Diaspora Tanzania

  • ZAMA MPYA: Diaspora sasa kushiriki shughuli za kiuchumi na kijamii kidijitali

    Mchango wa Watanzania waishio nje ya nchi na wale wenye asili ya Tanzania katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi umeendelea kukua mwaka hadi mwaka ambapo kwa mwaka 2022 waliwekeza nchini TZS bilioni 2.5 kupitia Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja. Aidha, takwimu za Benki ya Kuu ya Tanzania (BoT) zinaonesha kuwa Diaspora ambao hadi sasa ni milioni 1.5, mwaka 2021 walituma nchini TZS trilioni 1.3, huku kiwango hicho kikiongezeka mara mbili mwaka 2022 kufikia TZS trilioni 2.6. Kutokana na nafasi yao hii jalili katika ustawi wa jamii na maendeleo, Serikali imeandaa mfumo wa kidijitali wa kuwasajili Diaspora wenye asili ya Tanzania (Diaspora Digital Hub) utakaoiwezesha kupata taarifa zao na wao kupata taarifa muhimu kutoka nchini. Mfumo huo wa aina yake utawezesha Serikali kupata taarifa sahihi za Diaspora kama vile jinsia, elimu na utaalamu na kuwawezesha Diaspora kushiriki kidijitali katika shughuli mbalimbali za maendeleo ambapo wataweza kupata huduma za kibenki, hifadhi ya jamii, fursa za uwekezaji, biashara na masoko, masuala ya uhamiaji, vitambulisho vya taifa na huduma nyingine ambazo watazifikia kiurahisi. Diaspora wamekuwa wakichangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi kupitia biashara ya mali zisizohamishika (real estate) ambapo mwaka 2021 walinunua nyumba na viwanja vyenye thamani ya TZS bilioni 2.3 huku mwaka 2022 ununuzi huo ukipanda hadi TZS bilioni 4.4. Read More

  • Rais Samia afungua fursa: Mchango wa Diaspora wavuka trilioni 2

    Moja ya mikakati ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan aliyoiweka wazi baada ya kuingia madarakani ni kutoa fursa zaidi kwa Watanzania waishio nje kushiriki katika shughuli za maendeo na kijamii nchini kwa kuweka mazingira yatakayowawezesha kufanya shughuli zao nchini. Mafanikio yameendelea kuonekana ambapo kwa mwaka 2022 pekee diaspora walituma nchini TZS trilioni 2.6, na pia wamewekeza kupitia ununuzi wa nyumba na viwanja wenye thamani ya TZS bilioni 4.4 na ununuzi wa hisa za TZS bilioni 2.5. Ili kupanua ushiriki wa diaspora katika maendeo ya Tanzania Serikali inatarajia kuwa imekamilisha mfumo wa kidigitali wa uandikishaji wa diaspora Juni mwaka huu ili kuwezesha ukusanyaji endelevu wa takwimu zao. Mbali na kutuma fedha na kuwekeza nchini, diaspora pia huchangia ukuaji wa uchumi kwa kutangaza fursa za kiuchumi, biashara, utalii na uwekezaji zinazopatikana nchini. Mchango mwingine ni kuleta mitaji, utaalam na teknolojia ambavyo huchangia katika kukuza uzalishaji wa mazao, bidhaa na huduma mbalimbali zenye tija kiuchumi. Hadi sasa idadi ya diaspora wa Tanzania ni milioni 1.5, idadi ambayo Rais anaamini itakuwa na mchango mkubwa kwenye uchumi ikiwekewa mazingira rafiki. Read More