Mama yukokazini

  • Miaka 61 ya Uhuru: Rais Dkt. Samia anavyotumia misingi ya Mwl. Nyerere kuchochea maendeleo

    Tanzania Bara leo imeadhimisha miaka 61 tangu ipate Uhuru kutoka kwa Uingereza mwaka 1961, safari ambayo Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema “imekuwa safari yenye changamoto na mafanikio mengi ambayo Taifa letu linajivunia.” Katika kuadhimisha siku hii kubwa, mjadala mkubwa huzunguka mchango wa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Uhuru, na misimamo aliyoiweka ambayo imekuwa ikitumiwa kama rejea katika kuliongoza Taifa. Mambo mengi ambayo aliyahimiza, Rais Samia ameendelea kuyahimiza na kuyatekeleza ili kuchochea maendeleo ya Watanzania ambayo ni pamoja na; 1. Kupiga vita rushwa Mwalimu Nyerere alikiri kuwa, katika awamu ya kwanza kulikuwa na rushwa, lakini walikuwa wakali sana kuipinga. Serikali yake ilipitisha sheria, mtu akithibitika amepokea au ametoa rushwa, atahukumiwa kifungo kisichopungua miaka miwili na viboko 24 (12 akiingia na 12 akitoka). Vivyo hivyo, Dkt. Samia ameendeleza ari hiyo ya kupinga rushwa akiamini kuwa rushwa inaathiri utoaji haki kwa kumwacha mwenye hatia mtaani na kumfunga asiye na hatia, inawanyima wasio na uwezo fursa ya kupata huduma lakini pia ni kinyume na mafundisho wa kidini. 2. Huduma za Jamii (Elimu, Maji na Afya) Mara baada ya Uhuru, Mwalimu Nyerere aliainisha maadui watatu wa Taifa ambao ambao ni Ujinga, Maradhi na Umasikini. Katika miaka miwili ya Dkt. Rais madarakani amejipambanua kwa kupamba na maadui hao ambapo amewezesha ujenzi wa madarasa zaidi ya 23,000, shule mpya, ajira za walimu, vituo vya afya zaidi ya 230, kujenga na kukarabati hospitali, kufufua na kuanzisha na kukamilisha miradi ya maji pamoja na kuajiri watumishi katika sekta hizo ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi. 3. Kilimo cha kisasa “Tubadili kilimo chetu kusudi kilimo kitusukume kwa sababu hatuna kitu kingine cha kuisukuma nchi hii isipokuwa ni kilimo. Lakini kilimo hiki cha jembe la mkono, kilimo hiki cha kutegemea mvua peke yake, hakina mbolea, hakina dawa, unapanda hovyo hovyo tu, hakitusaidii sana,” alisema Hayati… Read More

  • Rais Dkt. Samia anavyoyaishi na kutekekeleza maono ya Mwalimu Nyerere ndani ya CCM

    Mwaka 1995 katika Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere alisema bila CCM imara nchi itayumba kwa kuwa Watanzania wanataka mabadiliko na wasipoyaona au kuyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya chama hicho. Nia hiyo ya Mwalimu Nyerere ya kuona chama kikiwa imara yanaendelezwa na mwenyekiti wa sasa wa chama hicho, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye amewasihi wanachama kurejea na kuwa wamoja baada ya kumalizika kwa chaguzi ndani ya chama ili kukiwezesha chama kutekeleza majukumu yake ikiwa ni pamoja na kuisimamia Serikali kwenye utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020/25. “Haitakuwa rahisi hata kidogo kwa CCM kutekeleza kwa ufanisi malengo yake […] iwapo wanachama na viongozi hatutakuwa wamoja na tulioshikamana kwa dhati,” amesema hayo huku akitoa rai kuwa “lengo la uchaguzi sio kutafuta ushindi wa mtu mmoja mmoja, bali ni makakati wa kujiimarisha na kujipanga kwa ajili ya kutafuta ushindi wa chama chetu katika chaguzi zijazo.” Aidha, amesema utekelezaji wa wa ilani ya chama hicho unakwenda vizuri na kwa kasi kubwa na kwamba wanaotaka kupima utekelezaji wake, wapime wakijua kwamba hadi sasa ni miaka miwili tu imepita tangu uchaguzi ufanyike. Amesisitiza kuwa CCM ni mfano wa kuigwa na vyama vingine, hivyo sheria kanuni na taratibu lazima zifuatwe, huku akimtaka kila mwanachama kuzingatia wajibu kama ilivyoainishwa kwenye katiba yake ili kuiendeleza CCM inayoamini katika haki, usawa na amani na maendeleo ya Taifa. Read More

  • Dhamira ya Dkt. Samia kuwasaidia wenye ulemavu, milioni 960 za Uhuru kujenga mabweni yao katika shule 8

    Desemba 9 kila mwaka Tanzania huadhimisha Siku ya Uhuru ambapo kwa mwaka 2022 maadhimisho hayo yatakuwa ya 61 tangu nchi ipate uhuru kutoka kwa wakoloni. Hata hivyo, maadhimisho hayo yatafanyika tofauti na miaka mingine ambapo hakutakuwa na sherehe za kitafa baada ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu kuelekeza fedha zilizokuwa zimetengwa kujenga mabweni kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum. Kufuatia uamuzi huo, TZS milioni 960 zitatumika kujenga mabweni kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum kutoka katika shule nane ambazo ni, Longido (Arusha), Songambele (Manyara), Buhangija (Shinyanga), Goeko (Tabora), Darajani (Singida), Msanzi (Rukwa), Idofi (Njombe) na Mtanga (Lindi). Kwa hatua hii ambayo imepokewa kwa furaha na wananchi wengine, Rais Samia ameendelea kudhihirisha dhamira yake ya boresha mazingira ya kujifunzia kwa watu wenye ulemavu pamoja na kuwawezesha kiuchumi ili kutekeleza dhana ya maendeleo jumuishi. Kwa ufupi, miongoni mwa mambo aliyofanya kwa ajili ya wenye ulemavu ni pamoja na kuwezesha ujenzi wa mabweni 50 kwa wanafunzi wenye ulemavu mwaka 2021, na pia kupitia mkopo wa TZS trilioni 1.3 kutoka Shirika la Fedha Dunia wa kukabiliana na athari za UVIKO-19,TZS bilioni 5 zilikwenda kuwasaidia wanawake na watu wenye ulemavu. Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/22 Serikali ilitenga TZS bilioni 3.46 kwa ajili ukarabati wa vyuo vya watu wenye ulemavu ambapo ukarabati wa Vyuo vya Ufundi Stadi na Marekebisho kwa Watu wenye Ulemavu vya Luanzari (Tabora) na Masiwani (Tanga) umekamilika, na ukarabati katika vyuo vinne katika mikoa ya Dar es Salaam, Mtwara, Singida na Tabora unaendelea. Mbali na kuzisimamia mamlaka za Serikali kutoa ajira kwa watu wenye ulemavu, Serikali inaendelea na maboresho ya Sera ya Taifa ya Huduma na Maendeleo ya watu wenye ulemavu, kuhakikisha upatikanaji wa vifaa saidizi na kuendelea kuhamasisha jamii kuondokana na unyanyapaa dhidi ya watu wenye ulemavu. Asilimia 10 inayotokana na makusanyo ya halmashauri imeendelea kuboresha maisha ya wenye ulemavu ambapo hadi Desemba… Read More

  • Baada ya kusubiri kwa miaka 9, Rais Samia aongeza mishahara ya watumishi sekta binafsi

    Baada ya kusubiri kwa zaidi ya miaka tisa, hatimaye Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongeza kima cha chini cha mishahara kwa sekta binafsi ambacho kimewezesha watumishi katika kada mbalimbali kushuhudia kuongezwa kwa mishahara yao. Mara ya mwisho kutolewa kwa viwango vya kima cha chini kwa sekta binafsi ilikuwa mwaka 2013, na hivyo watumishi wa sekta hiyo walikuwa wakiisihi Serikali kupandisha viwango vya mishahara ili kuweza kumudu gharama za maisha. Katika viwango ambavyo vitaanza kutumika Januari 2023, mfano, watumishi wa majumbani watalipwa hadi TZS 250,000 kwa mwezi, huku wale wanaofanya katika sekta za huduma ya mawasiliano wakilipwa hadi TZS 500,000. Mbali na nyongeza hiyo, Serikali imeanisha maslahi mengine ambayo watumishi wa sekta binafsi watastahili ikiwa ni pamoja na likizo ya mwaka yenye malipo, posho itakayotolewa mara moja kwa kila miaka miwili na posho nyingine kama watakavyokubaliana. Aidha, dereva wa lori atastahili posho kwa ajili ya umbali wa safari, na kwa mtumishi ambaye kwa sasa anapokea mshahara na maslahi bora kuliko yaliyoanishwa na amri mpya ya kima cha chini, ataendelea kupokea mashahara huo huo ikiwa amejiriwa na mwajiriwa huyo huyo. Kuongezeka kwa viwango hivyo, kwanza ni hatua ya Rais Samia kutimiza ahadi yake ya kuboresha maslahi ya watumishi nchini kwa lengo la kuinua hali zao za kiuchumi ili waweze kumudu gharama za maisha. Pili, nyongeza hiyo ambayo itawagusa Watanzania wengi ambao wameajiriwa kwenye sekta hiyo itawawezesha kumudu gharama za maisha, ambapo awali ilikuwa changamoto kwao, itachochea ukuaji wa uchumi na kukuza sekta nyingine. Read More

  • Shahada ya Udakari ya Rais Samia ni kuendelea kutambua utumishi wake bora kwa Watanzania

    Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari (Doctor of Letters – Honoris Causa) ikiwa ni Shahada ya Udaktari wa Juu katika Humanitia na Sayansi Jamii ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kutokana na jitihada zake za kutafuta maarifa/kujifunza na kuchochea maendeleo ya kijamii. Akitoa wasifu wa Rais Samia kabla ya kutunukiwa shahada, Prof. Penina Mlama kutoka UDSM ameeleza mambo mbalimbali ambayo yamedhihirisha kuwa mtajwa amekidhi vigezo ambapo kwanza ni namna alivyogusa na kubadili maisha ya watu katika ngazi mbalimbali alizopita kutoka kuwa karani wa ofisi hadi kuwa Rais wa nchi. Katika sekta ya elimu ambayo ndiyo kigezo cha kutunukiwa shadaha hiyo, Prof. Mlama ametaja mengi yaliyofanyika kuwa ni pamoja na kuweka mazingira wezeshi kwa kila mtoto kupata elimu (kujenga shule, madarasa na kunua vitendea kazi), kuwekeza katika vyuo vya kati, ufundi na vyuo vikuu, kuhuisha mkakati wa kitaifa wa elimu jumuishi, kuongeza mikopo ya elimu ya juu, kufanya mapitio ya sera na mitaala ili itoe elimu-ujuzi kulingana na mazingira ya nchi na soko la ajira. Katika uchumi, Rais amefanya marekebisho ya sera, kanuni na sheria, ameboresha mazingira ya biashara ikiwemo kuweka mazingira rafiki kwa walipakodi, kuimarisha sekta za kiuchumi kama kilimo, viwanda, nishati na utalii, ameimarisha diplomasia ya kiuchumi na kuridhia mkataba wa Eneo Huru la Biashara Afrika ambavyo kwa pamoja vimewezesha uchumi kukua, kuvutia wawekezaji na kukuza sekta binafsi nchini. Kuhusu mageuzi yaliyofanywa kwenye kilimo ikiwemo ruzuku ya mbolea, ugawaji mbegu bora, kilimo cha umwagiliaji, kuongezeka kwa bajeti ya kilimo na kufungua masoko nje ya nchi, Prof. Mlama amesema “mpango huu inalenga kugusu uchumi wa mtu binafsi, kumwinua mwanamke na kuhakikisha pesa zinabaki katika mifuko ya watu.” “Katika kipindi kifupi cha uongozi wake ameudhihirishia ulimwengu kuwa ni rahisi mahiri ambaye ameweza kuutumikia umma wa Watanzania kwa viwango vya juu kabisa, na… Read More

  • BWAWA LA KIDUNDA: RAIS SAMIA ATEGUA KITENDAWILI KILICHOSHINDIKANA TANGIA UHURU

    Waswahili wana msemo wao usemao “Lisilo budi hutendwa”, kwa kadhia ya upatikanaji wa maji waliyoipata wakaazi wa mkoa wa Dar es Salaam na mkoa wa Pwani mtawalia ndani wiki kadhaa nyuma, serikali ya Rais Samia Suluhu haikuwa na budi kuidhinisha utekelezaji wa ujenzi wa bwawa la Kidunda. Leo tarehe 11.11.2022 Rais Samia Suluhu ameshuhudia utiaji wa saini wa ujenzi wa mradi wa bwawa kubwa la Kidunda, ambapo saini hiyo ilifuatia na kumkabidhi mkandarasi eneo la mradi tayari kwa kuanza utekelezaji. Wazo la kujenga bwana la Kidunda lilikuwepo tangu baada ya nchi yetu kupata Uhuru mwaka 1961. 1961 chini ya Shirika la Chakula Duniani (FAO) Tanzania ilifanya upembuzi yakinifu ya ujenzi wa bwawa hilo, 1992 ukafanyika utafiti kwa mara ya pili, utafiti wa tatu ukafanywa Shirika la Maendeleo ya Japan (JICA) mwaka 1994 na 2008 Wizara ya Maji na Umwagiliaji ikafanya nayo upembuzi yakinifu ya ujenzi wa mradi huo mkubwa. Katika nyakati zote hizo, licha ya maazimio mengi kuwekwa bungeni, mradi huo ulikuwa ni kitendawili kigumu kwenye utekelezaji kutokana na ufinyu wa bajeti. Baada ya miaka zaidi ya sitini leo tarehe 11.11.2022 Rais Samia Suluhu anashuhudia utiaji wa saini wa mradi mkubwa wa ujenzi wa bwana la Kidunda. Mradi huu unakwenda kuwa suluhu ya kudumu ya upungufu wa maji katika jiji la Dar es Salaam na mkoa wa Pwani na habari njema zaidi utatekelezwa kwa fedha za ndani. Bwawa la Kidunda litakuwa na uwezo wa kukusanya na kuhifadhi maji mita za ujazo milioni 150, na kisha kutiririsha maji hayo kwenye Mto Ruvu nyakati za uhaba na kupelekea uhakika wa kupatikana maji katika jiji la Dar es Salaam na Pwani ambao hutegemea maji katika Mto Ruvu kwa zaidi ya asilimia 90. Mradi huu utatumia gharama ya shilingi bilioni 329 na utatumia muda wa miaka miwili na miezi sita kukamilika. Mradi huu wa… Read More

  • Wanayoyatamani Watanzania kwenye ziara ya Mheshimiwa Rais Samia nchini China

    Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi ya siku tatu nchini China kuanzia Novemba 2 hadi 4 mwaka huu kufuatia mwaliko wa Rais Xi Jinping suala la uendelezaji wa eneo maalum la kiuchumila Bagamoyo (BSEZ) ni moja ya ajenda atakazozibeba. Mwaliko huo uliokuja siku chache baada ya Rais huyo wa Taifa kubwa la Asia kuchaguliwa kwa muhula wa tatu kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Kikomunisti cha Watu wa China (CCP) unamfanya Rais Samia kuwa mkuu wa nchi wa kwanza kutoka Afrika kuzuru nchi hiyo. Kufuatia mwaliko huo unaolenga kukuza ushirikiano baina ya mataifa haya mawili, baadhi ya Watanzania wameeleza matamanio yao ikiwa ni pamoja na China iombwe kukarabati reli ya TAZARA na kujenga daraja juu ya bahari kutoka Dar es Salaam hadi Zanzibar. “Ni faraja kusikia Rais Samia amepata mwaliko wa Rais Jinping, ningetamani sana pamoja na mambo mengine hili la kuboresha TAZARA na kujenga daraja yame miongoni mwa vitu ambavyo ataviomba,” amesema Profesa Humphrey Moshi. Kwa upande wake Msemaji Mkuu Serikali, Gerson Msigwa amesema miradi inayofanyika na nchi hizi mbili ni mingi na mingine inakuja na kwamba na kwamba itakapokamilika Watanzania watajulishwa. Kwa mujibu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) hadi January 2021 kwa upande wa Tanzania Bara China ilikuwa ina jumla ya miradi 940 iliyozalisha ajira takribani 120,000. Read More

  • Rais Samia aja na suluhu kukamilisha mradi wa maji Same – Mwanga – Korogwe baada ya kukwama kwa zaidi ya miaka 10

    “Katika miradi mirefu, ya siku nyingi, inatengenezwa na kusita, na kusimama, ni Same – Mwanga. Tutakwenda kutafuta fedha tuhakikishe unatekelezwa na mwakani […] wapate maji.” Ni maneno ya matumani aliyoyatoa Rais Samia Suluhu Hassan Juni 2022 akiuelezea mradi wa maji wa Same – Mwanga – Korogwe ambao ulikwama kwa zaidi ya miaka 10, na kuyeyusha matumaini ya wananchi zaidi ya nusu milioni kupata maji safi, salama na ya uhakika. Alipoingia madarakani Machi 2021, Rais alikuta mradi huo wa bilioni 262 wenye uwezo wa kuzalisha maji lita milioni 65 kutoka katika Bwawa la Nyumba ya Mungu ukikabiliwa na changamoto za kisheria na kifedha, akafanikisha kutatuliwa kwa changamoto za kisheria na kuingiza TZS bilioni 36 ili mradi ukamilike wananchi wapate maji safi na salama. Kwa sasa, wakazi wa maeneno hayo wana matumaini ya kupata maji mapema mwaka 2023 ambapo hadi Aprili 2022 utekelezaji ulikuwa umefikia asilimia 70.4. Kutokana na changamoto za kisheria, Serikali ilivunja mkataba na wakandarasi M.A Kharafi & Sons na kampuni ya Badr East Africa Enterprises kwa makosa ya kugushi nyaraka muhimu za kimkataba pamoja na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, kisha mradi huo ukakabidhiwa kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA). Read More

  • Rais amesikia, ametekeleza: Watumishi 14,500 walioondolewa kwa vyeti feki kurejeshewa mafao yao

    Rais Samia Suluhu Hassan ameutafsiri kwa vitendo msemo ‘Haki haipaswi tu kutendeka, ni lazima ionekane inatendeka,’ baada ya kuridhia kurejeshwa michango ya watumishi 14,516 waliobainika kuwa na vyeti vya kughushi na waliondolewa kwenye utumishi wa umma. Ridhaa hiyo ya Rais inamaanisha kuwa Serikali itatoa TZS bilioni 46.8 ambazo zitarejeshwa kwa watumishi hao walioondolewa kazini kati ya mwaka 2016 na 2017 katika zoezi la uhakiki wa watumishi wa umma. Fedha hizo ni makato ya asilimia 5 ambayo watumishi hao walikatwa kwa muda waliofanya kazi. Kurejeshwa kwa fedha hizo kunadhihirisha azma ya Rais Samia kuona haki ikitendeka kwa Watanzania wote na kwa wakati wote. Ikiwa ni miaka 5 imepita tangu watumishi hao walipoondolewa kwenye utumishi wa umma, kwa muda wote wamekuwa wakiiomba Serikali kufanya hivyo, huku wabunge na vyama vya wafanyakazi pia vikishinikiza hilo, hivyo uamuzi wa kutekeleza ombi hilo kunaonesha namna Rais alivyomsikivu na anayafanyia kazi maoni na mapendekezo ya Watanzania. Wanufaika wote hao ambao waliondolewa kazini bila kujiandaa hivyo kukumbana na changamoto mbalimbali za kimaisha, sasa wataweza kutumia fedha hizo kuboresha maisha yaona kujiendeleza kiuchumi. Baadhi ya waliohojiwa na vyombo vya habari wamesema kwamba hawaamini hilo limefanyika huku wakielekeza shukrani zao kwa Rais Samia kwa kuwezesha jambo hilo ambalo lilikwama kwa muda mrefu, na kwamba tayari walikuwa wamekata tamaa kuwa hatitofanyika tena. Read More

  • Namna 5 ambazo umeme wa gridi ya Taifa unaubadili mkoa wa Kigoma

    Oktoba 17 mwaka huu ilikuwa siku ya historia kwa Tanzania, hasa mkoa wa Kigoma baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzima jenereta la kuzalisha umeme la Kasulu na kuwasha umeme wa gridi ya Taifa uliofika mkoani humo kwa mara ya kwanza. Jenereta la Kasulu ambalo lilikuwa likizalisha umeme megawati 3.75 zilizotumika wilayani Kasulu na Buhigwe lakini hazikutosheleza ni moja ya majenereta matano yaliyozimwa mengine yakiwa ni Loliondo, Biharamulo, Kibondo na Ngara. Kuzimwa kwa mtambo wa Kasulu na kuwashwa umeme wa gridi ya Taifa kutabadilisha kabisa hadithi ya mkoa wa Kigoma pamoja na maisha ya wakazi wa mkoa huo kwa namna tofauti pamoja na uendeshaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). 1. Kutaipunguzia TANESCO mzigo wa kuendesha mitambo hiyo ambapo kwa mwaka kwa mkoa wa Kigoma ilikuwa ikizalisha umeme kwa gharama ya TZS bilioni 52 huku ikikusanya TZS bilioni 14 tu, hivyo kupelekea kutenga zaidi ya TZS bilioni 38 kila mwaka ili kuhakikisha wananchi wa Kigoma wanapata nishati hiyo muhimu. Uwepo wa umeme wa gridi utaiwezesha Serikali kuelekeza fedha hizo kwenye shughuli nyingine za kimaendeleo na kijamii kama vile shule, afya, maji na miundombinu. 2. Uhitaji wa umeme kwa sasa katika mkoa wa ni megawati 14, lakini umeme uliopelekwa ni megawati 20, hivyo kuufanya kuwa na ziada, huku miradi mingine ya kuongeza umeme ikiendelea. Umeme wa uhakika utavutia wawekezaji hasa wa viwanda vikubwa kuwekeza mkoani humo katika viwanda vya kuchakata mawese na samaki, ambapo awali ingekuwa vigumu kutokana na kutokuwepo umeme wa kutosheleza. 3. Viwanda vikubwa na vidogo vitakavyoanzishwa kwa uwepo wa umeme vitawezesha wakazi wa mkoa huo, hasa vijana na wanawake kupata ajira za moja kwa moja au zisizo za moja kwa moja zitalazobadili maisha yao, na kuchangia ukuaji wa mkoa na Taifa. 4. Kukosekana kwa umeme wa uhakika kuliathiri hali ya maisha ya wakazi wa mkoa huo kutokana na… Read More