• Mheshimiwa Rais Samia atunukiwa tuzo ya Afrika kwa mageuzi makubwa na maendeleo ya kijamii

    Kazi ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kuwatumikia Watanzania na kuchochea mageuzi kwenye kila sekta inaendelea kutambuliwa ndani na nje ya nchi ambapo leo amepokea Tuzo ya Wanawake 100 wenye Nguvu Afrika (The Power of 100 Africa Women Award) kutoka Access Bank Group. Tuzo hiyo ina malengo makuu matatu ambayo ni kutambua na kusherehekea wanawake wa Kiafrika wanaotoa michango ya mageuzi kwa mataifa na jamii zao, kuhamasisha na kuhimiza kizazi kijacho cha viongozi Wanawake katika bara zima la Afrika na kupaza sauti za Wanawake katika kuleta maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii barani Afrika. “Mheshimiwa Raisi, leo hii, tunaungana na Waafrika wote kukukabidhi tuzo hii maalumu […] kama kiongozi wa kuigwa ambaye utawala wake shirikishi, mageuzi ya kiuchumi, na utetezi wa jinsia unaendelea kuinua mamilioni ya watu, siyo tu nchini Tanzania, bali barani Afrika na duniani kwa ujumla,” amesema Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Access Bank Group, Protase Ishengoma. Mageuzi ambayo Mheshimiwa Rais ameyafanya nchini yameongeza idadi ya wanawake katika nafasi za uongozi, yamechochea kuimarika kwa biashara na kuvutia uwekezaji, yameboresha huduma za kijamii (afya, maji, elimu), kuimarisha amani, utulivu na demokrasia nchini, pamoja na kuongeza uwezo wa serikali kutekeleza miradi ya kimkakati ambayo inaboresha maisha ya wananchi. Read More

  • Tanzania yaongoza Afrika Mashariki kwa kuwa nchi yenye amani zaidi

    Kazi ya Amiri Jeshi Mkuu, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kuendelea kulinda amani ya nchi yetu imeendelea kutuletea matunda na heshima ambapo Tanzania imetajwa kuwa nchi yenye amani zaidi Afrika Mashariki kwa mujibu wa ripoti ya Global Peace Index ya mwaka 2025. Amani ni msingi wa maendeleo yoyote ambayo jamii au taifa linalenga kuyafikia iwe kiuchumi, kijamii na kisiasa. Tanzania kutajwa miongoni mwa nchi zenye amani zaidi kunaendelea kuitangaza sifa njema kimataifa na hivyo kuifanya kuaminia na kuvutia biashara, uwekezaji na watalii zaidi, hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi. Akitoa hotuba ya kuhitimisha shunguli za Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Rais alisema nchi pamoja na wananchi wake wapo salama kutokana na kazi kubwa inayofanywa na vyombo vya dola. Aidha, uimara huo umetokana na serikali kuvipatia vifaa vya kisasa, mafunzo, kuboresha maslahi pamoja na kuajiri watumishi wapya hivyo kuviongezea uwezo wa kutekeleza majukumu yake. Ripoti hiyo ambayo imehusisha nchi 163 duniani imetumia vigezo 23 kupima amani ya nchi ikiwemo ulinzi na usalama wa jamii na kiwango cha migogoro ya kitaifa na kimataifa na matumizi. Tanzania imeshika nafasi ya kwanza ikiwafuatiwa na Rwanda, Uganda, Kenya, Burundi, Somali, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Sudan Kusini. Read More

  • MAMA aweka rekodi kubwa nne makusanyo ya kodi kwa mwaka 2024/25

    Mwaka 2024/25 umekuwa mwaka wa rekodi kwenye ukusanyaji wa mapato nchini, ukusanyaji wa mapato wa TZS shilingi 32.26, sawa na ufanisi wa asilimia 103.9, umeiwezesha Serikali ya Awamu ya Sita kuweka rekodi kubwa nne. Rekodi zilizoweka ni kuvuka kwa lengo la mwaka la makusanyo ya kodi kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2015/16. Rekodi ya pili ni kuvuka lengo la makusanyo ya kila mwezi kwa miezi 12 mfululizo kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mwaka 1996. Rekodi ya tatu ni kuongezeka kwa wastani wa makusanyo ya kila mwezi hadi shilingi trilioni 2.69, ambacho ni kiwango cha juu zaidi katika historia ya TRA. Aidha, rekodi ya nne ni kufanikisha makusanyo ya juu zaidi kwa mwezi mmoja ambapo shilingi trilioni 3.58 zilikusanywa Desemba 2024. Matokeo haya yamechangiwa na kazi kubwa iliyofanywa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ya kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini. Miongoni mwa aliyofanya ni kurekebisha sheria na kanuni 66 pamoja na kufuta au kupunguza kodi, ada na tozo 383 ili kuondoa adha kwa wafanyabiashara. Hatua hizo zimeongeza ushirikiano mzuri kati ya TRA na walipakodi jambo ambalo limeongeza utayari wa wananchi kulipa kodi, kukua kwa shughuli za biashara na uwekezaji, kuimarika kwa ufanisi wa TRA katika kushughulikia masuala ya wateja, hasa kutokana na mamlaka hiyo kuongezewa watumishi. Read More

  • Mheshimiwa Rais awaeleza wananchi sababu za kuongezeka kwa Deni la Serikali

    Katika hotuba ya zaidi ya saa tatu kuhitimisha shughuli za Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Rais Suluhu Hassan ametumia zaidi ya dakika nane kuwaeleza wananchi kuhusu Deni la Serikali kufuatia uwepo wa upotoshaji unaofanywa na baadhi ya watu juu ya sababu halisi ya kuongezeka kwa deni hilo kufikia TZS trilioni 107. Katika hotuba yake, Mheshimiwa Rais amesema moja ya sababu ni kupokewa kwa fedha za mikopo mipya na ya zamani ambayo mikataba yake ilisainiwa wakati wa awamu zilizopita kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. “… mkopo unaweza kusainiwa leo lakini fedha husika zikaanza kupokelewa baada maandalizi ya mradi kukamilika na mradi kuanza. Hivyo, ili mkopo huo uingie kwenye deni la serikali ni lazima serikali iwe imepokea fedha hizo,” amesema hayo na kuongeza kuwa Awamu ya Sita imepokea TZS trilioni 11.3 ikiwa mikopo ya awamu zilizopita. Aidha, sababu nyingine ni kuimarika kwa dola ya Marekani dhidi ya shilingi ya Tanzania ambapo kutokana na utofauti wa viwango vya kubadili fedha, deni hilo limeongezeka kwa TZS trilioni 3.9. Licha ya kuwa kwa upande wa dola linabakia kiwango kile kile, lakini linapotajwa kwa shilingi ya Tanzania lazima lionekane limeongezeka kutokana na kushuka thamani kwa shilingi. “Hatua ya kushuka thamani kwa shilingi dhidi ya dola ya Marekani isichukuliwe kama ni hatua hasi, bali ilikuwa ni hatua muhimu ya kukabiliana na mtikisiko wa uchumi wa dunia,” amesisitiza Mheshimiwa Rais. Kwa upande mwingine, ongezeko la Deni la Serikali la Ndani kumetokana na mikopo kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo na kulipa madeni ya ndani yaliyoiva. Pia, ongezeko limetokana na serikali kutambua madeni ya mifuko ya hifadhi ya jamii kwa serikali kupitia hati fungani maalum isiyo taslimu yenye thamani ya TZS trilioni 2.6. “Lengo la hatua hizi ni kunusu mifuko ya hifadhi ya jamii, lakini pia wastaafu wetu waliotumikia taifa… Read More

  • Siri nyuma ya gawio la kihistoria la zaidi ya TZS trilioni 1 toka Mashirika ya Umma

    Kwa mara nyingine tena Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kufanya makubwa na kuweka rekodi katika kuwatumikia wananchi. Rekodi hii mpya ni ya Gawio la Serikali ambapo kwa mwaka 2024/25 (hadi Juni 10, 2025) lilifikia TZS trilioni 1.028, kiwango cha juu zaidi katika historia ya nchi yetu. Gawio hilo ambalo ni ongezeko ya asilimia 34 ikilinganishwa na TZS bilioni 767 zilipokelewa mwaka 2023/24 ni matokeo ya mabadiliko ya Mheshimiwa Rais, chini ya Falsafa ya 4R. Awamu ya Sita imefanya maboresho makubwa ya kisera, kisheria na kikanuni yaliyochagia kuimarisha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini, na hivyo mashirika hayo yakapata faida. Aidha, kutokana na mabadiliko hayo, taasisi zilizotoa gawio hadi tarehe ya kupokea ziliongezeka kwa asilimia 47 toka taasisi 145 mwaka 2024 hadi taasisi 213 mwaka 2025, ikiwa ni kati ya taasisi/mashirika 309 ambayo serikali inamiliki/inaumiliki. Akipokea gawio hilo, Mheshimiwa Rais aliwaeleza viongozi wa mashirika hayo kuwa gawio sio fadhila, bali ni wajibu kutokana na uwekezaji wa serikali. Hata hivyo, amewataka kutoyakamua mashirika ili nao waonekane wametoa gawio, badala yake watoe kwa mujibu wa sheria na kulingana na faida waliyopata. Amesema kuwa lengo lake ni kuona mashirika yanachangia angalau asilimia 10 ya mapato yasiyo ya kodi kwa Serikali, ingawa sheria inataka yachangie asilimia 15. Alitumia wasaa huo kusisitiza umuhimu wa sekta binafsi katika kukuza uchumi akisema kuwa “sekta binafsi ni kiungo muhimu katika safari ya mageuzi ya sekta ya umma na kwamba popote uhitaji utakapokuwepo, watashirikiana nao. Read More

  • Mheshimiwa Rais aagiza Polisi kudhibiti viashiria vya uvunjifu wa amani nchini

    Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameliagiza Jeshi la Polisi kutosubiri amani ivunjwe ndipo wachukue hatua, badala yake wadhibiti viashiria vya uvunjifu wa amani, hasa wakati huu ambapo nchi inajiandaa kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 2025. “Niwatake mjipange vilivyo kuhakikisha mnaendelea kudhibiti viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani. Tusisubiri amani ivunjwe,” amesema Mheshimiwa Rais ambapo yeye kwa dhamana aliyonayo kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania ndiye mlinzi namba moja wa amani ya nchi. Akizungumza katika sherehe za kufunga kozi ya Maafisa na Wakaguzi Wasaidizi wa Jeshi la Polisi, mbali na suala la amani Mheshimiwa Rais ametoa maelekezo mengine kwa jeshi hilo ili kuimarisha ari na ufanisi katika ulinzi wa raia na mali zao, ikiwemo kuzingatia maadili kwa kila askari kumheshimu mwenzake na kuepuka vitendo visiyokubali kama vile rushwa. Maagizo mengine ni pamoja na kuzingatia haki, na kwamba askari hatakiwi kumwogopa mtu yeyote lakini hatakiwi kumwonea yeyote. Pia, amehimiza mafunzo ya utayari ambayo yanaendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia, kuimarisha matumizi ya teknolojia, matahali kusomana kwa mifumo, kudhibiti dawa za kulevya na kujenga uhusiano na ushirikiano mwema na jamii pamoja na vyombo vingine vya dola vya nje ya nchi, hasa katika kudhibiti uhalifu unaovuka mipaka. Aidha, amewataka wahitimu hao kuzingatia viapo vyao vya kazi, kuepuka vitendo vya rushwa na kuwa kielelezo cha mabadiliko chanya na maboresho ya kiutendaji kwenye maeneo yao ya kazi. Read More

  • Mama ameweka rekodi ya kwanza ndani ya Jeshi la Polisi, akifunga kozi wahitimu 954

    Kwa mara nyingine tena Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuweka rekodi kwenye sekta mbalimbali ambapo chini ya uongozi wake, Chuo cha Taalum ya Polisi Dar es Salaam (DPA) kimekuwa na idadi kubwa ya wahitimu kwa mara moja, katika historia ya chuo hicho na nchi kwa ujumla. Juni 9, 2025, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alifunga kozi ya Maafisa na Wakaguzi Wasaidizi ambapo kulikuwa na jumla ya wahitimu 954, kati yao maafisa wakiwa ni 780 na Wakaguzi Wasaidizi wakiwa 174. Idadi hii ni kubwa zaidi tangu kuanzishwa kwa chuo hicho mwaka 1961. Kuhitimu kwao kuna maanisha kuwa wamepanda vyeo, hatua ambayo kwa mara nyingine inathibitisha azma yake ya kuboresha ustawi wa watumishi wa jeshi hilo ili kuwaongezea ari na ufanisi katika kutekeleza jukumu lao la msingi la kulinda raia na mali zao. Mfano mmoja unaothibitisha hili, katika kipindi cha Julai 2024 hadi Aprili 2025 jumla ya maafisa, wakaguzi na askari 16,896 wamepandishwa vyeo ndani ya Jeshi la Polisi hatua ambayo imeongeza morali ya utendaji kazi na ufanisi. Aidha, katika mwaka ujao wa fedha (2025/26) Mheshimiwa Rais anakusudia kuwapandisha vyeo maafisa, wakaguzi na askari 8,325 wa jeshi hilo. Kupanda vyeo kuna ambatana na nyongeza za mishahara hatua ambayo inawawezesha watumishi hao kumudu gharama za maisha na kufanya shughuli zao za maendeleo. Read More

  • Mageuzi ya Rais Samia yaongeza gawio la mashirika ya umma hadi bilioni 900

    Moja ya ‘R’ katika falasafa ya 4R ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inawakilisha’Reforms’ (Mabadiliko) ambapo amelenga kutoa fursa zaidi kwa watu wengi zaidi kunufaika kiuchumi badala ya wachache. Matokeo ya mabadiliko hayo kiuchumi tunaendelea kuyashuhudia ambapo mabadiliko yaliyofanywa kwenye uendeshaji wa mashirika ya umma umeongeza gawio linalotolewa kwa Serikali kwa mwaka 2024/25. Gawio hilo limeongeza kwa asilimia 40 toka TZS bilioni 633.3 mwaka 2023/24 hadi zaidi ya TZS bilioni 900 iliyokusanywa hadi sasa ambapo lengo ni kukusanya TZS trilioni 1 kabla ya Juni 10 mwaka huu ambapo gawio hilo litakabidhiwa kwa Mheshimiwa Rais. Aidha, mabadiliko hayo si tu yameongeza gawio bali pia yameongeza mashirika yanayotoa gawio ambapo kwa mwaka huu ni zaidi ya 200 ikilinganishwa na wastani wa mashirika 146 kuanzia mwaka 2021/22 hadi mwaka 2023/24. Mageuzi yaliyofanywa ikiwemo kuyapa uhuru na kuyawezesha kujiendesha kibiashara yamewezesha mashirika yaliyokuwa yanapata hasara kuanza kupata faida. Mageuzi mengine ni kuunganishwa kwa taasisi 14 na kufutwa kwa taasisi nyingine, kuongeza uwazi na uwajibikaji pamoja na ufanisi katika kutathmini bodi za wakurugenzi. Haya ni mafanikio makubwa ya Serikali ya Awamu ya Sita kwani yanaipunguzia serikali mzigo wa kuhudumia taasisi hizo kwa kuzipa ruzuku, lakini pia kunaleta tija ya kuanzishwa kwa taasisi hizo hasa katika kuwahudumia wananchi na kuchangia katika ukuaji wa uchumi. Read More

  • Ilani ya CCM (2025-2030) imebeba ajenda zinazogusa maisha ya wananchi

    Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Ndugu Samia Suluhu Hassan Mei 30 mwaka huu ameongoza chama hicho kuzindua Ilani ya Uchaguzi (2025-2030) ambayo imebeba ajenda tisa, ambazo ni matamanio ya wananchi ambayo wamekuwa wakitaka kuona serikali ikiyafanyia kazi ili kuboresha maisha yao na kuchochea maendeleo ya Taifa. Katika kipindi hicho cha miaka mitano, lengo kuu la serikali litakuwa kukuza uchumi na kuimarisha ustawi wa wananchi. Ili kufikia lengo hilo, mkazo mkubwa utawekwa katika maeneo tisa ambayo ni, kuchochea mapinduzi ya kiuchumi, kuzalisha ajira, kuboresha maisha ya wananchi, kuimarisha miundombinu ya usafiri na usafirishaji, kukuza matumizi ya sayansi na teknolojia, kudumisha amani, utulivu na usalama, kudumisha utamaduni na kukuza sanaa na michezo na kuongeza kasi ya maendeleo vijijini. Ni wazi kuwa, maeneo yote tisa yanagusa maisha ya wananchi, na hili linadhihirisha dhamira ya Dkt. Samia katika kuendelea na mageuzi kwa lengo la kutokomeza umaskini, kuinua hali za maisha ya Watanzania wote na kuinua ustawi wa jamii na Taifa letu. Amewahakikisha wananchi kuwa, kutokana na mafanikio makubwa ambayo CCM imeyapata katika utekelezaji wa ilani ya mwaka 2020-2025, ni wazi kuwa inauwezo wa kutekeleza ilani mpya, ambayo imetengezwa kwa weledi mkubwa ikijumuisha maoni ya wananchi na wadau mbalimbali pamoja na mapendekezo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. “Kubwa kwa Watanzania, ni kuweka utulivu ndani ya nchi yetu, kufanya kazi kwa bidhii,” amesema Dkt. Samia huku akiwaasa wananchi kumwomba Mwenyezi Mungu awasaidie kufanikisha yote waliyojipangia. Wananchi na taasisi zilizotoa maoni yao kuhusu ilani hiyo wamekipongeza chama hicho kuwa kimezingatia maoni yaliyotolewa, ambayo kwa muda mrefu yalikuwa ni matamanio ya wananchi ikiwemo suala la Katiba Mpya ambapo chama hicho kimeahidi kuhuisha na kukamilisha mchakato wa katiba hiyo. Read More

  • MAMA aboresha Sera ya Mambo ya Nje ili kukuza Diplomasia ya Uchumi na kulinda utamaduni wetu

    AKIAHIDI, ANATIMIZA. Hayo ndiyo maneno mawili yanayoweza kutumika kueleza tukio la Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuzindua Sera ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001 (Toleo la Mwaka 2024), ambayo ni ahadi aliyoitoa Aprili 2021 wakati akihutubia bunge, mwenzi mmoja baada ya kuingia madarakani. Akizungumza bungeni alisema kuwa serikali itaifanyia maboresho sera hiyo ili iendane na mabadiliko ambayo yametokea ndani na nje ya nchi katika sekta mbalimbali. Ikiwa ni miaka 24 tangu kupitishwa kwa sera hiyo, leo Mei 19, 2025 Mheshimiwa Rais amezindua toleo hilo ambalo limejikita katika Diplomasia ya Uchumi likilenga kulisukuma Taifa mbele na kuimarisha ushiriki na ushindani katika siasa na maendeleo ya kimataifa, kulinda na kutetea maslahi ya Tanzania kupitia diplomasia makini na shirikishi. Toleo la mwaka 2024 limeleta maboresho mbalimbali ambayo ni pamoja na kuongeza msingi mmoja (wa nane) katika Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania. Msingi huo ni kulinda na kuendeleza maadili, mila na utamaduni wa Mtanzania ikiwemo kukuza matumizi ya lugha ya Kiswahili, hatua ambayo inalenga kukabiliana na uvamizi mkubwa wa utamaduni na ustaarabu unaoendelea. Aidha, mambo mengine manne yaliyoongezwa ni, moja, kuimarisha Diplomasia ya Uchumi kwa kuvutia uwekezaji wa mitaji mikubwa, kutumia vizuri fursa ya kijografia tuliyojaliwa na kufaidika na soko huru la biashara Afrika. Pili, ni matumizi ya lugha ya Kiswahili kama nyenzo ya kujenga ushawishi ili kupanua masoko ndani na nje ya Afrika. Tatu, kukuza ushiriki wa Diaspora katika kukuza uchumi wao binafsi na uchumi wa taifa, na nne ni kuangalia fursa mpya za ushirikiano wa kiuchumi ikiwemo uchumi wa buluu ili kuchochea ukuaji wa kiuchumi. Ametumia nafasi hiyo kuwapongeza wote walioshiriki kuandaa sera hiyo, hasa wananchi waliotoa maoni akisema kuwa “mmeshiriki katika kujenga hatma ya nchi yenu na mmeweka alama isiyofutika.” Read More

1 2 3 16