Mama yukokazini

  • Royal Tour Imejibu: Utalii waongoza katika kuingiza fedha za kigeni

    Kazi kubwa aliyoifanya na inayoendelea kufanywa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza fursa za utalii unaweza kusema ‘imejibu’ baada ya sekta hiyo kuendelea kuimarika na kupita madini ya dhahabu katika kuiingizia nchi fedha za kigeni, ikiwa ni kwa mara ya kwanza ndani ya miaka minne tangu ilipoanza kushuka. Mlipuko wa janga la kidunia la Ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO) mwaka 2019 kuliiathiri sekta hiyo ambapo mchango wake kwenye fedha za kigeni ulishuka kutoka dola za kimarekani bilioni 2.52 (TZS trilioni 6.3) mwishoni mwa mwaka 2019 hadi dola za Kimarekani bilioni 1 (TZS trilioni 2.5) mwishoni mwa mwaka 2020, na hivyo kupelekea dhahabu iliyoingiaza dola za Kimarekani bilioni 2.9 (TZS trilioni 7.2) kuongoza. Kuhakikisha sekta ya utalii ambayo inatoa ajira zaidi ya milioni 1.6, inachangia asilimia 25 ya fedha za kigeni na asilimia 21 ya Pato la Taifa inaimarika, Mheshimiwa Rais Samia alichukua jukumu la kurekodi filamu ya Tanzania: The Royal Tour ambayo ilizinduliwa nchini Marekani na hivyo kuiwezesha nchi kutangaza fursa za utalii na vivutio vya utalii kwa mamilioni ya watu dunia, hatua ambayo imepelea kuendelea kuongezeka kwa watalii kutoka ndani na nje ya nchi. Matokeo yameendelea kuonekana ambapo takwimu za Benki Kuu ya Tanzania zinaonesha kuwa mapato yatokanayo na utalii yamepanda kufikia dola za Kimarekani bilioni 2.999 (TZS trilioni 7.5) katika mwaka ulioishia Julai 2023 kutoka dola za Kimarekani bilioni 1.95 (TZS trilioni 4.8) mwaka ulioishia Julai 2022, huku mapato ya dhahabu kwa mwaka ulioishia Julai 2023 yakiwa dola za Kimarekani bilioni 2.9 (TZS trilioni 7.3). Mafanikio hayo yametokana na kuendeleo kuongezeka kwa watalii kutoka nje ya nchi ambapo ripoti ya BoT inaonesha kuwa watalii wameongezeka kwa asilimia 37.2 kufikia 1,658,043 katika mwaka huo, idadi ambayo haijawahi kufikiwa kabla. Licha ya mafanikio haya, Mheshimiwa Rais Samia anaendelea kutangaza utalii ili kufikia lengo la watalii milioni 5 ifikapo… Read More

  • Mheshimiwa Rais azipatia ufumbuzi changamoto kubwa nne za wananchi Mtwara

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan leo Septemba 17, 2023 amemaliza ziara yake siku nne mkoani Mtwara, ziara ambayo imekuwa na mafanikio makubwa ikiendelea kuifungua Mtwara kuwa kitovu cha biashara kwa ajili ya Kanda ya Kusini pamoja na nchi jirani za Msumbiji, Malawi na Comoro. Wakati wote wa ziara hiyo Mheshimiwa Rais alikagua na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuzungumzia na wananchi, ambapo walieleza changamoto kubwa nne ambazo ni suala la maji, umeme, bei za mazao pamoja na miundombinu ya usafiri na usafirishaji. Katika mkutano wake wa mwisho wilayani Masasi, ameeleza mkakati wa Serikali kutatua changamoto hizo ambazo kwa upande wa maji amesema kuwa kwa sasa mkoani Mtwara kuna miradi 66 inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali ambayo inanufaisha vijiji 190, hivyo kufanya jumla ya vijiji vyenye majisafi na salama kufikia 650 kati ya vijiji takribani 750. Aidha, amesema Serikali inaendelea na uchimbaji wa visima, ikiwemo wilayani Liwale ambapo mitambo ya kuchimba visima ilianza kazi saa 24 baada ya Rais kumtaka waziri wa maji kuhakikisha changamoto ya wananchi hao inatatuliwa. Kuhusu changamoto ya umeme, Mheshimiwa Rais amewaahidi wakazi wa mkoa huo baada ya miezi 18 changamoto hiyo itakuwa imekwisha kwa sababu miradi miwili mikubwa inatekeleza. Mradi wa kwanza ni wa kuunganisha Masasi kwenye gridi ya Taifa kwa kutoa umeme mkoani Ruvuma, na mradi wa pili ni kutoa umeme wilayani Ruangwa. Aidha, kwa upande wa bei za mazao, amesema mkakati wa Serikali umewezesha mazao ya ufuta na mbaazi kupata bei nzuri msimu huu na kwamba anaamini korosho nayo itauzwa kwa bei nzuri. Hata hivyo, amewahakikishia wananchi kuwa miaka miwili ijayo korosho yote utabanguliwa nchi kabla ya kusafirishwa, mkakati ambao utawanufaisha wakulima zaidi kwa kupandisha thamani zao hilo pamoja na ajira kwenye kongani ya viwanda ambayo itajengwa katika Kijiji cha Maranje wilayani Nanyumbu. Mageuzi makubwa yanaendelea kwenye upande wa miundombinu ambapo sambamba na… Read More

  • Mheshimiwa Rais Samia atoa mwelekeo mchakato wa katiba mpya

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amesema anatambua umuhimu wa katiba mpya kama ambavyo maoni ya makundi mbalimbali, ikiwemo kikosi kazi, yaliyotolewa na kusisitiza kuendelezwa kwa mchakato huo ambao ulikwama tangu mwaka 2014. Licha wa umuhimu huo ametahadhari kuwa upatikanaji wa katiba mpya ni mchakato na kwamba mchakato huo sio mali ya wanasiasa bali ni ya Watanzania wote, hivyo amewataka wanasiasa kutokuhodhi sauti kwenye mchakato huu. “Katiba ni ya Watanzania, awe ana chama, awe hana, awe ana dini, awe hana, awe mrefu, awe mfupi, mnene, mwembamba, mkubwa, mdogo. Kwa hiyo matengenezo yake yanahitaji tafakuri kubwa sana,” amesema Mheshimiwa Rais. Hata hivyo, amesema kuwa katiba si kitabu, bali ni misingi ya maadili, itikadi na namna ambavyo Watanzania wanakubaliana kuendesha Taifa lao, hivyo, makubaliano hayo yanaandikwa, hivyo, haiwezi kuwa sawa na nchi nyingine. “Tunaanza na elimu Watanzania wajue [katiba] ni kitu gani […] Kwa hiyo tusiwaburuze wananchi. Katiba viongozi wa kisiasa si mali yetu, ni mali ya Watanzania. Tunachokitaka kwenu ni maoni katiba iweje,” ameongeza. Aidha, ameongeza demokrasia lazima iakisi namna watu ndani ya nchi yanavyoendesha masuala yao ikiwemo tamaduni, maadili, mila, desturi, na kwamba huwezi kuchukua demokrasia kutoka nchi nyingine na kuiingiza nchini bila kuzingatia masuala ya ndani. Read More

  • Rais Samia anavyotumia Diplomasi ya Uchumi kuchochea maendeleo nchini

    Tanzania imeendelea kutekeleza sera yake ya Diplomasia ya Uchumi inayolenga kujenga na kuimarisha uhusiano wake wa kimataifa na kujenga mahusiano ya kibiashara na kiuchumi na taasisi pamoja na mataifa mengine ili kuchochea maendeleo. Historia nyingine imeandika baada ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kushiriki na kuhutubia katika Mkutano wa 15 wa BRICS (Brazil, Russia, India, China, South Africa) ambalo ni jukwaa la nchi ambazo uchumi wake unakua kwa kasi duniani ambapo pato la Taifa la mataifa hayo ni quadrilioni TZS 63.3, ambapo pia kutokana na kupokea wanachama wapya sita, kuanzia Januari 2024 nchi sita kati ya tisa zinazozalisha mafuta zaidi duniani zitakuwa mwanachama wa jukwaa hilo. Kwa kushiriki kwenye mkutano huo, Tanzania itapata manufaa makubwa kiuchumi na kibiashara kwani kunaiwezesha kujenga mahusiano ya kiuchumi na biashara na nchi hizo zenye nguvu hatua inayoweza kufungua fursa mpya au kupanua fursa zilizopo za kuuza bidhaa za Tanzania kwenye masoko ya nchi hizo, na hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi. Ni wazi pia kuwa mataifa ya BRICS yamepiga hatua kwenye teknolojia, hivyo Tanzania inaweza kujifunza matumizi bora ya teknolojia katika kurahisisha utoaji huduma na kuchochea maendeleo. China ambayo ni mwanachama wa BRICS ni mshirika mkubwa maendeleo wa Tanzania ambapo kwa miezi saba ya mwaka 2023 imeongoza kwa uwezekaji (Foreign Direct Investment) nchini ikiwekeza mtaji wa zaidi ta TZS trilioni 1.2 ambao pamoja na mambo mengi utazalisha ajira kwa maelfu ya Watanzania. Katika mkutano huo Rais Samia alipata nafasi ya kuzungumza na Rais wa China, Xi Jinping, ikiwa ni mara nyingine kwa viongozi hao kukutana baada ya ziara ya Rais Samia nchini China. Mazungumzo hayo huenda yakaongeza uwezekano wa kufadhili miradi muhimu kama miundombinu, nishati, kilimo, na teknolojia, uwekezaji pamoja ushirikiano wa kiusalama. Katika dunia ya sasa, nchi haiwezi kujitenga kama kisiwa, inailazimu kutoka, kukutana na kushirikiana na mataifa mengine ili kufanikisha masuala mbalimbali… Read More

  • Mheshimiwa Rais aanzisha mageuzi yatakayoleta ufanisi kwenye mashirika ya umma

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameianzisha safari itakayoshuhudia mageuzi makubwa ya mashirika ya umma, taasisi na wakala za Serikali ikiwa ni utekelezaji wa maono ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere pamoja na kuziwezesha taasisi hizo kujiendesha kwa tija na ufanisi ili kupunguza utegemezo kutoka Serikalini. Mageuzi hayo yametokana na uhalisia kuwa licha ya wingi wa mashirika na wakala hizo (248) ambazo Serikali imewekeza mtaji wa TZS trilioni 73, bado mchango wake kwenye uchumi ni mdogo sana, kwani kwa sasa taasisi hizo zinachangia asilimia 3 tu kwenye bajeti ya Serikali, huku nyingi zikitegemea ruzuku ili kujiendesha. Mheshimiwa Rais ameeleza kuwa maono ya Mwalimu Nyerere kuanzisha mashirika ya umma alitaka yamilikiwe na wananchi wenyewe kupitia hisa na kwamba wananchi washirikishwe kwenye masuala ya mashirika hayo, na hivyo ameagiza hatua zichukuliwe ili kurudi kwenye msingi huo. “Kwa kuwa kwa sasa wapo wananchi wenye uwezo wa kununua hisa, hata kama ni kidogo kidogo, nadhani turejee kwenye mwelekeo huo,” ameagiza. Ili kufikia malengo hayo, Mheshimiwa Rais ameridhia mabadiliko mbalimbali ambayo ni pamoja na kutoa uhuru kwa taasisi kujiendesha katika mambo ya msingi, kufanya maboresho katika taratibu za ajira kwa watumishi wao na katika sheria ya ununuzi wa umma, na kuongeza kusiwepo kwa kuingiliwa kisiasa kwenye utendaji wa taasisi hizi. Pia, Serikali ipo kwenye mchakato wa kutunga sheria itakayobadili hadhi ya Ofisi ya Msajili wa Hazina kuwa Mamlaka ya Uwekezaji wa Umma, na kuangalia uwezekano wa kuanzishwa kwa Mfuko wa Uwekezaji wa Umma ili kuondoa utegemezi kutoka mfuko mkuu wa Serikali. Kutokana na uchunguzi uliobaini uwepo wa taasisi ambazo majukumu yake yanashabihiana au hayana umuhimu kwa sasa na zile ambazo zinalega lega Serikali itaziunganisha au kutatua changamoto zao ziwezeshe kujiendesha kwani mashirika hayo ni muhimu kwa uchumi zikiwa zinatoa asilimia 17 ya ajira zote nchini. Amewatoa hofu watumishi kuwa mabadiliko yatakayofanyika hayataathiri ajira zao… Read More

  • Mageuzi ya Mheshimiwa Rais yanayoongeza ufanisi wa mashirika ya umma

    Katika kutelekeza maelekezo ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha kuwa mashirika na taasisi nyingine za Serikali au zile ambazo Serikali ina hisa nyingi zinajiendesha kwa faida, Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechua ameainisha hatua tano za kimkakati ambazo zitachochea mabadiliko katika ufanisi wa taasisi hizo. Kwanza amesema ni kujenga utamaduni wa kukutana katika kikao kazi kila mwaka na watendaji na wenyeviti wa taasisi hizo. Pili, ni mabadiliko ya sheria ambayo yatahusisha kuondoa sheria zilizopitwa na wakati au zinazokwamisha mashirika kujiendesha kwa ufanisi. Hatua ya tatu ni kuangalia namna ya kuwapata viongozi wa kuendesha taasisi hizo ili kuhakikisha kuwa wanaopewa dhamana ni wenye ujuzi stahiki ambapo Mheshimiwa Rais amewahi kupendekeza kuwa nafasi hizo ziwe zinatangazwa, ili watu wenye sifa watume maombi. Nne ni uboresha wa bodi za taasisi hizo kwa kuangalia namna zinavyoteuliwa ambapo amesema lengo ni kuchagua watu wenye uwezo wa kiutendaji na kukabiliana na changamoto zinazojitokeza. Hatua ya tano ni kutoa uhuru kwa taasisi hizo kuajiri ambapo mchakato huo tayari umeanza na kwa hatua ya kwanza wanaanza na taasisi za kibiashara na vyuo vikuu. Mchechu amesema baada ya hatua hizi, hatua zaidi za kimabadiliko zitachukuliwa ndani ya taasisi moja moja na viongozi husika na kuwa lengo ni kuziwezesha kuwa na ufanisi, kuongeza faida na kutoa gawio serikalini ili kupunguza utegemezi wa ruzuku. Read More

  • Madaktari Wamarekani walioalikwa na Rais kufanya upasuaji bure

    Madaktari bingwa 60 wa mifupa na nyonga kutoka Los Angeles, Marekani wanatarajiwa kuwasili nchi Agosti 10 mwaka huu kwa ajili ya kutoa huduma za matibabu bure ya upasuaji wa magoti na nyonga katika Hospitali ya Rufaa ya Seliani inayomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT). Madaktari hao wanakuja kwa mwaliko wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan na watawasili nchini kupitia Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa Kilimanjaro (KIA) ambapo wanatarajiwa kufanya upasuaji kwa wagonjwa 200 kwa wiki mbili ambapo walengwa ni wananchi wenye hali ya chini. Kuja kwa madaktari hao ni fursa kwa wananchi wenye changamoto hizo kupata msaada ambapo pengine wasingeweza kumudu gharama hizo kwani gharama za upasuaji huo ni kubwa ambazo hufika hadi TZS milioni 75, lakini zitatolewa bure na wataalamu hao. Mbali na kutoa huduma hiyo, madaktari hao pia watatoa mafunzo kwa madaktari bingwa wa hospitali hiyo kuhusu upasuaji wa magoti, mifupa na nyonga, ili hata watakapoondoka, huduma hizo ziendelee kutolewa kwa viwango vya juu zaidi. Ili kuwezesha hilo, Serikali sikivu chini ya Mheshimiwa Rais imeruhusu vifaa vitakavyotumika kwenye upasuaji, dawa na vitendea kazi vingine viingizwe nchini bila kulipiwa kodi. Read More

  • IMF yaipongeza Tanzania kwa hatua za kisera zilizodhibiti mfumuko wa bei

    Shirika la Kimataifa la Fedha (IMF) limeipongeza serikali ya Tanzania kwa kuimarisha utulivu wa kiuchumi wakati ambapo dunia ilikuwa inapitia changamoto mbalimbali ikiwemo janga la Ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO-19), vita vya Urusi na Ukraine na mabadiliko ya tabianchi. Pongezi hizo zimetolewa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa IMF, Bo Li baada ya kumaliza ziara yake nchini ambapo amesema “jitihada za haraka za serikali ya Tanzania zilisaidia kudhibiti mfumuko wa bei na kulinda uchumi dhidi ya athari za vita nchini Ukraine.” Licha ya mafanikio hiyo, taasisi hiyo imeihimiza Tanzania kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani ambayo yatakuza uwezo wa Serikali katika kugharamia huduma za kijamii na kuongeza uwekezaji katika elimu, afya, maji na sekta nyingine muhimu. Li akizungumza na wawakilishi wa sekta binafsi, asasi za kiraia na wadau wengine wa maendeleo ameeleza kuvutiwa sana na nguvu na uhai wa uchumi wa Tanzania. Tanzania ni moja ya nchi chache barani Afrika zenye kiwango cha chini zaidi cha mfumuko wa bei ambapo kwa miezi sita mfululizo umekuwa ukishuka kutoka asilimia 4.9 Januari hadi asilimia 3.6 Juni mwaka huu. Read More

  • Tanzania ni ya mfano Afrika kwa uwekezaji katika rasilimali watu

    Wakuu wa nchi za Afrika, viongozi wa ngazi mbalimbali na wadau wengine wamekusanyika Tanzania kujadili mustakabali wa rasilimali watu barani Afrika ambapo Rais wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu ametumia jukwaa hilo kueleza hatua mbalimbali ambazo Tanzania imezichukua kuimarisha sekta hiyo ambayo ni pamoja na kutenga fedha kwa ajili ya afua mbalimbali za lishe na huduma za afya ya uzazi wa mama na mtoto. Hatua nyingine ni kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya na elimu ili kuondoa udumavu ambao, mara nyingi, hupunguza kiwango cha uelewa na uwezo wa kusoma kwa waoto na kuhakikisha watoto wanaandaliwa kimwili, kiakili, kiisimu/kijinsia kiubunifu na kiakili-hisia. Aidha, Serikali imetoa afua kwa kaya masikini, inatoa elimu bila malipo kuanzia ngazi ya awali hadi kidato cha sita, inapanua elimu ya ufundi na mafunzo ya amali, imefuta ada kwa baadhi ya vyuo vya ufundi, imeanza kutoa mikopo kwa vyuo vya kati, inatoa mikopo kwa vijana, inaruhusu waliokatisha masomo kurejea shule pamoja na kuweka mkakati wa kuvutia vijana kwenye kilimo, yote haya yakilenga kuongeza mchango wao kwenye uchumi. Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022, vijana ndio kundi lenye watu wengi zaidi nchini Tanzania, hivyo hatua ambazo Rais ameeleza kuwa Tanzania imezichukua kwa asilimia kubwa zimewalenga vijana kwani anaamini kwamba maisha bora ambayo vijana wengi hukimbilia Ulaya kuyafuata yanaweza kupatikana barani Afrika endapo Serikali zao zitawawezesha. “Viongozi wenye maono hujenga sera zao kwenye maendeleo ya watu na kufuatiwa na maendeleo ya vitu,” amesema Rais Samia akitoa wito kwa viongozi wenzake wa Afrika na kusisitiza kwamba Afrika haitoweza kuendelea endapo rasilimali watu isipoendelezwa. Read More

  • Isome hapa hotuba ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu katika Mkutano wa Rasilimali Watu Afrika

    Read More