Ajenda ya 10/30 ambayo inalenga kuwezesha kilimo kukua kwa asilimia 10, kutoka asilimia 4 ya sasa, ifikapo mwaka 2030. Mheshimiwa Rais ametaja hatua ambazo Serikali imechukua na inaendelea kuchukua ikiwa ni pamoja na kutoa vivutio vya kikodi kwa sekta binafsi ili ishiriki kikamilifu kwenye kilimo. Vivutio hivyo ni pamoja na kutoa punguzo la kodi (capital allowance) kwa asilimia 100, kusamehe ushuru wa forodha na kodi ya ongezeko la thamani katika vifaa vya kilimo ikiwemo vya vifaa vitakavyotumika katika umwagiliaji, uongezaji thamani, kulima na nishati salama, hatua ambayo inalenga kupunguza gharama za uwekezaji. Hatua nyingine ni Mradi wa Jenga Kesho Bora (BBT) kwa ajili ya kuwawezesha vijana na wanawake kufanya kilimo cha kisasa, mradi ambao utawezesha kuongeza uzalishaji na kutunza mazingira. “Kutunza mazingira bila kupunguza umaskini tutakuwa tunafanya kazi bure,” amesema huku akiongeza kuwa kazi ya Serikali ni kuwapa vijana mafunzo na ardhi, hivyo sasa sekta binafsi inatakiwa iingie kwenye kutoa fedha, lakini pia mitambo kufanya kilimo chetu kiwe cha kisasa Pia, amebainisha kuwa mkazo umewekwa katika tafiti ili kuwezesha wananchi kufanya kilimo chenye uwezo wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi ikiwemo mafuriko, ukame, wadudu na kutunza mazingira. Katika eneo hili Serikali imejenga na inahamasisha sekta binafsi kujenga skimu za umwagiliaji na mabwawa ya kuvuna maji ya mvua. “Sekta binafsi itakuwa na kazi ya kuhakikisha wanaongeza thamani mazao yote yanayozalishwa, lakini pia biashara ya kilimo,” amesema Mheshimiwa Rais na kuongeza kuwa katika hili Serikali inahakikisha upatikanaji wa ardhi na utoaji wa leseni na vibali kwa wawekezaji wanaotaka kuingia kwenye kilimo cha… Read More

  • Mama Ameifungua Nchi: Miradi ya uwekezaji yaongezeka zaidi ya mara mbili

    Ripoti ya Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) imeonesha kuwa miradi ya uwekezaji katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2023/24 (Julai – Septemba) imeongezeka kufikia miradi 137 kutoka miradi 82 kwa kipindi kama hicho mwaka 2022/23, sawa na ongezeko la asilimia 67. Aidha, ongezeko hilo limechochea pia kupata ongezeko maradufu la ajira zinazotokana na miradi ya uwekezaji kufikia ajira 86,986 ikilinganishwa na ajira 12,008 zilizopatikana kipindi kama hicho mwaka 2022/23, ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 624. Matokeo ya kufurika kwa uwekezaji nchini Tanzania ni matunda ya kazi kubwa anayofanya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ya kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini kwa kuanzia kuwenye uboreshaji wa sheria, kanuni na taratibu, kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo nchini, kuimarisha amani na utulivu pamoja, matumizi ya TEHAMA na kurahisisha utoaji wa leseni na vibali. Pia, ziara za Mheshimiwa Rais Samia nje ya nchi zimechangia kuongezeka kwa uwekezaji nchini ambapo maeneo mengi anayokwenda amekuwa akiambatana na sekta binafsi ya Tanzania ambapo pia hukutana na kuzungumza na wafanyabiashara wakubwa wa nchi anayokwenda, hivyo kuwaeleza fursa za uwekezaji nchini, hatua inayowapelekea kuja kuwekeza nchini. Ongezeko hilo linafanya miradi ya uwekezaji iliyosajiliwa nchini kuanzia Januari hadi Septemba 2023 kufikia 366, sawa na asilimia 91.5 ya lengo la kusajili miradi 400 kwa mwaka huu. Miradi hiyo iliyosajiliwa hadi Septemba 2023 inatarajiwa kutoa ajira 116,986 pamoja na kuwekeza mtaji wenye thamani ya zaidi ya TZS trilioni 9.5 ambazo zitachochea ukuaji wa uchumi. Lengo la Mheshimiwa Rais Samia na kuiwezesha Tanzania kusajili miradi ya uwekezaji kutoka nje (FDI) yenye thamani ya dola za Kimarekani bilioni 15 (TZS trilioni 37.5) ifikapo mwaka 2025. Read More

  • Mama hana jambo dogo: Uchumi wakua kwa asilimia 5.2 robo ya pili ya mwaka 2023

    Ripoti ya uchumi ya robo ya pili imethibitisha kuwa hatua za kimkakati zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali zinaleta matokeo yanayowezesha uchumi kustahimili na kukua licha ya changamoto za janga UVIKO19, vita ya Urusi na Ukraine na mabadiliko ya tabianchi. Katika kipindi hicho (Aprili-Juni 2023) ripoti ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imeonesha kuwa uchumi umekua kwa asilimia 5.2, ikiwa ni hatua kubwa kutoka asilimia 4.7 na asilimia 3.8 zilizorekodiwa kipindi kama hicho mwaka 2022 na mwaka 2021, mtawalia. Shuguli zote za kiuchumi zilizofanyika katika kipindi hicho zimechangia katika ukuaji huo, lakini sekta iliyokuwa na mchango mkubwa zaidi kilimo (11.9%), hali inayoonesha mwitikio mkubwa wa mkazo ambao Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameuweka kwenye kilimo. Sekta nyingine ni usafiri na utunzaji mizigo (11.6%), fedha na bima (10.5%), biashara na ukarabati (10.3%), viwanda (9.2%) na ujenzi 6.9%). Aidha, sekta za kiuchumi zilizoshuhudia ukuaji mkubwa ni huduma za kifedha na bima (15.6%), umeme (12.4%), huduma nyinginezo zinazojumuisha sanaa, burudani na shughuli za majumbani (11.5%) usafiri na uhifadhi mizigo (7.6%), chakula na malazi (7.2%), biashara na ukarabati (7.6%) pamoja na madini (6.3%). Ukuaji huo unalandana na takwimu za ripoti ya Shirika la Kimataifa la Fedha (IMF) iliyotolewa Oktoba 2023 ambayo imeonesha kuwa uchumi wa Tanzania unatarajiwa kukua kwa asilimia 5.2 kwa mwaka 2023 kutoka asilimia 4.7 mwaka 2022, huku ukuaji kwa mwaka 2023 ukitarajiwa kufikia asilimia 6.1. Takwimu za IMF zinaifanya Tanzania kuwa moja kati ya nchi 10 za Kusini mwa Jangwa la Sahara ambazo uchumi wake unatazamiwa kukua kwa kasi. Read More

  • Mheshimiwa Rais azipatia ufumbuzi changamoto kubwa nne za wananchi Mtwara

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan leo Septemba 17, 2023 amemaliza ziara yake siku nne mkoani Mtwara, ziara ambayo imekuwa na mafanikio makubwa ikiendelea kuifungua Mtwara kuwa kitovu cha biashara kwa ajili ya Kanda ya Kusini pamoja na nchi jirani za Msumbiji, Malawi na Comoro. Wakati wote wa ziara hiyo Mheshimiwa Rais alikagua na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuzungumzia na wananchi, ambapo walieleza changamoto kubwa nne ambazo ni suala la maji, umeme, bei za mazao pamoja na miundombinu ya usafiri na usafirishaji. Katika mkutano wake wa mwisho wilayani Masasi, ameeleza mkakati wa Serikali kutatua changamoto hizo ambazo kwa upande wa maji amesema kuwa kwa sasa mkoani Mtwara kuna miradi 66 inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali ambayo inanufaisha vijiji 190, hivyo kufanya jumla ya vijiji vyenye majisafi na salama kufikia 650 kati ya vijiji takribani 750. Aidha, amesema Serikali inaendelea na uchimbaji wa visima, ikiwemo wilayani Liwale ambapo mitambo ya kuchimba visima ilianza kazi saa 24 baada ya Rais kumtaka waziri wa maji kuhakikisha changamoto ya wananchi hao inatatuliwa. Kuhusu changamoto ya umeme, Mheshimiwa Rais amewaahidi wakazi wa mkoa huo baada ya miezi 18 changamoto hiyo itakuwa imekwisha kwa sababu miradi miwili mikubwa inatekeleza. Mradi wa kwanza ni wa kuunganisha Masasi kwenye gridi ya Taifa kwa kutoa umeme mkoani Ruvuma, na mradi wa pili ni kutoa umeme wilayani Ruangwa. Aidha, kwa upande wa bei za mazao, amesema mkakati wa Serikali umewezesha mazao ya ufuta na mbaazi kupata bei nzuri msimu huu na kwamba anaamini korosho nayo itauzwa kwa bei nzuri. Hata hivyo, amewahakikishia wananchi kuwa miaka miwili ijayo korosho yote utabanguliwa nchi kabla ya kusafirishwa, mkakati ambao utawanufaisha wakulima zaidi kwa kupandisha thamani zao hilo pamoja na ajira kwenye kongani ya viwanda ambayo itajengwa katika Kijiji cha Maranje wilayani Nanyumbu. Mageuzi makubwa yanaendelea kwenye upande wa miundombinu ambapo sambamba na… Read More