Watumishi wa Umma

  • Mama ashusha neema kwa watumishi wa umma; kima cha chini cha mshahara ni laki 5

    Ni furaha furi furi kama sio furaha bojo bojo kwa watumishi wa umma na Watanzania kwa ujumla baada ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza nyongeza ya kima cha chini cha mshahara kwa asilimia 35.1. Kutokana na nyongeza hiyo, kima cha chini kuanzia Julai 1, 2025 kitakuwa TZS 500,000 toka kiwango cha TZS 370,000 cha sasa. Mheshimiwa Rais ametangaza neema hiyo katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Dunia (Mei Mosi) ambayo kitaifa imefanyika mkoani Singida ikiwa na kaulimbiu isemayo, “Uchaguzi Mkuu 2025 utuletee viongozi wanaojali haki na maslahi ya wafanyakazi wote, sote tushiriki.” Amesema nyongeza hiyo ni sehemu ya hatua ambazo serikali yake imeendelea kuchukua kuleta ustawi kwa wafanyakazi nchini, na kwamba uamuzi huo umewezeshwa na kasi ya ukuaji wa uchumi kupanda hadi kufikia 5.5% kwa mwaka, hali iliyochangiwa na wafanyakazi kujituma na kufanya kazi kwa bidii. Kupitia mitandao ya kijamii wananchi wamefurahia nyongeza hiyo ambapo wameandika jumbe za kumpongeza. Baadhi ya jumbe hizo ni; “Nakuamini na nakupenda sana mama maisha yangu yote sijawahi kupiga kura ila mwaka huu inshallah nna Imani kura yangu unayo ya kwanza kwenye maisha yangu,”- Hamoud Jimia. “Ubarkiwe mama ikulu yako huna mpinzani hata kidgo,”- Kisila Legandy “Safi mama Samia, wewe ndo unatudai na tunakuhakikishia lazima tukulipe,”- Julius Peter “Kima cha chini cha mashahara kinapanda kutoka 300k mpaka 500k nomaa,”- Msaki. Kuhusu sekta binafsi Mheshimiwa Rais amesema kuwa Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara inaendelea na tathmini kwa lengo la kuboresha viwango vya mishahara kwa sekta binafsi. “Tutaendelea kuboresha mazingira ya wafanyakazi ikiwemo maslahi ya wafanyakazi kwa kadiri hali itakavyoruhusu… Ili tuweze kujenga vyema Taifa letu ni lazima tulinde amani na utulivu nchini,” amesisitiza Rais Dkt. Samia. Read More

  • #MiakaMitatuYaMama amezipatia majawabu changomoto za muda mrefu za watumishi wa umma

    Watumishi wa umma wanayo mengi ya kufurahia na kuonesha katika miaka mitatu ya Mama kwani ametoa majawabu ya changamoto nyingi zilizokuwa za zinawakabili, hali iliyowaongezea motisha na ari ya kuwatumikia wananchi. Kubwa la kwanza ambalo katika kila Sikukuu ya Wafanyakazi (Mei Mosi) lilikuwa likisubiriwa tangu mwaka 2016 ni nyongeza ya mishahara. Ndani ya uongozi wa Mama hilo limepatiwa majibu ambapo alipandisha kima cha chini cha mishahara kwa asilimia 23, nyongeza ambayo imewawezesha watumishi wa umma kumudu gharama za maisha ambapo pia aliahidi nyongeza itakuwa kila mwaka. Kwa miaka saba, tangu mwaka 2016 watumishi hao hawakuwa wamepandishwa vyeo. Chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu watumishi 375,319 wamepandishwa vyeo ambapo Serikali imetumia TZS bilioni 85.89, fedha ambazo matumizi yake yamekwenda kuongeza mzunguko wa fedha na kuboresha maisha ya watumishi. Ajira kilikuwa ni kilio kikubwa ambapo mbali na kuweka mazingira rafiki yaliyozalisha maelfu ya ajira kwenye sekta binafsi, Serikali tayari imeajiri watumishi wapya 81,137 katika taasisi mbalimbali za umma. Aidha, imetenga TZS bilioni 230 ambazo zitatumika kuajiri watumishi wapya 47,374 kabla ya mwaka wa fedha 2023/24 kumalizika. Mama amekuwa akisisitiza kuwa yeye na wasaidizi wake si watawala bali ni watumishi wa wananchi. Ili kuhakikisha utumishi uliotukuka ameendelea kutatua changamoto zao ambao amewalipa malimbikizo maelfu ya watumishi. Ndani ya miaka mitatu ya Mama jumla ya watumishi 142,793 wamelipwa malimbikizo yenye thamani ya TZS bilioni 240.7. Kwa lengo la kuendelea kuongeza ufanisi, Serikali imewabadilishia kada watumishi 30,924 ambapo imewalipa mishahara mipya yenye thamani ya TZS bilioni 2.56, mafanikio ambayo hayakuwa yamepatikana katika kipindi cha zaidi ya miaka mitano kabla ya uongozi wa Mama. Kama hayo hayatoshi, kabla ya mwaka 2023/24 kumalizika, Serikali itakuwa imewapandisha vyeo watumishi 81,561 kwa gharama ya TZS bilioni 90.85, hatua hii mbali na kuongeza motisha kwa watumishi hao, utafungua fursa za ajira mpya. Mbali na maslahi yao, Serikali imeboresha pia maeneo… Read More