Maliasili na Utalii
-
Sekta ya Utalii nchini imeipita dhahabu kwa kuwa ya kwanza katika kuingiza fedha za kigeni nchini, ambapo mapato yake kwa mwaka ulioishia Mei 2025 yamefikia dola za Marekani bilioni 3.92 (TZS trilioni 10.2), ikiwa ni asilimia 55 ya mapato yote ya mauzo ya nje. Kiwango hicho ni ongezeko kutoka dola za Marekani bilioni 3.63 kwa kipindi kama hicho mwaka jana. Ongezeko hilo limeipita dhahabu ambayo imeingiza dola za Marekani bilioni 3.83 (TZS trilioni 9.9), na hivyo kuthibitisha ukuaji madhubuti wa sekta ya utalii na mchango wake katika uchumi wa nchi. Mafanikio haya ni matokeo ya hatua zinazoendelea kuchukuliwa na serikali ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan akitambua umuhimu wa sekta hii katika uchumi wetu ambayo inachangia asilimia 17.2 katika Pato ghafi la Taifa, inachangia asilimia 25 ya mapato ya fedha za kigeni na kuajiri zaidi ya milioni 3. Moja ya hatua iliyochukuliwa ni Julai 8 mwaka huu ambapo Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliruhusu kampuni za utalii kutumia fedha za kigeni katika maeneo mawili muhimu: wakati wa kulipia bidhaa na huduma kwa niaba ya watalii wasiokuwa wakazi, na wakati wa kununua magari maalum ya utalii kutoka kwa wasambazaji wa ndani. Uamuzi huo ulipokelewa kwa furaha na Chama cha Waendeshaji wa Utalii Tanzania (TATO) kikieleza kuwa serikali imedhamiria kukuza sekta hiyo yenye mnyororo mrefu wa thamani na kwamba wataendelea kushirikiana nayo ili kuikuza zaidi sekta hiyo. Read More
-
Kazi kubwa aliyoifanya na inayoendelea kufanywa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza fursa za utalii unaweza kusema ‘imejibu’ baada ya sekta hiyo kuendelea kuimarika na kupita madini ya dhahabu katika kuiingizia nchi fedha za kigeni, ikiwa ni kwa mara ya kwanza ndani ya miaka minne tangu ilipoanza kushuka. Mlipuko wa janga la kidunia la Ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO) mwaka 2019 kuliiathiri sekta hiyo ambapo mchango wake kwenye fedha za kigeni ulishuka kutoka dola za kimarekani bilioni 2.52 (TZS trilioni 6.3) mwishoni mwa mwaka 2019 hadi dola za Kimarekani bilioni 1 (TZS trilioni 2.5) mwishoni mwa mwaka 2020, na hivyo kupelekea dhahabu iliyoingiaza dola za Kimarekani bilioni 2.9 (TZS trilioni 7.2) kuongoza. Kuhakikisha sekta ya utalii ambayo inatoa ajira zaidi ya milioni 1.6, inachangia asilimia 25 ya fedha za kigeni na asilimia 21 ya Pato la Taifa inaimarika, Mheshimiwa Rais Samia alichukua jukumu la kurekodi filamu ya Tanzania: The Royal Tour ambayo ilizinduliwa nchini Marekani na hivyo kuiwezesha nchi kutangaza fursa za utalii na vivutio vya utalii kwa mamilioni ya watu dunia, hatua ambayo imepelea kuendelea kuongezeka kwa watalii kutoka ndani na nje ya nchi. Matokeo yameendelea kuonekana ambapo takwimu za Benki Kuu ya Tanzania zinaonesha kuwa mapato yatokanayo na utalii yamepanda kufikia dola za Kimarekani bilioni 2.999 (TZS trilioni 7.5) katika mwaka ulioishia Julai 2023 kutoka dola za Kimarekani bilioni 1.95 (TZS trilioni 4.8) mwaka ulioishia Julai 2022, huku mapato ya dhahabu kwa mwaka ulioishia Julai 2023 yakiwa dola za Kimarekani bilioni 2.9 (TZS trilioni 7.3). Mafanikio hayo yametokana na kuendeleo kuongezeka kwa watalii kutoka nje ya nchi ambapo ripoti ya BoT inaonesha kuwa watalii wameongezeka kwa asilimia 37.2 kufikia 1,658,043 katika mwaka huo, idadi ambayo haijawahi kufikiwa kabla. Licha ya mafanikio haya, Mheshimiwa Rais Samia anaendelea kutangaza utalii ili kufikia lengo la watalii milioni 5 ifikapo… Read More