• Mheshimiwa Rais aweka mikakati ya kuvutia uwekezaji wa trilioni 37 ifikapo 2025

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameweka wazi kuwa Tanzania inalenga kusajili miradi ya uwekezaji kutoka nje (FDI) yenye thamani ya dola za Kimarekani bilioni 15 (TZS trilioni 37.5) ifikapo mwaka 2025. Ameweka wazi mpango huo wakati akizungumza na wafanyabiashara wakubwa wa India katika jukwaa la uwekezaji la India na Tanzania jijini New Delhi ambapo amesema ili kufanikisha azma hiyo Serikali yake imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kuboresha mfumo wa kisheria kwa kuufanya kuwa rafiki zaidi. Ameeleza kuwa Serikali yake inatambua umuhimu wa sekta binafsi na uwekezaji kama vichocheo vya ukuaji wa kiuchumi, hivyo mazingira ya biashara yameboreshwa ili kupanua biashara zilizopo na kuvutia uwekezaji mpya, jambo ambalo ni moja ya malengo ya ziara yake ya kimkakati nchini India. Kama sehemu ya mageuzi makubwa, Tanzania imeboresha matumizi ya teknolojia kuruhusu wawekezaji kusajili miradi popote pale duniani kupitia dirisha la kuhudumia wawekezaji kielektroniki, na hivyo kupata majibu kabla hata ya kutembelea Tanzania. “Tumepiga hatua kutoka kusajili uwekezaji wa dola bilioni 2 [TZS trilioni 5] mwaka 2020 hadi dola bilioni 5 [TZS trilioni 12.5] katika mwaka ulioishia Juni 2023. Lengo letu ni kufikia dola bilioni 15 kwa mwaka ifikapo mwisho wa 2025,” amesema. Tangu mwaka 1997 Tanzania imepokea jumla ya dola bilioni 3.87 za uwekezaji katika miradi 675 kutoka India ambayo imezalisha ajira zaidi ya 61,000, hivyo kufanya India kuwa miongoni mwa wawekezaji watano bora nchini Tanzania. Read More

  • Shilingi na Rupia kutumika zaidi katika biashara kati ya Tanzania na India

    Tanzania na India zimefikia makubaliano ya kuongeza matumizi ya fedha za nchi husika katika biashara, badala ya kutegemea dola ya Marekani kama ilvyokuwa hapo awali. Azimio hilo limefikiwa katika mazungumzo kati ya Rais wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu wa India, Mheshimiwa Narendra Modi ambapo itawezesha kupunguza mfumuko wa bei tofauti na awali ambapo Tanzania ingelazimika kutumia fedha nyingi kupata dola ya Marekani ili kuagiza bidhaa. Utekelezaji wa uamuzi huo ulishaanza kufanyiwa kazi ambapo hadi sasa biashara yenye thamani ya TZS bilioni 125 imefanyika kwa fedha za nchi husika, hatua inayodhihirisha utayari wa nchi zote kutekeleza makubaliano haya, na sasa hatua inayofuata ni kuongeza matumizi ya fedha hizo. Katika hatua nyingine, India na Tanzania zimebadili uhusiano wao kutoka wa kawaida kidiplomasia kuwa wa mkakati, ambapo nchi zote mbili zimeainisha maeneo mahususi ya kushirikiana yenye maslahi kwa pande zote mbili. Tanzania inatarajia kuendelea kunufaika na ushirikiano wake wa kimkakati na India ikizingatiwa kuwa ni nchi ya tano kwa kuwa na uchumi mkubwa duniani, ikiwa imepiga hatua katika sekta za afya, TEHAMA, nishatia, miundombinu, ulinzi na usalama ambazo ni kipaumbele kwa Tanzania. Hadi mwaka 2022, kiwango cha biashara kati ya nchi hizo mbili kilifikia TZS trilioni 7.7, hivyo kuifanya India kuwa mshirika wa tatu kwa ukubwa katika biashara na mwekezaji wa tano kwa ukubwa nchini Tanzania. Read More

  • Ziara ya Mheshimiwa Rais Samia nchini India itakavyofungua fursa kwa Tanzania

    Mwaka 2022 Tanzania iliuza zaidi bidhaa zake nchini India, biashara ambayo ilichangia asilimia 17.3 ya mauzo yote, huku India ikiwa ni nchi ya tatu ambayo Tanzania iliagiza bidhaa nyingi zaidi (asilimia 12.5), takwimu ambazo zinadhihirisha namna mataifa haya yanauhusiano wa kibiashara wenye manufaa kwa pande zote. Katika muktadha wa kukuza zaidi biashara na ushirikiano katika sekta nyingine, Rais wa Tanzania, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufanya ziara ya kimkakati ya kitaifa ya siku tatu nchini India (Oktoba 8-10, 2023) kwa mwaliko wa Serikali ya India, ziara ambayo inatarajiwa kuwa matokeo chanya kwa Tanzania hasa katika sekta za afya, diplomasia, elimu, biashara na uwekezaji, uchumi wa bluu, maji, kilimo na teknolojia. Ziara hiyo ni kubwa kwani inafanyika miaka na tangu kiongozi wa mwisho wa Tanzania kutembelea nchi hiyo, na inatarajiwa kuimarisha ushirikiano wa miaka 62 wa nchi hizo, ambao chimbuko lake ni Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Waziri Mkuu wa India, Hayati Jawaharlal Nehru. Ziara ya Mheshimiwa Rais nchini India ina malengo makubwa mawili ambayo ni kudumisha, kuimarisha na kuendelea uhusiano uliopo katika sekta takribani 10 na kufungua fursa za biashara na uwekezaji, ikifahamika kuwa India ni moja ya nchi zenye uchumi mkubwa duniani na ni moja yenye miradi mingi ya uwekezaji nchini. Matarajio ya mafanikio kutokana na ziara hiyo; ELIMU 1. Fursa za mafunzo kwa Watanzania katika nyanja mbalimbali nchini India ambapo kwa kuanzia kutatolewa nafasi 1,000. BIASHARA VYA UWEKEZAJI 1. Kuongezeka kwa uwekezaji nchini hasa viwanda vya kutengeneza simu na vifaa vya kielektroniki AFYA 1. Kuanzishwa kwa taasisi ya upandikizaji wa figo hapa nchini 2. Kuanzishwa kwa kiwanda cha kutengeneza chanjo za binadamu na wanyama 3. Kuongeza ushirikiano kati ya hospitali za Tanzania na India ili kuimarisha uwezo na weledi katika utoaji wa huduma za afya. 4. Kuongezeka kwa upatikanaji wa dawa (ubora na unafuu)… Read More

  • Maonesho ya mboga na matunda Qatar kufungua fursa kwa wakulima wa Tanzania

    Doha- Qatar: Oktoba 2 mwaka huu Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan alishiriki uzinduzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Mboga na Matunda (Doha International Horticulture Expo 2023) ambayo yanatoa fursa kwa wafanyabiashara na wajasiriamali kujifunza na kuwekeza katika kilimo, hususani kwenye teknolojia rafiki ya mazingira. Kazi kubwa ya kuimarisha sekta ya mboga na matunda inayagusa moja kwa moja maisha ya vijana na wanawake ambao ndio wanufaika wakubwa wa ajira takribani milioni 6.5 zinazotokana na sekta, hivyo kuwa na mchango mkubwa katika ukuzaji wa uchumi wa familia na taifa kwa ujumla. Ushiriki wake kwenye jukwaa hilo la kimataifa ni mwendelezo wa mageuzi ya kilimo aliyoyaanzisha nchini ambapo Serikali ya Tanzania kupitia taasisi zake mbalimbali na sekta binafsi inashiriki maonesho hayo kwa lengo la kutafuta masoko ya mazao ya kilimo pamoja na kuvutia uwekezaji kwenye sekta hiyo iliyoajiri zaidi ya asilimi 65 ya Watanzania. Mkakati wa Mheshimiwa Rais ni kuona kilimo kinakuwa kwa wastani wa asilimia 10 ifikapo mwaka 2030, ambapo mbali na kufungua fursa za masoko kimataifa, hatua nyingine za kimkakati alizochukua kutimiza lengo ni pamoja na upatikanaji wa mbegu bora, miundombinu ya umwagiliaji, utafiti na upatikanaji wa mbolea nafuu na viuatilifu. Juhudi hizi zinalenga kupunguza gharama za uzalishaji kwa mkulima na kuongeza tija na uzalishaji, kuimarisha usalama wa chakula nchini na kuiwezesha Tanzania kuuza chakula nje, ikiendelea ushiriki wake katika kuongeza usalama wa chakula duniani na kutunza mazingira kwa wakati mmoja. Read More

  • Serikali ya matokeo: Thamani ya uwekezaji nchini yaongezeka zaidi ya mara mbili

    Ripoti ya Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) imeonesha kuwa thamani ya miradi ya uwekezaji imeongezeka kwa mwezi mmoja kufikia TZS trilioni 2.33 kwa Agosti mwaka huu kutoka TZS trilioni 1.06 kwa Julai mwaka huu, sawa na ukuaji wa asilimia 120. Aidha, ripoti hiyo imeonesha kuwa miradi ya uwekezaji imeongezeka kufikia 58 kutoka 40 katika kipindi tajwa, ambapo kwa miradi iliyosajiliwa Agosti mwaka huu inatarajiwa kuzalisha ajira 25,700. Ongezeko la miradi limeendelea kusadifu mikakati na mkazo uliowekwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan katika kilimo ili kuboresha maisha ya Watanzania ikizangatiwa sekta hii kwa takwimu za mwaka 2021 ilichangia asilimia 26.1 katika Pato la Taifa, ilitoa ajira kwa wananchi kwa wastani wa asilimia 65.6 na kuchangia asilimia 65 ya malighafi za viwanda. Matokeo ya kazi kubwa anayofanya Mheshimiwa Rais imeendelea kuonekana ambapo thamani ya uwekezaji kwenye kilimo imeongezeka kwa zaidi ya TZS bilioni 275.53 kufikia TZS bilioni 849.13 kutoka TZS bilioni 571.1 kwa Julai mwaka huu. Wakati uwekezaji kwenye kilimo ukiendele kukua, Serikali imeendelea kuchua hatua kumwezesha mkulima mdogo ikiwemo kuimarisha huduma za ugani, kutoa ruzuku na pembejeo za kilimo, kufungua fursa za masoko, kujenga mifumo ya umwagiliaji, kutoa elimu ya kilimo cha kisasa, hasa kwa vijana, pamoja na afua nyingine ili kuwezesha kilimo kuchangia asilimia 10 kwenye pato la Taifa ifikapo mwaka 2030. Wanazuoni wamepongeza mageuzi yanayoendelea kufanyika kwenye kilimo ambapo Profesa Mshiriki kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Abel Kinyondo amesema mafanikio hayo ni matokeo ya mkakati wa Serikali ya awamu ya sita kuwekeza zaidi kwenye kilimo, huku Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA), Profesa Haji Semboja amesema Tanzania inatambulika duniani kwa fursa nyingi kwenye kilimo. Read More

  • BoT kununua dhahabu inathibitisha nia ya Serikali kuimarisha utulivu wa kiuchumi

    Dar es Salaam, Tanzania – Serikali chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kuimarisha uchumi wa nchi, ambapo sasa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imechukua hatua kubwa ya kimkakati ya kununua dhahabu ya ndani ili kuimarisha hifadhi ya fedha za kigeni na kuongeza nguvu ya shilingi ya Tanzania. Tayari BoT inanunua dhahabu kutoka kwa wachimbaji na wafanyabiashara wa ndani kwa kutumia shilingi ya Tanzania ambapo tayari imenunua kilogramu 418, lengo likiwa ni kununua kilogramu 6,000 katika mwaka wa fedha 2023/24. Hatua hii muhimu ina manufaa mbalimbali kwa taifa na wananchi kwa kununua dhahabu kwa ajili ya kuongeza akiba ya fedha za kigeni, taifa letu linajikinga dhidi ya athari zitokanazo na mabadiliko ya ghafla (kutokuwepo kwa uhakika) ya kiuchumi wa kimataifa. Dhahabu imekuwa kimbilio la thamani kwa miongo mingi wakati wa migogoro ya kiuchumi na kisiasa duniani. Kwa hivyo, kwa kuchanganya dhahabu katika akiba ya fedha za kigeni, Tanzania inaweza kusaidia kulinda thamani ya shilingi ya nchi wakati wa mazingira magumu ya kiuchumi duniani. Pia, hatua ya kununua dhahabu kutoka kwa wazalishaji wa ndani kutachangia kukuza uchumi wa ndani kwani itachochea uzalishaji wa dhahabu. Kukua kwa uzalishaji kunaenda moja kwa moja na kuongezeka kwa ajira, kwani shughuli za uchimbaji na biashara ya dhahabu zinahitaji wafanyakazi, na pia ongezeko la wachimbaji litanufaisha sekta nyingine zinazofungamana na sekta hiyo ikiwemo ya huduma (chakula, maji, nishati, mawasiliano). Uamuzi wa Benki Kuu ya Tanzania wa kununua dhahabu kwa ajili ya kuongeza akiba ya fedha za kigeni na kulinda uchumi unathibitisha nia ya serikali ya kusimamia utulivu wa kiuchumi na kujenga nguvu za kifedha, hatua ambayo inaweza kuwa na athari chanya kwa maendeleo na ustawi wa nchi. Read More

  • Royal Tour Imejibu: Utalii waongoza katika kuingiza fedha za kigeni

    Kazi kubwa aliyoifanya na inayoendelea kufanywa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza fursa za utalii unaweza kusema ‘imejibu’ baada ya sekta hiyo kuendelea kuimarika na kupita madini ya dhahabu katika kuiingizia nchi fedha za kigeni, ikiwa ni kwa mara ya kwanza ndani ya miaka minne tangu ilipoanza kushuka. Mlipuko wa janga la kidunia la Ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO) mwaka 2019 kuliiathiri sekta hiyo ambapo mchango wake kwenye fedha za kigeni ulishuka kutoka dola za kimarekani bilioni 2.52 (TZS trilioni 6.3) mwishoni mwa mwaka 2019 hadi dola za Kimarekani bilioni 1 (TZS trilioni 2.5) mwishoni mwa mwaka 2020, na hivyo kupelekea dhahabu iliyoingiaza dola za Kimarekani bilioni 2.9 (TZS trilioni 7.2) kuongoza. Kuhakikisha sekta ya utalii ambayo inatoa ajira zaidi ya milioni 1.6, inachangia asilimia 25 ya fedha za kigeni na asilimia 21 ya Pato la Taifa inaimarika, Mheshimiwa Rais Samia alichukua jukumu la kurekodi filamu ya Tanzania: The Royal Tour ambayo ilizinduliwa nchini Marekani na hivyo kuiwezesha nchi kutangaza fursa za utalii na vivutio vya utalii kwa mamilioni ya watu dunia, hatua ambayo imepelea kuendelea kuongezeka kwa watalii kutoka ndani na nje ya nchi. Matokeo yameendelea kuonekana ambapo takwimu za Benki Kuu ya Tanzania zinaonesha kuwa mapato yatokanayo na utalii yamepanda kufikia dola za Kimarekani bilioni 2.999 (TZS trilioni 7.5) katika mwaka ulioishia Julai 2023 kutoka dola za Kimarekani bilioni 1.95 (TZS trilioni 4.8) mwaka ulioishia Julai 2022, huku mapato ya dhahabu kwa mwaka ulioishia Julai 2023 yakiwa dola za Kimarekani bilioni 2.9 (TZS trilioni 7.3). Mafanikio hayo yametokana na kuendeleo kuongezeka kwa watalii kutoka nje ya nchi ambapo ripoti ya BoT inaonesha kuwa watalii wameongezeka kwa asilimia 37.2 kufikia 1,658,043 katika mwaka huo, idadi ambayo haijawahi kufikiwa kabla. Licha ya mafanikio haya, Mheshimiwa Rais Samia anaendelea kutangaza utalii ili kufikia lengo la watalii milioni 5 ifikapo… Read More

  • Mheshimiwa Rais azipatia ufumbuzi changamoto kubwa nne za wananchi Mtwara

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan leo Septemba 17, 2023 amemaliza ziara yake siku nne mkoani Mtwara, ziara ambayo imekuwa na mafanikio makubwa ikiendelea kuifungua Mtwara kuwa kitovu cha biashara kwa ajili ya Kanda ya Kusini pamoja na nchi jirani za Msumbiji, Malawi na Comoro. Wakati wote wa ziara hiyo Mheshimiwa Rais alikagua na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuzungumzia na wananchi, ambapo walieleza changamoto kubwa nne ambazo ni suala la maji, umeme, bei za mazao pamoja na miundombinu ya usafiri na usafirishaji. Katika mkutano wake wa mwisho wilayani Masasi, ameeleza mkakati wa Serikali kutatua changamoto hizo ambazo kwa upande wa maji amesema kuwa kwa sasa mkoani Mtwara kuna miradi 66 inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali ambayo inanufaisha vijiji 190, hivyo kufanya jumla ya vijiji vyenye majisafi na salama kufikia 650 kati ya vijiji takribani 750. Aidha, amesema Serikali inaendelea na uchimbaji wa visima, ikiwemo wilayani Liwale ambapo mitambo ya kuchimba visima ilianza kazi saa 24 baada ya Rais kumtaka waziri wa maji kuhakikisha changamoto ya wananchi hao inatatuliwa. Kuhusu changamoto ya umeme, Mheshimiwa Rais amewaahidi wakazi wa mkoa huo baada ya miezi 18 changamoto hiyo itakuwa imekwisha kwa sababu miradi miwili mikubwa inatekeleza. Mradi wa kwanza ni wa kuunganisha Masasi kwenye gridi ya Taifa kwa kutoa umeme mkoani Ruvuma, na mradi wa pili ni kutoa umeme wilayani Ruangwa. Aidha, kwa upande wa bei za mazao, amesema mkakati wa Serikali umewezesha mazao ya ufuta na mbaazi kupata bei nzuri msimu huu na kwamba anaamini korosho nayo itauzwa kwa bei nzuri. Hata hivyo, amewahakikishia wananchi kuwa miaka miwili ijayo korosho yote utabanguliwa nchi kabla ya kusafirishwa, mkakati ambao utawanufaisha wakulima zaidi kwa kupandisha thamani zao hilo pamoja na ajira kwenye kongani ya viwanda ambayo itajengwa katika Kijiji cha Maranje wilayani Nanyumbu. Mageuzi makubwa yanaendelea kwenye upande wa miundombinu ambapo sambamba na… Read More

  • Mheshimiwa Rais Samia atoa mwelekeo mchakato wa katiba mpya

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amesema anatambua umuhimu wa katiba mpya kama ambavyo maoni ya makundi mbalimbali, ikiwemo kikosi kazi, yaliyotolewa na kusisitiza kuendelezwa kwa mchakato huo ambao ulikwama tangu mwaka 2014. Licha wa umuhimu huo ametahadhari kuwa upatikanaji wa katiba mpya ni mchakato na kwamba mchakato huo sio mali ya wanasiasa bali ni ya Watanzania wote, hivyo amewataka wanasiasa kutokuhodhi sauti kwenye mchakato huu. “Katiba ni ya Watanzania, awe ana chama, awe hana, awe ana dini, awe hana, awe mrefu, awe mfupi, mnene, mwembamba, mkubwa, mdogo. Kwa hiyo matengenezo yake yanahitaji tafakuri kubwa sana,” amesema Mheshimiwa Rais. Hata hivyo, amesema kuwa katiba si kitabu, bali ni misingi ya maadili, itikadi na namna ambavyo Watanzania wanakubaliana kuendesha Taifa lao, hivyo, makubaliano hayo yanaandikwa, hivyo, haiwezi kuwa sawa na nchi nyingine. “Tunaanza na elimu Watanzania wajue [katiba] ni kitu gani […] Kwa hiyo tusiwaburuze wananchi. Katiba viongozi wa kisiasa si mali yetu, ni mali ya Watanzania. Tunachokitaka kwenu ni maoni katiba iweje,” ameongeza. Aidha, ameongeza demokrasia lazima iakisi namna watu ndani ya nchi yanavyoendesha masuala yao ikiwemo tamaduni, maadili, mila, desturi, na kwamba huwezi kuchukua demokrasia kutoka nchi nyingine na kuiingiza nchini bila kuzingatia masuala ya ndani. Read More

  • Rais Samia anavyotumia Diplomasi ya Uchumi kuchochea maendeleo nchini

    Tanzania imeendelea kutekeleza sera yake ya Diplomasia ya Uchumi inayolenga kujenga na kuimarisha uhusiano wake wa kimataifa na kujenga mahusiano ya kibiashara na kiuchumi na taasisi pamoja na mataifa mengine ili kuchochea maendeleo. Historia nyingine imeandika baada ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kushiriki na kuhutubia katika Mkutano wa 15 wa BRICS (Brazil, Russia, India, China, South Africa) ambalo ni jukwaa la nchi ambazo uchumi wake unakua kwa kasi duniani ambapo pato la Taifa la mataifa hayo ni quadrilioni TZS 63.3, ambapo pia kutokana na kupokea wanachama wapya sita, kuanzia Januari 2024 nchi sita kati ya tisa zinazozalisha mafuta zaidi duniani zitakuwa mwanachama wa jukwaa hilo. Kwa kushiriki kwenye mkutano huo, Tanzania itapata manufaa makubwa kiuchumi na kibiashara kwani kunaiwezesha kujenga mahusiano ya kiuchumi na biashara na nchi hizo zenye nguvu hatua inayoweza kufungua fursa mpya au kupanua fursa zilizopo za kuuza bidhaa za Tanzania kwenye masoko ya nchi hizo, na hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi. Ni wazi pia kuwa mataifa ya BRICS yamepiga hatua kwenye teknolojia, hivyo Tanzania inaweza kujifunza matumizi bora ya teknolojia katika kurahisisha utoaji huduma na kuchochea maendeleo. China ambayo ni mwanachama wa BRICS ni mshirika mkubwa maendeleo wa Tanzania ambapo kwa miezi saba ya mwaka 2023 imeongoza kwa uwezekaji (Foreign Direct Investment) nchini ikiwekeza mtaji wa zaidi ta TZS trilioni 1.2 ambao pamoja na mambo mengi utazalisha ajira kwa maelfu ya Watanzania. Katika mkutano huo Rais Samia alipata nafasi ya kuzungumza na Rais wa China, Xi Jinping, ikiwa ni mara nyingine kwa viongozi hao kukutana baada ya ziara ya Rais Samia nchini China. Mazungumzo hayo huenda yakaongeza uwezekano wa kufadhili miradi muhimu kama miundombinu, nishati, kilimo, na teknolojia, uwekezaji pamoja ushirikiano wa kiusalama. Katika dunia ya sasa, nchi haiwezi kujitenga kama kisiwa, inailazimu kutoka, kukutana na kushirikiana na mataifa mengine ili kufanikisha masuala mbalimbali… Read More