Uwekezaji Bandari
-
Falsafa ya 4R (Reconciliation, Resilience, Reform, and Rebuild) ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuleta mageuzi katika sekta mbalimbali zinazogusa maisha ya Watanzania na kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchini. Moja ya sekta hizo ni uchukuzi, ambapo Mageuzi (Reform) yaliyofanywa katika Bandari ya Dar es Salaam kwa kuingia ubia na Kampuni za DP World na Tanzania East Africa Gateway Terminal Limited (TEAGTL) katika kuendeleza na kuendesha baadhi ya maeneo ya bandari hiyo yameendelea kuleta matokeo, ikiwemo kuongeza mapato. Kati ya Julai, 2024 hadi Februari 2025, mapato yatokanayo na Kodi ya Forodha kutoka bandarini yanayokusanywa kutokana na shughuli za kibandari yamefikia TZS trilioni 8.26, ambalo ni ongezeko la TZS trillion 1.18 ikilinganishwa na makusanyo ya TZS trilioni 7.08 yaliyokusanywa kipindi kama hicho kwa mwaka 2023/24. Mafanikio hayo yametokana na wawekezaji hao kuwezesha upatikanaji wa vifaa na mitambo ya kisasa na mifumo ya TEHAMA inayoendelea kuleta ufanisi katika uendeshaji wa shughuli za kibandari, hasa kuondoa msongamano wa mizigo na foleni za meli, hali inayochochea wafanyabiashara zaidi kuchagua kutumia bandari hiyo, hivyo kuongeza mapato. Lengo la Mheshimiwa Rais Samia kushirikisha sekta binafsi ni kuongeza tija katika utendaji wa bandari nchini ili kuziwezesha zichangie zaidi katika ukuaji wa uchumi wa Taifa letu na maendeleo ya wananchi kwa ujumla kwa kuwafanya wanufaike na rasilimali za nchi yao. Read More
-
Tanzania imefungua ukurasa mpya kwenye uwekazaji katika sekta ya uchukuzi kwa kusaini mikataba mitatu na kampuni ya DP World kwa ajili ya uwekezaji bandarini, uwekezaji ambao utashuhudia ufungwaji wa mifumo na mitambo ya kisasa itakayoleta mageuzi kwenye bandari, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuhakikisha inakuwa kitovu cha biashara na usafirishaji Afrika Mashariki na Kati. Utiaji saini wa mikatanba mitatu ambayo ni mkataba wa nchi mwenyeji (HGA), mkataba wa uendeshaji gati namba 4 hadi 7 na mkataba wa ukodishaji gati namba 4 hadi 7 umetoa majibu kwenye hoja au maswali yaliyoibuliwa na wananchi yaliyotokana na mkataba wa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai (IGA). Moja ya hoja kubwa iliyoibuka wakati wa mjadala wa IGA ilikuwa ni ukomo wa mikataba, ambapo baadhi ya watoa hoja, hususani wanasiasa na wanaharakati walisema kuwa bandari hizo zimekabidhiwa kwa mwekezaji kwa muda usio na ukomo, wengine wakisema ni miaka 100. Hata hivyo, taarifa ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaa ya Bandari Tanzania imeeleza kuwa mikataba hiyo ni ya miaka 30, na kwamba mapitio ya utendaji wa mwekezaji yatafanyika kila baada ya miaka mitano kuona kama anatimiza vigezo alivyowekewa. Pia, baadhi ya watoa hoja walidai kuwa Tanzania haiwezi kujitoa kwenye mikataba, lakini taarifa ya TPA imeeleza kuwa Serikali ya Tanzania inayohaki na inaweza kujitoa kwenye mikataba hiyo pindi itakapoona ni muhimu kufanya hivyo. Aidha, mambo mengine yaliyoelezwa kutoka kwenye mikataba hiyo ambayo yanajibu maswali ya wananchi ni pamoja na sheria za Tanzania kutumika kwenye mikataba husika, serikali kuwa na umiliki wa hisa kwenye kampuni itakayoendesha sehemu ya bandari, mwekezaji kulipa kodi kwa mujibu wa sheria, masuala ya usalama kubaki kwa mamlaka za ndani, hakuna mtumishi wa bandari atakayepoteza kazi yake na kuwa uwekezaji huo utaihusu bandari ya Dar es Salaam. Kwa upande wake Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amesema maoni ya watu wote… Read More