Kilimo Tanzania

  • #MiakaMitatuYaMama: Wananchi waanza kunufaika na mageuzi ya sekta ya kilimo

    Kujua unakokwenda ni muhimu ili kuweza kufika, lakini njia ipi uitumie si tu ili ufike, bali ufike kwa wakati, ni muhimu zaidi. Tanzania inalenga kujenga uchumi ambao pamoja na mambo mengine utapunguza kiwango cha umasikini kwa mamilioni ya wananchi, ili kufanikisha hilo Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameamua kuitumia sekta ya kilimo ambayo inagusa maisha ya Watanzania saba katika kila Watanzania 10. Takwimu zinaunga mkono uamuzi wake kuwa kilimo kinachangia asilimia 26 ya Pato la Taifa, kinatoa ajira kwa zaidi ya asilimia 62 ya wananchi, kinachangia dola bilioni 2.3 kwa mwaka, hutoa malighafi za kiwandani kwa asilimia 65 na kinahakikisha usalama wa chakula nchini kwa asilimia 100. Hili ni wazi kuwa mageuzi ya kweli katika maisha ya wananchi ni lazima yahusishe kilimo, siri ambayo MAMA anaijua. Ni vigumu kueleza yote yaliyofanyika katika miaka mitatu ya MAMA madarakani kwani ni mengi mno. Baadhi ya mambo hayo ni bajeti ya kilimo imeongezwa zaidi ya mara tatu kutoka TZS bilioni 294 mwaka 2021/22 hadi TZS bilioni 970 mwaka 2023/24, ongezeko ambalo ni msingi wa mageuzi yote kwenye sekta hiyo. Ongezeko hilo limepelekea mafanikio makubwa katika uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia ambapo matumizi ya mbolea yameongezeka kutoka tani 363,599 hadi tani 580,628 kutokana na mpango wa mbolea ya ruzuku. Matumizi ya mbolea yameongeza uzalishaji wa mazao ulioiwezesha nchi kuongeza mauzo ya nje takribani mara mbili kutoka TZS trilioni 3 hadi TZS trilioni 5.7. Mageuzi yaliyofanyika yamemfikia mkulima katika ngazi ya kijiji kupitia vifaa vilivyotolewa kwa maafisa ugani wa halmashauri 166 zikiwemo pikipiki 5,889, vishkwambi 805, seti za vifaa vya kupimia udogo 143 ambavyo vimemwezesha mkulima kulima kisasa akijua atumie mbegu gani na mbolea gani kwenye aina fulani ya udongo. Kama hayo hayatoshi kuondoa kilimo cha mazoea tena cha msimu, MAMA amewekeza katika kilimo umwagiliaji kwa kuongeza bajeti ya umwagiliaji kwa takribani mara nane kutoka TZS… Read More

  • Tanzania yatenga hekta 63,000 za uwekezaji mkubwa wa kilimo na ufugaji

    Serikali kupitia Kituo cha Uwekezaji Tanzania imetenga eneo lenye rutuba la ukubwa wa hekta 60,103 kwaajili ya mji wa kilimo (kilimo kikubwa cha kibiashara pamoja na ufugaji wa kisasa) litakalotolewa kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi. Eneo hilo lipo Mkulazi mkoani Morogoro, pembezoni mwa reli ya TAZARA na linafaa kwaajili ya kilimo cha miwa, mpunga, mahindi, mtama na mengineyo. Kupitia uwekezaji huo, Tanzania inakusudia kupunguza uagizaji wa mazao kutoka nje, pamoja na kuwa kapu la chakula la kulisha nchi nyingine. Kilimo cha miwa kitaongeza malighafi kwenye viwanda vya uzalishaji wa sukari na hivyo kuiwezesha nchi kuachana na uagizaji wa bidhaa hiyo kutoka nje. Katika kipindi cha mwaka 2021/22 Tanzania iliagiza tani 30,000 za sukari ili kufidia nakisi ya uzalishaji wa ndani. Mashamba manne (kila moja likiwa na ukubwa wa hekta 10,000) zitatumiwa kwa ajili kilimo cha mazao mbalimbali kulingana na aina ya udongo, shamba jingine lenye ukubwa wa hekta 10,000 litatengwa kwa ajili ya ufugaji wa kisasa na usindikaji wa mazao ya mifugo, huku hekta 10,103 zilizobaki zikihifadhiwa kwa matumizi ya baadaye kwa ajili ya kuanzisha maeneo ya usindikaji wa bidhaa za kilimo na viwanda vya kuongezea thamani bidhaa za kilimo. Katika hatua nyingine ya kuvutia uwekezaji, TIC imetenga eneo lenye ukubwa wa hekta 3,200 mkoani Kigoma kwa ajili kilimo cha michikichi, usindikaji wa mawese na kilimo cha mazao mengine. Hatua hii pia itaiwezesha nchi kupunguza uagizaji wa mafuta ya kula ambapo kwa takwimu za sasa 60% ya bidhaa hiyo muhimu inatoka nje ya nchi ikiigharimu nchi zaidi ya TZS bilioni 627 kwa mwaka. Ripoti ya Benki ya Dunia (WB) inaonesha kuwa Tanzania imetumia 33% tu ya ardhi yote inayofaa kwa kilimo, hivyo kuwa na fursa kubwa ya kujikuza kupitia kilimo cha kibiashara, ambapo sasa serikali imeweka mkakati wa kuifungua. Read More

  • Mheshimiwa Rais Samia alivyoipa kipaumbele sekta binafsi kwenye mageuzi ya kilimo nchini

    Tanzania imeweka mkakati wa kutumia mageuzi ya kilimo kupunguza umaskini wa wananchi ikizingatiwa kuwa takribani asilimia 70 ya Watanzania wanategemea sekta hiyo. Akizungumza katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi na Usalama wa Chakula, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu amesema Tanzania imekuja na Ajenda ya 10/30 ambayo inalenga kuwezesha kilimo kukua kwa asilimia 10, kutoka asilimia 4 ya sasa, ifikapo mwaka 2030. Mheshimiwa Rais ametaja hatua ambazo Serikali imechukua na inaendelea kuchukua ikiwa ni pamoja na kutoa vivutio vya kikodi kwa sekta binafsi ili ishiriki kikamilifu kwenye kilimo. Vivutio hivyo ni pamoja na kutoa punguzo la kodi (capital allowance) kwa asilimia 100, kusamehe ushuru wa forodha na kodi ya ongezeko la thamani katika vifaa vya kilimo ikiwemo vya vifaa vitakavyotumika katika umwagiliaji, uongezaji thamani, kulima na nishati salama, hatua ambayo inalenga kupunguza gharama za uwekezaji. Hatua nyingine ni Mradi wa Jenga Kesho Bora (BBT) kwa ajili ya kuwawezesha vijana na wanawake kufanya kilimo cha kisasa, mradi ambao utawezesha kuongeza uzalishaji na kutunza mazingira. “Kutunza mazingira bila kupunguza umaskini tutakuwa tunafanya kazi bure,” amesema huku akiongeza kuwa kazi ya Serikali ni kuwapa vijana mafunzo na ardhi, hivyo sasa sekta binafsi inatakiwa iingie kwenye kutoa fedha, lakini pia mitambo kufanya kilimo chetu kiwe cha kisasa Pia, amebainisha kuwa mkazo umewekwa katika tafiti ili kuwezesha wananchi kufanya kilimo chenye uwezo wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi ikiwemo mafuriko, ukame, wadudu na kutunza mazingira. Katika eneo hili Serikali imejenga na inahamasisha sekta binafsi kujenga skimu za umwagiliaji na mabwawa ya kuvuna maji ya mvua. “Sekta binafsi itakuwa na kazi ya kuhakikisha wanaongeza thamani mazao yote yanayozalishwa, lakini pia biashara ya kilimo,” amesema Mheshimiwa Rais na kuongeza kuwa katika hili Serikali inahakikisha upatikanaji wa ardhi na utoaji wa leseni na vibali kwa wawekezaji wanaotaka kuingia kwenye kilimo cha… Read More

  • #MiakaMiwiliYaMama: Amewajengea vijana uwezo wa kujiajiri kupitia kilimo

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anadhihirisha kwa vitendo kauli yake aliyotoa kuwa hataki kuingia katika historia ya kuwa mmoja wa wanaowalaumu vijana kuwa hawajiajiri, badala yake anawawekea mazingira wezeshi ya kujiajiri kupitia kilimo ambapo lengo ni kuzalisha ajira milioni 3, kipaumbele kikiwa vijana na wanawake. Machi 20 mwaka huu amezindua mashamba ya pamoja (Block Farms) zaidi ya ekari 12,000 ambazo zitagawawiwa kwa vijana, kila mmoja kwa ukubwa usiozidi ekari 10, pia alizindua ndege zisizo na rubani, mashine za umwagiliaji na magari kwa ajili ya maafisa wa wilaya ili kuhakikisha vijana popote walipo nchini wanapata usaidizi wa kitaalamu katika kufanya kilimo cha kibiashara. Katika azma ya kukifanya kilimo kuwa cha vijana, ameahidi kuendelea kutenga bajeti mahsusi kwa ajili ya watendaji kwenye sekta ya kilimo ili shughuli zote zifanyike kwa usasa kuanzia uzalishaji hadi uuzaji mazao na bidhaa. “Tunasema ni kilimo cha vijana, hivyo vijana wawepo shambani, wawepo kwenye utaalamu, wawepo kwenye kuendesha mitambao, sehemu zote kuwa na vijana wanaokwenda kwenye sekta ya kilimo,” amesema akizindua programu ya Building a Better Tomorrow. Katika miaka miwili ya uongozi wake, kilimo ni moja tu ya njia anazotumia kumwinua kijana wa Kitanzania na kukabiliana na changamoto ya ajira inayoisumbua dunia. Ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi katika kila wilaya, mikopo ya halmashauri, kuboresha mazingira ya biashara hasa kwa wajasiriamali ni maeneo mengine ambayo yametoa ajira kwa vijana wengi. Read More

  • Mheshimiwa Rais Samia atatua changamoto zinazozuia vijana kushiriki kwenye kilimo

    Kupitia mpango wa Building a Better Tomorrow (Ujenzi wa Kesho Bora) Serikali imeanzisha mfuko wa dhamana kwa vijana na huduma za mikopo nafuu chini ya Mfuko wa Pembejeo ili kuwavutia kushiriki katika ukuzaji wa uchumi kupitia kilimo. Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania imeamua kuanzisha mpango huo kutokana na idadi kubwa ya vijana na wanawake kukosa sifa zinazohitajika na taasisi za fedha wanapoomba mikopo. Zaidi ya theluthi moja (34%) ya Watanzania wakiwa ni vijana ambao ndio nguvu kazi kubwa, Rais Samia amechukua jukumu la kutatua changamoto zao kwenye kilimo, ili kuongeza tija na kuvutia vijana wengi zaidi, ambapo changamoto zilizotatuliwa ni pamoja na mafunzo, upatikanaji wa ardhi, teknolojia na fedha. Kutokana na mkakati wa Rais Samia wa kufanikisha mapinduzi ya kilimo Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) imetangaza kuipatia Tanzania mkopo wa TZS bilioni 280 kwa ajili ya sekta ya kilimo ikiwemo umwagiliaji na kujenga kituo cha usafirishaji na usambazaji mbolea. Tangu kuanzishwa kwa mpango wa BBT miezi sita iliyopita, tayari imetenga zaidi eka 600,000 nchi nzima na shughuli ya kusafisha mashamba hayo inaendelea. Read More

  • Mpango wa Mheshimiwa Rais Samia wa kuvutia vijana kwenye kilimo wavuka lengo

    Serikali kupitia mpango wa Building a Better Tomorrow inakusudia kuzalisha ajira milioni 1 kupitia kilimo hadi ifikapo mwaka 2025, ambapo mwamko wa vijana kujiunga na programu hiyo itakayowawezesha kupatiwa elimu, mashamba, pembejeo na masoko umekuwa mkubwa. Akishiriki mkutano wa chakula na kilimo wa wakuu wa nchi za Afrika nchini Senegal, Rais amesema mpango huo wa kuvutia vijana kwenye kilimo ambacho kitakuwa cha kibiashara Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amesema hadi Januari 25, 2023 tayari vijana 7,000 wamesajiliwa kujiunga na programu hiyo, kiwango ambacho kimevuka lengo. “Pia tumekuwa tukifanya kazi na benki kwa ajili ya mikopo kwa vijana na wanawake. Tuliweza kupunguza riba kutoka asilimia 15 hadi asilimia tisa,” amesema Rais akibainisha lengo ni kuifanya Tanzania kuwa mfuko wa chakula cha Afrika kupitia nguvu kazi ya vijana ambao ni asilimia 34.5 ya Watanzania wote. #KilimoBiashara Tanzania ya kesho, ni Tanzania ya kilimo cha kisasa kinachofanywa na vijana, na hivi ndivyo Mheshimiwa Rais Samia Suluhu anavyowezesha vijana. #MamaYukoKazini pic.twitter.com/psP2HkxlxO — Mama yuko Kazini (@mamayukokazini) January 18, 2023 Kupitia mpango huo vijana watapatiwa elimu ya kufanya kilimo cha kibiashara, mashamba yao yatajengewa miundombinu ya umwagiliaji na ghala la kuhifadhi mazao, watapatiwa teknolojia ya kisasa ya uzalishaji, mitaji, pembejeo za kilimo na kuunganishwa na masoko ya mazao yao. Tayari TZS bilioni 3 ambazo zimetengwa kwa ajili ya kufanikisha mpango huo zimeanza kutumika kuwawezesha walengwa lengo likiwa ni kuongeza uzalishaji wa chakula, malighafi, kuzalisha ajira na kubadili fikra na dhana kuwa kilimo hakilipi. Kwa maelezo zaidi namna ya kushirikia katika programu hiyo bonyeza hapa Read More

  • Mheshimiwa Rais Samia na mapinduzi katika Sekta ya Kilimo

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amesema sekta ya kilimo nchini inatarajiwa kukua kwa asilimia 10 ifikapo mwaka 2030 ikilinganisha na ukuaji wa sasa wa takribani asilimia 3.6. Akizungumza kwenye mdahalo wa ‘Food Action Partnership: Investing in Greater Resilience’ nchini Uswisi amesema Tanzania imetengeneza fursa za kitaifa kwa ajili ya mabadiliko ya mfumo wa chakula unaotarajia kuongeza uzalishaji wa chakula, kuimarisha maisha ya watu na kusaidia kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa. Katika kudhibiti mfumo endelevu wa chakula nchini, Rais Samia amesema jitihada kadhaa zimefanyika, ikiwemo kuanzisha mradi kwa ajili ya vijana huku wakiendelea kuimarisha ukuaji wa shoroba za kilimo pamoja na kuongeza bajeti ya kilimo mara 4 ukilinganisha na ile iliyopita. Serikali ya Tanzania inaendelea kutekeleza miradi na mafunzo mbalimbali ya kilimo kwa vijana ili kuongeza tija kwenye kilimo na kuwezesha vijana kushiriki kwenye uchumi wa Tanzania ambapo lengo ni kuzalisha ajira milioni 1 ifikapo mwaka 2025. Mdahalo huo uliohudhuriwa na zaidi ya viongozi 50 kutoka Afrika, Asia, Ulaya na Marekani mbali na Rais Samia wachangiaji wengine walikuwa Rais Gustavo Petro wa Colombia, Tran Hong Ha, Naibu Waziri Mkuu wa Vietnam na Alvaro Lario, Rais wa Wakfu wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Roma. Read More