- ๐๐ก๐๐ฆ๐๐ง๐ข ๐ฒ๐ ๐ฎ๐ฐ๐๐ค๐๐ณ๐๐ฃ๐ข ๐ข๐ฆ๐๐จ๐ง๐ ๐๐ณ๐๐ค๐ ๐ค๐ฐ๐ ๐๐ฌ๐ข๐ฅ๐ข๐ฆ๐ข๐ ๐๐
- ๐๐ข๐ฉ๐ฅ๐จ๐ฆ๐๐ฌ๐ข๐ ๐ฒ๐ ๐๐๐ก๐ฎ๐ฆ๐ข ๐ง๐ ๐ฎ๐ข๐ฆ๐๐ซ๐ข๐ฌ๐ก๐๐ฃ๐ข ๐ฆ๐๐ณ๐ข๐ง๐ ๐ข๐ซ๐ ๐ฒ๐ ๐๐ข๐๐ฌ๐ก๐๐ซ๐ ๐ง๐๐ข๐ณ๐จ ๐ฌ๐ข๐ซ๐ข ๐ณ๐ ๐ฆ๐๐๐๐ง๐ข๐ค๐ข๐จ
Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimesajili miradi yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 1.4 (takribani TZS trilioni 4) ndani ya miezi mitatu ya mwisho ya mwaka jana, sawa na ongezeko la 80% ikilinganishwa na miradi yenye thamani ya dola za Marekani milioni 769.6 iliyosajiliwa kipindi kama hicho mwaka 2022.
Ongezeko hilo kubwa la uwekezaji limetokana na ziara za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan nje ya nchi ambazo zimevutia wawekezaji kupitia utekelezaji wa Sera ya Diplomasia ya Uchumi na kuimarishwa kwa mazingira ya biashara na uwekezaji nchini ambayo yamevutia wawekezaji wengi zaidi.
Katika ziara hizo Mheshimiwa Rais Samia amekuwa akiambatana na wafanyabiashara kutoka Tanzania ambao hupata wasaa wa kuzungumza na wafanyabiashara kwenye nchi anazokwenda, hatua ambayo hutoa fursa ya kuwepo ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji kati yao.
Ripoti mpya ya TIC inaonesha kuwa miradi 161 ilisajiliwa kati ya Oktoba-Desemba 2023 ikilinganishwa na miradi 58 kwenye kipindi kama hicho mwaka 2022, ikiwa ni ongezeko la asilimia 178, ambapo sekta tano zilizoongoza kwenye uwekezaji huo ni viwanda, usafirishaji, huduma, kilimo na utalii.
Miradi iliyosajiliwa Oktoba-Desemba 2023 inatarajiwa kutengeneza jumla ya ajira mpya 18,390, kutoka ajira 10,216 za kipindi kama hicho kilichopita kwa mwaka 2022 ambapo mikoa iliyoongoza kwa uwekezaji mkubwa ni Dar es Salaam na Pwani.
Aidha, ili kutoa fursa pia kwa wawekezaji wa ndani, pamoja na mambo mengine TIC imeanzisha kampeni maalumu ya kukuza uwekezaji wa ndani lengo likiwa ni kusajili miradi ya uwekezaji wa ndani yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 3.5 (TZS trilioni 9) ifikapo mwaka 2028.