January 2025
-
Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA imevunja rekodi ya makusanyo tangu kuanzishwa kwake kwa kukusanya Shilingi Trilioni 3.587 kwa Mwezi wa Desemba sawa na asilimia 103.52 ya lengo ambalo lilikuwa ni kukusanya Shilingi Trilion 3.465. Makusanyo hayo ni sawa na ukuaji wa asilimia 17.59 ukilinganisha na kiasi cha Shilingi Trilioni 3.050 zilizokusanywa mwezi Desemba mwaka 2023. Taarifa iliyotolewa TRA imeeleza kuwa mbali na kuvuka malengo ya Mwezi Desemba katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2024/2025 (Oktoba-Desemba 2024) imefanikiwa kukusanya kiasi cha Shilingi Trilioni 8.741 sawa na ufanisi wa asilimia 104.63 ya lengo la kukusanya Shilingi Trilioni 8.354 ambayo ni sawa na ukuaji wa asilimia 19.05 ukilinganisha na kiasi cha Shilingi Trilioni 7.342 zilizokusanywa katika kipindi kama hicho mwaka wa fedha 2023/24. Vilevile TRA imeandika rekodi mpya ya kuweza kufikia na kuvuka lengo la makusanyo kwa miezi sita mfululizo katika nusu ya kwanza ya mwaka wa fedha 2024/2025. Kamishna Mkuu wa TRA Bwn. Yusuph Mwenda amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa miongozo mizuri iliyowawezesha kukusanya kodi kwa hiari na kuvuka malengo. Read More