May 2025

  • MAMA aboresha Sera ya Mambo ya Nje ili kukuza Diplomasia ya Uchumi na kulinda utamaduni wetu

    AKIAHIDI, ANATIMIZA. Hayo ndiyo maneno mawili yanayoweza kutumika kueleza tukio la Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuzindua Sera ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001 (Toleo la Mwaka 2024), ambayo ni ahadi aliyoitoa Aprili 2021 wakati akihutubia bunge, mwenzi mmoja baada ya kuingia madarakani. Akizungumza bungeni alisema kuwa serikali itaifanyia maboresho sera hiyo ili iendane na mabadiliko ambayo yametokea ndani na nje ya nchi katika sekta mbalimbali. Ikiwa ni miaka 24 tangu kupitishwa kwa sera hiyo, leo Mei 19, 2025 Mheshimiwa Rais amezindua toleo hilo ambalo limejikita katika Diplomasia ya Uchumi likilenga kulisukuma Taifa mbele na kuimarisha ushiriki na ushindani katika siasa na maendeleo ya kimataifa, kulinda na kutetea maslahi ya Tanzania kupitia diplomasia makini na shirikishi. Toleo la mwaka 2024 limeleta maboresho mbalimbali ambayo ni pamoja na kuongeza msingi mmoja (wa nane) katika Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania. Msingi huo ni kulinda na kuendeleza maadili, mila na utamaduni wa Mtanzania ikiwemo kukuza matumizi ya lugha ya Kiswahili, hatua ambayo inalenga kukabiliana na uvamizi mkubwa wa utamaduni na ustaarabu unaoendelea. Aidha, mambo mengine manne yaliyoongezwa ni, moja, kuimarisha Diplomasia ya Uchumi kwa kuvutia uwekezaji wa mitaji mikubwa, kutumia vizuri fursa ya kijografia tuliyojaliwa na kufaidika na soko huru la biashara Afrika. Pili, ni matumizi ya lugha ya Kiswahili kama nyenzo ya kujenga ushawishi ili kupanua masoko ndani na nje ya Afrika. Tatu, kukuza ushiriki wa Diaspora katika kukuza uchumi wao binafsi na uchumi wa taifa, na nne ni kuangalia fursa mpya za ushirikiano wa kiuchumi ikiwemo uchumi wa buluu ili kuchochea ukuaji wa kiuchumi. Ametumia nafasi hiyo kuwapongeza wote walioshiriki kuandaa sera hiyo, hasa wananchi waliotoa maoni akisema kuwa “mmeshiriki katika kujenga hatma ya nchi yenu na mmeweka alama isiyofutika.” Read More

  • DP World yaongeza mapato Bandari ya Dar kwa zaidi ya TZS trilioni 1

    Falsafa ya 4R (Reconciliation, Resilience, Reform, and Rebuild) ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuleta mageuzi katika sekta mbalimbali zinazogusa maisha ya Watanzania na kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchini. Moja ya sekta hizo ni uchukuzi, ambapo Mageuzi (Reform) yaliyofanywa katika Bandari ya Dar es Salaam kwa kuingia ubia na Kampuni za DP World na Tanzania East Africa Gateway Terminal Limited (TEAGTL) katika kuendeleza na kuendesha baadhi ya maeneo ya bandari hiyo yameendelea kuleta matokeo, ikiwemo kuongeza mapato. Kati ya Julai, 2024 hadi Februari 2025, mapato yatokanayo na Kodi ya Forodha kutoka bandarini yanayokusanywa kutokana na shughuli za kibandari yamefikia TZS trilioni 8.26, ambalo ni ongezeko la TZS trillion 1.18 ikilinganishwa na makusanyo ya TZS trilioni 7.08 yaliyokusanywa kipindi kama hicho kwa mwaka 2023/24. Mafanikio hayo yametokana na wawekezaji hao kuwezesha upatikanaji wa vifaa na mitambo ya kisasa na mifumo ya TEHAMA inayoendelea kuleta ufanisi katika uendeshaji wa shughuli za kibandari, hasa kuondoa msongamano wa mizigo na foleni za meli, hali inayochochea wafanyabiashara zaidi kuchagua kutumia bandari hiyo, hivyo kuongeza mapato. Lengo la Mheshimiwa Rais Samia kushirikisha sekta binafsi ni kuongeza tija katika utendaji wa bandari nchini ili kuziwezesha zichangie zaidi katika ukuaji wa uchumi wa Taifa letu na maendeleo ya wananchi kwa ujumla kwa kuwafanya wanufaike na rasilimali za nchi yao. Read More

  • MAMA akamilisha miradi ya maji zaidi ya 2,000; mamilioni ya wananchi wapata maji safi

    Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuleta mageuzi makubwa katika sekta mbalimbali nchini ambapo katika sekta ya maji, ndani ya kipindi cha miaka minne amekamilisha miradi ya maji zaidi ya 2,331 mijini na vijijini ambayo imefikisha maji kwa mamilioni ya wananchi. Kutokana na ufanisi huo asilimia 83 ya wakazi wote wa vijijini wanapata maji safi na salama ikiwa ni ongezeko toka asilimia 72.3 alizokuta wakati anaingia madarakani Machi 2021. Aidha, kwa sasa asilimia 91.6 ya wananchi wa mijini wanapata huduma ya maji safi na salama ikilinganishwa na wastani wa asilimia 86 aliyoikuta. Mafanikio haya yanakaribia lengo lililoanishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (2020-2025) ambayo inaielekeza serikali kuongeza kasi ya usambazaji majisafi na salama ili kutosheleza mahitaji kwa zaidi ya asilimia 85 vijijini na zaidi ya asilimia 95 kwa mijini, kwa upande wa Tanzania Bara, ifikapo Desemba 2025. Ili kuhakikisha lengo la ilani, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji 1,544. Hatua hii inadhihirisha dhamira ya dhati ya Mheshimiwa Rais kufikisha maji kwa kila mwananchi popote alipo akitambua kuwa maji ni uhai, maendeleo na usalama kwa wananchi. Read More

  • Mama ashusha neema kwa watumishi wa umma; kima cha chini cha mshahara ni laki 5

    Ni furaha furi furi kama sio furaha bojo bojo kwa watumishi wa umma na Watanzania kwa ujumla baada ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza nyongeza ya kima cha chini cha mshahara kwa asilimia 35.1. Kutokana na nyongeza hiyo, kima cha chini kuanzia Julai 1, 2025 kitakuwa TZS 500,000 toka kiwango cha TZS 370,000 cha sasa. Mheshimiwa Rais ametangaza neema hiyo katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Dunia (Mei Mosi) ambayo kitaifa imefanyika mkoani Singida ikiwa na kaulimbiu isemayo, “Uchaguzi Mkuu 2025 utuletee viongozi wanaojali haki na maslahi ya wafanyakazi wote, sote tushiriki.” Amesema nyongeza hiyo ni sehemu ya hatua ambazo serikali yake imeendelea kuchukua kuleta ustawi kwa wafanyakazi nchini, na kwamba uamuzi huo umewezeshwa na kasi ya ukuaji wa uchumi kupanda hadi kufikia 5.5% kwa mwaka, hali iliyochangiwa na wafanyakazi kujituma na kufanya kazi kwa bidii. Kupitia mitandao ya kijamii wananchi wamefurahia nyongeza hiyo ambapo wameandika jumbe za kumpongeza. Baadhi ya jumbe hizo ni; “Nakuamini na nakupenda sana mama maisha yangu yote sijawahi kupiga kura ila mwaka huu inshallah nna Imani kura yangu unayo ya kwanza kwenye maisha yangu,”- Hamoud Jimia. “Ubarkiwe mama ikulu yako huna mpinzani hata kidgo,”- Kisila Legandy “Safi mama Samia, wewe ndo unatudai na tunakuhakikishia lazima tukulipe,”- Julius Peter “Kima cha chini cha mashahara kinapanda kutoka 300k mpaka 500k nomaa,”- Msaki. Kuhusu sekta binafsi Mheshimiwa Rais amesema kuwa Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara inaendelea na tathmini kwa lengo la kuboresha viwango vya mishahara kwa sekta binafsi. “Tutaendelea kuboresha mazingira ya wafanyakazi ikiwemo maslahi ya wafanyakazi kwa kadiri hali itakavyoruhusu… Ili tuweze kujenga vyema Taifa letu ni lazima tulinde amani na utulivu nchini,” amesisitiza Rais Dkt. Samia. Read More