Mama Yukokazini
-
Sekta ya uwekezaji nchini Tanzania imeendelea kuimarika ambapo katika robo ya kwanza ya mwaka 2025/26 (Julai – Septemba) kumeshuhudiwa ongezeko la miradi ya uwekezaji, thamani yake na ajira zitakazotokana na uwekezaji huo. Katika kipindi hicho, Tanzania imesajili miradi 201 ya uwekezaji, yenye thamani ya shilingi trilioni 6.2 ambapo inatarajiwa kuzalisha ajira 20,808. Ufanisi huu unathibitisha kuimarika kwa imani ya wawekezaji nchini, ikiwa ni matokeo ya uongozi bora na mabadiliko ya kisera na kikodi yaliyotekelezwa na serikali. Sekta ya uzalishaji wa viwandani imeongoza kwa kuvutia miradi mingi (85) ikifuatiwa na majengo ya biashara (30), usafirishaji (29), utalii (24) na kilimo (13). Uwekezaji viwandani umeendelea kuongoza kwa idadi kubwa ya miradi na uzalishaji wa ajira, sambamba na azma ya serikali ya kuchochea mapinduzi ya uchumi wa kisasa, fungamanishi, jumuishi na shindani uliojengwa katika msingi wa kuongeza thamani rasilimali zinazozalishwa nchini. Katika hatua nyingine, miradi inayomilikiwa na wazawa imeongezeka kufikia 74 kutoka miradi 70 iliyosajiliwa kipindi kama hicho mwaka 2024/25. Hatua hii inaonesha kuwa mageuzi yaliyofanyika si tu yanawanufaisha wageni, bali pia wazawa ambao ni nguzo muhimu katika kukuza uchumi. Umoja wa Falme za Kiarabu ndiyo nchi iliyoongoza kwa uwekezaji nchini kwa kipindi hicho ikiwa na miradi ya TZS trilioni 1.2 ikizitangulia China (TZS trilioni 1.1), India (TZS bilioni 432.5), Singapore (TZS bilioni 342.5) na Ufaransa (TZS bilioni 250.4). Uwekezaji huu unaifanya Tanzania kuendelea kuwa lango la biashara, uwekezaji na usafirishaji katika ukanda wa Mashariki na Kusini mwa Afrika. Read More
-
Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuweka mazingira wezeshi kwa vijana kujikwamua kiuchumi ambapo serikali yake ikitangaza mikakati nane inayolenga kukuza uwekezaji kwa mwaka 2025/26, vijana wamepewa kipaumbele ili kuwa miongoni mwa wawekezaji wakubwa nchini. Moja ya hatua ambayo Serikali imepanga kuchukua ni kuanzisha kituo cha kuhudumia na kuwezesha wawekezaji vijana ambacho kitatoa huduma za mafunzo, uwezeshaji na usaidizi. Kituo hicho kinatarajiwa kuanzishwa kabla mwaka huu haujaisha ambapo makao makuu yake yatakuwa Dar es Salaam, huku kikiwa na uwakilishi wa maeneo yote. Aidha, sambamba na hilo serikali inakusudia kuanzisha programu maalum ya kuwezesha wawekezaji vijana kubuni na kuanzisha uwekezaji wa viwandani. Programu hiyo itahusisha mafunzo, uwezeshaji wa kupewa ardhi, kuunganishwa na wauzaji wa mitambo na malighafi na benki. Kwa kuanza maeneo yaliyotengwa kwa vijana yapo Nala, Dodoma; Bunda, Mara; Songea, Ruvuma; na Bagamoyo. Pwani. Hatua hizi zinachukuliwa ikiwa ni mwendelezo wa kufungua fursa kwa vijana kujiajiri na kuajiriwa. Mkakati mwingine uliochukuliwa ni Mheshimiwa Rais Samia kuunda wizara maalum ya vijana ili masuala yao yashughulikiwe kwa uharaka. Mheshimiwa Rais amekuwa akisisitiza kuwa ana imani na vijana na kwamba wao ni sehemu muhimu ya maendeleo ya nchi. Read More
-
“Kwa wale ambao wanaonekana walifuata mkumbo, na hawakudhamiria kufanya uhalifu, wawafutie makosa yao.” Hayo ni maneno ya Rais, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa vyombo vya kisheria akivielekeza kuwaachia huru washtakiwa ambao vinaona walifuata mkumbo wakafanya uhalifu wakati wa vurugu za Oktoba 29 na siku zilizofuatia. Kufuatia maelekezo hayo, Novemba 24 mwaka huu jumla ya washtakiwa 210, wakiwemo wa uhaini, wameachiwa baada ya Mwendesha Mashtaka kuwasilisha taarifa ya kutokuwa na nia ya kuendelea na kesi zao. Walioachiwa ni kutoka katika mikoa mitatu ambayo ni Dar es Salaam (washtakiwa 47), Arusha (washtakiwa 24) na Mwanza (washtakiwa 139). Mheshimiwa Dkt. Samia amewasihi vijana kuipenda, kuilinda na kuitunza nchi yao iliyojengwa kwenye misingi ya amani na utulivu wa kisiasa na kwamba kama wazazi wao wanggeshawishika kuyafanya ambayo vijana walifanya wakati wa vurugu, kusingekuwa na neema na maendeleo mnayoyaona leo. Pia, ameahidi kuendelea kuchukua hatua za kurejesha amani, usalama na utulivu ikiwemo kufanya mazungumzo na makundi mbalimbali ili kujenga maelewano na umoja wa kimataifa. Read More
-
Rais Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan leo amewaapisha Mawaziri na Naibu Mawaziri Ikulu Chamwino mkoani Dodoma. Akizungumza baada ya kuwaapisha, hotuba yake imetoa maelekezo mbalimbali yakiwemo; 1. Dhamana waliyopewa si fahari bali ni dhamana na kufanya kazi kwa ajili ya wananchi na Taifa letu sambamba na kaulimbinu “Kazi na Utu, Tunasonga Mbele. 2. Hatosita kubadili viongozi endapo ataona hawatimizi au hawafanikishi matokeo yanayotakiwa. “Nabadili mpaka nipate yule atakayefanya kazi na mimi kwa moyo mkuu na moyo mmoja.” 3. Kazi ya utendaji kazi inaanza mara moja na inaanza kwa kasi kwani yaliyoahidiwa kwa wananchi ni mengi, na muda ni mchache, hivyo lazima wakimbie badala ya kutembea. 4. Vurugu za Oktoba 29 huenda zikapunguzia nchi sifa ya kupata mikopo kwa urahisi kama ilivyokuwa awali. Hivyo, lazima kuwa na usimamizi madhubuti ya rasilimali za ndani ili utekelezaji miradi uanze kwa fedha za ndani badala ya kusubiri misaada/mikopo kutoka nje. 5. Ambao Ahadi za Siku 100 za Kwanza zinagusa wizara zao wakazitekeleza kwa kasi kubwa. 6. Amesema hataki masuala ya “tunaendelea,” au “mchakato uko mbioni,” badala yake anataka kuona matokeo kwa wananchi ndani ya muda uliokubaliwa Read More
-
Hotuba ya Rais wa Tanzania, Mhehsimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akifungua Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma. Read More
-
Rais Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema nafasi ya Uwaziri Mkuu haina urafiki, udugu na jamaa, badala yake ni nafasi ya kulitumikia Taifa na kuwatumikia wananchi wote. Akizungumza baada ya kumwapisha Mbunge wa Iramba Magharibi, Mheshimiwa Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania jijini Dodoma leo, Dkt. Samia amemuasa kiongozi kuwa makini kwani kwa umri alionao wadhifa huo ni mzigo mkubwa kwake, na kwamba atakumbwa na vishawishi vya ndugu, jamaa na marafiki. Katika hatua nyingine amemuagiza Waziri Mkuu kusimamia kikamilifu utekelezaji wa miradi na programu za maendeleo zilizopo na kuongeza kasi ya utekelezaji na ufuatiliaji wa karibu wa shughuli za Serikali, ikiwemo ahadi zilizotolewa wakati wa uchaguzi, ili malengo ya Serikali yatimie kwa muda uliopangwa. “Kuna mengi tumewaahidi wananchi. Ukiangalia mambo yote na muda tulionao, muda ni mfinyu. Hivyo, hatuna budi kuongeza kasi katika utendaji wetu,” amesema Dkt. Samia. Awali alieleza kuwa uteuzi wa kiongozi huyo ulikuwa na ushindani na kwamba moja ya kigezo kikubwa kilichotumika kumpata ni uwezo wa kuwatumikia wananchi, kasi ambayo amemsisitiza aifanye kwa ukamilifu huku akimwahidi ushirikiano. Read More
-
Kwa mara nyingine Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameendelea kudhihirisha namna anavyosikiliza na kuzipatika majawabu changamoto za wananchi wake, ambapo sasa Serikali imeweka zuio katika baadhi ya biashara kutofanywa na raia wa kigeni. Uamuzi huo umetokana na malalamiko ya wananchi juu ya uwepo wa raia wa kigeni kufanya kazi ambazo zingeweza kufanywa na wazawa. Kwa mujibu wa Amri ya Leseni za Biashara (Zuio la Shughuli za Kibiashara kwa wasio Raia), 2025, serikali imezuia wageni kufanya aina 15 za biashara, zikiwemo biashara ya bidhaa ya jumla na rejareja, isipokuwa supermarkets au maduka yanayouza kwa jumla kwajili ya wazawa. Biashara nyingine zilizozuiwa ni huduma ya uwakala wa fedha kwa simu, ufundi wa simu na bidhaa za kieleketroniki, uchimbaji mdogo, kuongoza watalii, huduma za posta na usafirishaji vipeto, uanzisha na uendeshaji wa redio na televisheni, uendeshaji wa maeneo ya makumbusho pamoja na udalali. Aidha, wamezuiwa kufanya biashara ya huduma za forodha na usafirishaji, ununuzi wa mazao shambani, umiliki na uendeshaji wa mashine za kamari isipokuwa ndani ya viunga vya casino pamoja na umiliki na uendeshaji wa viwanda vya chini na vidogo. Kumekuwa na malalamiko ya wananchi kuwa raia wa kigeni, hasa wa China wanafanya biashara za wazawa ikiwemo uuzaji wa nguo Kariakoo, udalali wa nyumba pamoja na uwakala wa fedha. Hatua hii ni mwendelezo wa Mheshimiwa Rais kukabiliana na changamoto ya ajira nchini, hasa kwa vijana, ambapo pia serikali yake imeendelea kutoa mikopo, kupanua fursa za elimu ya ufundi stadi, kuwapatia elimu ya kilimo-biashara pamoja na kufungua fursa za masoko ndani na nje ya nchi. Uamuzi huu umepongezwa na wananchi, hasa kwenye mitandao ya kijamii, ambapo wengi wamempongeza Mheshimiwa Rais kuwa amesikia na kujibu kilio chao cha muda mrefu. Read More
-
Tanzania imeongoza Afrika Mashariki kwa kasi kubwa ya ongezeko la thamani ya uwekezaji kutoka nje ya nchi ambapo imeongezeka kwa asilimia 28.3 kutoka dola za Marekanili bilioni 1.34 (TZS trilioni 3.5) mwaka 2023 hadi kufikia dola za Marekani bilioni 1.72 (TZS trilioni 4.4) mwaka 2024. Aidha, kasi hiyo kubwa ya ongezeko la uwekezaji imeifanya Tanzania kushika namba 11 Afrika kwa kiwango kikubwa cha uwekezaji toka nje, na nafasi ya 13 kwa ukuaji wa thamani ya uwekezaji. Pia, umeiwezesha Tanzania kuvuka kiwango cha asilimia 12 cha ukuaji wa uwekezaji kilichowekwa kwa nchi za Afrika Mashariki na bara la Afrika. Ukuaji huo ni matokeo ya kazi kubwa ya Serikali ya Awamu ya Sita ikiongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ambapo ameendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini, kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi pamoja na kutangaza fursa zilizopo kimataifa na hivyo kupelekea kuongeza kwa miradi ya uwekezaji. Mwaka 2024 Tanzania iliweka rekodi kwa kusajili miradi 901 ya uwekezaji kutoka miradi 526 mwaka 2023 ambapo maelfu ya wananchi watanufaika na ajira, na miradi hii itachagiza ukuaji wa sekta nyingine kama nishati, maji, mawasiliano, usafirisha, huduma na uzalishaji. Read More
-
Soma na pakua hapa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Dira hii ya pili isiyofungama na chama cha kisiasa kwa nchi yetu ni matokeo ya maoni ya wananchi ambapo sehemu kubwa ya waliotoa maoni ni vijana. Read More