• Siri nyuma ya gawio la kihistoria la zaidi ya TZS trilioni 1 toka Mashirika ya Umma

    Kwa mara nyingine tena Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kufanya makubwa na kuweka rekodi katika kuwatumikia wananchi. Rekodi hii mpya ni ya Gawio la Serikali ambapo kwa mwaka 2024/25 (hadi Juni 10, 2025) lilifikia TZS trilioni 1.028, kiwango cha juu zaidi katika historia ya nchi yetu. Gawio hilo ambalo ni ongezeko ya asilimia 34 ikilinganishwa na TZS bilioni 767 zilipokelewa mwaka 2023/24 ni matokeo ya mabadiliko ya Mheshimiwa Rais, chini ya Falsafa ya 4R. Awamu ya Sita imefanya maboresho makubwa ya kisera, kisheria na kikanuni yaliyochagia kuimarisha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini, na hivyo mashirika hayo yakapata faida. Aidha, kutokana na mabadiliko hayo, taasisi zilizotoa gawio hadi tarehe ya kupokea ziliongezeka kwa asilimia 47 toka taasisi 145 mwaka 2024 hadi taasisi 213 mwaka 2025, ikiwa ni kati ya taasisi/mashirika 309 ambayo serikali inamiliki/inaumiliki. Akipokea gawio hilo, Mheshimiwa Rais aliwaeleza viongozi wa mashirika hayo kuwa gawio sio fadhila, bali ni wajibu kutokana na uwekezaji wa serikali. Hata hivyo, amewataka kutoyakamua mashirika ili nao waonekane wametoa gawio, badala yake watoe kwa mujibu wa sheria na kulingana na faida waliyopata. Amesema kuwa lengo lake ni kuona mashirika yanachangia angalau asilimia 10 ya mapato yasiyo ya kodi kwa Serikali, ingawa sheria inataka yachangie asilimia 15. Alitumia wasaa huo kusisitiza umuhimu wa sekta binafsi katika kukuza uchumi akisema kuwa “sekta binafsi ni kiungo muhimu katika safari ya mageuzi ya sekta ya umma na kwamba popote uhitaji utakapokuwepo, watashirikiana nao. Read More

  • Mheshimiwa Rais aagiza Polisi kudhibiti viashiria vya uvunjifu wa amani nchini

    Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameliagiza Jeshi la Polisi kutosubiri amani ivunjwe ndipo wachukue hatua, badala yake wadhibiti viashiria vya uvunjifu wa amani, hasa wakati huu ambapo nchi inajiandaa kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 2025. “Niwatake mjipange vilivyo kuhakikisha mnaendelea kudhibiti viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani. Tusisubiri amani ivunjwe,” amesema Mheshimiwa Rais ambapo yeye kwa dhamana aliyonayo kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania ndiye mlinzi namba moja wa amani ya nchi. Akizungumza katika sherehe za kufunga kozi ya Maafisa na Wakaguzi Wasaidizi wa Jeshi la Polisi, mbali na suala la amani Mheshimiwa Rais ametoa maelekezo mengine kwa jeshi hilo ili kuimarisha ari na ufanisi katika ulinzi wa raia na mali zao, ikiwemo kuzingatia maadili kwa kila askari kumheshimu mwenzake na kuepuka vitendo visiyokubali kama vile rushwa. Maagizo mengine ni pamoja na kuzingatia haki, na kwamba askari hatakiwi kumwogopa mtu yeyote lakini hatakiwi kumwonea yeyote. Pia, amehimiza mafunzo ya utayari ambayo yanaendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia, kuimarisha matumizi ya teknolojia, matahali kusomana kwa mifumo, kudhibiti dawa za kulevya na kujenga uhusiano na ushirikiano mwema na jamii pamoja na vyombo vingine vya dola vya nje ya nchi, hasa katika kudhibiti uhalifu unaovuka mipaka. Aidha, amewataka wahitimu hao kuzingatia viapo vyao vya kazi, kuepuka vitendo vya rushwa na kuwa kielelezo cha mabadiliko chanya na maboresho ya kiutendaji kwenye maeneo yao ya kazi. Read More

  • Mama ameweka rekodi ya kwanza ndani ya Jeshi la Polisi, akifunga kozi wahitimu 954

    Kwa mara nyingine tena Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuweka rekodi kwenye sekta mbalimbali ambapo chini ya uongozi wake, Chuo cha Taalum ya Polisi Dar es Salaam (DPA) kimekuwa na idadi kubwa ya wahitimu kwa mara moja, katika historia ya chuo hicho na nchi kwa ujumla. Juni 9, 2025, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alifunga kozi ya Maafisa na Wakaguzi Wasaidizi ambapo kulikuwa na jumla ya wahitimu 954, kati yao maafisa wakiwa ni 780 na Wakaguzi Wasaidizi wakiwa 174. Idadi hii ni kubwa zaidi tangu kuanzishwa kwa chuo hicho mwaka 1961. Kuhitimu kwao kuna maanisha kuwa wamepanda vyeo, hatua ambayo kwa mara nyingine inathibitisha azma yake ya kuboresha ustawi wa watumishi wa jeshi hilo ili kuwaongezea ari na ufanisi katika kutekeleza jukumu lao la msingi la kulinda raia na mali zao. Mfano mmoja unaothibitisha hili, katika kipindi cha Julai 2024 hadi Aprili 2025 jumla ya maafisa, wakaguzi na askari 16,896 wamepandishwa vyeo ndani ya Jeshi la Polisi hatua ambayo imeongeza morali ya utendaji kazi na ufanisi. Aidha, katika mwaka ujao wa fedha (2025/26) Mheshimiwa Rais anakusudia kuwapandisha vyeo maafisa, wakaguzi na askari 8,325 wa jeshi hilo. Kupanda vyeo kuna ambatana na nyongeza za mishahara hatua ambayo inawawezesha watumishi hao kumudu gharama za maisha na kufanya shughuli zao za maendeleo. Read More

  • Mageuzi ya Rais Samia yaongeza gawio la mashirika ya umma hadi bilioni 900

    Moja ya ‘R’ katika falasafa ya 4R ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inawakilisha’Reforms’ (Mabadiliko) ambapo amelenga kutoa fursa zaidi kwa watu wengi zaidi kunufaika kiuchumi badala ya wachache. Matokeo ya mabadiliko hayo kiuchumi tunaendelea kuyashuhudia ambapo mabadiliko yaliyofanywa kwenye uendeshaji wa mashirika ya umma umeongeza gawio linalotolewa kwa Serikali kwa mwaka 2024/25. Gawio hilo limeongeza kwa asilimia 40 toka TZS bilioni 633.3 mwaka 2023/24 hadi zaidi ya TZS bilioni 900 iliyokusanywa hadi sasa ambapo lengo ni kukusanya TZS trilioni 1 kabla ya Juni 10 mwaka huu ambapo gawio hilo litakabidhiwa kwa Mheshimiwa Rais. Aidha, mabadiliko hayo si tu yameongeza gawio bali pia yameongeza mashirika yanayotoa gawio ambapo kwa mwaka huu ni zaidi ya 200 ikilinganishwa na wastani wa mashirika 146 kuanzia mwaka 2021/22 hadi mwaka 2023/24. Mageuzi yaliyofanywa ikiwemo kuyapa uhuru na kuyawezesha kujiendesha kibiashara yamewezesha mashirika yaliyokuwa yanapata hasara kuanza kupata faida. Mageuzi mengine ni kuunganishwa kwa taasisi 14 na kufutwa kwa taasisi nyingine, kuongeza uwazi na uwajibikaji pamoja na ufanisi katika kutathmini bodi za wakurugenzi. Haya ni mafanikio makubwa ya Serikali ya Awamu ya Sita kwani yanaipunguzia serikali mzigo wa kuhudumia taasisi hizo kwa kuzipa ruzuku, lakini pia kunaleta tija ya kuanzishwa kwa taasisi hizo hasa katika kuwahudumia wananchi na kuchangia katika ukuaji wa uchumi. Read More

  • Ilani ya CCM (2025-2030) imebeba ajenda zinazogusa maisha ya wananchi

    Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Ndugu Samia Suluhu Hassan Mei 30 mwaka huu ameongoza chama hicho kuzindua Ilani ya Uchaguzi (2025-2030) ambayo imebeba ajenda tisa, ambazo ni matamanio ya wananchi ambayo wamekuwa wakitaka kuona serikali ikiyafanyia kazi ili kuboresha maisha yao na kuchochea maendeleo ya Taifa. Katika kipindi hicho cha miaka mitano, lengo kuu la serikali litakuwa kukuza uchumi na kuimarisha ustawi wa wananchi. Ili kufikia lengo hilo, mkazo mkubwa utawekwa katika maeneo tisa ambayo ni, kuchochea mapinduzi ya kiuchumi, kuzalisha ajira, kuboresha maisha ya wananchi, kuimarisha miundombinu ya usafiri na usafirishaji, kukuza matumizi ya sayansi na teknolojia, kudumisha amani, utulivu na usalama, kudumisha utamaduni na kukuza sanaa na michezo na kuongeza kasi ya maendeleo vijijini. Ni wazi kuwa, maeneo yote tisa yanagusa maisha ya wananchi, na hili linadhihirisha dhamira ya Dkt. Samia katika kuendelea na mageuzi kwa lengo la kutokomeza umaskini, kuinua hali za maisha ya Watanzania wote na kuinua ustawi wa jamii na Taifa letu. Amewahakikisha wananchi kuwa, kutokana na mafanikio makubwa ambayo CCM imeyapata katika utekelezaji wa ilani ya mwaka 2020-2025, ni wazi kuwa inauwezo wa kutekeleza ilani mpya, ambayo imetengezwa kwa weledi mkubwa ikijumuisha maoni ya wananchi na wadau mbalimbali pamoja na mapendekezo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. “Kubwa kwa Watanzania, ni kuweka utulivu ndani ya nchi yetu, kufanya kazi kwa bidhii,” amesema Dkt. Samia huku akiwaasa wananchi kumwomba Mwenyezi Mungu awasaidie kufanikisha yote waliyojipangia. Wananchi na taasisi zilizotoa maoni yao kuhusu ilani hiyo wamekipongeza chama hicho kuwa kimezingatia maoni yaliyotolewa, ambayo kwa muda mrefu yalikuwa ni matamanio ya wananchi ikiwemo suala la Katiba Mpya ambapo chama hicho kimeahidi kuhuisha na kukamilisha mchakato wa katiba hiyo. Read More

  • MAMA aboresha Sera ya Mambo ya Nje ili kukuza Diplomasia ya Uchumi na kulinda utamaduni wetu

    AKIAHIDI, ANATIMIZA. Hayo ndiyo maneno mawili yanayoweza kutumika kueleza tukio la Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuzindua Sera ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001 (Toleo la Mwaka 2024), ambayo ni ahadi aliyoitoa Aprili 2021 wakati akihutubia bunge, mwenzi mmoja baada ya kuingia madarakani. Akizungumza bungeni alisema kuwa serikali itaifanyia maboresho sera hiyo ili iendane na mabadiliko ambayo yametokea ndani na nje ya nchi katika sekta mbalimbali. Ikiwa ni miaka 24 tangu kupitishwa kwa sera hiyo, leo Mei 19, 2025 Mheshimiwa Rais amezindua toleo hilo ambalo limejikita katika Diplomasia ya Uchumi likilenga kulisukuma Taifa mbele na kuimarisha ushiriki na ushindani katika siasa na maendeleo ya kimataifa, kulinda na kutetea maslahi ya Tanzania kupitia diplomasia makini na shirikishi. Toleo la mwaka 2024 limeleta maboresho mbalimbali ambayo ni pamoja na kuongeza msingi mmoja (wa nane) katika Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania. Msingi huo ni kulinda na kuendeleza maadili, mila na utamaduni wa Mtanzania ikiwemo kukuza matumizi ya lugha ya Kiswahili, hatua ambayo inalenga kukabiliana na uvamizi mkubwa wa utamaduni na ustaarabu unaoendelea. Aidha, mambo mengine manne yaliyoongezwa ni, moja, kuimarisha Diplomasia ya Uchumi kwa kuvutia uwekezaji wa mitaji mikubwa, kutumia vizuri fursa ya kijografia tuliyojaliwa na kufaidika na soko huru la biashara Afrika. Pili, ni matumizi ya lugha ya Kiswahili kama nyenzo ya kujenga ushawishi ili kupanua masoko ndani na nje ya Afrika. Tatu, kukuza ushiriki wa Diaspora katika kukuza uchumi wao binafsi na uchumi wa taifa, na nne ni kuangalia fursa mpya za ushirikiano wa kiuchumi ikiwemo uchumi wa buluu ili kuchochea ukuaji wa kiuchumi. Ametumia nafasi hiyo kuwapongeza wote walioshiriki kuandaa sera hiyo, hasa wananchi waliotoa maoni akisema kuwa “mmeshiriki katika kujenga hatma ya nchi yenu na mmeweka alama isiyofutika.” Read More

  • DP World yaongeza mapato Bandari ya Dar kwa zaidi ya TZS trilioni 1

    Falsafa ya 4R (Reconciliation, Resilience, Reform, and Rebuild) ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuleta mageuzi katika sekta mbalimbali zinazogusa maisha ya Watanzania na kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchini. Moja ya sekta hizo ni uchukuzi, ambapo Mageuzi (Reform) yaliyofanywa katika Bandari ya Dar es Salaam kwa kuingia ubia na Kampuni za DP World na Tanzania East Africa Gateway Terminal Limited (TEAGTL) katika kuendeleza na kuendesha baadhi ya maeneo ya bandari hiyo yameendelea kuleta matokeo, ikiwemo kuongeza mapato. Kati ya Julai, 2024 hadi Februari 2025, mapato yatokanayo na Kodi ya Forodha kutoka bandarini yanayokusanywa kutokana na shughuli za kibandari yamefikia TZS trilioni 8.26, ambalo ni ongezeko la TZS trillion 1.18 ikilinganishwa na makusanyo ya TZS trilioni 7.08 yaliyokusanywa kipindi kama hicho kwa mwaka 2023/24. Mafanikio hayo yametokana na wawekezaji hao kuwezesha upatikanaji wa vifaa na mitambo ya kisasa na mifumo ya TEHAMA inayoendelea kuleta ufanisi katika uendeshaji wa shughuli za kibandari, hasa kuondoa msongamano wa mizigo na foleni za meli, hali inayochochea wafanyabiashara zaidi kuchagua kutumia bandari hiyo, hivyo kuongeza mapato. Lengo la Mheshimiwa Rais Samia kushirikisha sekta binafsi ni kuongeza tija katika utendaji wa bandari nchini ili kuziwezesha zichangie zaidi katika ukuaji wa uchumi wa Taifa letu na maendeleo ya wananchi kwa ujumla kwa kuwafanya wanufaike na rasilimali za nchi yao. Read More

  • MAMA akamilisha miradi ya maji zaidi ya 2,000; mamilioni ya wananchi wapata maji safi

    Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuleta mageuzi makubwa katika sekta mbalimbali nchini ambapo katika sekta ya maji, ndani ya kipindi cha miaka minne amekamilisha miradi ya maji zaidi ya 2,331 mijini na vijijini ambayo imefikisha maji kwa mamilioni ya wananchi. Kutokana na ufanisi huo asilimia 83 ya wakazi wote wa vijijini wanapata maji safi na salama ikiwa ni ongezeko toka asilimia 72.3 alizokuta wakati anaingia madarakani Machi 2021. Aidha, kwa sasa asilimia 91.6 ya wananchi wa mijini wanapata huduma ya maji safi na salama ikilinganishwa na wastani wa asilimia 86 aliyoikuta. Mafanikio haya yanakaribia lengo lililoanishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (2020-2025) ambayo inaielekeza serikali kuongeza kasi ya usambazaji majisafi na salama ili kutosheleza mahitaji kwa zaidi ya asilimia 85 vijijini na zaidi ya asilimia 95 kwa mijini, kwa upande wa Tanzania Bara, ifikapo Desemba 2025. Ili kuhakikisha lengo la ilani, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji 1,544. Hatua hii inadhihirisha dhamira ya dhati ya Mheshimiwa Rais kufikisha maji kwa kila mwananchi popote alipo akitambua kuwa maji ni uhai, maendeleo na usalama kwa wananchi. Read More

  • Mama ashusha neema kwa watumishi wa umma; kima cha chini cha mshahara ni laki 5

    Ni furaha furi furi kama sio furaha bojo bojo kwa watumishi wa umma na Watanzania kwa ujumla baada ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza nyongeza ya kima cha chini cha mshahara kwa asilimia 35.1. Kutokana na nyongeza hiyo, kima cha chini kuanzia Julai 1, 2025 kitakuwa TZS 500,000 toka kiwango cha TZS 370,000 cha sasa. Mheshimiwa Rais ametangaza neema hiyo katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Dunia (Mei Mosi) ambayo kitaifa imefanyika mkoani Singida ikiwa na kaulimbiu isemayo, “Uchaguzi Mkuu 2025 utuletee viongozi wanaojali haki na maslahi ya wafanyakazi wote, sote tushiriki.” Amesema nyongeza hiyo ni sehemu ya hatua ambazo serikali yake imeendelea kuchukua kuleta ustawi kwa wafanyakazi nchini, na kwamba uamuzi huo umewezeshwa na kasi ya ukuaji wa uchumi kupanda hadi kufikia 5.5% kwa mwaka, hali iliyochangiwa na wafanyakazi kujituma na kufanya kazi kwa bidii. Kupitia mitandao ya kijamii wananchi wamefurahia nyongeza hiyo ambapo wameandika jumbe za kumpongeza. Baadhi ya jumbe hizo ni; “Nakuamini na nakupenda sana mama maisha yangu yote sijawahi kupiga kura ila mwaka huu inshallah nna Imani kura yangu unayo ya kwanza kwenye maisha yangu,”- Hamoud Jimia. “Ubarkiwe mama ikulu yako huna mpinzani hata kidgo,”- Kisila Legandy “Safi mama Samia, wewe ndo unatudai na tunakuhakikishia lazima tukulipe,”- Julius Peter “Kima cha chini cha mashahara kinapanda kutoka 300k mpaka 500k nomaa,”- Msaki. Kuhusu sekta binafsi Mheshimiwa Rais amesema kuwa Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara inaendelea na tathmini kwa lengo la kuboresha viwango vya mishahara kwa sekta binafsi. “Tutaendelea kuboresha mazingira ya wafanyakazi ikiwemo maslahi ya wafanyakazi kwa kadiri hali itakavyoruhusu… Ili tuweze kujenga vyema Taifa letu ni lazima tulinde amani na utulivu nchini,” amesisitiza Rais Dkt. Samia. Read More

  • Isome hapa hotuba ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu katika Miaka 61 ya Muungano wa Tanzania

    Isome hapa hotuba ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika maadhimisho ya Miaka 61 ya Muungano wa Tanzania. Read More

1 2 3 16