Rais Samia Suluhu Hassan
-
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia ombi la wanafunzi wa elimu ya juu nchini kwa kuongeza fedha za kujikimu kutoka TZS 8,500 HADI TZS 10,000, kauli ambayo iliibua shangwe huku wanafunzi wakiimbia “tuna imani na Samia,” pamoja na kupiga makofi ya furaha. Wakati wanafunzi hao wakishangilia kwa aamuzi huo uliokonga nyoyo zao, Rais Samia amesema ombi lao la wanafunzi wa ngazi ya stashahada na astashahada kupatiwa mikopo litawekewa mipango kwanza. “Kwa kazi tunazozifanya sasa hivi na hali ya bajeti, hili bado hatujafikia huko, kwa hiyo tunalifikiria, tunaliweka kwenye mipango yetu,” amesema Rais Samia huku akieleza amemuagiza waziri wa fedha aangalie uwezekano wa kupata fedha, akifanikiwa atamuongezea nyingine ili wananchi hao wanufaike. Wakati hayo yakiendelea, Rais Samia ameeleza mikakati ambayo Serikali yake inachukua kuwawezesha wahitimu kujiajiri pindi wanapohitimu masomo yao ikiwa ni pamoja na mapitio ya mitaala na kuhimiza elimu na matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano. “Tunataka elimu isiwe chanzo cha changamoto ya ajira, bali itoe suluhisho […] Ndio maana tumejielekeza sana sasa kwenye elimu ya TEHAMA ili vijana muweze kujiajiri wenyewe,” amesema Rais Samia. Wanafunzi wa elimu ya juu wakiwakilishwa na viongozi wao wamemshukuru Rais Samia kwa hatua ambazo ameendelea kuchukua kuboresha elimu ya juu nchini ambapo wameanza kuona matokeo. Read More
-
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anaendelea kuongeza nafasi za ajira katika taasisi mbalimbali za Serikali ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi. POST: ASSISTANT LECTURER (ACCOUNTING) – 1 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04 Login to Apply POST: ASSISTANT LECTURER (ENVIRONMENTAL ECONOMICS) – 1 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04 Login to Apply POST: ASSISTANT LECTURER (ENVIRONMENTAL ECONOMICS) – 1 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04 Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT- CLINICAL NUTRITION AND DIETETICS – 5 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04 Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT-NURSING MANAGEMENT AND EDUCATION – 2 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04 Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT -BIOSTATISTICS – 1 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04 Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT -EPIDEMIOLOGY – 1 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04 Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT -PHARMACOLOGY – 1 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04 Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT -PSYCHIATRY – 2 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04 Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT -PARASITOLOGY – 1 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04 Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT (CHINESE LANGUAGE) – 3 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04 Login to Apply POST: TUTORIAL ASSISTANT- CLINICAL NUTRITION AND DIETETICS – 5 POST Employer: The University of Dodoma (UDOM) More Details 2023-02-04 Login to Apply Read More
-
Akiendelea kufanya vizuri kwenye mageuzi ya kiuchumi na kisiasa, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amegeukia sekta ya haki ambapo leo amezindua Tume ya Kuangalia Jinsi ya Kuimarisha Taasisi za Haki Jinai ili kuhakikisha zinatoa haki kwa wananchi wa wakati na kwa misingi ya kisheria. Taasisi ambazo zinakwenda kufanyiwa maboresho ni Jeshi la Polisi, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Jeshi la Magereza pamoja na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Wakati wa mapitio tume hiyo itaangalia masuala mbalimbali kwenye taasisi husika ikiwa ni pamoja na mifumo ya utendaji, mafunzo, mifumo ya ajira, matumizi ya TEHAMA, fikra za kiutendaji na mahusiano kati ya taasisi hizo na raia. Katika maboresho hayo Rais Samia anelenga kukomesha vitendo mbalimbali ambavyo vimekuwa vikilalamikiwa na wananchi ikiwa ni pamoja na mamlaka husika kuwabambikia kesi, kucheleweshwa kwa upelelezi, msongamano mkubwa wa mahabusu magerezani, kupambana na rushwa pamoja na kuimarisha uwezo wa taasisi hizo katika kulinda na kutetea maslahi ya nchi kwa kuhakikisha ajira zinatolewa kwa mujibu wa sheria na kunakuwepo mafunzo ya mara kwa mara. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo amesema “hakuna kitu kibaya duniani kukichepusha kama haki ya mtu,” na hivyo kama ambavyo hakuna atakaye haki yake ipokonywe, vivyo hivyo anatakiwa kuhakikisha hashiriki katika upokonyaji wa haki ya mwingine. Read More
-
Serikali kupitia mpango wa Building a Better Tomorrow inakusudia kuzalisha ajira milioni 1 kupitia kilimo hadi ifikapo mwaka 2025, ambapo mwamko wa vijana kujiunga na programu hiyo itakayowawezesha kupatiwa elimu, mashamba, pembejeo na masoko umekuwa mkubwa. Akishiriki mkutano wa chakula na kilimo wa wakuu wa nchi za Afrika nchini Senegal, Rais amesema mpango huo wa kuvutia vijana kwenye kilimo ambacho kitakuwa cha kibiashara Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amesema hadi Januari 25, 2023 tayari vijana 7,000 wamesajiliwa kujiunga na programu hiyo, kiwango ambacho kimevuka lengo. “Pia tumekuwa tukifanya kazi na benki kwa ajili ya mikopo kwa vijana na wanawake. Tuliweza kupunguza riba kutoka asilimia 15 hadi asilimia tisa,” amesema Rais akibainisha lengo ni kuifanya Tanzania kuwa mfuko wa chakula cha Afrika kupitia nguvu kazi ya vijana ambao ni asilimia 34.5 ya Watanzania wote. #KilimoBiashara Tanzania ya kesho, ni Tanzania ya kilimo cha kisasa kinachofanywa na vijana, na hivi ndivyo Mheshimiwa Rais Samia Suluhu anavyowezesha vijana. #MamaYukoKazini pic.twitter.com/psP2HkxlxO — Mama yuko Kazini (@mamayukokazini) January 18, 2023 Kupitia mpango huo vijana watapatiwa elimu ya kufanya kilimo cha kibiashara, mashamba yao yatajengewa miundombinu ya umwagiliaji na ghala la kuhifadhi mazao, watapatiwa teknolojia ya kisasa ya uzalishaji, mitaji, pembejeo za kilimo na kuunganishwa na masoko ya mazao yao. Tayari TZS bilioni 3 ambazo zimetengwa kwa ajili ya kufanikisha mpango huo zimeanza kutumika kuwawezesha walengwa lengo likiwa ni kuongeza uzalishaji wa chakula, malighafi, kuzalisha ajira na kubadili fikra na dhana kuwa kilimo hakilipi. Kwa maelezo zaidi namna ya kushirikia katika programu hiyo bonyeza hapa Read More
-
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amesema sekta ya kilimo nchini inatarajiwa kukua kwa asilimia 10 ifikapo mwaka 2030 ikilinganisha na ukuaji wa sasa wa takribani asilimia 3.6. Akizungumza kwenye mdahalo wa ‘Food Action Partnership: Investing in Greater Resilience’ nchini Uswisi amesema Tanzania imetengeneza fursa za kitaifa kwa ajili ya mabadiliko ya mfumo wa chakula unaotarajia kuongeza uzalishaji wa chakula, kuimarisha maisha ya watu na kusaidia kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa. Katika kudhibiti mfumo endelevu wa chakula nchini, Rais Samia amesema jitihada kadhaa zimefanyika, ikiwemo kuanzisha mradi kwa ajili ya vijana huku wakiendelea kuimarisha ukuaji wa shoroba za kilimo pamoja na kuongeza bajeti ya kilimo mara 4 ukilinganisha na ile iliyopita. Serikali ya Tanzania inaendelea kutekeleza miradi na mafunzo mbalimbali ya kilimo kwa vijana ili kuongeza tija kwenye kilimo na kuwezesha vijana kushiriki kwenye uchumi wa Tanzania ambapo lengo ni kuzalisha ajira milioni 1 ifikapo mwaka 2025. Mdahalo huo uliohudhuriwa na zaidi ya viongozi 50 kutoka Afrika, Asia, Ulaya na Marekani mbali na Rais Samia wachangiaji wengine walikuwa Rais Gustavo Petro wa Colombia, Tran Hong Ha, Naibu Waziri Mkuu wa Vietnam na Alvaro Lario, Rais wa Wakfu wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Roma. Read More
-
Kutokana na mageuzi makubwa yanayoendelea kufanyika nchini kwa kuboresha mazingira ya biashara kupitia mabadiliko ya kisheria na kanuni, ujenzi wa miundombinu na uainishaji maeneo muhimu kwa uwekezaji na biashara, uchumi wa Tanzania kwa mwaka 2023 unatarajiwa kukua kwa asilimia 5 kutoka asilimia 4.7 mwaka 2022. Akizungumza na mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa katika sherehe za mwaka mpya kwa mabalozi (Diplomatic Sherry Party), Mheshimiwa Rais Samia Suluhu amesema mwaka 2022 ulikuwa mwaka wa mageuzi ya kisiasa na kiuchumi ambapo kwa kipindi kifupi cha Julai hadi Novemba kilishuhudia ongezeko la asilimia 22 la miradi iliyosajiliwa nchini kwa kipindi hicho kufikia miradi 132 yenye thamani ya TZS trilioni 7 ambayo itatoa ajira 21,297. “Mabadiliko mbalimbali kupitia Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (Blueprint) yamechochea ukuaji wa sekta binafsi na kurejesha nguvu ya soko na kupunguza mwingilio wa serikali katika shughuli za kiuchumi, jambo ambalo limepelekea kuongezeka kwa uwekezaji nchini,” amesema Rais Samia. Mkakati wa Rais Samia wa kuimarisha sekta binafsi ambayo ina mchango mkubwa katika maendeleo ya Taifa kunawezesha kupunguza tatizo la ajira nchini, kwa vijana wengi kujiajiri na kuajiri kupitia sekta hiyo, kwani takribani vijana milioni 1 huingia kwenye soko la ajira nchini kila mwaka, idadi ambayo Serikali pekee haiwezi kuwahudumia. Kupitia ujenzi wa miradi ya kimkakati unaoendelea nchini ikiwemo Bwawa la Umeme la Julius Nyerere (JNHPP), reli ya kisasa, ujenzi na ukarabati wa meli mbalimbali, bomba la mafuta (EACOP) na mradi wa kuchakata gesi asilia mkoani Lindi, anaamini kuwa uchumi wa Tanzania utaendelea kuimarika na kuwanufaisha Watanzania zaidi. Wakati huo huo, amesema ana imani kuwa kila Mtanzania anayo nafasi katika maendeleo na mustakabali wa Tanzania na kuwa wananchi wanahaki na uhuru ambao wanastahili kuufurahia kwa mujibu wa kanuni na sheria zilizopo nchini. Read More
-
Wanafunzi zaidi ya milioni 1 wakianza kidato cha kwanza kwa pamoja leo Januari 9, 2023, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amevuka lengo la ujenzi wa vyumba vya madarasa, ambao umetoa nafasi kwa kila mwenye sifa kuanza masomo kwa wakati. Katika Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2021/22 – 2025/26), Serikali ilikuwa imepanga kujenga vyumba vya madarasa 4,040, ambapo kwa mwaka 2022 pekee Serikali imejenga madarasa 8000, ikiwa ni takribani mara mbili ya lengo. Kwa ujumla katika miaka miwili ya uongozi wa Rais Samia Serikali imejenga madarasa 2,3000 katika ngazi zote za elimu, huku ikikarabati yaliyokuwa yamechakaa pamoja na kujenga shule mpya zikiwemo shule maalum za sayansi za wasichana kila mkoa. Kwa miaka miwili ya uongozi wake, Rais Samia ameweka rekodi iliyowezesha wanafunzi wote wanaoanza kidato cha kwanza kufanya hivyo kwa pamoja, hivyo kuondoa utaratibu wa chaguzi za awamu ya pili au zaidi, ambazo hushuhudia wanafunzi wakichelewa kuanza masomo. Mafanikio haya ni utekelezaji wa dira ya Serikali anayoiongoza ambayo inalenga kuboresha elimu nchini na kuhakikisha kuwa hakuna mwanafunzi anayekosa fursa ya masomo kwa uhaba wa madarasa. Read More
-
Mkakati wa kibiashara wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan unaendelea kuwa na matokeo chanya katika dira ya Serikali ya kukuza uchumi ambapo takwimu za hivi karibuni zinaonesha kuwa thamani ya miradi ya uwekezaji imeongezaka karibu mara tatu ndani ya kipindi cha miezi mitano. Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimetoa taarifa inayoonesha kuwa kimesajili miradi 132 yenye thamani ya TZS trilioni 7 kati ya Julai hadi Novemba mwaka huu ambapo sekta ya viwanda, usafirishaji na utalii ndizo zimeongoza kwa uwekezaji. Usajili huo ni ongezeko la miradi 24 kutoka miradi 108 yenye thamani ya TZS trilioni 2.06 iliyosajiliwa kipindi kama hicho mwaka 2021. Miradi hiyo ambayo imeongezeka kwa idadi na thamani, itatoa ajira 21,297 ambazo ni ongezeko la asilimia 57 kutoka ajira 13,578 za mwaka jana ni matokeo ya Diplomasia ya Uchumi ambayo Rais amekuwa akiitekeleza kwa vitendo. Rais Samia ameendelea kuimarisha mahusiano ya kibiashara ndani ya nchi, kikanda na kimataifa katika ziara mbalimbali anazofanya ambazo huambatana na wafanyabiashara wa ndani ambao hupata fursa ya kuzungumza na wafanyabiashara wa nje, lakini pia huwezesha Tanzania na nchi nyingine kuingia makubaliano ya kibiashara na uwekezaji. Tangu aingie madarakani Rais amefanikiwa kurejesha imani ya wawekezaji ambao sasa wanaamani ya kuja na kuwekeza nchini. Katika muda huo ametatua changamoto mbalimbali za kibiashara kama vile kupunguza muda wa kupata vibali vya uwekezaji, kurekebisha mifumo ya kikodi, kuondoa ukiritimba wa vibali vya kazi na kuwepo kwa maeneo maalum ya uwekezaji. Read More
-
Safari ya miaka 50 ya kuelekea umeme wa kutosha leo imepiga hatua kubwa baada ya Bwawa la Kufua Umeme wa Maji la Julius Nyerere (JNHPP) kuanza kujazwa maji leo zoezi ambalo limezinduliwa la Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan baada ya kufunga mahandaki yaliyokuwa yakichepusha maji ili kupisha ujenzi. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dkt. Samia amesema kuwa mradi huu ambao ujenzi wake ulianza mwaka 2018 ni mojawapo ya miradi mikubwa ya umeme barani Afrika ambapo bwawa hilo litaweza kuhifadhi maji lita bilioni 32, hivyo kuwezesha shughuli za umeme kuendelea pindi mvua zinapopungua. Dkt. Samia amekuwa na mchango mkubwa katika mradi huo ambao utaleta manufaa ya kiuchumi na kijamii, ambapo ndani ya miezi 22 amefanikiwa kujenga asilimia 41.68 ya mradi huo, wakati hapo awali ulijengwa asilimia 37 kwa muda wa miezi 27. Akitaja manufaa mengine ya mradi huo mbali na umeme utakaokizi mahitaji ya ndani na hata kuuzwa nje, amesema kuwa utachochea ukuaji wa sekta ya utalii, kutokana na kuwa katika Hifadhi ya Taifa ya Nyerere, na pia kuwezesha fursa za uvuvi, ambapo bwawa hilo lenye urefu wa kilomita 100 litakapojaa litakuwa na ukubwa kuliko Ziwa Rukwa, hivyo ametaka ufanyike uvuvi wa kisasa. Kuhusu kilimo, amesema mradi huo utafungua fursa za kilimo katika Delta ya Rufiji na hivyo ameiagiza wizara ya kilimo, wizara ya ardhi na TAMISEMI kupima eneo la ekari 400,000 linalofaa kwa kilimo na kufanya mnada wa wazi kwa wawekezaji wa uhakika katika kilimo. “Nawasihi pia, tutenge maeneo maalum kwa ajili ya wakulima wadogo wadogo, hasa wa maeneo haya, yatakayokuwa na miundombinu ya umwagiliaji,” ameagiza. Aidha, katika mradi huo limejengwa daraja la kudumu ambalo linaiunganisha mikoa ya kusini na mikoa ya kati na kaskazini mwa Tanzania, ambapo msafiri ataweza kutoka Mtwara kwenda Dodoma, Arusha au Kilimanjaro bila kupita Dar es Salaam. Pia, kutokana na bwawa hilo kuwa na maji… Read More
-
“Si wakati wakati wote ni wa kupongezana na si wakati wote ni wa kupingana. Kwenye kujenga Tanzania bora natamani kujenga jamii yenye maridhiano na maelewano. Natamani kujenga umoja pasipo kujali tofauti zetu za kisiasa, kidini, kikabila na nyingine zote.” Hayo ni maneno ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika barua yake aliyoitoa Tanzania ikiadhimisha miaka 30 tangu kurejea kwenye mfumo wa vyama vingi, ambapo alieleza azma yake ya kujenga jamii inayopata haki sawa mbele ya sheria, isiyobaguana na inayotoa fursa sawa za kiuchumi kwa wote. Katika kufanikisha nia hiyo, Rais ametimiza kiu ya muda mrefu ya vyama vya upinzani kwanza kwa kukutana na kuzungumza na wanasiasa wa upinzani akiwemo viongozi wa CHADEMA, CUF na ACT-Wazalendo, mazungumzo ambayo yameendelea kujenga imani miongoni mwa viongozi hao kuhusu nia thabiti ya Rais kujenga umoja wa kitaifa. Aidha, katika kutekeleza matakwa na viongozi wa vyama vya upinzani ambayo ni pamoja na kufufuliwa kwa mchakato wa katiba mpya na kuundwa tume huru ya uchaguzi, Rais aliunda kikosi kazi kilichojumuisha wawakilishi kutoka vyama vya upinzani, na tayari kimewasilisha mapendekezo serikali juu ya namna ya kuyafikia matamanio hayo. “Mama Samia amekuwa Rais wa kwanza kwenye nchi yetu baada ya ujio wa pili wa vyama vingi mwaka [19]92 kusimama hadharani, na nilisimama naye Ikulu, tukazungumza na vyombo vya habari mimi na yeye, kwamba tufanye nini kila mmoja […] tuondoe maumivu yaliyopo katika Taifa hili,” alisema Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe Machi 2022. Uamuzi wa Mbowe kusimama kwenye maridhiano umeungwa mkono na viongozi wa CHADEMA ambapo aliyewahi kuwa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi amesema kwa sababu njia za maandamano walizowahi kujaribu huko nyuma hazikufanikiwa, basi, sasa njia ya kuelekea ni maridhiano. Kwa upande wake kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe alisema “hakuna njia yoyote ya kuifanya nchi yetu iweze kwenda mbele isipokuwa njia hii ambayo [Rais Dkt. Samia… Read More