Rais Samia Suluhu Hassan
-
Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuleta mageuzi makubwa katika sekta mbalimbali nchini ambapo katika sekta ya maji, ndani ya kipindi cha miaka minne amekamilisha miradi ya maji zaidi ya 2,331 mijini na vijijini ambayo imefikisha maji kwa mamilioni ya wananchi. Kutokana na ufanisi huo asilimia 83 ya wakazi wote wa vijijini wanapata maji safi na salama ikiwa ni ongezeko toka asilimia 72.3 alizokuta wakati anaingia madarakani Machi 2021. Aidha, kwa sasa asilimia 91.6 ya wananchi wa mijini wanapata huduma ya maji safi na salama ikilinganishwa na wastani wa asilimia 86 aliyoikuta. Mafanikio haya yanakaribia lengo lililoanishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (2020-2025) ambayo inaielekeza serikali kuongeza kasi ya usambazaji majisafi na salama ili kutosheleza mahitaji kwa zaidi ya asilimia 85 vijijini na zaidi ya asilimia 95 kwa mijini, kwa upande wa Tanzania Bara, ifikapo Desemba 2025. Ili kuhakikisha lengo la ilani, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji 1,544. Hatua hii inadhihirisha dhamira ya dhati ya Mheshimiwa Rais kufikisha maji kwa kila mwananchi popote alipo akitambua kuwa maji ni uhai, maendeleo na usalama kwa wananchi. Read More
-
Isome hapa hotuba ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika maadhimisho ya Miaka 61 ya Muungano wa Tanzania. Read More
-
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anaendelea kuongeza nafasi za ajira katika taasisi mbalimbali za Serikali ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi. Read More
-
Utekelezaji imara wa sera za kiuchumi, kuimarika kwa amani na utulivu na mikakati ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu kuifungua nchi kumeendelea kuimarisha uchumi wa Tanzania licha ya changamoto zilizotokana na mtikisiko katika uchumi wa dunia, uimara unaotarajiwa kuendelea katika siku zijazo, hususan robo ya pili ya mwaka 2024. Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeainisha maeneo matano ambayo yameendelea kudhihirisha kuimarika kwa uchumi wa Tanzania katika robo ya kwanza ya mwaka 2024 ambapo kwanza ni ukuaji wa uchumi unakadiriwa kufikia asilimia 5.1 ikiwa ni matokeo ya uwekezaji unaofanywa na Serikali kuongeza uwekezaji kwa sekta binafsi. Ripoti ya BoT imeeleza kuwa hatua zinazochukuliwa na Mheshimiwa Rais Samia zinachangia kuongezeka kwa mikopo kwa sekta binafsi na uwekezaji kutoka nje ya nchi. Mikopo hiyo ambayo inatarajiwa kuendelea kuongezeka ilielekezwa zaidi katika shughuli za kilimo, uchimbaji wa madini, usafirishaji na uzalishaji viwandani sawasawa na malengo ya Serikali. Eneo jingine ni mfumuko wa bei ambao umeendelea kuwa tulivu, kwa wastani wa asilimia 3, hali inayotokana na utekelezaji wa sera madhubuti ya fedha na uwepo wa chakula cha kutosha nchini, hivyo kuifanya Tanzania moja ya nchi chache zenye kiwango kidogo cha mfumuko wa bei Afrika. Kiwango hicho kipo ndani ya lengo la nchi la mfumuko wa bei usiozidi asilimia 5 na vigezo vya kikanda kwa jumuiya ambazo Tanzania ni mwanachama. Matokeo ya uwekezaji na uzalishaji yameendelea kuzaa matunda ambapo nakisi ya urari wa biashara nje ya nchi iliendelea kupungua kutokana na kupungua kwa gharama za uagizaji wa bidhaa na kuongezeka kwa mauzo nje ya nchi. Nakisi imepungua kwa zaidi ya asilimia 50, kufikia dola milioni 2,701.4 mwaka unaoishi Februari 2024, kutoka dola milioni 5,133.6 katika kipindi kama hicho mwaka 2023. Kuongezeka kwa mauzo nje kumechangia kuongeza akiba ya fedha za kigeni ambapo imeendelea kuwa ya kutosha, kufikia zaidi ya dola za Marekani bilioni 5.3 mwishoni mwa Machi… Read More
-
Miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Sita, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amefanya mageuzi makubwa yaliyoboresha sekta ya afya nchini na kufanya huduma za afya kuwa karibu, bora na nafuu zaidi. Vituo vya kutolewa huduma za afya (zahanati, vituo vya afya, hospitali za wilaya, mikoa, rufaa na za kanda) 1,061 vimejengwa ambapo ni wastani wa vituo 353 kila mwaka. Ujenzi wa vituo hivi umeenda sambamba na ununuzi wa vifaa tiba vya kisasa vya uchunguzi wa magonjwa ambavyo vimetoa ahueni kubwa kwa wananchi. MAMA amenunua mashine mpya za CT Scan 27, na kufanya mashine hizo nchini kufikia 45, kutoka 13 za awali. Hivi sasa mashine hizo za kiuchunguzi zinapatikana kwenye hospitali zote za rufaa za mikoa. Manufaa makubwa yanaonekana ambapo awali wakazi wa Katavi walilazimika kusafiri zaidi ya kilomita 600 kwenda Hospitali ya Rufaa ya Kanda, Mbeya, lakini sasa huduma hiyo inapatikana mkoani mwao. Tangu tupate uhuru, kwa miaka 61, Tanzania ilinunua mashine za MRI saba, lakini ndani ya miaka mitatu MAMA amenunua mashine sita na kuifanya nchi kuwa na MRI 13 ambazo zimefungwa kwenye hospitali za rufaa za kanda. Mashine za X-Ray ambazo awali hazikupatikana kwa wingi kwenye vituo vya afya, sasa zimejaa tele baada ya kununuliwa kwa Digital X-Ray 199, na kuifanya nchi kuwa namashine 346. MAMA pia amenunua mashine za ultrasound 192 na kuifanya nchi kuwa na mashine 668 ambazo ni muhimu hasa katika kufuatilia ukuaji wa mimba. Vifaa tiba vingine vilivyoongezwa ni Echocardiogram kutoka 95 mwaka 2021 hadi 102 mwaka 2024, Cathlab kutoka moja mwaka 2021 hadi nne mwaka 2024 pamoja na PET Scan ambayo ndiyo ya kwanza nchini mwetu. Vitanda vipya 40,078 vya kulaza wagonjwa, vitanda vipya 1,104 vya vya ICU pamoja na kuongeza hali ya upatikanaji wa dawa kufikia asilimia 84 kutoka asilimia 58 mwaka 2022. Mageuzi haya yaliyofanyika yamewezesha kupungua kwa vifo vinavyoepukika… Read More
-
Sera nzuri za uchumi za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu zimeendelea kuweka rekodi ambazo hazijawahi kufikiwa katika historia ya taifa letu ambapo shughuli kuu za kiuchumi za utalii, madini na uzalishaji viwandani zimeendelea kufanya vizuri zaidi. Mwaka 2023 mapato yatokanayo na utalii na dhahabu kwa mara ya kwanza yalivuka dola za Kimarekani bilioni 3 (zaidi ya TZS trilioni 7.6), huku uuzaji nje wa bidhaa za viwandani ukiendelea kuwa juu ya kiwango cha dola za Kimarekani bilioni 1 tangu MAMA aingie madarakani. Matokeo haya ambayo hayakuwahi kufikiwa kabla ni ushahidi kuwa sera nzuri za Rais Samia zinalipa ambapo kupaa kwa mapato ya utalii na dhahabu kumeiwezesha nchini kupunguza urari wa biashara kutoka TZS trilioni 13.6 mwaka 2022 hadi kufikia TZS trilioni 7.2 mwaka 2023. Takwimu toka Benki Kuu ya Tanzania zinaonesha kuwa shughuli mbalimbali za kiuchumi zimeimarika kuvuka kiwango kilichokuwepo kabla ya janga la UVIKO19, hali inayothibitisha kuwa, sio tu uchumi unaimarika kutoka kwenye janga hilo, bali unakuwa kwa kasi ambayo haijawahi kufikiwa kabla. Wakati sekta za kiuchumi zikiendelea kufanya vizuri, mfumuko wa bei umeendelea kushuka ambapo kwa wastani mwaka 2023 ulikuwa asilimia 3 kutoka asilimia 3.2 mwaka 2022, sawa na malengo ya nchi na ukanda wa Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika. Read More
-
Katika kitabu cha historia na rekodi za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa taifa letu, leo amefungua sura mpya ambapo Tanzania kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa mara ya kwanza limeongeza hisa za umiliki na ushiriki kwenye kitalu cha gesi kwa kununua hisa asilimia 20 kati ya hisa asilimia 31.94 za kampuni ya WentWorth Resources katika kitalu cha gesi asilia cha Mnazi Bay mkoani Mtwara. Kufuatia hatua hiyo, umiliki wa Tanzania kwenye kitalu hicho umefikia asilimia 40, huku kampuni ya Maurel & Prom Tanzania ikinunua hisa asilimia 11.94, na hivyo kufikisha umiliki wa asilimia 60 wa kitalu hicho, na leo kampuni hizo mbili zimesaini mikataba miwili; wa kwanza wa mauziano ya hisa na wa pili wa uendeshaji wa kitalu cha gesi asilia cha Mnazi Bay Hatua ya Tanzania kuongeza umiliki kwenye kitalu hicho ina manufaa mengi ikiwa ni pamona na kuongeza mapato ya Serikali, kuimarisha usalama wa upatikanaji wa nishati nchini, ikiwafahamika kuwa asilimia 65 ya umeme unaotumika nchini ni wa gesi asilia. Manufaa mengine ni kuepusha kitalu kumilikiwa na kuendeshwa na kampuni moja, pamoja na TPDC kuwa na nguvu katika uendeshaji na uendelezaji za kitalu hicho hatua itakayowajengea uwezo zaidi. Kupitia mkataba mpya, sasa uamuzi wa uendeshaji na uendelezaji wa kitalu utafanywa na wanahisa wote, tofauti na awali ambapo Maurel & Prom ambayo ilikuwa inamiliki asilimia 48.05 ilikuwa ifanya shughuli hizo kwa niaba ya wanahisa wengine. Aidha, TPDC imepata haki ya kupeleka wafanyakazi katika shughuli za uendeshaji na uendelezaji kitalu kwa muda mrefu tofauti na awali ambapo walikuwa wanakwenda kwa muda mfupi tu, hivyo kutawajengea uwezo wataalamu wa ndani. Mageuzi haya ya kihistoria yanayofanyika chini ya Mheshimiwa Rais Samia ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (2020-2025) ambayo imeelekeza Serikali kutekeleza mapinduzi ya kiuchumi kwa maendeleo ya watu ambao ndio wanapaswa kuwa wanufaika wakuu wa… Read More
-
Katika kuendelea kufungua fursa za ajira ndani na nje ya nchi, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imetangaza neema ya uwepo wa ajira 500 za wauguzi wa kike kuajiriwa na Serikali ya Saudi Arabia mapema Januari 2024. Ajira hizo ni matokeo ya Mheshimiwa Rais Samia kuendelea kuimarisha uhusiano mzuri baina ya Tanzania na mataifa mbalimbali duniani, ambapo mwishoni mwa Novemba na mwanzoni wa Desemba 2023 Tanzania imesaini hati mbili za makubaliano ya ushirikiano katika masuala ya kazi na ajira na Saudi Arabia pamoja na Umoja wa Falme za Kiarabu. Hati hizo zinatoa fursa za ajira kwenye mataifa husika kwa kada na sekta zenye kutumia ujuzi wa chini, ujuzi wa kati na ujuzi wa juu na pia zinaweka utaratibu rasmi wa kuratibu ajira za Watanzania wanaoenda kufanya kazi nje, ili kuhakikisha wajibu na haki za zao zinalindwa na kuzingatiwa ipasavyo. Alisema watanzania wote wenye sifa na ujuzi uliobainishwa wanataarifiwa kuomba kazi husika kwa kujisajili https://jobs.kazi.go.tz na kutuma wasifu binafsi (CV) kwa njia ya barua pepe esu@taesa.go.tz, ambapo mwisho wa kutuma maombi ni Desemba 27, 2024. Wakati huo huo, Serikali inaendelea kufanya mashauriano katika hatua mbalimbali na nchi nyingine zaidi ya 10 kwa lengo la kuwa na makubaliano ya ushirikiano utakaowezesha Watanzania kunufaika na fursa za ajira kwenye nchi husika. Read More
-
Tanzania ipo katika mchakato wa kuandaa dira mpya ya Taifa ya maendeleo ya miaka 25 (mwaka 2025 hadi mwaka 2050) ambayo itakuwa ni dira ya pili kuandaliwa nchini baada ya ile iliyoanza mwaka 2000 na inatarajiwa kumalizika mwaka 2025. Akizindua mchakato wa kukusanya maoni ya wananchi kwa ajili ya kuandaa dira mpya, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameainisha maeneo nane ya kipaumbele katika dira mpya ambayo yanatokana na mahitaji ya sasa ya dunia, makosa na mafanikio yaliyotokana na utekelezaji wa dira inatoelekea ukomo pamoja na mahitaji mengine ya kitaifa. Kwanza, ukuaji wa uchumi kufungamanishwa na sekta za uzalishaji zinazowagusa wananchi wengi zaidi na kutengeneza ajira kwaajili yao kama vile sekta ya kilimo. Pili, kukusanywa kwa takwimu kutoka sekta isiyo rasmi ili kupata hali halisi ya uchumi badala ya kutumia takwimu za sekta rasmi pekee, hali inayosababisha kukosa uhalisia wa hali ya uchumi. Eneo la tatu ni tathmini na ufuatiliaji ambao utawezesha kubaini viashiria vya kasoro kwenye utekelezaji wa dira mapema na kuzifanyia kazi ili kuhakikisha malengo yanafikiwa. Nne, uratibu wa kufungamanisha miradi ya kipaumbele kwa sekta zinazohusika katika uzalishaji. Katika hili Mheshimiwa Rais amesisitiza kuwa mipango ya sekta moja inapotekelezwa iwe na mwingiliano na mchango katika sekta nyingine ili kutumia rasilimali chache kwa matokeo makubwa. Tano, amesisitiza dira iweke mwelekeo wa uwekezaji na usimamizi wa maboresho ya kiutendaji wa mashirika ya serikali ili yaongeze ufanisi katika uendeshaji na yaweze kuhimili ushindani wa kikanda na kimataifa. Ushiriki wa sekta binafsi katika kukuza uchumi ni eneo la sita alilolitaja ambapo amesema lazima sekta binafsi iimarishwe na iwe tayari kuimarika ili ziwe na uwezo na utayari wa kufanya biashara, kutengeneza ajira pamoja na kushirikiana na sekta binafsi nje ya nchi. Uimarishaji huo unajumuisha uwepo wa mifumo rafiki ya kisheria, upatikanaji wa mitaji na rasilimali watu yenye ujuzi. Kuzingatiwa kwa maadili ya Taifa ni sehemu… Read More
-
Kutokana na mafuriko yaliyotokea wilayani Hanang mkoani Manyara na kupelekea vifo vya zaidi ya watu 50, kujeruhi wengine zaidi ya 80 pamoja na kuharibu makazi ya watu na mali mbalimbali, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu amekatisha ziara yake iliyokuwa inaendelea Dubai. Mheshimiwa Rais ambaye alikuwa Dubai kushiriki Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi (COP28) amekatisha safari hiyo na anarejea nchini ili kushughulikia kwa karibu janga hilo. Aidha, ametoa maelekezo kuwa serikali igharamie mazishi ya wote waliofariki na majeruhi wote ambao wapo kwenye hospitali mbalimbali wapate matibabu yote yanayostahili kwa gharama za Serikali na vyombo vya ulinzi na usalama viendelea kutoa msaada wa dharura na uokoaji. Pia, ameelekeza Serikali ya Mkoa na Kitengo cha Maafa cha Ofisi ya Waziri Mkuu kuhakikisha wananchi wote ambao makazi yao yamesombwa na maji wapate makazi ya muda kwa ajili ya kuwastiri wananchi hao. Wakati huo huo, Mheshimiwa Rais Samia ameelekeza tathmini ya kina ifanyike juu ya maafa hayo na vitengo na taasisi zote za Serikali zinazohusika kuwepo eneo la tukio na kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha hali inarejea kawaida. Ametoa pole kwa wafiwa wote kutokana na msiba mkubwa uliowakumba na pia amewahakikishia wananchi walioathirika kuwa serikali iko pamoja nao na itahakikisha inashughulikia masuala yote yaliotokana na janga hili. Read More