Miaka 61 ya Uhuru

  • Miaka 61 ya Uhuru: Rais Dkt. Samia anavyotumia misingi ya Mwl. Nyerere kuchochea maendeleo

    Tanzania Bara leo imeadhimisha miaka 61 tangu ipate Uhuru kutoka kwa Uingereza mwaka 1961, safari ambayo Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema “imekuwa safari yenye changamoto na mafanikio mengi ambayo Taifa letu linajivunia.” Katika kuadhimisha siku hii kubwa, mjadala mkubwa huzunguka mchango wa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Uhuru, na misimamo aliyoiweka ambayo imekuwa ikitumiwa kama rejea katika kuliongoza Taifa. Mambo mengi ambayo aliyahimiza, Rais Samia ameendelea kuyahimiza na kuyatekeleza ili kuchochea maendeleo ya Watanzania ambayo ni pamoja na; 1. Kupiga vita rushwa Mwalimu Nyerere alikiri kuwa, katika awamu ya kwanza kulikuwa na rushwa, lakini walikuwa wakali sana kuipinga. Serikali yake ilipitisha sheria, mtu akithibitika amepokea au ametoa rushwa, atahukumiwa kifungo kisichopungua miaka miwili na viboko 24 (12 akiingia na 12 akitoka). Vivyo hivyo, Dkt. Samia ameendeleza ari hiyo ya kupinga rushwa akiamini kuwa rushwa inaathiri utoaji haki kwa kumwacha mwenye hatia mtaani na kumfunga asiye na hatia, inawanyima wasio na uwezo fursa ya kupata huduma lakini pia ni kinyume na mafundisho wa kidini. 2. Huduma za Jamii (Elimu, Maji na Afya) Mara baada ya Uhuru, Mwalimu Nyerere aliainisha maadui watatu wa Taifa ambao ambao ni Ujinga, Maradhi na Umasikini. Katika miaka miwili ya Dkt. Rais madarakani amejipambanua kwa kupamba na maadui hao ambapo amewezesha ujenzi wa madarasa zaidi ya 23,000, shule mpya, ajira za walimu, vituo vya afya zaidi ya 230, kujenga na kukarabati hospitali, kufufua na kuanzisha na kukamilisha miradi ya maji pamoja na kuajiri watumishi katika sekta hizo ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi. 3. Kilimo cha kisasa “Tubadili kilimo chetu kusudi kilimo kitusukume kwa sababu hatuna kitu kingine cha kuisukuma nchi hii isipokuwa ni kilimo. Lakini kilimo hiki cha jembe la mkono, kilimo hiki cha kutegemea mvua peke yake, hakina mbolea, hakina dawa, unapanda hovyo hovyo tu, hakitusaidii sana,” alisema Hayati… Read More

  • Dhamira ya Dkt. Samia kuwasaidia wenye ulemavu, milioni 960 za Uhuru kujenga mabweni yao katika shule 8

    Desemba 9 kila mwaka Tanzania huadhimisha Siku ya Uhuru ambapo kwa mwaka 2022 maadhimisho hayo yatakuwa ya 61 tangu nchi ipate uhuru kutoka kwa wakoloni. Hata hivyo, maadhimisho hayo yatafanyika tofauti na miaka mingine ambapo hakutakuwa na sherehe za kitafa baada ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu kuelekeza fedha zilizokuwa zimetengwa kujenga mabweni kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum. Kufuatia uamuzi huo, TZS milioni 960 zitatumika kujenga mabweni kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum kutoka katika shule nane ambazo ni, Longido (Arusha), Songambele (Manyara), Buhangija (Shinyanga), Goeko (Tabora), Darajani (Singida), Msanzi (Rukwa), Idofi (Njombe) na Mtanga (Lindi). Kwa hatua hii ambayo imepokewa kwa furaha na wananchi wengine, Rais Samia ameendelea kudhihirisha dhamira yake ya boresha mazingira ya kujifunzia kwa watu wenye ulemavu pamoja na kuwawezesha kiuchumi ili kutekeleza dhana ya maendeleo jumuishi. Kwa ufupi, miongoni mwa mambo aliyofanya kwa ajili ya wenye ulemavu ni pamoja na kuwezesha ujenzi wa mabweni 50 kwa wanafunzi wenye ulemavu mwaka 2021, na pia kupitia mkopo wa TZS trilioni 1.3 kutoka Shirika la Fedha Dunia wa kukabiliana na athari za UVIKO-19,TZS bilioni 5 zilikwenda kuwasaidia wanawake na watu wenye ulemavu. Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/22 Serikali ilitenga TZS bilioni 3.46 kwa ajili ukarabati wa vyuo vya watu wenye ulemavu ambapo ukarabati wa Vyuo vya Ufundi Stadi na Marekebisho kwa Watu wenye Ulemavu vya Luanzari (Tabora) na Masiwani (Tanga) umekamilika, na ukarabati katika vyuo vinne katika mikoa ya Dar es Salaam, Mtwara, Singida na Tabora unaendelea. Mbali na kuzisimamia mamlaka za Serikali kutoa ajira kwa watu wenye ulemavu, Serikali inaendelea na maboresho ya Sera ya Taifa ya Huduma na Maendeleo ya watu wenye ulemavu, kuhakikisha upatikanaji wa vifaa saidizi na kuendelea kuhamasisha jamii kuondokana na unyanyapaa dhidi ya watu wenye ulemavu. Asilimia 10 inayotokana na makusanyo ya halmashauri imeendelea kuboresha maisha ya wenye ulemavu ambapo hadi Desemba… Read More