Mama yukokazini

  • Taarifa ya nafasi zaidi za ajira Januari – Machi 2023

    Tanzania imevutia uwekezaji wa TZS trilioni 2.8 katika kipindi cha miezi mitatu (Januari – Machi 2023) kutokana na mikakati ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ya kuifanya Tanzania kuwa eneo bora la biashara na uwekezaji. Takwimu za Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) za Machi 2023 zinaonesha kuwa kutokana na miradi 93 iliyosajiliwa katika robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2022/23, Watanzania watanufaika na fursa za ajira zaidi ya 16,400. Idadi hiyo ya uwekezaji ni ukuaji wa asilimia 48.9 ikilinganishwa na miradi ya uwekezaji wa TZS trilioni 1.8 iliyosajiliwa kipindi kama hicho mwaka 2022. Aidha, ni ongezeko la asilimia 160 ikilinganishwa na uwekezaji wa TZS trilioni 1.1 uliosajiliwa kipindi kama hicho mwaka 2021. Kwa miradi 37 iliyosajiliwa Machi 2023 pekee, nusu inamilikiwa na wazawa, huku wageni na ubia ikiwa ni asilimia 31 na asilimia 19 mtawala, hali inayoashiria kukua kwa uchumi na mazingira bora ya uwekezaji. Ziara ya Rais Samia nchini Afrika Kusini na ziara ya Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Harris nchini Tanzania imetoa fursa ya kutangaza fursa za uwekezaji, ambapo kati ya kampuni 12 za Afrika Kusini zilizoonesha utayari wa kuwekezaji nchini, tayari moja imekuja kuangalia fursa za uwekezaji. Uamuzi wa Tanzania kurejea kwenye taasisi za kimataifa za usuluhishi pia umechangia kuongeza wawekezaji, ikiwa ni pamoja na kuimarika kwa huduma za usafirishaji, pamoja na ufanisi wa bandari. Read More

  • Benki ya Dunia: Tanzania ni nchi ya mfano katika usimamizi wa uchumi

    Benki ya Dunia imeimwagia sifa Tanzania chini Rais Rais Samia Suluhu Hassan kwa usimamizi mzuri wa uchumi na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayopata fedha kutoka kwenye taasisi hiyo ikilinganishwa na nchi nyingine nyingi za Afrika. Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayesimamia Kundi la Kwanza la nchi za Kanda ya Afrika (Africa Group 1 Constituency), Dkt. Floribert Ngaruk amesema Tanzania ni nchi ya mfano katika usimamizi wa sera za uchumi na fedha ambapo licha ya changamoto za UVIKO-19 na vita inayoendelea baina ya Urusi na Ukraine, tathimini ya benki hiyo inaonesha kuwa uchumi wa Tanzania uko imara ikilinganishwa na nchi nyingine za Afrika. “Tanzania ni nchi ya kupigiwa mfano kwa usimamizi mahiri wa masuala ya uchumi mpana, si tu kwa nchi za Afrika Mashariki, bali kwa nchi za Afrika, ambapo kiwango cha ukuaji uchumi cha wastani wa asilimia 5.4 ni cha juu, na ninawapongeza sana” amesema Dkt. Ngaruko Aidha, amepongeza uhusiano imara uliopo kati ya Tanzania na Benki ya Dunia na kuahidi kuwa benki yake itaendelea kuisaidia Tanzania katika jitihada zake za kukuza uchumi na kuwaondolea umasikini wananchi wake kwa kusaidia fedha zitakazotumika kutekeleza miradi mbalimbali ya kiuchumi na kijamii pamoja na kutoa misaada ya kiufundi. Mpaka sasa Benki ya Dunia imewekeza zaidi ya TZS trilioni 16.7 kwa ajili ya kutekeleza miradi zaidi ya 29 nchini ambapo kati ya miradi hiyo, 24 yenye thamani ya TZS trilioni 15 ni ya kitaifa, na mingine 5 yenye thamani ya TZS trilioni 1.7 ni ya kikanda. Read More

  • Taratibu za kuomba ajira zaidi ya 21,000 zilizotangazwa na Serikali

    Read More

  • Ziara ya Kamala Harris yaleta TZS Trilioni 3.5 za maendeleo Tanzania

    Ziara ya Makamu wa Rais wa Marekani nchini Tanzania, Kamala Harris si tu imekuwa na matokeo chanya kwenye kuendeleza ushirikiano wa kisiasa, bali pia ina mafanikio kiuchumi ambapo Tanzania imepata TZS trilioni 3.5 zitakazotumika kuiwezesha Tanzania kufikia malengo yake. Fedha hizo zitagusa maisha ya Watanzania kupitia sekta mbalimbali ikiwemo biashara, kuunganishwa na huduma za kidijitali, kuinua ustawi wa wanawake na vijana, kuimarisha usalama wa chakula, uhifadhi wa rasilimali za baharini na maziwa pamoja na afya. Aidha, taarifa kutoka Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania imeeleza baadhi ya maeneo ambayo wafanyabiashara wa Marekani wamevutiwa nayo ni biashara na uwekezaji hasa katika kilimo, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, huduma za afya na madini. Wakati Serikali ya Rais Samia Suluhu ikiweka mkazo kwenye kilimo ambacho kimetoa ajira kwa mamilioni ya Watanzania, TZS bilioni 89 zitatumika kuongeza tija kwenye kilimo hasa cha mbogamboga na matunda, mkazo zaidi ukiwa kwa wanawake na vijana ambao pia ndio wanufaika wa mradi wa Building A Better Tommorow. Read More

  • Mkakati wa Mheshimiwa Rais kuondoka kodi za mabavu waongeza ukusanyaji mapato kwa 38%

    Siku chache baada ya kuingia madarakani, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan aliweka wazi msimamo wake kuhusu ukusanyaji wa kodi akiitaka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kutotumia mabavu na ubabe kukusanya kodi, kwani kufanya hivyo ni kuua biashara na mfumo huo sio endelevu. “Kodi tunazitaka, na mimi nasema mwende mkakusanye kodi, lakini kodi za dhuluma, hapana, kwa sababu hata hizo hazitatufikisha mbali,” alisistiza Rais na kueleza kuwa anajua kwa uamuzi huo ukusanyaji mapato ungeshuka kwa muda, lakini baada ya muda biashara zikiimarika, makusanyo yatakua. Miaka miwili tangu kutolewa kwa agizo hilo, Tanzania imeendelea kuweka rekodi ya makusanyo ya kodi, ambapo wastani wa ukusanyaji mapato umeongezeka kutoka TZS trilioni 1.45 kwa mwezi mwaka 2021 hadi TZS trilioni 2 kwa mwezi mwaka 2022, sawa na ongezeko la asilimia 38. Ukuaji huo umechangiwa na masuala mbalimbali, kubwa likiwa ni kuimarika kwa mazingira ya biashara na uwekezaji ambapo biashara na miradi mipya ya uwekezaji imefunguliwa nchini pamoja na iliyokuwepo kuimarika. Sababu nyingine kuimarika kwa mifumo ya ukusanyaji kodi, kuongezeka kwa uwezo wa walipakodi na kuimarika kwa uhusiano wa TRA na walipakodi. Kodi ndio nyenzo muhimu inayoiwezesha Serikali kutekeleza majukumu yake ikiwemo kufikisha huduma za kijamii na kimaendeleo kwa wananchi kupitia sekta mbalimbali ikiwemo elimu, afya, kilimo, maji na miundombinu. Read More

  • #MiakaMiwiliYaMama: Marekani yampongeza Rais Samia, yaahidi uwekezaji zaidi kukuza uchumi

    ‘Champion’ wa mageuzi ya demokrasia, ndiyo sifa Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Harris aliyompa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na mageuzi ya kisiasa aliyofanya nchini ikiwa ni pamoja na kuruhusu mikutano ya hadhara, kukutana na viongozi wa vyama vya siasa na kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari. Kutokana na uongozi bora wa Rais Samia, Marekani na Tanzania zimekubaliana kupanua ushirikiano ambao utawezesha upatikanaji wa dola za Kimarekani milioni 500 (TZS trilioni 1.2) kugharamia uletaji wa bidhaa na huduma nchini Tanzania katika sekta za usafirishaji, nishati salama, teknolojia ya kidijitali na miundombinu. Aidha, katika muktadha huo wa kukuza uchumi amesema kazi ya ujenzi wa kiwanda cha kwanza na cha aina yake Afrika kitakachotumika kuchakata madini yanayotengeneza betri za magari ya umeme ambayo yatakuwa yanatumika duniani kote ikiwepo Marekani inandelea na uzalishaji utaanza mwaka 2026. Kuongezeka kwa fursa hizi kutazalisha ajira kwa maelfu ya Watanzania, na kuimarisha nafasi ya Tanzania katika ramani ya kiuchumi Afrika na duniani. Wakati huo huo, Kamala amempongeza Rais Samia kwa namna miaka miwili ya uongozi wake imewezesha kumwinua mwanamke kiuchumi, akisisitiza kuwa mwanamke akiinuliwa kiuchumi, basi familia na jamii nzima inanufaika. Read More

  • #MiakaMiwiliYaMama: Ziara ya Kamala Harris nchini na fursa za kiuchumi kwa Tanzania

    Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Harris akianza ziara yake ya siku tatu (Machi 29-31) nchini leo, wachambuzi wa masuala ya kisiasa na uchumi wameeleza kuwa ujio wake ni matokeo ya kazi kubwa ya kuimarisha diplomasia ya uchumi na ushirikiano wa kimataifa iliyofanywa katika miaka miwili ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan. Kwa Tanzania, ziara hiyo inalenga pamoja na mambo mengine, kuimarisha ushirikiano hususani kwenye maeneo ya kimkakati ambayo yanagusa maisha ya Watanzania ikiwa ni pamoja na biashara, uwekezaji, utalii, elimu, afya na utunzaji wa mazingira. Ziara hiyo imekuja takribani mwaka mmoja tangu Rais Samia alipofanya ziara nchini Marekani, ambapo alimwalika Kamala kuzuru Tanzania, hivyo kuitikia wito huo kunadhihirisha uhusiano mzuri kati ya Tanzania na Marekani ambao umedumu kwa zaidi ya miaka 62. Marekani ni moja ya washirika wakubwa wa maendeleo nchini ambapo imewekeza kwenye miradi 266 yenye thamani ya takribani trilioni 11 ambayo imetengeneza ajira zipatazo 54,584 kwa Watanzania. Itakumbukwa pia katika ziara ya Rais Samia nchini Marekani Aprili 2022 alifanikiwa kuvutia uwekezaji wa zaidi ya TZS trilioni 2, hivyo ujio wa kiongozi huyo wa juu wa Marekani unatazamiwa kuwa na matokeo zaidi ya hayo katika sekta ya biashara na uwekezaji. Ni dhahiri kuwa Tanzania kuchaguliwa miongoni mwa nchi zaidi ya 50 za Afrika ni fursa muhimu ambayo inathibitisha kuimarika kwa mazingira ya kisiasa na kiuchumi, na hivyo ziara hiyo itaitangaza zaidi Tanzania kimataifa na kuvutia uwekezaji kutoka Marekani na sehemu nyingine. Read More

  • #MiakaMiwiliYaMama: Ajira za moja kwa moja Watanzania zaidi ya 85,000

    Mkakati wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan wa kuboresha mazingira ya biashara nchini na kuvutia uwakezaji umezaa matunda ambapo takwimu kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) zinaonesha kuwa thamani ya uwekezaji nchini umekua kwa asilimia 173. Ripoti ya TIC inaonesha kuwa thamani ya uwekezaji imepanda kufikia TZS trilioni 19.87 katika miaka miwili ya Serikali ya awamu ya sita, kutoka TZS trilioni 7.27 iliyorekodiwa katika miaka miwili kabla hajaingia madarakani. Ongezeko hilo ni matokeo ya kazi kubwa ya Rais ya kurejesha imani ya wawekezaji ndani na nje ya nchi ambao amekuwa akikutana katika ziara zake nje ya nchi na ndani ya nchi ambapo pamoja na kutangaza fursa za uwekezaji, pia alizipatia ufumbuzi changamoto zilizowakabili. Kati ya Machi 2021 na Februari 2023 idadi ya miradi iliyosajiliwa imeongezeka kutoka 455 hadi 575, ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 26. Kati ya miradi hiyo, asilimia 32 inamilikiwa na Watanzania, asilimia 42 ni ya wageni na asilimi 27 ni ubia kati ya wageni na wazawa. Kutokana na uwekezaji huo, idadi ya ajira zilizozalishwa kwa Watanzania zimeongezeka kutoka 61,900 hadi 87,187, uwekezaji mkubwa ukiwa kwenye sekta za viwanda, ujenzi wa majengo ya kibiashara na usafirishaji. Mafanikio haya yamehusishwa pia na Tanzania kushiriki katika mikutano ya kimataifa. Read More

  • #MiakaMiwiliYaMama: Amewajengea vijana uwezo wa kujiajiri kupitia kilimo

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anadhihirisha kwa vitendo kauli yake aliyotoa kuwa hataki kuingia katika historia ya kuwa mmoja wa wanaowalaumu vijana kuwa hawajiajiri, badala yake anawawekea mazingira wezeshi ya kujiajiri kupitia kilimo ambapo lengo ni kuzalisha ajira milioni 3, kipaumbele kikiwa vijana na wanawake. Machi 20 mwaka huu amezindua mashamba ya pamoja (Block Farms) zaidi ya ekari 12,000 ambazo zitagawawiwa kwa vijana, kila mmoja kwa ukubwa usiozidi ekari 10, pia alizindua ndege zisizo na rubani, mashine za umwagiliaji na magari kwa ajili ya maafisa wa wilaya ili kuhakikisha vijana popote walipo nchini wanapata usaidizi wa kitaalamu katika kufanya kilimo cha kibiashara. Katika azma ya kukifanya kilimo kuwa cha vijana, ameahidi kuendelea kutenga bajeti mahsusi kwa ajili ya watendaji kwenye sekta ya kilimo ili shughuli zote zifanyike kwa usasa kuanzia uzalishaji hadi uuzaji mazao na bidhaa. “Tunasema ni kilimo cha vijana, hivyo vijana wawepo shambani, wawepo kwenye utaalamu, wawepo kwenye kuendesha mitambao, sehemu zote kuwa na vijana wanaokwenda kwenye sekta ya kilimo,” amesema akizindua programu ya Building a Better Tomorrow. Katika miaka miwili ya uongozi wake, kilimo ni moja tu ya njia anazotumia kumwinua kijana wa Kitanzania na kukabiliana na changamoto ya ajira inayoisumbua dunia. Ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi katika kila wilaya, mikopo ya halmashauri, kuboresha mazingira ya biashara hasa kwa wajasiriamali ni maeneo mengine ambayo yametoa ajira kwa vijana wengi. Read More

  • #MiakaMiwiliYaMama: Fursa zaidi kwa vijana, sasa Serikali kuwapatia pembejeo za kilimo

    Katika moja ya hotuba zake kwa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere alieleza umuhimu wa kubadili mfumo wa kilimo nchini akisema kuwa kilimo cha kutegemea mvua, kisicho na mbolea, dawa na maarifa, hakitusaidii sana. Anayoyafanya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Kupitia Mfuko wa Pembejeo za Kilimo (AGITF) ni kuyaishi maono ya Mwalimu Nyerere kwani anakuza kilimo kwa kuwapatia vijana pembejeo (dawa, mbegu bora, viuatilifu), ili kubadili kilimo na kufikia lengo la kumnufaisha mkulima, kukuza mchango wake kwenye uchumi, kuongeza uzalishaji wa chakula na malighafi za viwandani. Kama hilo halitoshi, Machi 20 mwaka huu Rais atazindua programu ya Building a Better Tomorrow – Youth Agribusiness Initiative (BBT-YIA) ambapo katika awamu ya kwanza vijana 812 watapatiwa mafunzo kwa miezi minne bure, kisha watapewa mashamba ambayo tayari yamewekewa mifumo ya umwagiliaji kwa ajili ya kilimo. Ikiwa kati ya Watanzania 10, saba wanajishughulisha na kilimo, na ikiwa vijana ndio nguvu kazi kubwa, uamuzi wa Rais kuwekeza kwa vijana kwenye kilimo utabadili dhana kuwa kilimo hakilipi, kilimo ni cha wazee na changamoto ya ajira ambayo inawakabili vijana duniani kote itapungua nchini. Rais ametoa wito wa sekta binafsi na taasisi za kimataifa kushirikiana na Serikali katika kuwawezesha vijana na wanawake, hasa kuwapatia mitaji ya shughuli za kilimo, uvuvi na ufugaji ili kuwawezesha kufikia malengo binafsi na ya kitaifa. Read More