Mama Yukokazini

  • Tanzania imevunja rekodi ya makusanyo ya juu zaidi ya kodi tangu kuanzishwa kwa TRA

    Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA imevunja rekodi ya makusanyo tangu kuanzishwa kwake kwa kukusanya Shilingi Trilioni 3.587 kwa Mwezi wa Desemba sawa na asilimia 103.52 ya lengo ambalo lilikuwa ni kukusanya Shilingi Trilion 3.465. Makusanyo hayo ni sawa na ukuaji wa asilimia 17.59 ukilinganisha na kiasi cha Shilingi Trilioni 3.050 zilizokusanywa mwezi Desemba mwaka 2023. Taarifa iliyotolewa TRA imeeleza kuwa mbali na kuvuka malengo ya Mwezi Desemba katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2024/2025 (Oktoba-Desemba 2024) imefanikiwa kukusanya kiasi cha Shilingi Trilioni 8.741 sawa na ufanisi wa asilimia 104.63 ya lengo la kukusanya Shilingi Trilioni 8.354 ambayo ni sawa na ukuaji wa asilimia 19.05 ukilinganisha na kiasi cha Shilingi Trilioni 7.342 zilizokusanywa katika kipindi kama hicho mwaka wa fedha 2023/24. Vilevile TRA imeandika rekodi mpya ya kuweza kufikia na kuvuka lengo la makusanyo kwa miezi sita mfululizo katika nusu ya kwanza ya mwaka wa fedha 2024/2025. Kamishna Mkuu wa TRA Bwn. Yusuph Mwenda amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa miongozo mizuri iliyowawezesha kukusanya kodi kwa hiari na kuvuka malengo. Read More

  • Wanafunzi wote 974,332 kujiunga na kidato cha kwanza 2025.

    Serikali imetangaza wanafunzi wote 974,332 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2025 bila kusubiri machaguo kama ilivyokuwa ikifanyika miaka iliyopita. Kwa miaka kadhaa iliyopita ilizoeleka wanafunzi waliohitimu darasa la saba aidha kushindwa kujiunga au kujiunga na elimu ya sekondari kwa mafungu kutokana na sababu mbalimbali lakini chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan suala hilo limefikia ukomo. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi ya Rais-TAMISEMI wanafunzi wote waliofaulu wataanza masomo kwa wakati mmoja ikiwa ni matokeo ya maandalizi ya mapema yaliyofanywa na Serikali ili kuhakikisha kuwa wanafunzi wote watakaofaulu mtihani wa kumaliza darasa la saba mwaka 2024 wanajiunga na elimu ya sekondari ifikapo Januari 13, 2025. Miongoni mwa shughuli za maandalizi zilizofanyika ni kujenga na kuboresha miundombinu ya shule ikiwemo vyumba vya madarasa, nyumba za walimu pamoja na uwepo wa madawati na walimu wa kutosha ikikukmbukwa kuwa serikali imetangaza ajira mpya za walimu 3,633 hivi karibuni. Kati ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wasichana ni 525,225 na wavulana ni 449,107. Read More

  • Rais Samia akutana na viongozi wa Ngorongoro, kuunda Tume mbili

    Jumapili, Desemba mosi, 2024 katika Ikulu ndogo ya Arusha, Rais wa Jamhuri ya Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa kisiasa na wa kimila wa jamii ya Kimaasai (Malaigwanani) wanaoishi eneo la Ngorongoro na maeneo ya jirani. Mkutano huo umefanyika kwa lengo la kuwasikiliza viongozi hao kufuatia kuwepo kwa malalamiko dhidi ya baadhi ya maamuzi ya Serikali yanayohusu eneo la Ngorongoro. Katika mazungumzo hayo Rais Dkt. Samia amesema ataunda Tume mbili ambapo moja itachunguza na kutoa mapendakezo kuhusu masuala ya ardhi yanayolalamikiwa na wakazi wa Ngorongoro na nyingine itaangalia utekelezaji wa zoezi zima la uhamiaji kwa hiari kutoka eneo la Hifadhi ya Ngorongoro. Rais Dkt. Samia amewahakikishia kuwa Serikali itaendelea kuimarisha utendaji kazi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA) kwa lengo la kuimarisha mahusiano kati ya Serikali na jamii hiyo huku pia akisisitiza ulazima wa wananchi kushirikishwa ipasavyo katika upangaji na utekelezaji miradi inayopita kwenye maeneo yao. Aidha, Rais Dkt. Samia amesisitiza kuwa Tanzania ni nchi inayojivunia umoja wa kitaifa na yenye Serikali inayowahudumia Watanzania wote. Hivyo, ameitaka Ofisi ya Rais TAMISEMI kushughulikia changamoto zinazojitokeza ikiwemo kukosekana kwa baadhi ya huduma za msingi za kijamii katika eneo la  Ngorongoro.   Read More

  • Rais Samia anavyoacha alama za kipekee katika soka la bongo

    Zaidi ya mashabiki 60,000 walioujaza Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam walilipuka kwa shangwe baada ya mwamuzi kupuliza filimbi ya kumaliza mchezo dhidi ya Guinea na kuibuka na ushindi wa goli 1-0, ushindi uliomaanisha kuwa Tanzania kwa mara ya nne imefuzu kushiriki michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 itakayofanyika nchini Morroco Tanzania inafuzu kushiriki michuano hii kwa mara ya nne ikiwa imefanya hivyo mwaka 1981, 2019, 2023 na sasa 2025. Kwa hatua hii Mheshimiwa Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan anaingia katika vitabu vya kumbukumbu na historia ya michezo nchini kwa kuwa Rais ambaye chini ya uongozi wake timu ya Taifa imefanikiwa kufuzu kushiriki mashindano haya makubwa zaidi kwa ngazi ya nchi barani Afrika mara mbili tena mfululizo. Mafanikio haya hayatokei kwa bahati mbaya na ni dhahiri kuwa ni matokeo uongozi thabiti na motisha kutoka kwa Rais Samia Suluhu Hassan. Sote tunafahamu namna ambavyo amekuwa akichochea timu za Taifa na hata vilabu vinavyoshiriki michuano ya kimataifa kupata matokeo chanya kwa kuweka motisha ya goli la Mama. Katika mchezo dhidi ya Ethiopia uliofanyika nchini Congo, Rais Samia alitoa ndege maalum iliyowapeleka wachezaji katika mchezo ule na kuwawezeshea kurejea kwa wakati nchini kujiandaa na mchezo dhidi ya Guinea ambao ndio umeipatia Tanzania tiketi ya kufuzu Afcon 2025. Ushindi dhidi ya Guinea ulichagizwa kwa kiasi kikubwa na nguvu ya mashabiki zaidi ya 60,000 walioujaza uwanja wa Taifa. Nakukumbusha tu mashabiki hawa wote waliingia bure kwani Rais Samia aliwalipia wote viingilio ili tu wajitokeze kwa wingi kuiunga mkono Taifa Stars. Habari njema zaidi ni kwamba baada ya Afcon 2025, michuano inayofuata mwaka 2027 Tanzania pia imo ndani kwani kwa mara ya kwanza michuano hii itafanyika katika ardhi ya Afrika Mashariki kwa ushirikiano wa Tanzania, Kenya na Uganda hivyo tayari tuna tiketi ya moja kwa moja. Mashindano haya kuja Afrika Mashariki… Read More

  • Ajira 600,000 zazalishwa nchini ndani ya miezi saba

    Kati ya mwezi Januari hadi Julai 2024 jumla ya ajira 607,475 zimezalishwa nchini ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali kufikia lengo la kuzalisha ajira milioni 1.2 kila mwaka. Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Patrobas Katambi ameeleza hayo bungeni jijini Dodoma. Jitihada za kuhakikisha watanzania wanapata ajira zinaakisi lengo la kuzalisha ajira milioni nane kama ilivyoelezwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) 2020-2025. Akizungumzia maeneo ambayo Serikali inayaangazia katika kuzalisha ajira ameeleza kuwa Serikali inatumia balozi zake kutafuta nafasi za kazi kwa watanzania kwenye maeneo yalipo balozi hizo.  Vilevile ametaja njia nyingine kuwa ni kupitia taasisi za elimu, wizara na vyuo vikuu ambako baadhi ya watanzania wanapata ajira nje ya nchi, zikiwamo nafasi za utafiti na fursa kupitia mashirika ya Umoja wa Mataifa. Pia Naibu Waziri Katambi ameeleza kuwa Serikali tayari imeanza kutekeleza mpango maalumu kupitia Kitengo cha Huduma za Ajira Tanzania (TaESA) ili kubaini ajira zinazotangazwa mtandaoni na kuwafikia watanzania katika kanzidata, pia kuwasaidia kwa mafunzo ili kuhakikisha wanastahili kupata ajira hizo. Read More

  • Mama anaiimarisha TAKUKURU mapambano dhidi ya rushwa nchini.

    Ili kuongeza tija na kuboresha utendaji kazi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) Serikali imekabidhi magari 88 kwa taasisi hiyo. Magari hayo ambayo yatasambazwa mikoa yote Tanzania yamekabidhiwa na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa  kwa niaba ya Mhe. Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan wakati wa kufunga mafunzo ya awali ya uchunguzi ya Taasisi hiyo, hafla iliyofanyika kwenye Shule ya Polisi Tanzania, Moshi mkoani Kilimanjaro. Katika kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan madarakani, TAKUKURU imepatiwa jumla ya Shilingi bilioni 30 za kununulia magari 195 ambapo 88 yameshanunuliwa huku mchakatio wa kununua magari 107 yaliyobakia unaendelea. Read More

  • Barua ya wazi ya Rais Samia Suluhu

    Tanzania inatimiza miaka 30 tangu turejee rasmi katika siasa za mfumo wa vyama vingi katika kipindi hicho, Taifa letu limepitia kipindi cha furaha, majonzi, misukusuko na changamoto zote wakati Taifa linapoanza njia mpya. Jambo hili si jepesi, kwa sababu nyakati hizo hazikuwa rahisi duniani kote. Miaka ambayo Tanzania ilirejea katika mfumo huo ilikuwa migumu. Miaka ya mwanzoni ya 1990, ndiyo ilishuhudia changamoto kama vile kuanguka kwa iliyokuwa Urusi, vita vya wenyewe kwa wenyewe Afrika, mauaji ya Kimbari na migogoro mingi ya kisiasa na kiuchumi katika nchi zinazoendelea kama yetu Lakini Watanzania walipita wakati wote huo, wakiwa wamoja na tumeendeleza utamaduni huo miaka 30 baadaye. Napenda kutumia nafasi hii kuwapongeza wote, na ni matumaini yangu makubwa, kwamba viongozi watakaokuja miaka 50 hadi 100 baadaye wataendelea kuongoza nchi iliyo moja na wananchi wasiobaguana na kupigana, hata kama wanapingana kuhusu namna ya kuendesha nchi yao. Ni vizuri kuzungumza kuhusu nana tulivyoingia katika mfumo huu. Rais Ali Hassan Mwinyi aliunde Tume ya Jaji Francis Nyalali iliykuja na majibu kwamba ni azilimia 20 tu ya Watanzania ndio walitaka mfumo wa vyama vingi. Ni busara ya Mzee Mwinyi na viongozi wenzake wa wakati huo walioamua kusikiliza wachache. Kama wazee wetu wangesubiri mpaka asilimia 80 itake vyama vingi ndiyo tukubali pengine leo tusingekuwa tulipo. Hili ni miongoni mwa mafunzo makubwa kwa wanasiasa wa kizazi changu na watakaokuja baadaye. Kwenye jambo la maslahi ya nchi, maarifa na busara ndiyo muhimu kuliko namba. Kutoka kuwa na chama kimoja cha siasa – Chama Cha Mapinduzi (CCM), sasa tuna vyama vilivyosajiliwa 20. Badala ya kusikia sauti moja. Badala ya kusikia sauti moja na wakati mwingine tukisema “Zidumu Fikra za Mwenyekiti”. Sasa Watanzania wanasikia kuhusu fikra za sauti tofauti. Kwa bahati nzuri, hata Mwenyekiti Mao alipata kusema “acha maua 100 yamee kwa pamoja”. Kipekee kabisa, nitumie nafasi hi kuwapongeza wote waliofanikisha safari… Read More