Kitaifa

  • Viongozi wa upinzani waiunga mkono njia ya Rais Dkt. Samia kujenga maridhiano

    “Si wakati wakati wote ni wa kupongezana na si wakati wote ni wa kupingana. Kwenye kujenga Tanzania bora natamani kujenga jamii yenye maridhiano na maelewano. Natamani kujenga umoja pasipo kujali tofauti zetu za kisiasa, kidini, kikabila na nyingine zote.” Hayo ni maneno ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika barua yake aliyoitoa Tanzania ikiadhimisha miaka 30 tangu kurejea kwenye mfumo wa vyama vingi, ambapo alieleza azma yake ya kujenga jamii inayopata haki sawa mbele ya sheria, isiyobaguana na inayotoa fursa sawa za kiuchumi kwa wote. Katika kufanikisha nia hiyo, Rais ametimiza kiu ya muda mrefu ya vyama vya upinzani kwanza kwa kukutana na kuzungumza na wanasiasa wa upinzani akiwemo viongozi wa CHADEMA, CUF na ACT-Wazalendo, mazungumzo ambayo yameendelea kujenga imani miongoni mwa viongozi hao kuhusu nia thabiti ya Rais kujenga umoja wa kitaifa. Aidha, katika kutekeleza matakwa na viongozi wa vyama vya upinzani ambayo ni pamoja na kufufuliwa kwa mchakato wa katiba mpya na kuundwa tume huru ya uchaguzi, Rais aliunda kikosi kazi kilichojumuisha wawakilishi kutoka vyama vya upinzani, na tayari kimewasilisha mapendekezo serikali juu ya namna ya kuyafikia matamanio hayo. “Mama Samia amekuwa Rais wa kwanza kwenye nchi yetu baada ya ujio wa pili wa vyama vingi mwaka [19]92 kusimama hadharani, na nilisimama naye Ikulu, tukazungumza na vyombo vya habari mimi na yeye, kwamba tufanye nini kila mmoja […] tuondoe maumivu yaliyopo katika Taifa hili,” alisema Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe Machi 2022. Uamuzi wa Mbowe kusimama kwenye maridhiano umeungwa mkono na viongozi wa CHADEMA ambapo aliyewahi kuwa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi amesema kwa sababu njia za maandamano walizowahi kujaribu huko nyuma hazikufanikiwa, basi, sasa njia ya kuelekea ni maridhiano. Kwa upande wake kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe alisema “hakuna njia yoyote ya kuifanya nchi yetu iweze kwenda mbele isipokuwa njia hii ambayo [Rais Dkt. Samia… Read More

  • Rais Dkt. Samia atunukiwa tuzo ya kimataifa kukuza sekta ya utalii

    Utendaji kazi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan umeendelea kutambulika kimataifa ambapo siku chache tangu atajwe miongoni mwa wanawake 100 wenye nguvu zaidi duniani kwa mwaka wa pili mfululizo, sasa ametunukiwa tuzo ya Mwongozaji Bora wa Watalii, tuzo iliyotolewa na Taasisi ya Kimataifa ya International Iconic Awards ya nchini India. Taasisi hiyo imemtunuku Dkt. Samia tuzo hiyo kutokana na mchango wake katika uandaaji wa filamu ya Tanzania: The Royal Tour ambayo imekuwa na mchango mkubwa sana katika kukuza sekta ya utalii, hasa baada ya kuathiriwa na janga la UVIKO19 tangu mwaka 2019. Akipokea tuzo hiyo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Pindi Chana amesema itaipa Serikali ari ya kuendelea kuboresha sekta ya utalii ambayo imeendelea kukua ambapo mwaka 2021 Tanzania ilipokea watalii 992,692 lakini mwaka 2022 tayari imepokea watalii zaidi ya milioni 1, huku wengine wakiendelea kuingia. Mbali na kutangaza utalii filamu hiyo imeonesha fursa za biashara na uwekezaji zilizomo nchini ambapo wafanyabiashara na wawekezaji kutoka mataifa mbalimbali, ikiwemo Marekani, wamefika nchini kwa ajili ya kuangalia fursa za biashara na uwekezaji. Read More

  • Miaka 61 ya Uhuru: Rais Dkt. Samia anavyotumia misingi ya Mwl. Nyerere kuchochea maendeleo

    Tanzania Bara leo imeadhimisha miaka 61 tangu ipate Uhuru kutoka kwa Uingereza mwaka 1961, safari ambayo Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema “imekuwa safari yenye changamoto na mafanikio mengi ambayo Taifa letu linajivunia.” Katika kuadhimisha siku hii kubwa, mjadala mkubwa huzunguka mchango wa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Uhuru, na misimamo aliyoiweka ambayo imekuwa ikitumiwa kama rejea katika kuliongoza Taifa. Mambo mengi ambayo aliyahimiza, Rais Samia ameendelea kuyahimiza na kuyatekeleza ili kuchochea maendeleo ya Watanzania ambayo ni pamoja na; 1. Kupiga vita rushwa Mwalimu Nyerere alikiri kuwa, katika awamu ya kwanza kulikuwa na rushwa, lakini walikuwa wakali sana kuipinga. Serikali yake ilipitisha sheria, mtu akithibitika amepokea au ametoa rushwa, atahukumiwa kifungo kisichopungua miaka miwili na viboko 24 (12 akiingia na 12 akitoka). Vivyo hivyo, Dkt. Samia ameendeleza ari hiyo ya kupinga rushwa akiamini kuwa rushwa inaathiri utoaji haki kwa kumwacha mwenye hatia mtaani na kumfunga asiye na hatia, inawanyima wasio na uwezo fursa ya kupata huduma lakini pia ni kinyume na mafundisho wa kidini. 2. Huduma za Jamii (Elimu, Maji na Afya) Mara baada ya Uhuru, Mwalimu Nyerere aliainisha maadui watatu wa Taifa ambao ambao ni Ujinga, Maradhi na Umasikini. Katika miaka miwili ya Dkt. Rais madarakani amejipambanua kwa kupamba na maadui hao ambapo amewezesha ujenzi wa madarasa zaidi ya 23,000, shule mpya, ajira za walimu, vituo vya afya zaidi ya 230, kujenga na kukarabati hospitali, kufufua na kuanzisha na kukamilisha miradi ya maji pamoja na kuajiri watumishi katika sekta hizo ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi. 3. Kilimo cha kisasa “Tubadili kilimo chetu kusudi kilimo kitusukume kwa sababu hatuna kitu kingine cha kuisukuma nchi hii isipokuwa ni kilimo. Lakini kilimo hiki cha jembe la mkono, kilimo hiki cha kutegemea mvua peke yake, hakina mbolea, hakina dawa, unapanda hovyo hovyo tu, hakitusaidii sana,” alisema Hayati… Read More

  • Rais Dkt. Samia anavyoyaishi na kutekekeleza maono ya Mwalimu Nyerere ndani ya CCM

    Mwaka 1995 katika Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere alisema bila CCM imara nchi itayumba kwa kuwa Watanzania wanataka mabadiliko na wasipoyaona au kuyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya chama hicho. Nia hiyo ya Mwalimu Nyerere ya kuona chama kikiwa imara yanaendelezwa na mwenyekiti wa sasa wa chama hicho, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye amewasihi wanachama kurejea na kuwa wamoja baada ya kumalizika kwa chaguzi ndani ya chama ili kukiwezesha chama kutekeleza majukumu yake ikiwa ni pamoja na kuisimamia Serikali kwenye utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020/25. “Haitakuwa rahisi hata kidogo kwa CCM kutekeleza kwa ufanisi malengo yake […] iwapo wanachama na viongozi hatutakuwa wamoja na tulioshikamana kwa dhati,” amesema hayo huku akitoa rai kuwa “lengo la uchaguzi sio kutafuta ushindi wa mtu mmoja mmoja, bali ni makakati wa kujiimarisha na kujipanga kwa ajili ya kutafuta ushindi wa chama chetu katika chaguzi zijazo.” Aidha, amesema utekelezaji wa wa ilani ya chama hicho unakwenda vizuri na kwa kasi kubwa na kwamba wanaotaka kupima utekelezaji wake, wapime wakijua kwamba hadi sasa ni miaka miwili tu imepita tangu uchaguzi ufanyike. Amesisitiza kuwa CCM ni mfano wa kuigwa na vyama vingine, hivyo sheria kanuni na taratibu lazima zifuatwe, huku akimtaka kila mwanachama kuzingatia wajibu kama ilivyoainishwa kwenye katiba yake ili kuiendeleza CCM inayoamini katika haki, usawa na amani na maendeleo ya Taifa. Read More

  • Dhamira ya Dkt. Samia kuwasaidia wenye ulemavu, milioni 960 za Uhuru kujenga mabweni yao katika shule 8

    Desemba 9 kila mwaka Tanzania huadhimisha Siku ya Uhuru ambapo kwa mwaka 2022 maadhimisho hayo yatakuwa ya 61 tangu nchi ipate uhuru kutoka kwa wakoloni. Hata hivyo, maadhimisho hayo yatafanyika tofauti na miaka mingine ambapo hakutakuwa na sherehe za kitafa baada ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu kuelekeza fedha zilizokuwa zimetengwa kujenga mabweni kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum. Kufuatia uamuzi huo, TZS milioni 960 zitatumika kujenga mabweni kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum kutoka katika shule nane ambazo ni, Longido (Arusha), Songambele (Manyara), Buhangija (Shinyanga), Goeko (Tabora), Darajani (Singida), Msanzi (Rukwa), Idofi (Njombe) na Mtanga (Lindi). Kwa hatua hii ambayo imepokewa kwa furaha na wananchi wengine, Rais Samia ameendelea kudhihirisha dhamira yake ya boresha mazingira ya kujifunzia kwa watu wenye ulemavu pamoja na kuwawezesha kiuchumi ili kutekeleza dhana ya maendeleo jumuishi. Kwa ufupi, miongoni mwa mambo aliyofanya kwa ajili ya wenye ulemavu ni pamoja na kuwezesha ujenzi wa mabweni 50 kwa wanafunzi wenye ulemavu mwaka 2021, na pia kupitia mkopo wa TZS trilioni 1.3 kutoka Shirika la Fedha Dunia wa kukabiliana na athari za UVIKO-19,TZS bilioni 5 zilikwenda kuwasaidia wanawake na watu wenye ulemavu. Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/22 Serikali ilitenga TZS bilioni 3.46 kwa ajili ukarabati wa vyuo vya watu wenye ulemavu ambapo ukarabati wa Vyuo vya Ufundi Stadi na Marekebisho kwa Watu wenye Ulemavu vya Luanzari (Tabora) na Masiwani (Tanga) umekamilika, na ukarabati katika vyuo vinne katika mikoa ya Dar es Salaam, Mtwara, Singida na Tabora unaendelea. Mbali na kuzisimamia mamlaka za Serikali kutoa ajira kwa watu wenye ulemavu, Serikali inaendelea na maboresho ya Sera ya Taifa ya Huduma na Maendeleo ya watu wenye ulemavu, kuhakikisha upatikanaji wa vifaa saidizi na kuendelea kuhamasisha jamii kuondokana na unyanyapaa dhidi ya watu wenye ulemavu. Asilimia 10 inayotokana na makusanyo ya halmashauri imeendelea kuboresha maisha ya wenye ulemavu ambapo hadi Desemba… Read More

  • Baada ya kusubiri kwa miaka 9, Rais Samia aongeza mishahara ya watumishi sekta binafsi

    Baada ya kusubiri kwa zaidi ya miaka tisa, hatimaye Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongeza kima cha chini cha mishahara kwa sekta binafsi ambacho kimewezesha watumishi katika kada mbalimbali kushuhudia kuongezwa kwa mishahara yao. Mara ya mwisho kutolewa kwa viwango vya kima cha chini kwa sekta binafsi ilikuwa mwaka 2013, na hivyo watumishi wa sekta hiyo walikuwa wakiisihi Serikali kupandisha viwango vya mishahara ili kuweza kumudu gharama za maisha. Katika viwango ambavyo vitaanza kutumika Januari 2023, mfano, watumishi wa majumbani watalipwa hadi TZS 250,000 kwa mwezi, huku wale wanaofanya katika sekta za huduma ya mawasiliano wakilipwa hadi TZS 500,000. Mbali na nyongeza hiyo, Serikali imeanisha maslahi mengine ambayo watumishi wa sekta binafsi watastahili ikiwa ni pamoja na likizo ya mwaka yenye malipo, posho itakayotolewa mara moja kwa kila miaka miwili na posho nyingine kama watakavyokubaliana. Aidha, dereva wa lori atastahili posho kwa ajili ya umbali wa safari, na kwa mtumishi ambaye kwa sasa anapokea mshahara na maslahi bora kuliko yaliyoanishwa na amri mpya ya kima cha chini, ataendelea kupokea mashahara huo huo ikiwa amejiriwa na mwajiriwa huyo huyo. Kuongezeka kwa viwango hivyo, kwanza ni hatua ya Rais Samia kutimiza ahadi yake ya kuboresha maslahi ya watumishi nchini kwa lengo la kuinua hali zao za kiuchumi ili waweze kumudu gharama za maisha. Pili, nyongeza hiyo ambayo itawagusa Watanzania wengi ambao wameajiriwa kwenye sekta hiyo itawawezesha kumudu gharama za maisha, ambapo awali ilikuwa changamoto kwao, itachochea ukuaji wa uchumi na kukuza sekta nyingine. Read More

  • Shahada ya Udakari ya Rais Samia ni kuendelea kutambua utumishi wake bora kwa Watanzania

    Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari (Doctor of Letters – Honoris Causa) ikiwa ni Shahada ya Udaktari wa Juu katika Humanitia na Sayansi Jamii ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kutokana na jitihada zake za kutafuta maarifa/kujifunza na kuchochea maendeleo ya kijamii. Akitoa wasifu wa Rais Samia kabla ya kutunukiwa shahada, Prof. Penina Mlama kutoka UDSM ameeleza mambo mbalimbali ambayo yamedhihirisha kuwa mtajwa amekidhi vigezo ambapo kwanza ni namna alivyogusa na kubadili maisha ya watu katika ngazi mbalimbali alizopita kutoka kuwa karani wa ofisi hadi kuwa Rais wa nchi. Katika sekta ya elimu ambayo ndiyo kigezo cha kutunukiwa shadaha hiyo, Prof. Mlama ametaja mengi yaliyofanyika kuwa ni pamoja na kuweka mazingira wezeshi kwa kila mtoto kupata elimu (kujenga shule, madarasa na kunua vitendea kazi), kuwekeza katika vyuo vya kati, ufundi na vyuo vikuu, kuhuisha mkakati wa kitaifa wa elimu jumuishi, kuongeza mikopo ya elimu ya juu, kufanya mapitio ya sera na mitaala ili itoe elimu-ujuzi kulingana na mazingira ya nchi na soko la ajira. Katika uchumi, Rais amefanya marekebisho ya sera, kanuni na sheria, ameboresha mazingira ya biashara ikiwemo kuweka mazingira rafiki kwa walipakodi, kuimarisha sekta za kiuchumi kama kilimo, viwanda, nishati na utalii, ameimarisha diplomasia ya kiuchumi na kuridhia mkataba wa Eneo Huru la Biashara Afrika ambavyo kwa pamoja vimewezesha uchumi kukua, kuvutia wawekezaji na kukuza sekta binafsi nchini. Kuhusu mageuzi yaliyofanywa kwenye kilimo ikiwemo ruzuku ya mbolea, ugawaji mbegu bora, kilimo cha umwagiliaji, kuongezeka kwa bajeti ya kilimo na kufungua masoko nje ya nchi, Prof. Mlama amesema “mpango huu inalenga kugusu uchumi wa mtu binafsi, kumwinua mwanamke na kuhakikisha pesa zinabaki katika mifuko ya watu.” “Katika kipindi kifupi cha uongozi wake ameudhihirishia ulimwengu kuwa ni rahisi mahiri ambaye ameweza kuutumikia umma wa Watanzania kwa viwango vya juu kabisa, na… Read More

  • BWAWA LA KIDUNDA: RAIS SAMIA ATEGUA KITENDAWILI KILICHOSHINDIKANA TANGIA UHURU

    Waswahili wana msemo wao usemao “Lisilo budi hutendwa”, kwa kadhia ya upatikanaji wa maji waliyoipata wakaazi wa mkoa wa Dar es Salaam na mkoa wa Pwani mtawalia ndani wiki kadhaa nyuma, serikali ya Rais Samia Suluhu haikuwa na budi kuidhinisha utekelezaji wa ujenzi wa bwawa la Kidunda. Leo tarehe 11.11.2022 Rais Samia Suluhu ameshuhudia utiaji wa saini wa ujenzi wa mradi wa bwawa kubwa la Kidunda, ambapo saini hiyo ilifuatia na kumkabidhi mkandarasi eneo la mradi tayari kwa kuanza utekelezaji. Wazo la kujenga bwana la Kidunda lilikuwepo tangu baada ya nchi yetu kupata Uhuru mwaka 1961. 1961 chini ya Shirika la Chakula Duniani (FAO) Tanzania ilifanya upembuzi yakinifu ya ujenzi wa bwawa hilo, 1992 ukafanyika utafiti kwa mara ya pili, utafiti wa tatu ukafanywa Shirika la Maendeleo ya Japan (JICA) mwaka 1994 na 2008 Wizara ya Maji na Umwagiliaji ikafanya nayo upembuzi yakinifu ya ujenzi wa mradi huo mkubwa. Katika nyakati zote hizo, licha ya maazimio mengi kuwekwa bungeni, mradi huo ulikuwa ni kitendawili kigumu kwenye utekelezaji kutokana na ufinyu wa bajeti. Baada ya miaka zaidi ya sitini leo tarehe 11.11.2022 Rais Samia Suluhu anashuhudia utiaji wa saini wa mradi mkubwa wa ujenzi wa bwana la Kidunda. Mradi huu unakwenda kuwa suluhu ya kudumu ya upungufu wa maji katika jiji la Dar es Salaam na mkoa wa Pwani na habari njema zaidi utatekelezwa kwa fedha za ndani. Bwawa la Kidunda litakuwa na uwezo wa kukusanya na kuhifadhi maji mita za ujazo milioni 150, na kisha kutiririsha maji hayo kwenye Mto Ruvu nyakati za uhaba na kupelekea uhakika wa kupatikana maji katika jiji la Dar es Salaam na Pwani ambao hutegemea maji katika Mto Ruvu kwa zaidi ya asilimia 90. Mradi huu utatumia gharama ya shilingi bilioni 329 na utatumia muda wa miaka miwili na miezi sita kukamilika. Mradi huu wa… Read More

  • Wanayoyatamani Watanzania kwenye ziara ya Mheshimiwa Rais Samia nchini China

    Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi ya siku tatu nchini China kuanzia Novemba 2 hadi 4 mwaka huu kufuatia mwaliko wa Rais Xi Jinping suala la uendelezaji wa eneo maalum la kiuchumila Bagamoyo (BSEZ) ni moja ya ajenda atakazozibeba. Mwaliko huo uliokuja siku chache baada ya Rais huyo wa Taifa kubwa la Asia kuchaguliwa kwa muhula wa tatu kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Kikomunisti cha Watu wa China (CCP) unamfanya Rais Samia kuwa mkuu wa nchi wa kwanza kutoka Afrika kuzuru nchi hiyo. Kufuatia mwaliko huo unaolenga kukuza ushirikiano baina ya mataifa haya mawili, baadhi ya Watanzania wameeleza matamanio yao ikiwa ni pamoja na China iombwe kukarabati reli ya TAZARA na kujenga daraja juu ya bahari kutoka Dar es Salaam hadi Zanzibar. “Ni faraja kusikia Rais Samia amepata mwaliko wa Rais Jinping, ningetamani sana pamoja na mambo mengine hili la kuboresha TAZARA na kujenga daraja yame miongoni mwa vitu ambavyo ataviomba,” amesema Profesa Humphrey Moshi. Kwa upande wake Msemaji Mkuu Serikali, Gerson Msigwa amesema miradi inayofanyika na nchi hizi mbili ni mingi na mingine inakuja na kwamba na kwamba itakapokamilika Watanzania watajulishwa. Kwa mujibu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) hadi January 2021 kwa upande wa Tanzania Bara China ilikuwa ina jumla ya miradi 940 iliyozalisha ajira takribani 120,000. Read More

  • Rais Samia aja na suluhu kukamilisha mradi wa maji Same – Mwanga – Korogwe baada ya kukwama kwa zaidi ya miaka 10

    “Katika miradi mirefu, ya siku nyingi, inatengenezwa na kusita, na kusimama, ni Same – Mwanga. Tutakwenda kutafuta fedha tuhakikishe unatekelezwa na mwakani […] wapate maji.” Ni maneno ya matumani aliyoyatoa Rais Samia Suluhu Hassan Juni 2022 akiuelezea mradi wa maji wa Same – Mwanga – Korogwe ambao ulikwama kwa zaidi ya miaka 10, na kuyeyusha matumaini ya wananchi zaidi ya nusu milioni kupata maji safi, salama na ya uhakika. Alipoingia madarakani Machi 2021, Rais alikuta mradi huo wa bilioni 262 wenye uwezo wa kuzalisha maji lita milioni 65 kutoka katika Bwawa la Nyumba ya Mungu ukikabiliwa na changamoto za kisheria na kifedha, akafanikisha kutatuliwa kwa changamoto za kisheria na kuingiza TZS bilioni 36 ili mradi ukamilike wananchi wapate maji safi na salama. Kwa sasa, wakazi wa maeneno hayo wana matumaini ya kupata maji mapema mwaka 2023 ambapo hadi Aprili 2022 utekelezaji ulikuwa umefikia asilimia 70.4. Kutokana na changamoto za kisheria, Serikali ilivunja mkataba na wakandarasi M.A Kharafi & Sons na kampuni ya Badr East Africa Enterprises kwa makosa ya kugushi nyaraka muhimu za kimkataba pamoja na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, kisha mradi huo ukakabidhiwa kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA). Read More