• #ZiaraYaMamaUturuki ni heshima na fursa kwa Tanzania kidiplomasia, kiuchumi na kijamii

    Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameanza ziara yake rasmi nchini Uturuki kwa mwaliko wa Rais wa nchi hiyo, Mheshimiwa Recep ErdoฤŸan. Ziara hiyo ya kimkakati inatarajiwa kuwa na matokeo chanya kidiplomasia, kiuchumi na kimaendeleo ambapo inafanyika kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 14 (tangu mwaka 2010), na miaka saba tangu ziara ya Rais ErdoฤŸan nchini. Tanzania na Uturuki zina uhusiano wa miaka 61 (tangu mwaka 1963), ambapo Uturuki ilifungua ubalozi wake nchini mwaka 1969, ikaufunga mwaka 1984 na kuufungua tena mwaka 2009, na hivyo kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano na uhusiano baina ya mataifa haya. Malengo makuu matatu ya ziara hiyo ya kimkakati ni kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia uliopo, kufungua fursa mpya za ushirikiano wa kiuchumi, na kuendeleza ushirikiano wa kimaendeleo. Maeneo hayo yanatarajia yatapewa uzito katika mazungumzo atakayofanya na mwenyeji wake, Mheshimiwa Rais ErdoฤŸan. Nchi hizi zina ushirikiano mkubwa kwenye biashara na uwekezaji ambapo Uturuki ni miongoni mwa nchi 20 zenye uchumi mkubwa zaidi duniani imewekeza nchini zaidi ya TZS trilioni 1.3 na kuzalisha ajira zaidi ya 6,700. Kwa upande wa Tanzania, huuza wastani wa bidhaa zenye thamani ya TZS bilioni 41 kila mwaka nchini Uturuki. Mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) unaotekelezwa na kampuni ya Uturuki, Yapi Merkez ni kielelezo kikubwa cha ushirikiano baina ya nchi, na ziara hii inatarajiwa kuwa chachu ya kuongeza kasi ya kutekeleza mradi huo utakaobadili maisha na uchumi wa Tanzania. Aidha, Uturuki ni mshirika mkubwa katika kukuza utalii nchini ambapo safari za ndege za moja kwa moja kwenda Dar es Salaam na Kilimanjaro zimerahisisha usafiri wa watalii, sekta ambayo ina mchango mkubwa katika uchumi wetu. Katika kufanikisha lengo la kufungua fursa mpya za ushirikiano, akiwa nchini Uturuki, Mheshimiwa Rais Samia atashiriki jukwaa la uwekezaji pamoja na kuzungumza na kampuni 15 kubwa zaidi nchini humo na kuwashawishi kuja kuwekeza nchini. Mheshimiwa Rais… Read More

  • Mafanikio makubwa ya kiuchumi robo ya kwanza mwaka 2024 yamedhihirisha maono ya MAMA

    Utekelezaji imara wa sera za kiuchumi, kuimarika kwa amani na utulivu na mikakati ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu kuifungua nchi kumeendelea kuimarisha uchumi wa Tanzania licha ya changamoto zilizotokana na mtikisiko katika uchumi wa dunia, uimara unaotarajiwa kuendelea katika siku zijazo, hususan robo ya pili ya mwaka 2024. Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeainisha maeneo matano ambayo yameendelea kudhihirisha kuimarika kwa uchumi wa Tanzania katika robo ya kwanza ya mwaka 2024 ambapo kwanza ni ukuaji wa uchumi unakadiriwa kufikia asilimia 5.1 ikiwa ni matokeo ya uwekezaji unaofanywa na Serikali kuongeza uwekezaji kwa sekta binafsi. Ripoti ya BoT imeeleza kuwa hatua zinazochukuliwa na Mheshimiwa Rais Samia zinachangia kuongezeka kwa mikopo kwa sekta binafsi na uwekezaji kutoka nje ya nchi. Mikopo hiyo ambayo inatarajiwa kuendelea kuongezeka ilielekezwa zaidi katika shughuli za kilimo, uchimbaji wa madini, usafirishaji na uzalishaji viwandani sawasawa na malengo ya Serikali. Eneo jingine ni mfumuko wa bei ambao umeendelea kuwa tulivu, kwa wastani wa asilimia 3, hali inayotokana na utekelezaji wa sera madhubuti ya fedha na uwepo wa chakula cha kutosha nchini, hivyo kuifanya Tanzania moja ya nchi chache zenye kiwango kidogo cha mfumuko wa bei Afrika. Kiwango hicho kipo ndani ya lengo la nchi la mfumuko wa bei usiozidi asilimia 5 na vigezo vya kikanda kwa jumuiya ambazo Tanzania ni mwanachama. Matokeo ya uwekezaji na uzalishaji yameendelea kuzaa matunda ambapo nakisi ya urari wa biashara nje ya nchi iliendelea kupungua kutokana na kupungua kwa gharama za uagizaji wa bidhaa na kuongezeka kwa mauzo nje ya nchi. Nakisi imepungua kwa zaidi ya asilimia 50, kufikia dola milioni 2,701.4 mwaka unaoishi Februari 2024, kutoka dola milioni 5,133.6 katika kipindi kama hicho mwaka 2023. Kuongezeka kwa mauzo nje kumechangia kuongeza akiba ya fedha za kigeni ambapo imeendelea kuwa ya kutosha, kufikia zaidi ya dola za Marekani bilioni 5.3 mwishoni mwa Machi… Read More

  • #MiakaMitatuYaMama: Mageuzi sekta ya afya ameweka rekodi na kuimarisha huduma za afya

    Miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Sita, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amefanya mageuzi makubwa yaliyoboresha sekta ya afya nchini na kufanya huduma za afya kuwa karibu, bora na nafuu zaidi. Vituo vya kutolewa huduma za afya (zahanati, vituo vya afya, hospitali za wilaya, mikoa, rufaa na za kanda) 1,061 vimejengwa ambapo ni wastani wa vituo 353 kila mwaka. Ujenzi wa vituo hivi umeenda sambamba na ununuzi wa vifaa tiba vya kisasa vya uchunguzi wa magonjwa ambavyo vimetoa ahueni kubwa kwa wananchi. MAMA amenunua mashine mpya za CT Scan 27, na kufanya mashine hizo nchini kufikia 45, kutoka 13 za awali. Hivi sasa mashine hizo za kiuchunguzi zinapatikana kwenye hospitali zote za rufaa za mikoa. Manufaa makubwa yanaonekana ambapo awali wakazi wa Katavi walilazimika kusafiri zaidi ya kilomita 600 kwenda Hospitali ya Rufaa ya Kanda, Mbeya, lakini sasa huduma hiyo inapatikana mkoani mwao. Tangu tupate uhuru, kwa miaka 61, Tanzania ilinunua mashine za MRI saba, lakini ndani ya miaka mitatu MAMA amenunua mashine sita na kuifanya nchi kuwa na MRI 13 ambazo zimefungwa kwenye hospitali za rufaa za kanda. Mashine za X-Ray ambazo awali hazikupatikana kwa wingi kwenye vituo vya afya, sasa zimejaa tele baada ya kununuliwa kwa Digital X-Ray 199, na kuifanya nchi kuwa namashine 346. MAMA pia amenunua mashine za ultrasound 192 na kuifanya nchi kuwa na mashine 668 ambazo ni muhimu hasa katika kufuatilia ukuaji wa mimba. Vifaa tiba vingine vilivyoongezwa ni Echocardiogram kutoka 95 mwaka 2021 hadi 102 mwaka 2024, Cathlab kutoka moja mwaka 2021 hadi nne mwaka 2024 pamoja na PET Scan ambayo ndiyo ya kwanza nchini mwetu. Vitanda vipya 40,078 vya kulaza wagonjwa, vitanda vipya 1,104 vya vya ICU pamoja na kuongeza hali ya upatikanaji wa dawa kufikia asilimia 84 kutoka asilimia 58 mwaka 2022. Mageuzi haya yaliyofanyika yamewezesha kupungua kwa vifo vinavyoepukika… Read More

  • #MiakaMitatuYaMama amezipatia majawabu changomoto za muda mrefu za watumishi wa umma

    Watumishi wa umma wanayo mengi ya kufurahia na kuonesha katika miaka mitatu ya Mama kwani ametoa majawabu ya changamoto nyingi zilizokuwa za zinawakabili, hali iliyowaongezea motisha na ari ya kuwatumikia wananchi. Kubwa la kwanza ambalo katika kila Sikukuu ya Wafanyakazi (Mei Mosi) lilikuwa likisubiriwa tangu mwaka 2016 ni nyongeza ya mishahara. Ndani ya uongozi wa Mama hilo limepatiwa majibu ambapo alipandisha kima cha chini cha mishahara kwa asilimia 23, nyongeza ambayo imewawezesha watumishi wa umma kumudu gharama za maisha ambapo pia aliahidi nyongeza itakuwa kila mwaka. Kwa miaka saba, tangu mwaka 2016 watumishi hao hawakuwa wamepandishwa vyeo. Chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu watumishi 375,319 wamepandishwa vyeo ambapo Serikali imetumia TZS bilioni 85.89, fedha ambazo matumizi yake yamekwenda kuongeza mzunguko wa fedha na kuboresha maisha ya watumishi. Ajira kilikuwa ni kilio kikubwa ambapo mbali na kuweka mazingira rafiki yaliyozalisha maelfu ya ajira kwenye sekta binafsi, Serikali tayari imeajiri watumishi wapya 81,137 katika taasisi mbalimbali za umma. Aidha, imetenga TZS bilioni 230 ambazo zitatumika kuajiri watumishi wapya 47,374 kabla ya mwaka wa fedha 2023/24 kumalizika. Mama amekuwa akisisitiza kuwa yeye na wasaidizi wake si watawala bali ni watumishi wa wananchi. Ili kuhakikisha utumishi uliotukuka ameendelea kutatua changamoto zao ambao amewalipa malimbikizo maelfu ya watumishi. Ndani ya miaka mitatu ya Mama jumla ya watumishi 142,793 wamelipwa malimbikizo yenye thamani ya TZS bilioni 240.7. Kwa lengo la kuendelea kuongeza ufanisi, Serikali imewabadilishia kada watumishi 30,924 ambapo imewalipa mishahara mipya yenye thamani ya TZS bilioni 2.56, mafanikio ambayo hayakuwa yamepatikana katika kipindi cha zaidi ya miaka mitano kabla ya uongozi wa Mama. Kama hayo hayatoshi, kabla ya mwaka 2023/24 kumalizika, Serikali itakuwa imewapandisha vyeo watumishi 81,561 kwa gharama ya TZS bilioni 90.85, hatua hii mbali na kuongeza motisha kwa watumishi hao, utafungua fursa za ajira mpya. Mbali na maslahi yao, Serikali imeboresha pia maeneo… Read More

  • #MiakaMitatuYaMama: Wananchi waanza kunufaika na mageuzi ya sekta ya kilimo

    Kujua unakokwenda ni muhimu ili kuweza kufika, lakini njia ipi uitumie si tu ili ufike, bali ufike kwa wakati, ni muhimu zaidi. Tanzania inalenga kujenga uchumi ambao pamoja na mambo mengine utapunguza kiwango cha umasikini kwa mamilioni ya wananchi, ili kufanikisha hilo Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameamua kuitumia sekta ya kilimo ambayo inagusa maisha ya Watanzania saba katika kila Watanzania 10. Takwimu zinaunga mkono uamuzi wake kuwa kilimo kinachangia asilimia 26 ya Pato la Taifa, kinatoa ajira kwa zaidi ya asilimia 62 ya wananchi, kinachangia dola bilioni 2.3 kwa mwaka, hutoa malighafi za kiwandani kwa asilimia 65 na kinahakikisha usalama wa chakula nchini kwa asilimia 100. Hili ni wazi kuwa mageuzi ya kweli katika maisha ya wananchi ni lazima yahusishe kilimo, siri ambayo MAMA anaijua. Ni vigumu kueleza yote yaliyofanyika katika miaka mitatu ya MAMA madarakani kwani ni mengi mno. Baadhi ya mambo hayo ni bajeti ya kilimo imeongezwa zaidi ya mara tatu kutoka TZS bilioni 294 mwaka 2021/22 hadi TZS bilioni 970 mwaka 2023/24, ongezeko ambalo ni msingi wa mageuzi yote kwenye sekta hiyo. Ongezeko hilo limepelekea mafanikio makubwa katika uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia ambapo matumizi ya mbolea yameongezeka kutoka tani 363,599 hadi tani 580,628 kutokana na mpango wa mbolea ya ruzuku. Matumizi ya mbolea yameongeza uzalishaji wa mazao ulioiwezesha nchi kuongeza mauzo ya nje takribani mara mbili kutoka TZS trilioni 3 hadi TZS trilioni 5.7. Mageuzi yaliyofanyika yamemfikia mkulima katika ngazi ya kijiji kupitia vifaa vilivyotolewa kwa maafisa ugani wa halmashauri 166 zikiwemo pikipiki 5,889, vishkwambi 805, seti za vifaa vya kupimia udogo 143 ambavyo vimemwezesha mkulima kulima kisasa akijua atumie mbegu gani na mbolea gani kwenye aina fulani ya udongo. Kama hayo hayatoshi kuondoa kilimo cha mazoea tena cha msimu, MAMA amewekeza katika kilimo umwagiliaji kwa kuongeza bajeti ya umwagiliaji kwa takribani mara nane kutoka TZS… Read More

  • Ukuaji wa sekta za utalii, madini na viwanda waweka rekodi chini ya Mheshimiwa Rais Samia

    Sera nzuri za uchumi za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu zimeendelea kuweka rekodi ambazo hazijawahi kufikiwa katika historia ya taifa letu ambapo shughuli kuu za kiuchumi za utalii, madini na uzalishaji viwandani zimeendelea kufanya vizuri zaidi. Mwaka 2023 mapato yatokanayo na utalii na dhahabu kwa mara ya kwanza yalivuka dola za Kimarekani bilioni 3 (zaidi ya TZS trilioni 7.6), huku uuzaji nje wa bidhaa za viwandani ukiendelea kuwa juu ya kiwango cha dola za Kimarekani bilioni 1 tangu MAMA aingie madarakani. Matokeo haya ambayo hayakuwahi kufikiwa kabla ni ushahidi kuwa sera nzuri za Rais Samia zinalipa ambapo kupaa kwa mapato ya utalii na dhahabu kumeiwezesha nchini kupunguza urari wa biashara kutoka TZS trilioni 13.6 mwaka 2022 hadi kufikia TZS trilioni 7.2 mwaka 2023. Takwimu toka Benki Kuu ya Tanzania zinaonesha kuwa shughuli mbalimbali za kiuchumi zimeimarika kuvuka kiwango kilichokuwepo kabla ya janga la UVIKO19, hali inayothibitisha kuwa, sio tu uchumi unaimarika kutoka kwenye janga hilo, bali unakuwa kwa kasi ambayo haijawahi kufikiwa kabla. Wakati sekta za kiuchumi zikiendelea kufanya vizuri, mfumuko wa bei umeendelea kushuka ambapo kwa wastani mwaka 2023 ulikuwa asilimia 3 kutoka asilimia 3.2 mwaka 2022, sawa na malengo ya nchi na ukanda wa Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika.   Read More

  • Diplomasia ya Uchumi: Mheshimiwa Rais Samia avutia wafanyabiashara zaidi wa Norway kuwekeza Tanzania

    Mwanadiplomasia namba moja wa Tanzania, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameendelea kutekeleza kwa vitendo Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania, Diplomasia ya Uchumi, katika ziara zake nje ya nchi kwa kutangaza fursa za biashara na uwekezaji zilizopo nchini pamoja na kukutanisha wafanyabiashara wa ndani na wale wa kimataifa. Matokeo ya mkakati huo yameendelea kuonekana ambapo kwa mwaka 2023 miradi ya uwekezaji iliongezeka kufikia 526 kutoka miradi 293 mwaka 2022, uwekezaji ambapo utazalisha ajira kwa maelfu ya Watanzania, utachochea ukuaji wa biashara, mzunguko wa fedha na kukuza kipato cha mwananchi mmoja mmoja na taifa kwa ujumla. Katika ziara yake ya kihistoria ya kitaifa nchini Norway Mheshimiwa Rais ameendeleza mkakati huo ambapo akizungumza katika Jukwaa la Biashara kati ya Tanzania na Norway ametaja sababu za Tanzania kuwa eneo zuri kwa uwekezaji ikiwa ni pamoja na ukweli kuwa itakuwa moja ya nchi 20 duniani ambazo uchumi wake utakua kwa kasi zaidi mwaka 2024 kwa mujibu wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF). Aidha, sababu nyingine ni amani chini ya demokrasia imara wa mfumo wa vyama vingi wenye kuzingatia tunu za utawala bora, kuheshimu haki za binadamu na utawala wa sheria. Kijiografia, amesema Tanzania inafaa kwa uwekezaji kwani ina Bandari ya Dar es Salaam katika Bahari ya Hindi, inayohudumia mataifa nane na ina usimamizi madhubuti wa uchumi na sera ya fedha. Rais Samia amesisitiza fursa tano za kipaumbele zikiwemo uwekezaji katika nishati mbadala, kilimo, mafuta na gesi, mifuko ya uwekezaji, miundombinu na usafirishaji. Tanzania na Norway zinaadhimisha miaka 60 ya ushirikiano ambapo katika mazungumzo ya Rais Samia na viongozi waandamizi wa taifa hilo wamefikia makubaliano ya kukuza ushirikiano wa kiuchumi kuendana na ukubwa wa historia ya uhusiano uliopo.   Read More

  • Mheshimiwa Rais Samia: Chaguzi zitakuwa huru na haki

    Watanzania mwaka huu na mwaka 2025 watatimiza haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi ambao watawaongoza kwa miaka mitano ijayo, ambapo katika mchakato wote huo, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu ameahidi kuwa misingi ya demokrasia, utawala wa sheria, haki vitadumishwa ili wananchi wapate viongozi wanaostahili. Ili kutimiza azma hiyo, ameeleza kuwa mabadiliko ya sheria zinazosimamia vyama vya siasa na uchaguzi yamefanyika kwa kuzingatia maoni yaliyotolewa na wananchi na wadau mbalimbali baada ya kuunda kikosi kazi huru kupitia mazingira ya kisiasa nchini, ambapo kwa kiasi kikubwa maoni yaliyotolewa yamehimiza kuongeza uwazi katika michakato ya uchaguzi ikiwa ni pamoja na uteuzi wa mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi. Maoni mengine ambayo tayari yamefanyiwa kazi ni kubadili jina la Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ili kuakisi uhuru wake. Aidha, amesema baadhi ya maoni yaliyotolewa yalikinzana na Katiba ya nchi, na kuahidi kuwa yatafanyiwa kazi wakati wa maboresho ya kati. “Maboresho haya yatawezesha uchaguzi kufanyika katika mazingira huru na ya haki. Muwe na uhakika kuwa amani na utulivu vitatawala wakati wote kwa gharama yoyote, amesema Rais Samia Suluhu. Akizungumza katika sherehe za mwaka mpya 2024 kwa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, amewahakikishia kuwa Tanzania itaendeleza ushirikiano ulipo kwa kuzingatia Katiba, tunu za taifa, usawa na umoja wetu wa kitaifa na kwamba watafuta sheria, na uingiliaji wa uchaguzi kutoka nje hautakuwepo.   Read More

  • ๐—›๐—”๐—œ๐—๐—”๐—ช๐—”๐—›๐—œ ๐—ž๐—จ๐—ง๐—ข๐—ž๐—˜๐—”: Tanzania yapata uwekezaji wa trilioni 4 ndani ya miezi mitatu

    ๐“๐ก๐š๐ฆ๐š๐ง๐ข ๐ฒ๐š ๐ฎ๐ฐ๐ž๐ค๐ž๐ณ๐š๐ฃ๐ข ๐ข๐ฆ๐ž๐จ๐ง๐ ๐ž๐ณ๐ž๐ค๐š ๐ค๐ฐ๐š ๐š๐ฌ๐ข๐ฅ๐ข๐ฆ๐ข๐š ๐Ÿ–๐ŸŽ ๐ƒ๐ข๐ฉ๐ฅ๐จ๐ฆ๐š๐ฌ๐ข๐š ๐ฒ๐š ๐”๐œ๐ก๐ฎ๐ฆ๐ข ๐ง๐š ๐ฎ๐ข๐ฆ๐š๐ซ๐ข๐ฌ๐ก๐š๐ฃ๐ข ๐ฆ๐š๐ณ๐ข๐ง๐ ๐ข๐ซ๐š ๐ฒ๐š ๐›๐ข๐š๐ฌ๐ก๐š๐ซ๐š ๐ง๐๐ข๐ณ๐จ ๐ฌ๐ข๐ซ๐ข ๐ณ๐š ๐ฆ๐š๐Ÿ๐š๐ง๐ข๐ค๐ข๐จ Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimesajili miradi yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 1.4 (takribani TZS trilioni 4) ndani ya miezi mitatu ya mwisho ya mwaka jana, sawa na ongezeko la 80% ikilinganishwa na miradi yenye thamani ya dola za Marekani milioni 769.6 iliyosajiliwa kipindi kama hicho mwaka 2022. Ongezeko hilo kubwa la uwekezaji limetokana na ziara za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan nje ya nchi ambazo zimevutia wawekezaji kupitia utekelezaji wa Sera ya Diplomasia ya Uchumi na kuimarishwa kwa mazingira ya biashara na uwekezaji nchini ambayo yamevutia wawekezaji wengi zaidi. Katika ziara hizo Mheshimiwa Rais Samia amekuwa akiambatana na wafanyabiashara kutoka Tanzania ambao hupata wasaa wa kuzungumza na wafanyabiashara kwenye nchi anazokwenda, hatua ambayo hutoa fursa ya kuwepo ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji kati yao. Ripoti mpya ya TIC inaonesha kuwa miradi 161 ilisajiliwa kati ya Oktoba-Desemba 2023 ikilinganishwa na miradi 58 kwenye kipindi kama hicho mwaka 2022, ikiwa ni ongezeko la asilimia 178, ambapo sekta tano zilizoongoza kwenye uwekezaji huo ni viwanda, usafirishaji, huduma, kilimo na utalii. Miradi iliyosajiliwa Oktoba-Desemba 2023 inatarajiwa kutengeneza jumla ya ajira mpya 18,390, kutoka ajira 10,216 za kipindi kama hicho kilichopita kwa mwaka 2022 ambapo mikoa iliyoongoza kwa uwekezaji mkubwa ni Dar es Salaam na Pwani. Aidha, ili kutoa fursa pia kwa wawekezaji wa ndani, pamoja na mambo mengine TIC imeanzisha kampeni maalumu ya kukuza uwekezaji wa ndani lengo likiwa ni kusajili miradi ya uwekezaji wa ndani yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 3.5 (TZS trilioni 9) ifikapo mwaka 2028.     Read More

  • Tanzania yaweka historia kununua hisa za kitalu gesi cha Mnazi Bay

    Katika kitabu cha historia na rekodi za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa taifa letu, leo amefungua sura mpya ambapo Tanzania kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa mara ya kwanza limeongeza hisa za umiliki na ushiriki kwenye kitalu cha gesi kwa kununua hisa asilimia 20 kati ya hisa asilimia 31.94 za kampuni ya WentWorth Resources katika kitalu cha gesi asilia cha Mnazi Bay mkoani Mtwara. Kufuatia hatua hiyo, umiliki wa Tanzania kwenye kitalu hicho umefikia asilimia 40, huku kampuni ya Maurel & Prom Tanzania ikinunua hisa asilimia 11.94, na hivyo kufikisha umiliki wa asilimia 60 wa kitalu hicho, na leo kampuni hizo mbili zimesaini mikataba miwili; wa kwanza wa mauziano ya hisa na wa pili wa uendeshaji wa kitalu cha gesi asilia cha Mnazi Bay Hatua ya Tanzania kuongeza umiliki kwenye kitalu hicho ina manufaa mengi ikiwa ni pamona na kuongeza mapato ya Serikali, kuimarisha usalama wa upatikanaji wa nishati nchini, ikiwafahamika kuwa asilimia 65 ya umeme unaotumika nchini ni wa gesi asilia. Manufaa mengine ni kuepusha kitalu kumilikiwa na kuendeshwa na kampuni moja, pamoja na TPDC kuwa na nguvu katika uendeshaji na uendelezaji za kitalu hicho hatua itakayowajengea uwezo zaidi. Kupitia mkataba mpya, sasa uamuzi wa uendeshaji na uendelezaji wa kitalu utafanywa na wanahisa wote, tofauti na awali ambapo Maurel & Prom ambayo ilikuwa inamiliki asilimia 48.05 ilikuwa ifanya shughuli hizo kwa niaba ya wanahisa wengine. Aidha, TPDC imepata haki ya kupeleka wafanyakazi katika shughuli za uendeshaji na uendelezaji kitalu kwa muda mrefu tofauti na awali ambapo walikuwa wanakwenda kwa muda mfupi tu, hivyo kutawajengea uwezo wataalamu wa ndani. Mageuzi haya ya kihistoria yanayofanyika chini ya Mheshimiwa Rais Samia ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (2020-2025) ambayo imeelekeza Serikali kutekeleza mapinduzi ya kiuchumi kwa maendeleo ya watu ambao ndio wanapaswa kuwa wanufaika wakuu wa… Read More

1 2 3 14