Rais Samia Suluhu Hassan
-
Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimesajili miradi ya uwekezaji 229 yenye thamani ya TZS trilioni 4.5 kati ya Januari hadi Juni mwaka huu, ambapo lengo ni kufikia miradi 400 ifikapo Desemba 2023. Idadi hiyo inadhihirisha kasi kubwa ya usajili wa miradi nchini ikilinganishwa na miradi 293 iliyosajiliwa mwaka 2022, hivyo kusajili asilimia 78 ya miradi hiyo ndani ya nusu mwaka ni mafanikio makubwa kwa nchi. Kusajiliwa kwa miradi hiyo inayotoa ajira zaidi ya 30,000 kwa Watanzania katika sekta mbalimbali ni matokeo ya sera ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu kuimarisha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini, ikiwemo kuboresha sheria, kupunguza tozo/kodi mbalimbali na kuimarisha amani na utulivu. Aidha, takwimu zinaonesha mkakati huo wa Rais umefanikiwa zaidi kwani kwa miaka sita ya Serikali ya awamu ya tano, jumla ya miradi ya TZS trilioni 45 ilisajiliwa, huku miaka miwili ya Serikali ya awamu ya sita ikisajili miradi ya trilioni 22 ndani ya miaka miwili, takwimu zinazoonesha kuwa itafanya vizuri kuliko awamu iliyopita. Aidha, sababu nyingine ni taasisi 12 za usimamizi kuwa katika jengo moja hivyo kurahisisha utoaji huduma pamoja na matumizi ya TEHAMA yaliyorahisisha utoaji wa leseni na vibali mbalimbali vya biashara na uwekezaji hasa kupitia dirisha ya kielektroniki ambapo mwekezaji sasa anaweza kuwasilisha maombi akiwa popote dunia Read More
-
Kwa mara ya kwanza Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amezungumza hadharani kuhusu suala la uwekezaji na uendeshaji wa Bandari ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na sekta binafsi akisisitiza kuwa ni mihimu kama nchi tukatumia fursa zinazojitokeza kabla hazijaondoka au kukwapuliwa na washindani wetu, wakati tukibaki kulumbana. Ametoa rai hiyo Ikulu jijini Dar es Salaam alipokuwa akiwaapisha viongozi aliowateua karibuni, mmoja wao akiwa ni Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo na kumueleza kwamba moja ya majukumu yake ni kuangalia changamoto na fursa zilizopo nchini ili zitumike vizuri kwa manufaa ya Watanzania. “Wakati sisi tunalumbana, bandari apewe nani, iende, isiende, wenzetu kwa kuona malumbano yetu wame-jump [kimbilia] wamekwenda kule kule […] sasa muone jinsi fursa zinavyokuja na kukimbia haraka haraka, na jinsi wengine wanavyoweza kuzitumia haraka haraka,” amesema. Amesema kazi kubwa iliyopo nchini ni kuleta mabadiliko, lakini kwenye nia safi ya kujenga nchi mabadiliko yanakaribishwa na kwamba licha ya kuwa watu hawajazoea, kwa kwenda nao taratibu na kadiri watakavyoendelea kuona matokeo, watazoea. Kupitia uwekezaji unaokusudiwa bandarini, Tanzania inalenga kuongeza uwezo wa bandari kufadhili bajeti ya nchi kw asilimia 30, kuzalisha ajira zaidi ya 70,000, kuongeza mapato ya Serikali, kupunguza muda wa kuhudumia meli, kuongeza uwezo wa bandari kupokea meli kubwa na kuifanya bandari hiyo kukidhi viwango vya kimataifa. Read More
-
Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) inakusudia kuipatia Tanzania TZS bilioni 244 kwa ajili ya kutekeleza programu ya kilimo ya ‘Building A Better Tomorrow-Youth Initiative for Agribusiness (BBT-YIA) na kilimo cha mashamba makubwa kwa mwaka 2023/24. Kupitia programu hiyo iliyoasisiwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, Serikali inakusudia kukuza ushiriki wa vijana na wanawake kwenye kilimo kwa kuwawezesha kufanya kilimo endelevu cha kibiashara, pamoja na kuondoa dhana kuwa kilimo hakilipi au kilimo sio kwa ajili ya vijana. Mkakati huo unaendana na malengo ya Serikali ya kukuza sekta ya kilimo kwa kuhakikisha wakulima wananufaika kwa kufanya kilimo cha kisasa, kuwezesha kuongeza akiba ya ya chakula nchini, pamoja na kufungua fursa za ajira kupitia sekta za uzalishaji ikiwemo kilimo, mifugo na uvuvi. Benki hiyo anaendelea kuimarisha mnyororo wa thamani wa kilimo ambapo mbali na fedha hizo imewezesha pia ujenzi wa vituo vya mazao mbalimbali mkoani Dar es Salaam kwa ajili ya kusafirisha nje ya nchi, na vitu vingine mkoani Mbeya, Njombe na Iringa kwa ajili ya matunda na mbogamboga ambavyo vitaanza kutumika mwaka ujao wa fedha. Aidha, kutokana na azma ya Rais ya kukuza kilimo, AfDB inakusudia kuendeleza ushirikiano na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ambayo inawezesha ujenzi wa miradi ya umwagiliaji pamoja na uongezaji thamani. Read More
-
Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania, Serikali imesaini mikataba saba ya ujenzi wa barabara kuu ambazo zina jumla ya urefu wa kilomita 2,035, ambapo kwa miaka ya nyuma ili kuwa ikijenga wastani wa kilomita 200 hado 250 kwa mwaka. Barabara hizo ambazo zitapita kwenye mikoa 13 zitaboresha mtandao wa barabara nchini na kuongeza ufanisi katika sekta ya usafiri na usafirishaji na kuchochea uzalishaji katika maeneo zinapopita hatua ambayo itaongeza kasi ya ukuaji wa uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla, pamoja na kuchochea ukuaji wa sekta nyingine. Zaidi ya Watanzania 20,000 watapata ajira za moja kwa moja, ikiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo wahitimu wa vyuo vikuu kwa masharti ya mikataba ya ujenzi na usimamizi ambapo wahitimu wasiopungua 70 watapata ajira. Barabara zikazojengwa pamoja na mikoa ambayo zitapita; i) Barabara ya Kidatu – Ifakara – Lupiro – Malinyi – Kilosa Kwa Mpepo – Londo – Lumecha/Songea (km 435.8) inapita katika mikoa ya Morogoro na Ruvuma na inapita pia katika Majimbo ya Kilombelo, Ulanga, Malinyi na Namtumbo; ii) Barabara ya Arusha – Kibaya – Kongwa (km 453.42) inapita katika Mikoa ya Arusha, Manyara na Dodoma na inapita katika Majimbo ya Arusha Mjini, Arumeru Magharibi, Simanjiro, Kiteto na Kongwa; iii) Barabara ya Handeni – Kiberashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Olboroti – Mrijo Chini – Dalai – Bicha – Chambolo – Chemba – Kwa Mtoro – Singida (km 384.33) inapita katika Mikoa ya Tanga, Manyara, Dodoma na Singida na inapita katika Majimbo ya Kilindi, Chemba, Kiteto, Singida Mashariki na Iramba Mashariki; iv) Barabara ya Igawa – Songwe – Tunduma (njia nne) (km 237.9) inapita katika Mikoa ya Mbeya na Songwe na inapita katika Majimbo ya Mbarali, Mbeya Vijijini, Mbeya Mjini, Mbozi, Vwawa na Tunduma; v) Barabara ya Masasi – Nachingwea – Liwale (km 175) inapita katika Mikoa ya… Read More
-
Hatua ya Bunge la Tanzania kupitisha azimio la kuridhia ushirikiano kati ya Tanzania na Dubai kuhusu ushirikiano wa kiuchumi na kijamii katika uendelezaji na uboreshaji utendaji kazi wa bandari Tanzania ni hatua nyingine kubwa katika mkakati wa Tanzania kuelekea kuwa kitovu cha biashara na uwekezaji Afrika Mashariki na Kati ndani ya muongo mmoja ujao. Kupitishwa kwa azimio hilo kunaipa nafasi Tanzania kupitia Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Dubai kupitia Kampuni ya DP World kuanza majadiliano yanayolenga kuangazia namna ya kushirikiana ili kuongeza ufanisi wa bandari nchini, hasa Bandari ya Dar es Salaam ambayo imekuwa lango la kibiashara kwa nchi za Afrika ya Mashariki, Kati na Kusini wa Afrika. Kufanikiwa kwa ushirikiano baina ya Serikali hizi mbili kutatimiza ndoto ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ya kuongeza mapato ya bandari kutoka TZS trilioni 7.7 za sasa hadi TZS trilioni 26 ndani ya muongo mmoja, ambayo yataweza kufadhili shughuli za kijamii na kimaendeleo nchini, hivyo kupunguza utegemezi kwa washirika wa maendeleo, jambo ambalo ni msingi katika kudhihirisha Uhuru wa nchi kwenye kupanga na kuamua mambo yake. Mafanikio mengine ambayo Tanzania itayapata ni kuongezeka kwa ajira kutoka nafasi 28,990 za sasa hadi ajira 71,907, kupunguza muda wa meli kukaa nangani kutoka siku 5 hadi saa 24, kupunguza muda wa ushushaji makontena kutoka siku 4.5 hadi siku 2, kupunguza muda wa uondoshaji mizigo kutoka saa 12 hadi saa 1, kupunguza gharama ya usafirishaji mizigo kutoka nje ya nchi kwenda nchi jirani kwa asilimia 50, pamoja na kuongeza shehena ya mizigo kutoka tani milioni 18 hadi tani milioni 47. Mbali na manufaa hayo, uendelezaji wa bandari pia utachochea ukuaji wa sekta nyingine kama uvuvi, kilimo, ufugaji, viwanda na biashara, usafirishaji (anga, reli, barabara), kiimarisha diplomasia pamoja na Watanzania kunufaika na teknolojia na ujuzi wa uendeshaji wa bandari kisasa. Ili kuendeleza uwazi na uwajibika, Serikali chini… Read More
-
Serikali chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anaiunda upya Tume ya Mipango ambayo itakuwa chini ya Rais ikiwa na jukumu la kubuni, kupanga, kuratibu na kusimamia mipango ya maendeleo ili kuwa na mfumo jumuishi wa ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa vipaumbele vya maendeleo ya Taifa. Kuunda upya kwa tume hiyo na kuiweka chini ya Rais ni kuendelea kuyaishi maono ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ambaye kwa mara ya kwanza alianzisha mwaka 1962 ikiwa ni idara ambapo wakati wa uanzishaji wake walisema “Nakusudia kuanzisha idara mpya, idara ya mipango ya maendeleo, idara hiyo itakuwa chini yangu mwenyewe.” Uamuzi wa Rais kurejesha tume hiyo utawezesha uwepo wa utaratibu wa kupanga pamoja mipango ya kisekta, hususani sekta zenye majukumu yanayotegemeana na kuwa na mfumo wa kisheria na chombo mahsusi cha kusimamia uandaaji, utekkelezaji wa mipango ya maendeleo, utafiti na kuishauri Serikali kuhusu vipaumbele vya maendeleo ya Taifa. Majukumu haya kwa sasa yanatekelezwa na Wizara ya Fedha na Mipango, lakini kumekuwepo na changamoto ya miradi inayoendana kutekelezwa kwa nyakati tofauti sehemu husika, mfano barabara inajengwa baada ya muda inavunjwa ili kupitisha bomba la maji. Hivyo kuwepo kwa tume maalum chini ya ofisi ya Rais kutaondoka mkanganyiko huo ili miradi kama hiyo itekelezwe kwa wakati mmoja ili kuleta ufanisi na kuipunguzia serikali gharama zisizo za lazima. Aidha, tofauti na tume iliyokuwepo awali ambayo ilikuwa ikiendeshwa kwa hati idhini (instruments) tume mpya itakuwa na hadhi ya kisheria ambayo itaipa tume nguvu zaidi na kulinda mawazo yanayotolewa na kuleta utofauti katika mfumo wa uendeshaji. Read More
-
Dunia ikiendelea kushika kasi katika matumizi ya kompyuta kwenye mambo mbalimbali, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan hajaiacha Tanzania nyuma kwani anatekeleza ahadi yake ya kukuza sekta ya teknolojia, habari na Mawasiliano (TEHAMA) ili vijana wengi zaidi waweze kujiajiri, lakini pia kurahisisha na kuboresha utoaji huduma kwa wananchi. Mei 13 mwaka huu aliongoza utiaji saini miradi miwili ya ujenzi wa minara 758 katika Kata 713 pamoja na mradi wa kuongeza uwezo wa minara 304 ya mawasiliano hatua ambayo itafikisha mawasiliano na huduma ya intaneti kwa Watanzania zaidi ya milioni nane waishio vijijini, maeneo ambayo awali hayakuwa na huduma hizo. Ili kuwezesha wananchi kunufaika na uwepo wa miundombinu hiyo, Rais Samia ameweka wazi dhamira ya Serikali anayoiongoza kupunguza gharama za intaneti kwa kuanza na kupunguza gharama za uendeshaji kampuni za mawasiliano, hatua ambayo itawezesha kampuni hizo kupunguza gharama za vifurushi, hivyo wananchi wengi, mathali waliojiajiri kupitia TEHAMA, waweza kumudu gharama. Asema kuwa Serikali inalifanyia kazi suala la gharama kubwa za kupitia mkongo kwa Taifa kwenye hifadhi ya barabara na pia Serikali itafikisha umeme kwenye minara ya mawasiliano ili kupunguza gharama za uendeleshaji mnara mmoja kutoka TZS shilingi milioni 1.8 kwa mwezi hadi TZS 400,000, hatua ambazo zitapunguza gharama za vifurushi. Rais Samia anachukua hatua hizi akiamini kuwa uwepo wa mawasiliano bora na intaneti nchi nzima kutachochea ukuaji wa sekta nyingine kama afya, elimu, kilimo, uchumi, haki pamoja na ulinzi na usalama kwani wananchi wataweza kupata taarifa sahihi kwa wakati, watapata njia ya kutoa maoni yao pamoja na kuimarika kwa biashara na uchumi wa kidijitali. Ni wazi pia kuwa, kwa hatua hizi za Rais Samia anaweka mazingira wezeshi ya kuanzisha viwanda vya uzalishaji wa vifaa vya TEHAMA vyenye uwezo wa kutoa ajira kwa wananchi wengi, kudhibiti majanga na kuchochea tafiti katika sekta mbalimbali. Read More
-
Uamuzi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan wa kufufua mchakato wa kuipata Katiba Mpya uliokwama tangu mwaka 2014 umeonesha utayari wa kisiasa wa ofisi hiyo ya juu zaidi nchini kuleta Mabadiliko (Reformation) kama alivyoeleza kwenye msingi wa 4R za uongozi wake. Aidha, kurejeshwa mezani kwa mchakato huo kumethibitisha pamoja na mambo mengine kuwa Rais Samia ni msikivu, na anafanyia kazi maoni anayopokea kwa pendekezo la kufufua mchakato huo lilitolewa na kikosi kazi alichokiunda mwaka jana kwa ajili ya kutathmini hali ya kisiasa nchini. Kama wasemavyo Wahenga kuwa Ukimulika Nyoka Anzia Miguuni Pako, ndivyo Rais alivyofanya kwani Kamati Kuu ya CCM, chama anachokiuongoza, Juni 2022 iliielekeza Serikali kuangalia namna ya kufufua mchakato huo ambapo sasa TZS bilioni 9 zimetengwa kwa ajili ya shughuli hiyo. Utayari wake wa kisiasa umeweza kuufikisha mchakato hadi ulipo sasa ambapo mwanga unaonekana kuelekea kulifikia lengo, huku wadau mbalimbali wakimpongeza kwa kuvuka vikwazo vyote ndani ya Serikali na chama chake kwani amewahi kusema yeye mwenyewe kuwa uamuzi huo si kila mmoja anakubaliana nao. Amepongezwa pia kwa namna anavyoufanya mchakato huo kuwa shirikishi ukihusisha majadiliano ya vyama vyote, wanadau na wananchi kwa ujumla akiamkini kuwa maboresho yanayokwenda kufanyika ni kwa ajili ya manufaa ya Watanzania, hivyo ni lazima washirikishwe. Read More
-
Serikali imetangaza kuwa huduma za vipimo vya awali kwa wajawazito ambazo zinahusisha kupima wingi wa damu, mkojo ili kuangalia wingi wa protini, shinikizo la damu pamoja na kusikiliza mapigo ya moyo ya mtoto, zitatolewa bure. Kutolewa bure kwa vipimo hivyo muhimu kutawawezesha wajawazito kujua mwenendo wa ujauzito, kuepuka kifafa cha mimba na vifo vya mama na mtoto ambapo lengo la Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2021/22-2025/26) ni kupunguza vifo vya uzazi kutoka vifo 321 kwa vizazi 100,000, hadi vifo 220 na vifo vya watoto kutoka vifo 51 kwa vizazi hai 1,000 hadi vifo 40. Aidha, hatua hii itaongeza zaidi idadi ya wajawazito wanaohudhuria kliniki pamoja na kujifungulia kwenye vituo vya afya ambapo Serikali imeahidi itahakikisha upatikanaji wa 100% wa dawa za kuzuia kutoka damu wakati wa kujifungua, dawa za kuongeza damu na dawa za kuzuia kifafa cha mimba katika vituo vyote afya vya umma. Hatua hizi ni mwendelezo wa kazi kubwa aliyofanya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu wa kujenga vituo vya afya, kuboresha miundombinu ya afya nchi nzima, kuajiri maelfu ya watumishi wa afya pamoja na kununua vifaa tiba, hivyo kuiarisha huduma za afya vijijini ambapo awali hali ilikuwa ngumu zaidi. Imani juu ya huduma za afya zinazoendelea kutolewa kwenye vituo vya afya imeendelea kuongezeka kwani kwa mujibu wa Utafiti wa Demografia na Afya mwaka 2022, idadi ya wajawazito waliotembelea kliniki walau mara nne kati ya wajawazito 100 imeongezeka kutoka 53 mwaka 2015/16 hadi 65 mwaka 201/22 kati huku wanaojifungua chini ya uangalizi wa mtoa huduma mwenye ujuzi ikiongezeka kutoka 66 hadi 85 katika kipindi hicho. Read More
-
“Wafanyakazi mambo ni moto, mambo ni fire,” ni maneno aliyoyatumia Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kuhitimisha hotuba yake ya Mei Mosi 2023 ambayo ilijaa matumaini kwa maelfu ya watumishi wa umma waliokuwa wameujaza uwanja wa Jamhuri Morogoro wakimsikiliza. Miongoni mwa mengi yaliyowafurahisha watumishi hao ambao wameendelea kushuhudia mabadiliko makubwa kwenye mazingira ya kazi na maslahi yao chini ya Rais Samia ni uamuzi wa Rais kurejesha nyongeza ya mishahara ya kila mwaka, ikiwa ni miaka saba tangu kuondolewa kwa mfumo huo. Itakumbukwa kuwa Mei 2022 Rais Samia aliridhia nyongeza ya mishahara ambapo alipandisha kima cha chini kwa watumishi wa umma kwa asilimia 23.3, ambapo TZS trilioni 1.59 zilitumika kwa ongezeko hilo kwa mwaka wa fedha 2021/2022. Aidha, mbali na kurejesha utaratibu huo, Rais amesema kuwa nyongeza ya posho ambayo ilipandishwa mwaka jana lakini baadhi ya watumishi hawakuanza kuipata kwa sababu bajeti za taasisi zao tayari zilishapitishwa, wataanza kupata fedha hizo mwaka wa fedha ujao. “Tumejiandaa pia kupandisha madaraja, vyeo vitaendelea kupandishwa, kutenganisha makundi na madaraja mserereko wale ambao hawakupata mwaka jana watapata mwaka huu” ameahidi. Pia, alisema Serikali anayoiongoza itaendelea kuwekeza na kuvutia uwekezaji nchini, ili kujenga uchumi na kuzalisha ajira kwa Watanzania na zipatikane fedha za kuboresha maslahi ya watumishi. Read More