Kitaifa

  • #MiakaMiwiliYaMama: Ajira za moja kwa moja Watanzania zaidi ya 85,000

    Mkakati wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan wa kuboresha mazingira ya biashara nchini na kuvutia uwakezaji umezaa matunda ambapo takwimu kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) zinaonesha kuwa thamani ya uwekezaji nchini umekua kwa asilimia 173. Ripoti ya TIC inaonesha kuwa thamani ya uwekezaji imepanda kufikia TZS trilioni 19.87 katika miaka miwili ya Serikali ya awamu ya sita, kutoka TZS trilioni 7.27 iliyorekodiwa katika miaka miwili kabla hajaingia madarakani. Ongezeko hilo ni matokeo ya kazi kubwa ya Rais ya kurejesha imani ya wawekezaji ndani na nje ya nchi ambao amekuwa akikutana katika ziara zake nje ya nchi na ndani ya nchi ambapo pamoja na kutangaza fursa za uwekezaji, pia alizipatia ufumbuzi changamoto zilizowakabili. Kati ya Machi 2021 na Februari 2023 idadi ya miradi iliyosajiliwa imeongezeka kutoka 455 hadi 575, ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 26. Kati ya miradi hiyo, asilimia 32 inamilikiwa na Watanzania, asilimia 42 ni ya wageni na asilimi 27 ni ubia kati ya wageni na wazawa. Kutokana na uwekezaji huo, idadi ya ajira zilizozalishwa kwa Watanzania zimeongezeka kutoka 61,900 hadi 87,187, uwekezaji mkubwa ukiwa kwenye sekta za viwanda, ujenzi wa majengo ya kibiashara na usafirishaji. Mafanikio haya yamehusishwa pia na Tanzania kushiriki katika mikutano ya kimataifa. Read More

  • #MiakaMiwiliYaMama: Amewajengea vijana uwezo wa kujiajiri kupitia kilimo

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anadhihirisha kwa vitendo kauli yake aliyotoa kuwa hataki kuingia katika historia ya kuwa mmoja wa wanaowalaumu vijana kuwa hawajiajiri, badala yake anawawekea mazingira wezeshi ya kujiajiri kupitia kilimo ambapo lengo ni kuzalisha ajira milioni 3, kipaumbele kikiwa vijana na wanawake. Machi 20 mwaka huu amezindua mashamba ya pamoja (Block Farms) zaidi ya ekari 12,000 ambazo zitagawawiwa kwa vijana, kila mmoja kwa ukubwa usiozidi ekari 10, pia alizindua ndege zisizo na rubani, mashine za umwagiliaji na magari kwa ajili ya maafisa wa wilaya ili kuhakikisha vijana popote walipo nchini wanapata usaidizi wa kitaalamu katika kufanya kilimo cha kibiashara. Katika azma ya kukifanya kilimo kuwa cha vijana, ameahidi kuendelea kutenga bajeti mahsusi kwa ajili ya watendaji kwenye sekta ya kilimo ili shughuli zote zifanyike kwa usasa kuanzia uzalishaji hadi uuzaji mazao na bidhaa. “Tunasema ni kilimo cha vijana, hivyo vijana wawepo shambani, wawepo kwenye utaalamu, wawepo kwenye kuendesha mitambao, sehemu zote kuwa na vijana wanaokwenda kwenye sekta ya kilimo,” amesema akizindua programu ya Building a Better Tomorrow. Katika miaka miwili ya uongozi wake, kilimo ni moja tu ya njia anazotumia kumwinua kijana wa Kitanzania na kukabiliana na changamoto ya ajira inayoisumbua dunia. Ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi katika kila wilaya, mikopo ya halmashauri, kuboresha mazingira ya biashara hasa kwa wajasiriamali ni maeneo mengine ambayo yametoa ajira kwa vijana wengi. Read More

  • #MiakaMiwiliYaMama: Fursa zaidi kwa vijana, sasa Serikali kuwapatia pembejeo za kilimo

    Katika moja ya hotuba zake kwa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere alieleza umuhimu wa kubadili mfumo wa kilimo nchini akisema kuwa kilimo cha kutegemea mvua, kisicho na mbolea, dawa na maarifa, hakitusaidii sana. Anayoyafanya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Kupitia Mfuko wa Pembejeo za Kilimo (AGITF) ni kuyaishi maono ya Mwalimu Nyerere kwani anakuza kilimo kwa kuwapatia vijana pembejeo (dawa, mbegu bora, viuatilifu), ili kubadili kilimo na kufikia lengo la kumnufaisha mkulima, kukuza mchango wake kwenye uchumi, kuongeza uzalishaji wa chakula na malighafi za viwandani. Kama hilo halitoshi, Machi 20 mwaka huu Rais atazindua programu ya Building a Better Tomorrow – Youth Agribusiness Initiative (BBT-YIA) ambapo katika awamu ya kwanza vijana 812 watapatiwa mafunzo kwa miezi minne bure, kisha watapewa mashamba ambayo tayari yamewekewa mifumo ya umwagiliaji kwa ajili ya kilimo. Ikiwa kati ya Watanzania 10, saba wanajishughulisha na kilimo, na ikiwa vijana ndio nguvu kazi kubwa, uamuzi wa Rais kuwekeza kwa vijana kwenye kilimo utabadili dhana kuwa kilimo hakilipi, kilimo ni cha wazee na changamoto ya ajira ambayo inawakabili vijana duniani kote itapungua nchini. Rais ametoa wito wa sekta binafsi na taasisi za kimataifa kushirikiana na Serikali katika kuwawezesha vijana na wanawake, hasa kuwapatia mitaji ya shughuli za kilimo, uvuvi na ufugaji ili kuwawezesha kufikia malengo binafsi na ya kitaifa. Read More

  • #MiakaMiwiliYaMama na Diplomasia ya Uchumi: Shilingi ya Tanzania kutumika kununua bidhaa nchini India

    Azma ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu kuimarisha diplomasia ya uchumi na kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji inazaa matunda ambapo Tanzania na India zimefikia makubaliano ya kibiashara ambayo yatawezesha wafanyabiashara kutoka pande zote kutumia fedha zao (shilingi na rupia) katika kufanya miamala ya kibiashara. Nafasi hii itarahisisha biashara ambapo India ni moja ya washirika wakubwa wa kibiashara na Tanzania ambapo thamani ya biashara kati ya nchi hizi ni TZS trilioni 10.4 katika mwaka ulioishia Machi 2022. Takwimu zinaonesha kuwa katika mwaka wa kwanza wa Rais Samia, India iliingiza nchini bidhaa zenye thamani ya TZS trilioni 5.3, huku ikipokea bidhaa za TZS trilioni 5.1 kutoka Tanzania. Utaratibu huu mpya si tu utakuza biashara kati ya mataifa haya kufikia lengo la zaidi ya TZS trilioni 13.8 mwaka huu, bali pia utaziwezesha kutunza akiba ya fedha za kigeni ambao sasa hazitahitajika kufanya miamala. Watanzania wanaofanya kazi katika sekta za kilimo na madini watanufaika zaidi kutokana na sekta hizo kuingiza bidhaa zaidi nchini India. Kwa mujibu wa wachumi na wataalamu wa biashara, uamuzi huo pia utaimarisha utabirikaji wa viwango vya ubadilishaji wa fedha za kigeni jambo ambalo ni la muhimu sana katika biashara za kimataifa kwani ina usimamizi wa fedha yake tofauti na awali ilipokuwa ikitumia dola za Marekani. Read More

  • Miaka Miwili: Mheshimiwa Rais alivyoiimarisha sekta ya sanaa na kuzalisha ajira kwa vijana

    Machi 2023 Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anatimiza miaka miwili tangu achukue usukani wa kuiongoza Tanzania. Watanzania wakitazama nyuma wanaona kuwa amefanya mambo mengi makubwa, ambayo yameboresha taswira ya nchi kikanda na kimataifa pamoja na kuchochea maendeleo ya Mtanzania mmoja mmoja. Sekta ya sanaa haikuwa mbali kufikiwa na mafanikio haya, ambapo kwa sasa wasanii wana mengi ya kuelekeza kwa namna walivyoshikwa mkono. Haya ni baadhi ya mengi aliyoyafanya; Kuwa Mwigizaji namba moja wa filamu Filamu ya kutangaza utalii nchini, Tanzania: The Royal Tour ilikuwa ishara ya kwanza kwa wasanii juu ya namna Rais anavyoitazama kwa umuhimu tasnia ya filamu, na hivyo kuwapa hamasa kubwa wasanii. Tuzo za Muziki Machi 2022 tuzo za muziki zilirejeshwa nchini ikiwa ni miaka sita tangu mara ya mwisho zilipotolewa na sasa zinasimamiwa na Serikali inayoongozwa na Rais Samia. Kurejeshwa kwa tuzo hizo kumewapa hamasa wasanii kufanya kazi bora zaidi za sanaa na kuonesha kuwa Serikali inatambua jitihada zao. Tuzo za Filamu Tangu Rais Samia aingie madarakani, tuzo za filamu zimetolewa mara mbili, utaratibu ambao awali haukuwepo, huku Watanzania wakiziona katika nchi nyingine. Mwaka 2021 tuzo zilitolewa jijini Mbeya na mwaka 2022 zilitolewa jijini Arusha, na hivyo kuongeza motisha kwa wasanii kufanya kazi bora kuanzia uandaaji, picha na maudhui. Mirabaha Ombi la miaka mingi la wasanii lilipata majibu ndani ya mwaka mmoja wa Rais Samia ambapo walilipwa fedha kutokana na kazi zao kutumika katika kipindi cha Julai hadi Desemba mwaka jana ambapo TZS milioni 312 zilitolewa. Mikopo kwa Wasanii TZS bilioni 2.5 zilizotengwa kwa ajili ya wasanii kupitia Mfuko wa Utamaduni na Sanaa zinawawezesha wasanii kuboresha kazi zao na kutoa fursa za ajira kwa vijana zaidi. Rais Samia alifufua mfuko huo ambao uliacha kufanya kazi tangu mwaka 2013, na tayari wasanii wamepewa mikopo ya hadi TZS milioni 40. Tanzania Mwenyeji mashindano ya kimataifa Mashindano ya urembo… Read More

  • Miaka miwili ya Mheshimiwa Rais inavyonufaisha vijana na wanawake kwa mitaji

    Msemo wa Wahenga kuwa Mgaagaa na upwa hali wali mkavu umejirihirisha kwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na manufaa lukuki yanayowafaidisha Watanzania kutokana na safari za nje ya nchi ambapo manufaa hayo awamu hii yanagusa zaidi wanawake na vijana. Ziara zake zimewezesha wafanyabiashara kutoka Ulaya kuja nchini wiki iliyopita ambapo kupitia Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (EIB) walitoa mikopo yenye masharti nafuu ya TZS trilioni 1.4 kwenye benki za CRDB, NBC na KCB ambayo itawanufaisha wajasiriamali, pamoja na TZS bilioni 318 kutoka Benki ya Maendeleo ya Ujasiriamali ya Uholanzi (FMO) na Taasisi ya Ufaransa ya Kufadhili Maendeleo (PROPARCO). Nusu ya fedha za EIB, TZS bilioni 700 zitatumika kukuza biashara za wajasiriamali ambapo TZS bilioni 421 zitaelekezwa kufanikisha miradi na biashara zinazoendeshwa na kusimamiwa na wanawake na TZS bilioni 248 zitatumika kwenye miradi iliyopo kwenye uchumi wa bahari. Kupitia mikopo hiyo, benki za ndani zitakuwa na uwezo wa kutoa mikopo kwa wanawake na wajasiriamali wengi zaidi ambao changamoto ya mitaji imekuwa kubwa kwao. Tukio hili moja ni ushuhuda namna kila safari ambayo Mheshimiwa Rais anafanya nje ya nchi imeleta fursa zaidi za kibiashara na kuvutia wawekezaji nchini. Read More

  • Una miaka kati ya 15 hadi 35? Bofya hapa kuona fursa kutoka Serikalini

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anafungua fursa zaidi za mafunzo ya ufundi ikiwa ni moja ya njia za kukabiliana na changamoto ya ajira nchini hasa kwa vijana na wanawake. Hapa chini ni tangazo la fursa za mafunzo kwa vijana wenye umri kati ya miaka 15 hadi 35 ambayo yanatolewa bure na Serikali katika vyuo 28 nchini. Hapa chini ni fomu ya kutuma maombi; Read More

  • Miaka Miwili: Mageuzi (Reforms) ya Mheshimiwa Rais Samia yanavyoimarisha biashara nchini

    Ikiwa mageuzi (reforms) ni moja ya nguzo nne (4Rs) za uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, ndani ya kipindi kifupi amefanya mageuzi makubwa kwa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji, hatua ambayo imefufua biashara na kuvutia uwekezaji ndani na nje ya nchi. Mageuzi hayo yaliyofanyika, Rais amelenga kuimarisha taasisi na kuhakikisha sera, sheria, na kanuni zinazosimamia biashara na uwekezaji zinatabirika, lakini pia zinachochea uwazi, zinaondoa ukiritimba na changamoto nyingine ambazo zimekuwa zikikwamisha ustawi wa biashara nchini. Mafanikio makubwa yamepatikana katika mageuzi hayo ambayo ni pamoja na kufuta kodi na tozo zaidi ya 230 ambazo ziliathiri ukuaji wa biashara. Aidha, Tanzania imeimarisha ushirikiano na mataifa mengine katika masuala ya kikodi ambapo tayari imetia saini makubaliano na nchi 10 kuondoa utoaji kodi mara mbili na kuzuia ukwepaji kodi, moja ya nchi hizo ni Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE). Zaidi ya hapo mageuzi yamefanyika katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji na usimamizi wa mapato ikiwa ni pamoja na kuhakikisha shughuli za ukadiriaji kodi zinafanyika kwa haki, kuhakiksha ritani za kodi zinafanyika kwa wakati, kutumia mifumo ya kodi ya kidijitali ikiwa ni pamoja na dirisha la mtandaoni linalowawezesha wateja kujihudumia na dirisha la pamoja la kielektroniki linalorahisisha ufanyaji wa miamala. Pia, Serikali imefanya mabadiliko Sheria ya Rufaa za Kodi, Sura ya 408 na kujumuisha njia mbadala ya usuluhishi wa migogoro na hivyo kupunguza mlolongo mrefu katika kushughulikia rufaa za kikodi. Katika muktadha huo huo, Rais Samia amefanikisha upatikanaji wa sheria mpya ya uwekezaji (Sheria ya Uwekezaji Tanzania ya Mwaka 2022) ambayo imeiondoa Sheria ya Uwekezaji Tanzania ya Mwaka 1997. Sheria mpya imeweka mazingira bora zaidi ya biashara ikipunguza muda wa kupata leseni kutoka siku 14 za kazi hadi siku 7 za kazi na pia kutoa nafasi usuluhishi wa migogoro kwenye taasisi za kimataifa. Kutokana na ukweli kuwa mazingira ya biashara yatafanikiwa kukiwa na… Read More

  • Fursa za ajira mpya kwa vijana kutoka Shirika la Posta Tanzania

    Read More

  • Changamkia nafasi mpya za ajira IFM, WCF, JKCI na KCMC

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anaendelea kuongeza nafasi za ajira katika taasisi mbalimbali za Serikali ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi. POST: ASSISTANT LECTURER – IN ACCOUNTING – 1 POST Employer: Institute Of Finance Management (IFM) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: COMPLIANCE OFFICER – 11 POST Employer: Workers Compensation Fund (WCF) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: ASSISTANT LECTURER – IN ACCOUNTING – 1 POST Employer: Institute Of Finance Management (IFM) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: ASSISTANT LECTURER – IN ACTUARIAL STUDIES/SCIENCE – 1 POST Employer: Institute Of Finance Management (IFM) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: ASSISTANT LECTURER – IN BANKING – 3 POST Employer: Institute Of Finance Management (IFM) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: COMPLIANCE OFFICER – 11 POST Employer: Workers Compensation Fund (WCF) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: TECHNICIAN II (ELECTRICAL)(RE-ADVERTISED) – 1 POST Employer: Kilimanjaro Christian Medical Centre(KCMC) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: COMPLIANCE OFFICER – 11 POST Employer: Workers Compensation Fund (WCF) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: MEDICAL SPECIALIST II (RE-ADVERTISED) – 6 POST Employer: Jakaya Kikwete Cardiac Institute (JKCI) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: TECHNOLOGIST II (DENTAL)(RE-ADVERTISED) – 1 POST Employer: Kilimanjaro Christian Medical Centre(KCMC) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: TECHNOLOGIST II (PHARMACY)(RE-ADVERTISED) – 1 POST Employer: Kilimanjaro Christian Medical Centre(KCMC) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: ASSISTANT NURSING OFFICER I(RE-ADVERTISED) – 3 POST Employer: Kilimanjaro Christian Medical Centre(KCMC) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: MEDICAL SPECIALIST II (RE-ADVERTISED) – 4 POST Employer: The Benjamin Mkapa Hospital More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: COMPLIANCE OFFICER – 11 POST Employer: Workers Compensation Fund (WCF) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: ASSISTANT LECTURER – IN PROGRAMMING – 1 POST Employer: Institute Of Finance Management (IFM) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: ICT OFFICER (COMPUTER SYSTEMS PROGRAMMER) – 4 POST Employer: Workers Compensation Fund (WCF) More Details 2023-02-19  Login to Apply POST: COMPLIANCE OFFICER – 11 POST… Read More