Mikataba saba

  • HISTORIA: Tanzania inajenga barabara 7 zenye kilomita 2,035 kwa wakati mmoja

    Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania, Serikali imesaini mikataba saba ya ujenzi wa barabara kuu ambazo zina jumla ya urefu wa kilomita 2,035, ambapo kwa miaka ya nyuma ili kuwa ikijenga wastani wa kilomita 200 hado 250 kwa mwaka. Barabara hizo ambazo zitapita kwenye mikoa 13 zitaboresha mtandao wa barabara nchini na kuongeza ufanisi katika sekta ya usafiri na usafirishaji na kuchochea uzalishaji katika maeneo zinapopita hatua ambayo itaongeza kasi ya ukuaji wa uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla, pamoja na kuchochea ukuaji wa sekta nyingine. Zaidi ya Watanzania 20,000 watapata ajira za moja kwa moja, ikiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo wahitimu wa vyuo vikuu kwa masharti ya mikataba ya ujenzi na usimamizi ambapo wahitimu wasiopungua 70 watapata ajira. Barabara zikazojengwa pamoja na mikoa ambayo zitapita; i) Barabara ya Kidatu – Ifakara – Lupiro – Malinyi – Kilosa Kwa Mpepo – Londo – Lumecha/Songea (km 435.8) inapita katika mikoa ya Morogoro na Ruvuma na inapita pia katika Majimbo ya Kilombelo, Ulanga, Malinyi na Namtumbo; ii) Barabara ya Arusha – Kibaya – Kongwa (km 453.42) inapita katika Mikoa ya Arusha, Manyara na Dodoma na inapita katika Majimbo ya Arusha Mjini, Arumeru Magharibi, Simanjiro, Kiteto na Kongwa; iii) Barabara ya Handeni – Kiberashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Olboroti – Mrijo Chini – Dalai – Bicha – Chambolo – Chemba – Kwa Mtoro – Singida (km 384.33) inapita katika Mikoa ya Tanga, Manyara, Dodoma na Singida na inapita katika Majimbo ya Kilindi, Chemba, Kiteto, Singida Mashariki na Iramba Mashariki; iv) Barabara ya Igawa – Songwe – Tunduma (njia nne) (km 237.9) inapita katika Mikoa ya Mbeya na Songwe na inapita katika Majimbo ya Mbarali, Mbeya Vijijini, Mbeya Mjini, Mbozi, Vwawa na Tunduma; v) Barabara ya Masasi – Nachingwea – Liwale (km 175) inapita katika Mikoa ya… Read More