Kitaifa

  • Nishati ya Uhakika ni Uhuru: Mheshimiwa Rais anavyovipa vijiji vya Tanzania Uhuru

    Maendeleo ya Watanzania na maendeleo ya nchi yanategemea sana upatikanaji wa nishati ya uhakika, na kwa kulitambua hilo, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu katika miaka yake miwili ya uongozi ameendelea kuimarisha sekta hiyo ambayo imefungua zaidi fursa za kiuchumi kwa wananchi, ushuhuda wa karibuni ukiwa ni wananchi wa Kigoma walioanza kunufaika na umeme wa gridi ya Taifa ambao ni wa uhakika zaidi kuliko uliokuwa ukizalishwa kwa majenereta. Katika muktadha huo huo wa kuwawezesha wananchi, Serikali imesaini mikataba ya utekelezaji wa miradi mikubwa mitatu ya kupelekea umeme zaidi vijijini kupitia Wakala wa Umeme Vijijini (REA), miradi ambayo itagusa sekta za kilimo, afya, maji, viwanda vidogo na madini. Mradi wa kwanza (Ujazilizi 2B) ambao utafikisha umeme katika vitongoji 1,522 ambao utaunganisha umeme kwa wananchi zaidi ya 88,000. Mradi wa pili unapeleka umeme kwenye migodi na maeneo yenye shughuli za kilimo 336 yaliyopo katika mikoa 25 ya Tanzania Bara. Mradi huu utawapunguzia gharama (fedha na muda) za uchimbaji madini wachimbaji wadogo, utazalisha ajira zaidi, utawawezesha kutumia teknolojia ya kisasa, utachochea ukuaji wa sekta ya madini pamoja na kuongeza mchango wake kwenye Pato la Taifa. Aidha, kwa kufikisha umeme katika maeneo yenye shughuli za kilimo kunaendana na lengo la Serikali la kuifanya Tanzania kuwa kapu la chakula kwa Afrika, kwa kuvutia vijana kufanya kilimo cha kibiashara. Umeme utasaidia katika umwagiliaji na uongezaji thamani wa mazao. Mradi wa tatu unahusisha kupeleka umeme katika vituo vya afya 63 na pampu za maji 333 vijijini katika mikoa 25. Kufika kwa nishati kwenye maeneo hayo kutaboresha utoaji huduma za afya, mathalani nyakati za usiku, kutapunguza vifo vya mama na mtoto, na kuwezesha upatikanaji huduma nyinginezo zinazohitaji umeme. Wakati huo huo, uwepo wa umeme unaosukuma maji katika pampu utahakikisha vijiji vinakuwa na maji ya uhakika, hatua ambayo itakuza usafi na kupambana na magonjwa ya mlipuko, lakini pia itapunguza muda wa… Read More

  • Mheshimiwa Rais amedhamiria kuboresha Taasisi za Haki Jinai nchini. Bonyeza hapa kutuma maoni kwa Tume aliyoiunda

    Kwa muda sasa kumekuwa na malalamiko kuhusu wananchi kutoridhishwa na utekelezaji wa majukumu ya taasisi zinazosimamia haki jinai nchini kuanzia kwenye ukamataji wa mtuhumiwa, upelelezi, utoaji wa dhamana, uendeshaji wa mashtaka, kesi na eneo ambalo aliyehukumiwa anatumikia kifungu chake. Kutokana na hali hiyo Tume ya Kuangalia Jinsi ya Kuboresha Taasisi za Haki Jinai, iliyoundwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan inakualika mwananchi na mdau wa haki kuwasilisha mapendekezo ya namna ya kuboresha taasisi hizo. Kwa maelezo zaidi soma tangazo hili; Read More

  • Mheshimiwa Rais Samia apongezwa kila kona kwa kuongeza ‘boom’ vyuo vikuu

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia ombi la wanafunzi wa elimu ya juu nchini kwa kuongeza fedha za kujikimu kutoka TZS 8,500 HADI TZS 10,000, kauli ambayo iliibua shangwe huku wanafunzi wakiimbia “tuna imani na Samia,” pamoja na kupiga makofi ya furaha. Wakati wanafunzi hao wakishangilia kwa aamuzi huo uliokonga nyoyo zao, Rais Samia amesema ombi lao la wanafunzi wa ngazi ya stashahada na astashahada kupatiwa mikopo litawekewa mipango kwanza. “Kwa kazi tunazozifanya sasa hivi na hali ya bajeti, hili bado hatujafikia huko, kwa hiyo tunalifikiria, tunaliweka kwenye mipango yetu,” amesema Rais Samia huku akieleza amemuagiza waziri wa fedha aangalie uwezekano wa kupata fedha, akifanikiwa atamuongezea nyingine ili wananchi hao wanufaike. Wakati hayo yakiendelea, Rais Samia ameeleza mikakati ambayo Serikali yake inachukua kuwawezesha wahitimu kujiajiri pindi wanapohitimu masomo yao ikiwa ni pamoja na mapitio ya mitaala na kuhimiza elimu na matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano. “Tunataka elimu isiwe chanzo cha changamoto ya ajira, bali itoe suluhisho […] Ndio maana tumejielekeza sana sasa kwenye elimu ya TEHAMA ili vijana muweze kujiajiri wenyewe,” amesema Rais Samia. Wanafunzi wa elimu ya juu wakiwakilishwa na viongozi wao wamemshukuru Rais Samia kwa hatua ambazo ameendelea kuchukua kuboresha elimu ya juu nchini ambapo wameanza kuona matokeo. Read More

  • Usuluhushi wa kihistoria wa Mheshimiwa Rais Samia katika migogoro ya ardhi

    Miongoni mwa sifa nyingi zinazomtambulisha Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na uongozi ni USULUHISHI na UPATANISHI. Sifa hizi mbili zimeonekana katika sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na siasa na kijamii (masuala ya ardhi). Tukiangazia migogoro ya ardhi, katika mwaka 2021/22, asilimia 86 ya migogoro yote ya ardhi iliyopokelewa ilipatiwa ufumbuzi. Miongoni mwa migogoro hiyo ipo iliyoshindikana kwa muda mrefu huku ikigharimu uhai wa baadhi ya wananchi na mali zao na kuleta mifarakano kwenye jamii. Baadhi tu ya migogoro mikubwa aliyoitatua ni pamoja na; Kwanza, ametatua mgogoro wa Bonde la Usangu mkoani Mbeya uliodumu kwa miaka 15 baada ya kumega eneo lenye ukubwa wa hekta 74,000 kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kufanya shughuli za kilimo na ufugaji. Pili, Mgogoro wa Gereza la King’ang’a na Kata ya Kingale juu ya eneo lenye ukubwa wa ekari 7,495.74 mkoani Dodoma ambapo ameamua ekari 3,272.4 zibaki kwa wananchi watumie kwa shughuli za kilimo, mifugo na za kiuchumi na Magereza wachukue zilizobaki. Tatu, aliruhusu kaya 269 zilizokuwa zinaishi kwenye eneo la kilomita za mraba 9.6 ambazo ni sehemu ya Pori la Akiba Swagaswaga kubaki kwenye eneo hilo, na wananchi hao watapatiwa elimu ya uhifadhi. Ili kupunguza migogoro ya ardhi na kuhakikisha haiwi na madhara zaidi Rais Samia ameendelea kuyawezesha mabaraza ya usuluhishi kutoa uamuzi kwa wakati, elimu kwa wananchi inaendelea kutolewa, mamlaka zinaendelea kupima ardhi kwa ajili ya kuanisha matumizi mbalimbali pamoja na kufanya maboresho ya sheria zinazosimamia sekta ya ardhi. Read More

  • Nafasi mpya za ajira Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anaendelea kuongeza nafasi za ajira katika taasisi mbalimbali za Serikali ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi. POST: ASSISTANT LECTURER (ACCOUNTING) – 1 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04  Login to Apply POST: ASSISTANT LECTURER (ENVIRONMENTAL ECONOMICS) – 1 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04  Login to Apply POST: ASSISTANT LECTURER (ENVIRONMENTAL ECONOMICS) – 1 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04  Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT- CLINICAL NUTRITION AND DIETETICS – 5 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04  Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT-NURSING MANAGEMENT AND EDUCATION – 2 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04  Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT -BIOSTATISTICS – 1 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04  Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT -EPIDEMIOLOGY – 1 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04  Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT -PHARMACOLOGY – 1 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04  Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT -PSYCHIATRY – 2 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04  Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT -PARASITOLOGY – 1 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04  Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT (CHINESE LANGUAGE) – 3 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04  Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT- CLINICAL NUTRITION AND DIETETICS – 5 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04  Login to Apply   Read More

  • Historia nyingine chini ya Mheshimiwa Rais Samia, faida ya benki yavunja rekodi ikivuka trilioni 1

    Faida ya benki za kibiashara nchini imeongezeka kwa TZS bilioni 400 mwaka 2022 na kuvuka ukomo wa shilingi trilioni moja kwa mara ya kwanza katika historia ya sekta ya fedha nchini Tanzania. Kwa mujibu wa taarifa za benki ambazo zimetoa taarifa zao za fedha hadi Januari 30 mwaka huu, zinaonesha kuwa zaidi ta TZS trilioni 1.164 zilikusanywa kama faida (net profit) ikiwa ni ongezeko kutoka TZS bilioni 740 zilizokusanywa mwaka 2021. Ongezeko hilo la faida ambalo limeambatana na kupungua kwa mikopo chechefu, kuongezeka kwa kiwango cha fedha kinachowekwa na wateja wa benki pamoja na mikopo kwa wateja kumetokana kuimarika kwa mazingira mazuri ya biashara nchini chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan. Benki hizo zimesema kuwa ongezeko hilo la faida ni ishara kuwa ajenda ya Serikali ya kukuza biashara inafanya vizuri ambayo inatokana na usimamizi mzuri ikiwemo wa kisera ambazo zinatoa nafasi kwa sekta binafsi kukua. Ukuaji huo unatarajiwa kuwa na matokeo chanya kwa wananchi kwani unaongeza uwezo wa benki kupanua huduma za kifedha kuwafikia wananchi wengi zaidi lakini pia kuongeza kiwango cha mikopo kwenda sekta binafsi ambayo ina mchango mkubwa kwa maendeleo na kuzalisha ajira. Read More

  • Mheshimiwa Rais Samia achochea mabadiliko kwenye vyombo vya dola ili kulinda haki za wananchi

    Akiendelea kufanya vizuri kwenye mageuzi ya kiuchumi na kisiasa, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amegeukia sekta ya haki ambapo leo amezindua Tume ya Kuangalia Jinsi ya Kuimarisha Taasisi za Haki Jinai ili kuhakikisha zinatoa haki kwa wananchi wa wakati na kwa misingi ya kisheria. Taasisi ambazo zinakwenda kufanyiwa maboresho ni Jeshi la Polisi, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Jeshi la Magereza pamoja na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Wakati wa mapitio tume hiyo itaangalia masuala mbalimbali kwenye taasisi husika ikiwa ni pamoja na mifumo ya utendaji, mafunzo, mifumo ya ajira, matumizi ya TEHAMA, fikra za kiutendaji na mahusiano kati ya taasisi hizo na raia. Katika maboresho hayo Rais Samia anelenga kukomesha vitendo mbalimbali ambavyo vimekuwa vikilalamikiwa na wananchi ikiwa ni pamoja na mamlaka husika kuwabambikia kesi, kucheleweshwa kwa upelelezi, msongamano mkubwa wa mahabusu magerezani, kupambana na rushwa pamoja na kuimarisha uwezo wa taasisi hizo katika kulinda na kutetea maslahi ya nchi kwa kuhakikisha ajira zinatolewa kwa mujibu wa sheria na kunakuwepo mafunzo ya mara kwa mara. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo amesema “hakuna kitu kibaya duniani kukichepusha kama haki ya mtu,” na hivyo kama ambavyo hakuna atakaye haki yake ipokonywe, vivyo hivyo anatakiwa kuhakikisha hashiriki katika upokonyaji wa haki ya mwingine. Read More

  • Nafasi mpya za Ajira Wizara ya Afya

    Read More

  • Mheshimiwa Rais Samia atatua changamoto zinazozuia vijana kushiriki kwenye kilimo

    Kupitia mpango wa Building a Better Tomorrow (Ujenzi wa Kesho Bora) Serikali imeanzisha mfuko wa dhamana kwa vijana na huduma za mikopo nafuu chini ya Mfuko wa Pembejeo ili kuwavutia kushiriki katika ukuzaji wa uchumi kupitia kilimo. Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania imeamua kuanzisha mpango huo kutokana na idadi kubwa ya vijana na wanawake kukosa sifa zinazohitajika na taasisi za fedha wanapoomba mikopo. Zaidi ya theluthi moja (34%) ya Watanzania wakiwa ni vijana ambao ndio nguvu kazi kubwa, Rais Samia amechukua jukumu la kutatua changamoto zao kwenye kilimo, ili kuongeza tija na kuvutia vijana wengi zaidi, ambapo changamoto zilizotatuliwa ni pamoja na mafunzo, upatikanaji wa ardhi, teknolojia na fedha. Kutokana na mkakati wa Rais Samia wa kufanikisha mapinduzi ya kilimo Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) imetangaza kuipatia Tanzania mkopo wa TZS bilioni 280 kwa ajili ya sekta ya kilimo ikiwemo umwagiliaji na kujenga kituo cha usafirishaji na usambazaji mbolea. Tangu kuanzishwa kwa mpango wa BBT miezi sita iliyopita, tayari imetenga zaidi eka 600,000 nchi nzima na shughuli ya kusafisha mashamba hayo inaendelea. Read More

  • TAKUKURU yatangaza nafasi 320 za kazi kwa vijana. Bonyeza kiungio kutuma maombi

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anaendelea kuongeza ajira katika taasisi za Serikali ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi. Read More