Majenereta Kigoma

  • Namna 5 ambazo umeme wa gridi ya Taifa unaubadili mkoa wa Kigoma

    Oktoba 17 mwaka huu ilikuwa siku ya historia kwa Tanzania, hasa mkoa wa Kigoma baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzima jenereta la kuzalisha umeme la Kasulu na kuwasha umeme wa gridi ya Taifa uliofika mkoani humo kwa mara ya kwanza. Jenereta la Kasulu ambalo lilikuwa likizalisha umeme megawati 3.75 zilizotumika wilayani Kasulu na Buhigwe lakini hazikutosheleza ni moja ya majenereta matano yaliyozimwa mengine yakiwa ni Loliondo, Biharamulo, Kibondo na Ngara. Kuzimwa kwa mtambo wa Kasulu na kuwashwa umeme wa gridi ya Taifa kutabadilisha kabisa hadithi ya mkoa wa Kigoma pamoja na maisha ya wakazi wa mkoa huo kwa namna tofauti pamoja na uendeshaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). 1. Kutaipunguzia TANESCO mzigo wa kuendesha mitambo hiyo ambapo kwa mwaka kwa mkoa wa Kigoma ilikuwa ikizalisha umeme kwa gharama ya TZS bilioni 52 huku ikikusanya TZS bilioni 14 tu, hivyo kupelekea kutenga zaidi ya TZS bilioni 38 kila mwaka ili kuhakikisha wananchi wa Kigoma wanapata nishati hiyo muhimu. Uwepo wa umeme wa gridi utaiwezesha Serikali kuelekeza fedha hizo kwenye shughuli nyingine za kimaendeleo na kijamii kama vile shule, afya, maji na miundombinu. 2. Uhitaji wa umeme kwa sasa katika mkoa wa ni megawati 14, lakini umeme uliopelekwa ni megawati 20, hivyo kuufanya kuwa na ziada, huku miradi mingine ya kuongeza umeme ikiendelea. Umeme wa uhakika utavutia wawekezaji hasa wa viwanda vikubwa kuwekeza mkoani humo katika viwanda vya kuchakata mawese na samaki, ambapo awali ingekuwa vigumu kutokana na kutokuwepo umeme wa kutosheleza. 3. Viwanda vikubwa na vidogo vitakavyoanzishwa kwa uwepo wa umeme vitawezesha wakazi wa mkoa huo, hasa vijana na wanawake kupata ajira za moja kwa moja au zisizo za moja kwa moja zitalazobadili maisha yao, na kuchangia ukuaji wa mkoa na Taifa. 4. Kukosekana kwa umeme wa uhakika kuliathiri hali ya maisha ya wakazi wa mkoa huo kutokana na… Read More

  • Historia, Rais Samia akizima majenereta na kuwasha umeme wa gridi ya Taifa Kigoma

    Rais Samia Suluhu Hassan leo Oktoba 17, 2022 kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi amewasha umeme wa Gridi ya Taifa katika Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma na kuzima mitambo mitatu ya mafuta yenye iliyokuwa ikizalisha umeme megawati 3.75 zilizotumika Wilaya ya Kasulu na Buhigwe. Uzimaji wa majenereta wilayani Kasulu ni mwendelezo wa uzimaji majenerata katika maeneo mbalimbali baada ya umeme wa gridi ya Taifa, ambapo maeneo mengine ni Kibondo, Loliondo, Ngara na Biharamulo. Kwa kuendesha majenereta kwa mkoa wa Kigoma pekee, Serikali ilikuwa ikipata hasara ya TZS bilioni 36 kila mwaka, kwani gharama za uendeshaji majenereta ilikuwa TZS bilioni 52 huku mapato yakiwa TZS bilioni 14. Mbali na kuondoa hasara hiyo umeme wa gridi ya Taifa utawezesha wakazi wa Kigoma kupata umeme wa kutosha ambapo uhitaji ni megawati 14, na Serikali imepeka megawati 20. Aidha, umeme utachochea shughuli za kiuchumi na uwekezaji katika sekta za biashara, viwanda, madini na kilimo, hivyo kuongeza mapato ya wananchi na Taifa. Pia, umeme utaimarisha shughuli za ulinzi na usalama na utoaji huduma zakijamii kwa wananchi na kuchochea ukuaji wa sekta nyingine. Read More