Mama yukokazini

  • Utayari wa kisiasa wa Rais Samia utakavyoipa Tanzania katiba bora

    Uamuzi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan wa kufufua mchakato wa kuipata Katiba Mpya uliokwama tangu mwaka 2014 umeonesha utayari wa kisiasa wa ofisi hiyo ya juu zaidi nchini kuleta Mabadiliko (Reformation) kama alivyoeleza kwenye msingi wa 4R za uongozi wake. Aidha, kurejeshwa mezani kwa mchakato huo kumethibitisha pamoja na mambo mengine kuwa Rais Samia ni msikivu, na anafanyia kazi maoni anayopokea kwa pendekezo la kufufua mchakato huo lilitolewa na kikosi kazi alichokiunda mwaka jana kwa ajili ya kutathmini hali ya kisiasa nchini. Kama wasemavyo Wahenga kuwa Ukimulika Nyoka Anzia Miguuni Pako, ndivyo Rais alivyofanya kwani Kamati Kuu ya CCM, chama anachokiuongoza, Juni 2022 iliielekeza Serikali kuangalia namna ya kufufua mchakato huo ambapo sasa TZS bilioni 9 zimetengwa kwa ajili ya shughuli hiyo. Utayari wake wa kisiasa umeweza kuufikisha mchakato hadi ulipo sasa ambapo mwanga unaonekana kuelekea kulifikia lengo, huku wadau mbalimbali wakimpongeza kwa kuvuka vikwazo vyote ndani ya Serikali na chama chake kwani amewahi kusema yeye mwenyewe kuwa uamuzi huo si kila mmoja anakubaliana nao. Amepongezwa pia kwa namna anavyoufanya mchakato huo kuwa shirikishi ukihusisha majadiliano ya vyama vyote, wanadau na wananchi kwa ujumla akiamkini kuwa maboresho yanayokwenda kufanyika ni kwa ajili ya manufaa ya Watanzania, hivyo ni lazima washirikishwe. Read More

  • Muda wa kulipa nyumba Magomeni Kota: Badala ya miaka 15, sasa ni miaka 30

    Wakazi 644 wa Magomeni Kota mkoani Dar es Salaam waligoma kusaini mkataba wa kuanza kununua nyumba za eneo hilo kwa madai kwamba bei pamoja na muda wa malipo uliopangwa haukuwa rafiki kwao na wala hauendani na hali zao za kiuchumi ambapo walipaza sauti zao kumuomba Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kuingilia kati suala hilo. Mwenyekiti wa Wakazi hao wa Magomeni Kota, George Abel alisema bei za nyumba hizo ni kubwa, zisizoendana na uwezo wao, hivyo hawawezi kuimudu licha ya Serikali kuzishusha bei ikilinganishwa na hali ya soko. Wakazi hao walipaza sauti wakimuomba Rais Samia kuongezewa muda wa kulipia nyumba hizo kutoka miaka 15 iliyokuwepo awali hadi miaka 30 hali ambayo itapunguza kwa asilimia 100 kiasi ambacho wananchi hao wanapaswa kulipa kila mwezi. Rais Samia Suluhu Hassan, aliye msikivu na anayejali wananchi wote, alipokea maombi hayo na ameyafanyia kazi na sasa wananchi wa Magomeni Kota watalipa nyumba zao kwa kipindi cha miaka 30 kama walivyoomba, muda ambao wakazi wote wa eneo hilo wamekiri kuwa ni rafiki na kila mmoja amekiri ataweza kukamilisha malipo yaliyopunguzwa Ikumbukwe pia Machi 23, 2021, wakati Rais Samia akizindua nyumba hizo aliitaka TBA kupunguza gharama za uuzaji wa nyumba hizo kwani zipo juu kwa wananchi wa kawaida, hivyo pamoja na kupunguzwa bei pia sasa wananchi watalipa nyumba hizo kwa muda mrefu zaidi “Pamoja na kuwa kipato chetu kimekuwa kidogo kwa sababu ya kustaafu lakini, tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kupata unafuu wa nyongeza hii ya muda, kwa sasa naamini sote tunaweza kujitahidi kukamilisha jambo hili (malipo),” alisema Ramadhan Mkenze mkazi wa Magomeni Kota. Read More

  • Rais anayejali: Sasa vipimo vya awali kwa wajawazito kutolewa bure

    Serikali imetangaza kuwa huduma za vipimo vya awali kwa wajawazito ambazo zinahusisha kupima wingi wa damu, mkojo ili kuangalia wingi wa protini, shinikizo la damu pamoja na kusikiliza mapigo ya moyo ya mtoto, zitatolewa bure. Kutolewa bure kwa vipimo hivyo muhimu kutawawezesha wajawazito kujua mwenendo wa ujauzito, kuepuka kifafa cha mimba na vifo vya mama na mtoto ambapo lengo la Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2021/22-2025/26) ni kupunguza vifo vya uzazi kutoka vifo 321 kwa vizazi 100,000, hadi vifo 220 na vifo vya watoto kutoka vifo 51 kwa vizazi hai 1,000 hadi vifo 40. Aidha, hatua hii itaongeza zaidi idadi ya wajawazito wanaohudhuria kliniki pamoja na kujifungulia kwenye vituo vya afya ambapo Serikali imeahidi itahakikisha upatikanaji wa 100% wa dawa za kuzuia kutoka damu wakati wa kujifungua, dawa za kuongeza damu na dawa za kuzuia kifafa cha mimba katika vituo vyote afya vya umma. Hatua hizi ni mwendelezo wa kazi kubwa aliyofanya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu wa kujenga vituo vya afya, kuboresha miundombinu ya afya nchi nzima, kuajiri maelfu ya watumishi wa afya pamoja na kununua vifaa tiba, hivyo kuiarisha huduma za afya vijijini ambapo awali hali ilikuwa ngumu zaidi. Imani juu ya huduma za afya zinazoendelea kutolewa kwenye vituo vya afya imeendelea kuongezeka kwani kwa mujibu wa Utafiti wa Demografia na Afya mwaka 2022, idadi ya wajawazito waliotembelea kliniki walau mara nne kati ya wajawazito 100 imeongezeka kutoka 53 mwaka 2015/16 hadi 65 mwaka 201/22 kati huku wanaojifungua chini ya uangalizi wa mtoa huduma mwenye ujuzi ikiongezeka kutoka 66 hadi 85 katika kipindi hicho. Read More

  • Shangwe la wafanyakazi baada ya nyongeza ya mishahara kutoka kwa Mheshimiwa Rais

    “Wafanyakazi mambo ni moto, mambo ni fire,” ni maneno aliyoyatumia Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kuhitimisha hotuba yake ya Mei Mosi 2023 ambayo ilijaa matumaini kwa maelfu ya watumishi wa umma waliokuwa wameujaza uwanja wa Jamhuri Morogoro wakimsikiliza. Miongoni mwa mengi yaliyowafurahisha watumishi hao ambao wameendelea kushuhudia mabadiliko makubwa kwenye mazingira ya kazi na maslahi yao chini ya Rais Samia ni uamuzi wa Rais kurejesha nyongeza ya mishahara ya kila mwaka, ikiwa ni miaka saba tangu kuondolewa kwa mfumo huo. Itakumbukwa kuwa Mei 2022 Rais Samia aliridhia nyongeza ya mishahara ambapo alipandisha kima cha chini kwa watumishi wa umma kwa asilimia 23.3, ambapo TZS trilioni 1.59 zilitumika kwa ongezeko hilo kwa mwaka wa fedha 2021/2022. Aidha, mbali na kurejesha utaratibu huo, Rais amesema kuwa nyongeza ya posho ambayo ilipandishwa mwaka jana lakini baadhi ya watumishi hawakuanza kuipata kwa sababu bajeti za taasisi zao tayari zilishapitishwa, wataanza kupata fedha hizo mwaka wa fedha ujao. “Tumejiandaa pia kupandisha madaraja, vyeo vitaendelea kupandishwa, kutenganisha makundi na madaraja mserereko wale ambao hawakupata mwaka jana watapata mwaka huu” ameahidi. Pia, alisema Serikali anayoiongoza itaendelea kuwekeza na kuvutia uwekezaji nchini, ili kujenga uchumi na kuzalisha ajira kwa Watanzania na zipatikane fedha za kuboresha maslahi ya watumishi. Read More

  • Umoja wa Mataifa: Tanzania ya tatu kwa kasi kubwa ya ukuaji wa uchumi Afrika

    Licha ya kuwa ukuaji wa bara la Afrika unatarajiwa kushuka kutoka asilimia 4.1 mwaka 2022 hadi asilimia 3.8 mwaka 2023, uchumi wa Tanzania unatarajiwa kukua zaidi huku Umoja wa Mataifa (UN) ukiitaja kuwa ni nchi ya tatu barani Afrika kwa kuwa na kasi kubwa ya ukuaji wa uchumi mwaka 2023. Tanzania ambayo inaendelea kuwa mfano Afrika kwa mageuzi makubwa ya kiuchumi chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, inatarajiwa kushuhudia ukuaji wa uchumi wa asilimia 5.6, ikitanguliwa na Ivory Coast ambayo uchumi wake utakua kwa asilimia 6.5 pamoja na Rwanda itakayoshuhudia ukuaji wa asilimia 7.8. Mafanikio hayo ni matokeo ya mikakati ya Rais Samia ambapo katika miaka miwili ya uongozi wake amesajili miradi ya uwekezaji ya TZS trilioni 17, ambayo imechochea ukuaji wa sekta nyingine pamoja na kutoa fursa za ajira kwa maelfu ya Watanzania. Mikakati hiyo pia imewezesha uchumi kukabiliana na changamoto za dunia kama mfumuko wa bei, gharama kubwa za ukopaji na mabadiliko ya tabianchi. Wakati ripoti ya UN ikionesha hivyo, Benki ya Dunia (WB) imeitaja Tanzania kuwa nchi ya 10 kwa utajiri barani Afrika kwa kwa kuzingatia Pato Ghafi la Taifa (FDP) kwa kuangalia viwango vya sasa vya kubadili fedha. Ukuaji huo mbali na kuendelea kuboresha maisha ya Watanzania lakini pia unawapa imani wawekezaji waliopo na wanaokusudia kuwekeza nchini, kwa kuwafanya waamini Tanzania ni sehemu salama kuwekeza mitaji yao ya mabilioni, hivyo kufanya uchumi kukua zaidi na zaidi. Read More

  • Matunda ya mikakati ya kiuchumi ya Rais Samia yanavyozidi kuonekana

    Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) limetoa takwimu zinazoonesha kuongezeka kwa pato la Taifa la Tanzania kutoka Dola za Marekani Bilioni 69.9 (TZS trilioni 163.5 trilioni) kwa mwaka 2021, wakati ambapo Rais Samia alipoingia madarakani hadi kufikia Dola za Marekani Bilioni 85.42 (TZS trilioni 200) kwa mwaka huu wa 2023, Huu ni ukuaji mkubwa zaidi katika kipindi cha muda mfupi cha uongozi wa awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ambapo ndani ya miaka miwili pato hilo limeongezeka kwa Dola za Marekani Bilioni 16 (TZS trilioni 37.616) ikilinganishwa na ukuaji wa miaka sita ya awamu ya tano ambapo pato hilo lilikua kwa Dola za Marekani Bilioni 12 pekee (TZS trilioni 28.212). Vilevile IMF imeonesha kuwa kwa mwenendo uliopo hadi mwaka 2028 Tanzania kutakuwa na watu milioni 73.36 huku pato la Taifa likitarajiwa kukua hadi dola bilioni 136.09 (TZS trilioni 318.8) na pato la mtu mmoja mmoja likitarajiwa kukua hadi dola 1,860 (TZS milioni 4.3), huku kasi ya ukuaji wa uchumi ikitarajiwa kuwa asilimia 7. Ukuaji huu wa uchumi ni matokeo ya jitihada za makusudi za Mheshimiwa Rais ambapo tangu alipoingia madarakani Machi mwaka 2021, ametekeleza sera rafiki kwa sekta binafsi, ambayo imeongeza kasi ya uwekezaji, biashara na ukuaji wa uchumi nchini huku akifungua fursa za ajira kwa wananchi kote nchini. Kazi hii kubwa ya ukuaji wa uchumi ni utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambayo inaeleza lengo la kukuza kwa Pato la Taifa pamoja na kujenga uchumi wa kisasa, shirikishi na shindani, utakaowezesha ustawi wa wananchi. Read More

  • Miaka miwili ya Mama: Uwekezaji wa trilioni 17 wazalisha maelfu ya ajira

    Katika kipindi cha mwaka 2021 hadi Januari 2023 Serikali imesajili miradi ya uwekezaji 537 yenye thamani ya TZS trilioni 17, ikiwa ni matokeo mazuri katika mkakati wa Mheshimiwa Rais wa kukuza biashara na uwekezaji nchini. Ongezeko la usajili wa miradi hiyo linatarajiwa kutoa ajira takribani 92,770 ikiwa ni kiwango kikubwa zaidi kuwahi kuandikishwa katika kipindi chochote tangu Tanzania ipate uhuru mwaka 1961. Hatua alizochukua Rais Samia kuboresha Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), kuimarisha Kituo cha Huduma za Mahala Pamoja na maboresho ya Sheria ya Uwekezaji Tanzania zimevutia wawekezaji wapya, zimetatua changamoto zilizokuwa zikiwakabilia wafanyabiashara na kuvutia wawekezaji na kurahisisha utoaji huduma. Aidha, Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Mauzo ya Nje (EPZA) imesajili miradi 38 yenye thamani ya TZS bilioni 327.7 na mauzo nje yenye thamani ya TZS bilioni 448.2. Miradi hiyo ni mahsusi katika sekta zinazozalisha bidhaa zitokanazo na kilimo, bidhaa za viwandani, bidhaa za mifugo, bidhaa za kemikali, bidhaa za madini na bidhaa za misitu. Kuendelea kuongezeka kwa uwekezaji nchini kunakuza mzunguko wa fedha nchini, kunajenga imani ya wawekezaji waliopo pamoja na kuvutia uwekezaji zaidi. Read More

  • Mheshimiwa Rais awezesha vijana wajasiriamali kupata mkopo wa bilioni 1.9

    Moja ya ahadi za Chama cha Mapinduzi (CCM) katika ilani ya mwaka 2020-2025 ni kutengeneza ajira zisizopungua milioni 8 katika sekta rasmi na isiyo rasmi kwa ajili ya vijana nchini. Ndani ya muda mfupi Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameendelea kuweka mikakati ya kufikia lengo hilo ambapo anaendelea kutoa ajira rasmi kwenye kada mbalimbali, ameboresha mazingira ya biashara yanayowezesha vijana kujiajiri na kupata ajira kupitia uwekezaji unaosajiliwa nchini pamoja na kuwezesha upatikanaji wa mitaji na mafunzo ya ujasirimali kwa vijana nchini. Kwa kutambua umuhimu mkubwa wa vijana katika maendeleo ikiwa ndio nguvu kazi kubwa, Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana imetoa mikopo ya TZS bilioni 1.88 kwa ajili ya kuwezesha miradi 85 ya vijana katika sekta za kilimo, viwanda na biashara kwenye halmashauri 28. Aidha, Serikali imetoa fursa za mafunzo ya ujuzi wa kujiajiri au kuajiriwa kwa vijana 118,415 katika fani za uanagenzi, uzoefu wa kazi, ufugaji wa samaki na viumbe maji na kilimo cha kisasa kwa njia ya vizimba. Pamoja na hayo, Serikali imefungua fursa zaidi kupitia kilimo, TEHAMA na pia vijana na wajasiriamali wengine wanaofungua biashara mpya wamepewa neema ya miezi sita hadi mwaka mmoja kutokulipa kodi tangu kuanza kwa biashara zao, mpango unaolenga kulea biashara ndogo ili ziweze kukua zaidi. Read More

  • Rais Samia afungua fursa: Mchango wa Diaspora wavuka trilioni 2

    Moja ya mikakati ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan aliyoiweka wazi baada ya kuingia madarakani ni kutoa fursa zaidi kwa Watanzania waishio nje kushiriki katika shughuli za maendeo na kijamii nchini kwa kuweka mazingira yatakayowawezesha kufanya shughuli zao nchini. Mafanikio yameendelea kuonekana ambapo kwa mwaka 2022 pekee diaspora walituma nchini TZS trilioni 2.6, na pia wamewekeza kupitia ununuzi wa nyumba na viwanja wenye thamani ya TZS bilioni 4.4 na ununuzi wa hisa za TZS bilioni 2.5. Ili kupanua ushiriki wa diaspora katika maendeo ya Tanzania Serikali inatarajia kuwa imekamilisha mfumo wa kidigitali wa uandikishaji wa diaspora Juni mwaka huu ili kuwezesha ukusanyaji endelevu wa takwimu zao. Mbali na kutuma fedha na kuwekeza nchini, diaspora pia huchangia ukuaji wa uchumi kwa kutangaza fursa za kiuchumi, biashara, utalii na uwekezaji zinazopatikana nchini. Mchango mwingine ni kuleta mitaji, utaalam na teknolojia ambavyo huchangia katika kukuza uzalishaji wa mazao, bidhaa na huduma mbalimbali zenye tija kiuchumi. Hadi sasa idadi ya diaspora wa Tanzania ni milioni 1.5, idadi ambayo Rais anaamini itakuwa na mchango mkubwa kwenye uchumi ikiwekewa mazingira rafiki. Read More

  • Uchumi wa Tanzania wakua kwa 23% miaka miwili ya Rais Samia

    Ndani ya miaka miwili ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan Pato la Ghafi la Taifa (GDP) limekua kutoka TZS trilioni 163.3 mwaka 2021 hadi TZS trilioni 200, sawa na ukuaji wa asilimia 23. Takwimu hizo za Shirika la Fedha Duniani (IMF) zinadhihirisha matokeo chanya ya mkakati wa Rais wa kuifungua nchi na kukaribisha wafanyabiashara na wawekezaji pamoja na kufufua biashara za ndani ambazo zilikuwa zimefungwa. Kwa ukuaji huo, ni dhahiri kuwa uchumi wa Tanzania sasa ni mkubwa kuliko baadhi ya nchi za Ulaya kama Croatia, Lithunia, Serbia na Slovenia, hatua ambayo imerejesha imani ya wawekezaji kuendelea kuwekeza nchini. Tanzania sasa inashika nafasi ya 6 kati ya nchi 10 za Kusini mwa Jangwa la Sahara zenye uchumi mkubwa zaidi, ikitanguliwa na Nigeria, Afrika Kusini, Ethiopia, Kenya na Angola. Aidha, kwa mujibu wa IMF, uchumi wa Tanzania unatarajiwa kukua kufikia TZS trilioni 318 ifikapo mwaka 2028, ukuaji ambapo utaakisi uwezo wa Serikali kutekeleza miradi ya maendeleo pamoja na huduma za kijamii. Read More